Black billionaire
JF-Expert Member
- Oct 16, 2018
- 455
- 526
Nimecheka sana[emoji23][emoji23]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwasababu wao wamejitoa sadaka kuacha kazi ili wewe wakuandalie vya rohoni halafu wewe uwape vya mwilini!Hawa kina gwajima na kina mwamposa wangeanzisha na vyuo vya ufundi wakatoa elimu bure wangepata masikini wengi sana makanisani hivyo kupitia sadaka wangetajirika zaidi.
Hivi Kwann padri au viongozi wa dini wao huwa awatoi sadaka?
Hii Ina mhusu systeme yoooteUSISAIDIE MASIKINI; ACHA WAFE
Na, Robert Heriel
Umasikini ni laana. Huwezi kuwa masikini kama hujalaaniwa. Ukiona wewe ni masikini jua tayari unalaana, ukiona ukoo wenu ni masikini jua koo yenu mnalaana. Ukiona kabila, taifa au bara lenu ni masikini basi fahamu kuwa hiyo ni laana. Huu ni ukweli mchungu.
Mimi ni masikini nafahamu kuwa nimelaaniwa. Siwezi kujidanganya kuwa ati umasikini wangu ni mipango ya Mungu, huko ni kujifariji. Umasikini ni laana, nimelaaniwa jamani, jamani masikini wenzangu tumelaaniwa, tuache kujifariji.
Ukitaka kujua umasikini ni laana angalia jinsi masikini wengi 90% tulivyo na roho mbaya, wengi tuna roho ya husda, wengi hatupendi maendeleo ya wengine, wengi tuwashirikina na wachawi, wengi tukisaidiwa hatuna shukrani, yaani masikini ni mashetani wenye vibali vya kufanya uovu duniani.
Kama kuna mistake utakayoifanya kwenye maisha, ni kusaidia masikini. Ndugu yangu, hata umuone masikini anakufa njaa hapo usimsaidie, muache afe, jitie kihere here kumsaidia yatakayokupata mimi simo.
Ni bora umpe hicho chakula mbwa wako usiku atakulinda. Bora uwape kuku hicho chakula utakula mayai yake. Lakini sio masikini, masikini kumsaidia ni kumsaidia shetani. Huwezi msaidia mtu aliyepewa laana na Mungu hata siku moja. 90% ya masikini wanalaana ya asili, iwe ni mimi au wewe, au yule ilimradi ni masikini basi usitusaidie.
Masikini wanaroho nzuri wakiwa wanashida ya kukuomba jambo fulani. Masikini ni wanafiki sana. Utakuta yanakuchekea na kukusifia lengo ni kukutapeli. Masikini wanajua kulia lia wakiomba mkopo, bahati nzuri kwa masikini wamepewa kauli thabiti ya kushawishi kama shetani ili uingie kingi. Ukijiloga kumkopesha utaipata fresh ya shamba. Utadai na kudai, limasikini litakuwa halipokei simu yako, halijibu sms zako, mwishowe litaku-block. Hahahahah! Sicheki kama mazuri lakini hayo ndiyo mambo yetu sisi masikini tuliojawa na laana.
Masikini usimsaidie.
Masikini usimsomeshe
Masikini usimpe kazi
Masikini usimuoe wala kuolewa naye. Kuoa masikini ni kuoa shetani na ukoo wake. Kisha utazaa matoto yenye roho za kishetani
Kumsomesha masikini ni kuyasomesha mashetani ili yazidi kutenda maovu.
Masikini usimkopeshe
Ukimpa kazi masikini ni kumpa shetani nguvu ya kupata kipato atazidisha maovu yake. Jamani jamani! Ngoja mtanielewa tuu! Bahati nzuri wengi wetu sisi ni masikini hivyo ni rahisi kuelewana, hata uwe kichwa ngumu.
Utakachoweza kumsaidia masikini ni kumzika siku akifa tena uchimbe shimo refu la futi ishirini, ulifukie na mchanga, huo ndio msaada pekee wa kumpa masikini ambao hautakuumiza lakini msaada mwingine wowote ule lazima ile kwako tuu.
