Usiyoyajua juu ya bonde la Ngorongoro

Usiyoyajua juu ya bonde la Ngorongoro

Maryam Malya

Senior Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
116
Reaction score
260
Na Lukumay M.

Ufinyu wa taarifa sahihi ni janga jipya katika Dunia ya sasa. Wanasiasa wanautumia mwanya huu kubeba ajenda zao binafsi bila kuzingatia ukweli. Kwanza kabisa niweke wazi mimi ni mzaliwa wa kijiji cha Enduleni ndani ya NCA hivyo naandika ili kukupa uhalisia na si vinginevyo.

Kuanzia mwaka 2000 zimefanyika tafiti zaidi ya 94 kutoka Taasisi mbalimbali za elimu ya juu na mashirika ya ndani na nje ya nchi. Mara nyingi matokeo ya tafiti hizi yamekuwa yakishahabiana katika vipengele vya uhai wa NCA na ustawi wa wakaazi wa eneo hili.

Baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikijirudia mara nyingi na wakaazi wa Ngorongoro tunafahamu ni kama zifuatazo;

1. Ongezeko kubwa la idadi ya watu kwa mwaka. Mfano mpaka mwaka 2015 katika kijiji cha Nainokanoka ongezeko la watu lilikuwa karibu 40% kwa mwaka.

2. Uharibifu wa uoto wa asili (Nature vegetation). Hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na ongezeko la mifugo kama vile Ng'ombe kwa kiasi kisicho stahimilivu kwa eneo la NCA. Ukifika Enduleni leo hii si Enduleni ile ya mwaka 2002, hamna kabisa uto wa asili.

3. Kusambaa kwa magonjwa ya wanyama wa kufugwa na wale wa porini kutokana na muingiliano usio dhibitiwa. Hii ni moja ya mambo yaliyoonyeshwa na kila tafiti niliyowahi kuisoma hapa Ngorongoro na tunashukuru Mungu kuna jitihada zimefanyika lakin bado hali inaendelea kuwa mbaya siku hadi siku.

4. Wimbi kubwa la wahamiaji ndani ya NCA. Watu tunaofahamu historia ya NCA tunaweza kuwatambua wavamizi lakini kimsingi ni ngumu kuzuia watu wasihamie NCA, wengine wanakuja kama watumishi na na baada ya kustaafu wanaweka makazi yao hapa.

5. Ukosefu wa huduma bora za jamii. Binafsi natambua kuwa wazawa wa hapa Ngorongoro ni kama walivyo watanzania wengine hivyo haki ya huduma bora za Afya ni lazima lakini swali kubwa ni kwa namna gani miundombinu itajengwa ikiwa tunahitaji kutunza uasili wa eneo la NCA?

6. Mahitaji ya kisiasa na maslahi binafsi. Kati ya mambo yanayoondoa uhalali wa baadhi ya viongozi wetu hapa Ngorongoro ni kila mmoja kujaribu kuchukua changamoto za NCA kujijenga kisiasa, wapo watu wanajifanya wenye haki kuliko wengine ili mradi tu waweze kutimiza haja zao kisiasa.

Nini kifanyike? Nashauri serikali iendelee kuchukua hatua za kina zenye kulenga kujenga ecosystem endelevu. Wanasiasa wapuuzwe kwa kuwa hawajui uhalisia bali wanafanya wanayoyafanya kwa maslahi yao. Wanaonufaika na NGO's tunawafahamu kwa majina na ukweli ni kwamba mipango yenu haina maslahi kwa Taifa letu.

Nawapongeza walioamua kuhama kwa hiari ndani ya Hifadhi ya NGORONGORO na pongezi kwa serikali kwa kutoa nyumba mpya na viwanja. Maeneo ya malisho ya kutosha, huduma za jamii ni baadhi ya mambo yanayoonyesha dhamira njema ya serikali.
 
Nawapongeza walioamua kuhama kwa hiari ndani ya Hifadhi ya NGORONGORO na pongezi kwa serikali kwa kutoa nyumba mpya na viwanja. Maeneo ya malisho ya kutosha, huduma za jamii ni baadhi ya mambo yanayoonyesha dhamira njema ya serikali.
Imekula kwao, Handeni ni kame kama jangwa. Wanaenda kuumiia. Tatizo la sisis ngozi nyeusi ni kuzaliana kama kuku! Kuna jirani yangu ana watoto sita na bado ni kijana wa late 40s yrs na kazi yake ni kibarua wa ujenzi........ Hakuna uzazi wa mpango maana dini ile inakataza. But kuiponya NCA , let it be done
 
Imekula kwao, Handeni ni kame kama jangwa. Wanaenda kuumiia. Tatizo la sisis ngozi nyeusi ni kuzaliana kama kuku! Kuna jirani yangu ana watoto sita na bado ni kijana wa late 40s yrs na kazi yake ni kibarua wa ujenzi........ Hakuna uzazi wa mpango maana dini ile inakataza. But kuiponya NCA , let it be done
Lazima waondoke. Wakikaa kule kuna siku tutaenda kuangalia wakaazi badala ya wanyama
 
Kwa mara ya kwanza nimesoma mada inayoeleweka. Kama nilivyosema mara nyingi na kama Unesco walivyosema pia binadamu wote wahame kutoka Ngorongoro wakae nje
 
Na Lukumay M.

