Usimwonee Wivu Mtu yeyote

Usimwonee Wivu Mtu yeyote

Bi zandile

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2024
Posts
301
Reaction score
856
Katika nchi hii kuna watu hujui wanapambana na nini.

Usidanganywe na jinsi baadhi ya wasichana wanavyojipiga picha na kupost makalio yao kwenye mitandao ya kijamii. Wengi wao huwa wamevunjika moyo tu. Kupitia picha hizo huwa wanatuma ujumbe kwa wale waliowakataa.

Usidanganywe na wanaume ambao daima hujipiga picha na kuonyesha magari ya kifahari, vifaa na karamu kwenye mitandao ya kijamii. Wengi wao huwa wamepigwa na kitu kizito hadi kushuka moyo - ndani kabisa ya shimo la mikopo - wanajaribu kuficha masaibu yao ya kifedha.

Watu wengi huvaa barakoa ili kufunika maumivu yao. Watakie mema lakini usiwaonee wivu. Sherehekea safari yako mwenyewe. Unatosha. Huna ushindani na mtu yeyote. Uko katika safari ya kibinafsi.

Zingatia mbio zako. Kuwa na shukrani kwa maisha yako. Maisha yako ni zawadi kutoka kwa Mungu. Unachofanya na maisha yako ni zawadi yako kumrudishia Mungu. Usipotoshwe na vitu vyenye kung'aa. Kuwa na kusudi. Kukumbatia ugunduzi binafsi.

Methali 23:17-18 BHN - Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi, bali uwe na bidii siku zote kwa ajili ya kumcha Mwenyezi-Mungu. Hakika kuna tumaini kwako wakati ujao, na tumaini lako halitakatiliwa mbali.
 
Kifupi ni usimuonee mtu wivu wenye chuki ndani yake.

Ila jitihada zao zikupe motisha ya kupambana. Usijipe moyo wa kipuuzi kuridhika na kidogo, UMASKINI unanuka, unaaibisha, unakera, unafadhaisha.

Ongeza juhudi. Kuwa na wivu utakaokuchochea kupambana zaidi.
 
Kifupi ni usimuonee mtu wivu wenye chuki ndani yake.

Ila jitihada zao zikupe motisha ya kupambana. Usijipe moyo wa kipuuzi kuridhika na kidogo, UMASKINI unanuka, unaaibisha, unakera, unafadhaisha.

Ongeza juhudi. Kuwa na wivu utakaokuchochea kupambana zaidi.
Hakika umaskini ni mbaya sana
 
Nilichogundua matajiri hawana shows off....yaan huoni akijionyesha ana vitu fulani Wala kujimwambafai public.

Kutana nasiye viokote🤗 ngiri utamwita Turbo V8🙌..... nikinunua kagari nimepost....kanyumba nimepost....mke au mume nimepost(hapa wanaibiwa wengi sababu ya hivyo vipost)
 
Nilichogundua matajiri hawana shows off....yaan huoni akijionyesha ana vitu fulani Wala kujimwambafai public.
Ni kweli kabisa, hata kimavazi matajiri wa ukweli huvaa nguo za kawaida sana
1729535554970.jpg
 
Maisha ni ushindani jamani, kila kitu hapa duniani ni kushindana anayeshinda anapewa taji, ukitaka kuwa na nguvu lazima ushindane na ili ushinde lazima uwe na technique za kushinda iwe kiroho au kimwili.

Mwanamke kuolewa ni mashindano angalia mnapokuwa kwenye uchumba ni wangapi wanamtaka huyo mwanaume? na kuwa kwenye ndoa ni mashindano sio kwamba ukipata ndoa ndio umemaliza no unahitaji technique za kuhakikisha unaulinda ushindi wako, ukizubaa unanyang'anywa kombe na hapo unakuwa umeshinda, kwenye biashara kuna mashindano, ukifirisika umeshindwa mashindano, usichukie mwenzio anaposhinda ila ikupe hasira za ndani kutafuta mbinu na bidii ili upate kushinda mchezo wako

Ambacho hakitakiwi ni mashindano ya maneno hayo hayana faida

2 Timotheo 2:14

[14]Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao.

Lakini kushindana kuliko halali kunaruhusiwa

1 Wakorintho 9:24-26

[24]Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

[25]Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

[26]Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
 
1)AMRI YA KUMI USITAMANI MALI/MAFANIKIO YA MTU MWINGINE WALA CHOCHOTE ALICHONACHO.
..Kimfaacho mtu chake,cha mtu mavi ukikiona kiteme mate.
..nguo ya kuazimia haisitiri..

2)USIFANYE JAMBO LOLOTE KWA MASHINDANO ..kila mmoja na amuhesabu amuone mwenzake kama ni bora kuliko yeye.
 

Attachments

  • images - 2024-10-25T094013.245.jpeg
    images - 2024-10-25T094013.245.jpeg
    21.1 KB · Views: 4
  • wafilipi-2-3.jpg
    wafilipi-2-3.jpg
    306.8 KB · Views: 3
  • images - 2024-10-25T094552.227.jpeg
    images - 2024-10-25T094552.227.jpeg
    12.1 KB · Views: 5
Kwenye mitandao ya kijamii kila mtu amefanikiwa na ni tajiri kama hapa JF ,hakuna anayepost unyonge kwwnye mitandao ya kijamii,kila mtu anavimba.
 

Attachments

  • images - 2024-10-25T100516.569.jpeg
    images - 2024-10-25T100516.569.jpeg
    16.1 KB · Views: 2
  • images - 2024-10-25T100410.186.jpeg
    images - 2024-10-25T100410.186.jpeg
    10.8 KB · Views: 2
Maisha ni ushindani jamani, kila kitu hapa duniani ni kushindana anayeshinda anapewa taji, ukitaka kuwa na nguvu lazima ushindane na ili ushinde lazima uwe na technique za kushinda iwe kiroho au kimwili.

Mwanamke kuolewa ni mashindano angalia mnapokuwa kwenye uchumba ni wangapi wanamtaka huyo mwanaume? na kuwa kwenye ndoa ni mashindano sio kwamba ukipata ndoa ndio umemaliza no unahitaji technique za kuhakikisha unaulinda ushindi wako, ukizubaa unanyang'anywa kombe na hapo unakuwa umeshinda, kwenye biashara kuna mashindano, ukifirisika umeshindwa mashindano, usichukie mwenzio anaposhinda ila ikupe hasira za ndani kutafuta mbinu na bidii ili upate kushinda mchezo wako

Ambacho hakitakiwi ni mashindano ya maneno hayo hayana faida

2 Timotheo 2:14

[14]Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao.

Lakini kushindana kuliko halali kunaruhusiwa

1 Wakorintho 9:24-26

[24]Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

[25]Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

[26]Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
Wewe ni askofu?
 
Kweli mkuu, mitandao ya kijamii inatengeneza furaha bandia.
 
Back
Top Bottom