Ninachowapendea matajiri hawawapendi masikini kabisa. Huwezikuta tajiri anamualika masikini nyumbani kwake. Matajiri wanajua kumuita masikini nyumbani ni kumkaribisha shetani ndani ya nyumba, mikosi na mabalaa yataandama nyumba hiyo mpaka wakome. Ndio maana majumba ya matajiri huwezikuta watu wanaingia ingia na kutoka.
Masikini hawapendi utulivu, utasikia makelele muda wote, huyu kawasha singeli, huyu taarabu, huyu ngoma ya Lugwadu yaani kelele tuu. Mara vigoma, sijui vigodoro, mtaa mzima matusi, yaani umasikini ni ushetani. Mitaa ya masikini ni kama kuzimu.
Uchafu kila pahala, nzi, mende, kunguni yaani vangala vangala. Masikini hawajipendi kwa nini wewe uwapendi.
Masikini unachoweza kumsaidia ni kumdhulumu, iwe pesa na vipesa vyake. Ukifika nyang'anya shamba lake, sijui kiwanja, akilia masikini kilio chake ndio baraka zako, niamini mimi.
Watu wote waliowadhulumu masikini walibarikiwa, kwa maana kumuangamiza mwenye laana ni kutafuta baraka kwa aliyempa huo umasikini. Lakini kumsaidia mwenye laana ya umasikini ni kupambana na aliyempa hiyo laana. Watu wote waliowasaidia masikini kwa nia njema walikufa vifo vibaya tena waliuawa na hao hao masikini.
Msaidie masikini kwa nia mbaya lakini mwonyeshee unania nzuri. Nafikiri mataifa makubwa yote hufanya hivyo. Wazungu wanajifanya wanania njema ya kuwasaidia masikini wa Afrika lakini ukweli ni kuwa wanawadhulumu kwa upande wa pili.
Msadie masikini shilingi 10 kisha jipatie shilingi elfu moja. Hapo masikini atakuheshimu, na utabarikiwa miaka nenda rudi wewe na ukoo wako. Matajiri wakubwa duniani, hata hapa nchini, matajiri wakubwa wote huwadhulumu masikini kwa kuwalipa mishahara ya misukule. Matajiri wanazidi kuneemeka wakati masikini wakizidi kuwa fukara na wanashangilia.
Ukitaka kushangiliwa na masikini basi mdhulumu kwa kumsadia ukiwa na lengo la kumnyonya kama agenda ya siri. Yaani humsaidii kutoka moyoni. Huoni huko kwenye makanisa ya siku hizi. Manabii na mitume wanavyopata utajiri. Wao wanajua siri hii; masikini hasaidiwi bali anapaswa kudhulumiwa ili azidi kuwa masikini asizidishe uovu wake.
MADHARA YA KUWASAIDIA MASIKINI
1. UKIMSOMESHA MASIKINI ATAFANYA HAYA;
Masikini nimeshakuambia hasomeshwi. Ukimsomesha cha moto utakipata. Akishamaliza shule atajiona yeye ndio yeye. Kazi kudharau wengine, kuwaona hawafai, Hatatumia elimu yake isaidie jamii yake. Badala yake elimu yake itaingamiza jamii. Kwanza atabadili mitindo ya maisha kuanzia mavazi, kuongea, atabagua kazi na kudharau baadhi ya kazi. Atataka mishahara mikubwa hata mara tatu ya watu wengine.
Masikini apike visheti, masikini auze mabumunda, auze kababu thubutuu! Masikini akipata matako hulia Mbwataa! Huoni masikini waliosomeshwa hapo mtaani?
Angalia matajiri waliosomeshwa, embu angalia watoto wa kihindi, kizungu, kiarabu, amemaliza shule utamkuta kwenye mgahawa anauza sambusa, nyama choma, piza, baga, dereva, fundi magari.
Usimsomeshe masikini, utaishia kudharauliwa.
