Usindikaji wa gesi ya kupikia Kinyerezi

Kwa tz hii tunataka maji kwanza.. Hizo pesa zakusambaza mabomba ya gesi wasambaze maji. Ona kipindu pindu sababu kuu nikutokua na maji safi na salama.
Hiyo misitu yenyewe ndio vyanzo vya maji. Tanzania tunapoteza misitu kwa kasi ya kutisha sana. Huwezi kuliona hilo kwa sasa ila lipo!
Serikali itasave hela nyingi sana watu wakianza kupikia gesi badala ya mkaa, fedha ambazo zinaweza kutumiwa kusambaza maji!
 
Kila inapotokea fursa mafisadi hutumia mwanya kupiga ela tukabaki kupewa visingizio lukuki
 
​Hivi gas ghali inaweza kutumika kuzalisha umeme cheap? Wachumi wetu mko wapi mtusaidie?
 

Kama Tz yetu hauijui vile. Mipango miji mibovu hayo mabomba lazima yahusike na bomoa bomoa lazima itachukua muda.. Na umeme tunao na baadhi pia yavijiji wanao, tatizo gharama, hatuwez shindwa kupikia umeme kama gharama zitapungua. Kuhusu mkaa mi sijasapot matumiz ya mkaa maana yanaharibu misitu ambayo unaweza ukaitumia kwa utalii ikaleta pesa kubwa zaidi ya huo mkaa.
 
Kwa tanzania hii maji kwanza huo umeme waweza ingizwa kwenye grid ya taifa tukapikia kwa gharama nafuu lkn cilitegemei hili kwa serikali ya ccm
Kaa ukijua hakuna mbadala wa maji lkn mbadala wa umeme upo
 



Mambo ambalo watanzania wengi hatulifahamu Ni kuwa Ni ngumu kwa mwananchi wa kawaida kunufaika kwa namna yoyote na gas ya Mtwara maama matumizi yake Ni ngumu kwa mwananchi wa kawaida kuitumia.

Gas inayosindikwa kwenye mitungi Si hii tulionayo sasa. Gas inayosindikwa kwenye mitungi Ni petroleum gas ambayo Ni bi-product ya kuchuja crude oil kupata kerosine, petrol na diesel.

Gas tulionayo hapa kwetu Ni natural gas. Ni gas ambayo Ni ngumu kuwa compressed na kuhifandiwa kwenye mitungi. Na emdapo ukafanikiwa kuicompress, gharama ya kuisindika itakuwa juu mno Mara dufu ya bei ya kununua petroleum gas kutoka Iran.

Tutaitumije hii gas?
Kwa vile hii gas Ni ngumu kuisindika, njia pekee ya mtanzania kuitumia Ni kwa kutumia mabomba ya gas au kupitia Umeme.

Njia ya mabomba ya gas Ni njema zaidi maama gas itamfikia mwananchi moja kwa moja. ILA miundombinu ya mabomba ya gas Ni ngumu Sana kuiweka katika makazi yetu ambayo hayajapangiliwa vyema
 

Kuna watu wamepanga chumba tu kimoja hakuna jiko wala sebure ikifika muda wa kupika wanatoa jiko nje anapika na unakuta nyumba moja inawapangaji hata 8 kwahiyo kwa umeme ni virahisi kuwafungia luku kwa kila mmoja.. Na anaweza kuvuta waya wake paka pale anapo pikia nikama kuchaji sim tu 🙂
 

sio hivo ndugu. Kasome tofauti ya LIQUIFIED PETROLEUM GAS (LPG) na NATURAL GAS.
 
Kupikia hii gesi inawezekana ila si kwa njia ya mitungi ni kwa njia ya bomba, kuna baadhi ya mahotel tayari wanapikia hii gesi toka Mtwara. Lakini hasa hasa serikali inahitaji gesi itumike kufua umeme tatizo la umeme liishe nchini na tayari Tanesco imeanza kuitumia kufua umeme.
 

Najaribu kufikiria mabomba ya gas yatapoanza kuvuja km mabomba ya ...wasa!!!!
 
Sio ajabu umeme ukapanda bei.kisa tutaambiwa gharama za uzalishaji zimeongezeka kutokana na matumizi ya gesi kuzalishia umeme.
 
Yale alivyosema Maalim Seif ya ukhanisi! Si walisema tutakuwa na gesi ya kutosha kwa Bei rahisi na kuuza nje? Sasa eti gesi imepanda soko la dunia na hivyo kutupandishia..ndio ukhanisi wenyewe
 
Kwamba kampuni ndizo zitaamua lini zipandishe na kwa kiasi gani.!
 
Mbona kila siku wana sema, kupata LPG ambayo ndio tuna tumia kuna uwekezaji unahitajika wa icho kiwanda zaidi ya trillion sijui 40, kwahiyo ni uwekezaji mkubwa sana. Wataalamu wata ni sahihisha
 

Thread ina umri wa miaka sita, bado tumeshindwa..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…