Ufinyu wa taarifa sahihi ni janga jipya katika Dunia ya sasa. Wanasiasa wanautumia mwanya huu kubeba ajenda zao binafsi bila kuzingatia ukweli. Kwanza kabisa niweke wazi mimi ni mzaliwa wa kijiji cha Enduleni ndani ya NCA hivyo naandika ili kukupa uhalisia na si vinginevyo.

Kuanzia mwaka 2000 zimefanyika tafiti zaidi ya 94 kutoka Taasisi mbalimbali za elimu ya juu na mashirika ya ndani na nje ya nchi. Mara nyingi matokeo ya tafiti hizi yamekuwa yakishahabiana katika vipengele vya uhai wa NCA na ustawi wa wakaazi wa eneo hili.

Baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikijirudia mara nyingi na wakaazi wa Ngorongoro tunafahamu ni kama zifuatazo;

1. Ongezeko kubwa la idadi ya watu kwa mwaka. Mfano mpaka mwaka 2015 katika kijiji cha Nainokanoka ongezeko la watu lilikuwa karibu 40% kwa mwaka.

2. Uharibifu wa uoto wa asili (Nature vegetation). Hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na ongezeko la mifugo kama vile Ng'ombe kwa kiasi kisicho stahimilivu kwa eneo la NCA. Ukifika Enduleni leo hii si Enduleni ile ya mwaka 2002, hamna kabisa uto wa asili.

3. Kusambaa kwa magonjwa ya wanyama wa kufugwa na wale wa porini kutokana na muingiliano usio dhibitiwa. Hii ni moja ya mambo yaliyoonyeshwa na kila tafiti niliyowahi kuisoma hapa Ngorongoro na tunashukuru Mungu kuna jitihada zimefanyika lakin bado hali inaendelea kuwa mbaya siku hadi siku.

4. Wimbi kubwa la wahamiaji ndani ya NCA. Watu tunaofahamu historia ya NCA tunaweza kuwatambua wavamizi lakini kimsingi ni ngumu kuzuia watu wasihamie NCA, wengine wanakuja kama watumishi na na baada ya kustaafu wanaweka makazi yao hapa.

5. Ukosefu wa huduma bora za jamii. Binafsi natambua kuwa wazawa wa hapa Ngorongoro ni kama walivyo watanzania wengine hivyo haki ya huduma bora za Afya ni lazima lakini swali kubwa ni kwa namna gani miundombinu itajengwa ikiwa tunahitaji kutunza uasili wa eneo la NCA?

6. Mahitaji ya kisiasa na maslahi binafsi. Kati ya mambo yanayoondoa uhalali wa baadhi ya viongozi wetu hapa Ngorongoro ni kila mmoja kujaribu kuchukua changamoto za NCA kujijenga kisiasa, wapo watu wanajifanya wenye haki kuliko wengine ili mradi tu waweze kutimiza haja zao kisiasa.

Nini kifanyike? Nashauri serikali iendelee kuchukua hatua za kina zenye kulenga kujenga ecosystem endelevu. Wanasiasa wapuuzwe kwa kuwa hawajui uhalisia bali wanafanya wanayoyafanya kwa maslahi yao. Wanaonufaika na NGO's tunawafahamu kwa majina na ukweli ni kwamba mipango yenu haina maslahi kwa Taifa letu.

Nawapongeza walioamua kuhama kwa hiari ndani ya Hifadhi ya NGORONGORO na pongezi kwa serikali kwa kutoa nyumba mpya na viwanja. Maeneo ya malisho ya kutosha, huduma za jamii ni baadhi ya mambo yanayoonyesha dhamira njema ya serikali.
Pole Lukumay, na unisamehe mimi pia kwa kukurupuka.

Kwa jina inawezekana wewe ni Mmmasai na kwa vile unatoka hapo katika maeneno ya umasaini, basi sina budi kukubali tu wewe ni Mmasai? Kama unavyodai.

Nitajibu kiunagaubaga kwa uliyo yaandika hapa, niseme tu kuwa mimi sio mwanasiasa, na sio mkazi wa maeneo hayo lakini ni Mtanzania mwenye kujali utu na Kilio cha Wamasai-sio Wanasiasa.

Lukumay,
=Unadai ng'ombe ni waharibifu wa uoto asilia, binafsi naelewa ng'ombe ni moja ya wanyama ambao ni wazuri katika "ecosystem' ya uoto asilia. Yaani uhusiano wa viumbe hawa na mazingira waishio huwa ni kinzani, sasa niulize ni ng'ombe tu? Je taka wanazotupa watalii? au Mvua zinazonyesha zinafikia mahitaji ya uoto asilia? Barabara zilizojengwa jebkwa sababu zinahitaji kila aina ya nguvu-petroli, oil n.k na ni uelewa wangu haya yanaweza dumaza "uoto asilia"au? ni ng'ombe peke yake?