2. USIMPE KAZI MASIKINI
Masikini ukimpa kazi utakuwa umeamua kumpa shetani nguvu ya kiuchumi kufanyia maovu. Atazilewea hizo hela bila akili, ataiba wake za watu kwa kuwahonga kimshahara chake, atatia watoto wa watu mimba na kuwatelekeza, kazini atakuwa na nyodo na dharau kwa wateja wake, atadharau wasio na kazi na kujiona Mungu mtu.
Masikini akipata kazi atasahau hata marafiki zake aliosota nao kipindi hana kazi. Masikini akipata kazi anaweza muacha hata mchumba wake au mke/mume wake kisa sasa anajiweza. Masikini ndiye shetani anayeombewa kanisani na misikitini kila siku.
Usiombe Limasikini ndio liwe polisi, hahahah! Mbona utakoma ukiingia kwenye anga zake. Litakupa kesi ya kubambikiza ili ulipe pesa, litakuomba rushwa, litakupiga bila sababu kama sio kukuua kabisa, yaani jitu ni masikini alafu ulipe kazi ya upolisi hahaha! Umechanganyikiwa wewe. Au ulipe kazi ya uhakimu, yaani hapo umekabidhi mahakama kwa shetani.
Umpe masikini kazi ya udaktari, litaiba madawa na kuuza, litauza viungo vya watu, litaua watu kwa makusudi tuu, yaani tafrani
Limasikini liwe Lichungaji, hahaha! Mara litajiita nabii, litajiita mtume, yaani majina yote yenye sifa, unajua masikini wanapenda sifa sana kama Shetani. Sasa angalia kwenye sadaka litakavyowapiga, na ninyi kwa vile limetumia mbinu ya kuwachota kisaikolojia na kupewa psychological effects ambazo wengi huziita imani, utajikuta unatoa pesa ukiamini kuwa siku moja nawe utakuwa tajiri wa majumba na magari ya kifahari. Hahahah! Hayo yanaitwa matatizo ya kisaikolojia. Kumbuka masikini humuwezi kwa mdomo, ni kama shetani, ni muongo balaa.
3. USIMPE MASIKINI UONGOZI
Kumpa masikiniuongozi ni kumpa shetani usukani wa kuwaongoza. Masikini ni mtu wa visasi kama alivyo shetani. Masikini anataka kusikilizwa yeye tuu kama Mungu, huyo Mungu mwenyewe ameacha uhuru. Masikini kuua ni kitu cha kawaida. Ukimpa masikini uongozi ni lazima vifo viwepo.
KAINI mtoto wa kwanza wa Adamu alikuwa ni Masikini lakini Mungu alimpa uongozi(uzaliwa wa kwanza). Umasikini wa KAINI ulitokana na kutokuwa mwaminifu katika kutoa dhabihu, alikuwa akimpunja Mungu, wakati mdogo wake alikuwa mwaminifu hali iliyofanya Mungu ambariki(akawa tajiri). Jambo hilo limfanya KAINI kuwa na wivu mbaya kwa mdogo wake.
Kumbuka uchoyo wa kutoa dhabihu kwa Mungu ndio chanzo cha umasikini wake. Masikini wote duniani ni wachoyo. Mbili, wanawivu mbaya, mwisho huwa wauaji.
Kaini akaamua kumua mdogo wake kisa utajiri(kubarikiwa) yeye ni masikini na ndiye kiongozi kwani ni mzaliwa wa kwanza.
Masikini akipewa uongozi uwe wa kifamilia, kijamii, kikampuni, au Kinchi hakika hakuna namba mtakazo acha kuzisoma.
4. USIOE/KUOLEWA NA MASIKINI
Kuoa/kuolewa na masikini ni kuoa/kuolewa na shetani. Hakuna rangi hutaacha kuziona. Umalaya yeye, ugomvi yeye, ubahaili yeye, wivu yeye, vizinga yeye, uchawi yeye, ulevi yeye, dharau yeye, matusi yeye, sasa hapo utasema unaishi na binadamu? huyo ni shetani, hakuna binadamu wa hivyo.
