Usithubutu kujivunia Cheo cha Kuteuliwa, yasije kukukuta ya Chalamila

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hebu fikiria mtu ambaye alikuwa analindwa na Jeshi la Polisi huku akipigiwa salute na RPC, usafiri wake ukiwa ni V-8, leo anaondoka Mwanza bila hata Mgambo wa KK SECURITY, tena kwenye gari ya kupewa lift na Msamalia Mwema

Katika kipindi kifupi sana cha miaka 6 Taifa hili limefundishwa mambo mengi sana na Mwalimu Mkuu ambaye ni Mungu Mwenyewe, kama kuna asiyeelewa basi hatuna cha kumsaidia

 
Wafiche hizo Kudu huwa hawachelewi
 
Huyo ni Lecture wa Iringa university

Anarudi kufundisha chuo kikuu

Ana Akili sana, Sema ana masihara sana na mizaha mingi sana

Ni msomi mzuri tu wa falsafa na saikolojia, Tatizo Lake ni anaongea mambo kinyume nyume sana, Usipokuwa makini anakuingiza chaka huyo Chalamila

Anaweza akawa anakusifia kumbe anakukejeli

Anaweza akawa anakukejeli kumbe anakusifia

Juzi kaongea Mwanza kwa lengo la kusifia kuwa watu hawatabeba mabango , Mama kamshutukia kuwa mnafiki mkubwa chalamila

Anaongea mambo zig zag sana

Alitaka kugombea ubunge enzi za JPM, Ghafla akapiga u turn na kujifanya Mbeya kuna miradi mingi ya kusimamia hivyo bora abaki Mbeya, Kumbe alikuwa anaogopa kutumbuliwa na JPM

Huyo janja janja sana
 
Kama aliondoka vizuri,wengine hujisahau na kuondoka kwa nyodo...
 
Kwa kuwa maisha yanaendelea mwacheni brother Chala akapumzike. Tunamshukuru kwa jitihada zake na alipokosea ni ktk mapungufu yake..! Yake yashapita tugange yajayo..
 
Suala zima la majivuno kwa ujumla wake sio jambo la kiungwana hata kidogo achilia mbali nafasi za kisiasa ama kuwa na pesa nyingi.

Be humble, you won't stay fresh for ever.
 
Ukisema "Huyo ni Lecture wa Iringa University" una maana gani? Mtu anawezaje kuwa "Lecture"!!?? How? Au ulikua una maana ya "Lecturer" .... Don't say it was a typing error. Vijana wengi wa siku hizi mmekua mkitumia hili neno "Lecture" mkiwa na maana ya mtu yaani "Lecturer"

Lecture ni kile kinachotolewa na mtu ambaye ni Lecturer.
 
Mkuu watanzania wengi hawajui kiingereza ila wanakipenda sana. Maadamu wanaelewana au umemwelewa unakausha tu maana utajichosa kusahihisha.
 
Hata vyeo vya kupigiwa kura sio vya kujivunia kabisa. Just imagine, leo Msigwa, Prof. Jay, Mbowe, Sugu, Heche hakuna tena neno Mheshimiwa! Ahahahahahahah!!!
 
Kama huyo ni msomi mzuri wa saikolojia na falsafa basi taifa letu ni giza totoro na halina tofauti na kusadikika.
 
Hata vyeo vya kupigiwa kura sio vya kujivunia kabisa. Just imagine, leo Msigwa, Prof. Jay, Mbowe, Sugu, Heche hakuna tena neno Mheshimiwa! Ahahahahahahah!!!
Nani kakudanganya kwamba uliowataja walishindwa uchaguzi ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…