Usitoe misaada hovyo hovyo

Usitoe misaada hovyo hovyo

Kuna ule usemi wa kichina,unasema"nikikupa samaki nimekulisha kwa siku moja lkn nikikufundisha kuvua samaki nimekulisha maisha yako yote"

Ni hivi!....
Njia nzuri ya kusaidia watu sio kuwapa wanachotaka Bali ni kuwapa means ya kupata wanachotaka..
 
Linda uchumi wako Kwa wivu mkubwa
Huu ni uzi tu wa kukumbushana. Kuna wale wenzetu wanaojifanya wakristo kuliko kristo mwenyewe nawasihi muache ujinga. Kusaidia sio jambo baya ila unaposaidia kiasi cha kutaka kujiyumbisha kiuchumi inakuwa sio sahihi. Saidia kulingana na uwezo wako na usisaidie hovyo hovyo. Watu wasikuzoee.

Kumbuka kabla ya kukuomba msaada watu walikuwa wanaishi maisha yao. Kwahiyo hata usiposaidia watapata jinsi ya kujinasua. Epuka kuwekewa alama kama mtoa misaada. Ukifilisika watakuhama na kutafuta mhanga mwingine. Watasahau kila kitu ulichowasaidia na wengine watakucheka na kukuona mpuuzi.

Hata ukiwa kanisani usibabaike na mchungaji anavyosema "toeni ili madirisha ya mbinguni yafunguliwe baraka kwenu"... pale church wanakuwekea na vijana wazuri kukuimbia nyimbo tamu ili utoe hiyo hela. Tafadhali chukua tahadhari.

Linda uchumi wako kwa wivu mkubwa.
 
Siku za nyuma nilikuwa namsaidia sana shemeji yangu, kuna siku aliniomba ela bahati mbaya sikuwa na ela na mshahara ulichelewa sana kutoka bahati mbaya hakakosa uvumilivu kwa kuniandikia msg "samahani shemeji kwa kukusumbua acha nikae na shida zangu'kiukweli niliumia sana ikabidi nimkope mtu nimtumie na toka siku hiyo nikakata mazoea nae
 
Screenshot_20241207_160123_WhatsAppBusiness.jpg
 
Back
Top Bottom