Masikini hupenda kupendelewa sana. Ukioa masikini unatafuta balaa. Ukisaidia kwenu kelele, ukisaidia kwao kimya, ndugu zako wakija kelele, ndugu zake wakija kimyaaa!
Wanaume masikini 90% wakianza kupata pesa huanza umalaya, na mara nyingi hufikiri walikosea kufanya uchaguzi kukuoa wewe. Ndio mashetani yalivyo.
Wanawake masikini 90% wakijiweza na kuwa na uchumi wa uhakika, huanza dharau, majibu ya shombo, vijembe hata wakati wa kiangazi utaviona, wengi hudai talaka kwa dizaini nyingi iwe kwa kusema au kwa matendo.
Usioe mwanamke/usiolewe na mwanaume masikini, hapo umechukua shetani ndani ya nyumba.
5. USIMKOPESHE MASIKINI
Masikini hakopeshwi. Kumkopesha masikini ni kumpa sadaka shetani. Kumsaidia masikini ni kutoa sadaka kwa Mungu. Yaani Ukiona umemkopa masikini ujue umezua balaa, kwanza unatafuta ugomvi, mbili unatafuta kufilisika kama umekopa kiasi kikubwa, tatu umedhamiria jamii ikuone wewe huna subira kwani muda wa kukurudishia hela yako utakapopita na hajalipa deni mtaanza kukimbizana. Masikini husikilizwa mbele ya baraza kwani uso wake ni wa huruma lakini moyo wa ibilisi.
Masikini anamaneno laini akikukopa, lakini utajuta ukienda kumdai, hutaamini maneno atakayokupa.
Masikini akikuomba umkopeshe 100,000 mpe elfu kumi mwambie huna pesa, na hiyo elfu kumi mwambie hutamdai. Hapo utapata baraka kwa Mungu kuliko umkope masikini laki moja ili akusajili kwenye timu zake za kishetani za kudaiana.
Hakuna tajiri anayeweza kumsadia masikini bila kujua atapata faida gani?
Hakuna Mungu atakayesaidia masikini bila kujua atapata faida gani?
Je wewe unamsaidia masikini bure ni nani kama sio mwendawazimu?
Tangu umeanz kusaidia masikini kuna lolote umelipata zaidi ya lawama, ugomvi, kukimbizana na hao hao masikini?
Masikini tulishapa laana kwa Mungu, kumsaidia masikini ni kupambana na Mungu. Kumuangamiza masikini ni kutafuta baraka kwa Mungu.
MUHIMU: Sisi masikini tubadilike, roho mbaya tuache. Tumuombe Mung atuondolee hii laana ya umasikini kwa maana sisi ni kama mashetani.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Zanzibar
Hamtakiwi kukomenti nyie mmetetewa mkuumatajiri tuna coment wapi?
Sio kila yatima Ni MASKINI bali Kuna MASKINI yatima.ILA KUNA UKWELI KUMBUKA usemi huu wa wahenga " MASKINI AKIPATA .......HULIA MBWATA.bila kukupesa watu masikini wakutupwa wakipewa nafasi huwa wanafanya maajabu makubwa sana katika taasisi na nyanja mbalimbali, hata mashuleni fuatilia vizuri utaona mayatima wanavyoperform vizuri sana na wana nidhamu ya juu sana....
Naona umefananisha umasikini na ushamba kwasababu ukimsomesha mtu mshamba na akajanjaruka, ataanza kweli kuwa na tabia za ajabu, lakini ukimsomesha masikini atakulipa fadhira na ataweka mazingira yawewe kuendelea kumuamini....
Nimejibu kwa kuzingatia muktadha wa mada, ila najua unaweza kuwa umemaanisha vitu vingine kabisa kama fasihi inavyokupa uwanda mpana......
Sio kila yatima Ni MASKINI bali Kuna MASKINI yatima.ILA KUNA UKWELI KUMBUKA usemi huu wa wahenga " MASKINI AKIPATA .......HULIA MBWATA.
I wish I could Unsee this.
Masikini hata akipata, umasikini wake hauondoki akilini, kuna watu hawana pesa lakini ni matajiri, as hawana attributes za kimasikini, lakini masikini hata akipewa bado umasikini wake hauondoki.
Wewe ndio umeongea kile ambacho kilikuwa kichwani mwangu kwa wepesi zaidi.
Mtu mwenye rich spirit hata kama hana anakuwa hana tatizo na mtu. Na akiwa nacho ndio kabisaa yani wote mtafurahi. Wako positive mda wote!
Ila wenye roho ya kimaskini ndio wanakuwaga na attitude ya kilimbukeni tu. Hawa ndio wale anawaza apate ili awakomeshe akina flani..Ata strive kupata recognition akipata nafasi na sio kwa nia ya kusaidia kuwainua walio karibu nae bali kuwa oppress ili awe ni mtu wa kutukuzwa, ili akusaidie ni lazma umsujudie na msaada unaambatana na matangazo.Husda na choyo ndio vimeijaza mioyo ya hawa watu.
So kwangu tafsiri ya umaskini ina stem kwenye roho ya mtu. Haijalishi una hela au hauna ila umaskini upo rohoni. Binafsi naweza kuwa sina kitu ila siji count kama maskini sababu najua i have a rich heart na nikiwa nacho im good at giving a hand to others sibaguagi watu.
Mada fikirishi sana hii... Mleta mada kama nilivyomuelewa hajazungumzia umasikini kipato bali umasikini wa roho.
Mtu hata kama ni ana mali nyingi kama ni masikini wa roho haoni tabu uwezo wake kuwa anguko la wengine. Nawafahamu matajiri wengi wengi waliofariki wakiwa hawana mali zozote na wapo masikini waliokufa wakaacha mapesa kwenye mabenki(sijui kama ntaeleweka hapa).
Soma, tafakari, jitafute na uchukue hatua.
Naunga mkono hoja
Umaskini kwa mtazamo upi?
Kidini/kiroho?
Kiuchumi?
Kimawazo?
Nafkiri mtoa mada ana Umaskini wa ufafanuaji wa aina ya Umaskini ktk andiko lake
Nilicho kielewa hapo zinaongelewa tabia za kimasikini na sio kiwango cha pesa kwa maana hyo unaweza kua na pesa kidogo ukawa na tabia za kitajili vile vile unaweza kua na pesa nyingi ukawa na tabia za kimasikini kwahiyo msiumie sana wakuu jitafakari tabia zako zina kaa upande upi
Najiweka kwa matajiri maana ukijinenea ufukara nature Ina respond ulichotaka so I'm rich and striving hard, nauchukia umaskini wa kimwili n kiroho pia always nawaza yaliyo mema, hata kuchukia wengine ni sadists behavior na ni roho ya kimaskini pia
Ila kwa nilivyoelewa umasikini Ni roho na sio levo ya kimaisha , Maana kuna watu wana maisha ya levo ya chini Ila roho zao zimejawa na furaha sana kumaanisha roho zao zina utajiri ndani yake, Ila pia Kuna wenye mali nyingi Ila roho zao zina umasikini ndani yake wao hawana furaha kabisa rohoni na wamejawa ubaya nadhani unazungumzia hao.
What a wonderful article[emoji116][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]Biblia ktk kitabu cha 2Wakorintho 8:9, inasema;
Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwa Umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri.
Uko sahihi ndugu Robert, labda kwa mtu ambaye hayajui Maandiko. Bwana Yesu Kristo alikuja kutukomboa wanadamu na LAANA. Umaskini umo ndani ya Laana, hivyo, ni laana kama unavyosema.
Naamini Umaskini unaoongelewa nawe Robert ni ule wa Kipato. Ni Umaskini mbaya sana hakika. Tuuchukie kwa nguvu zote. Mwenyezi Mungu anataka tuwe Maskini wa roho. Una faida kubwa kwani utakusaidia kukupa njaa na kiu ya kuutafuta Uso wa BWANA Mungu kwa Bidii; Na hatimaye utafuzu kuingia rahani Mwake mbinguni.