Lukumay, Magonjwa ya wanyama
=Wakati naanza kupata uelewa wa dunia na mazingira yake nilipata kuelewa kuwa yamo magonjwa, na vile vile wapo watabibu, wamasai ni wabobezi wa nyanja hii ya utabibu wa kutumia njia asilia(nasikia hata viagara wanayo huko) yaani wamasai ni watunzi wazuri wa wanyama wao"ng'ombe" na vilevile ni watabibu au hujapata simulizi za kihistoria-eneway unauwezekano mkubwa kuwa wewe ni mmasai kwa hiyo nisije changanya mambo hapa. Najiuliza, miaka yote hiyo amabayo waliishi "NGORONGORO" waliishi vipi na wanyama pori pembezoni mwa maeneo yao bila kuathiri hayo Mazingira? " Watalii hawahesabiki kwenye hili la kusambaa kwa magonjwa, yaani hata waujumu uchwara(wanaolisha maplastiki wanyama pori) hawahesabiki na hili?


Lukumay,
binafsi sijui kumumunya na huwa nakurupuka sana tu na kama nilivyo teta huko juu, naandika kiunagaubaga.

Mosi- niwapongeze Wamasai wote huko kwa kusimama kidete kwenye mambo yao bila kuburuzwa buruzwa "SERIKALI" haitaji pongezi kwa kuburuza.
pili,sijawahi sikia wamasai wakilalamika kuwa hawana maeneno ya malisho au kupungukiwa na maeneno yao-i stand to be corrected.
...tatu huwezi ondoa uhusiano wa viumbe(wamasai ni viumbe) na mazingira yao na kudai hapo hapobkuna umuhimu wa "Ecosystem endelevu" au? Nimekosea?
nne ni mahitaji gani ya kisiasa, ni nani hasa hapa duniani ambaye hajui maslahi yake kwenye eneo analoishi? Hao wanasiasa ni wa chama kipi? CCM, ACT au? dhana unayoielezea hili ni potofu na ni yakuchanganya- deflection at best. Jee hiyo haki wanazodai zimefinywa ni za Wanyama tu? Wakati kenge wanauliwa msasani, mikocheni oysterbay mbona hao wakazi hawakuamishwa? au nazusha hili? mambo ya Ecosystem endelevu hayakuwepo?


Huduma bora za kijamii mmhh takwimu zipo wapi hapa? wimbi gani hilo? 40%? watumishi gani hao? Wangapi? wapi? watumishi gani hao wasiokuwa na huduma za kijamii? waliburuzwa Kutumikia? bila huduma.

Lukumay, wataje hao wanasiasa, tupatie hizo ripoti za"vyuo vikuu" na takwimu nasi tuone kama tutafikia ulipofika kuwapa pongezi serikali pamoja na kuwaponda ng'ombe na watu uanoishi nao huko.

Wacha porojo za kuhalilisha uangamizaji wa kabila la Wamasai na kutuletea umuhimu wa kuuzwa vitalu vya biashara kwa manufaa na maslahi ya hao wanasiasa ambao ni CCM na mamlaka wanayohodhi.

Usiku mwema.
 
Kwa mara ya kwanza nimesoma mada inayoeleweka. Kama nilivyosema mara nyingi na kama Unesco walivyosema pia binadamu wote wahame kutoka Ngorongoro wakae nje
Hayo mamlaka mnayodai sijui Unesco au vyuo vikuu ni mazingaombwe tuu.
 
Lazima waondoke. Wakikaa kule kuna siku tutaenda kuangalia wakaazi badala ya wanyama
Hao unaodai waondolewe ndio walikuwa wanapigwa picha ili kuleta watalii, ili watu waje kutoka nje na kufika maeneo yao-wamehujumiwa sana sana-pale walipostukia na kudai maafa yao- wakapewa na masharti-moja yapo ambao bado mimi nitaita GENOCIDAL ni lile la kuacha kuwinda simba wakati vijana wao wanabalehe-

Vitabu, majarida, magazeti yameuza mbuga kwa sura ya MMasai. yeroo!
 
Imekula kwao, Handeni ni kame kama jangwa. Wanaenda kuumiia. Tatizo la sisis ngozi nyeusi ni kuzaliana kama kuku! Kuna jirani yangu ana watoto sita na bado ni kijana wa late 40s yrs na kazi yake ni kibarua wa ujenzi........ Hakuna uzazi wa mpango maana dini ile inakataza. But kuiponya NCA , let it be done
Unayoelezea yanafanana na ya waurigi wa uchina. Kupelekwa handeni sio kwa kuwa handeni kuna nafasi tu, bali wapelekwe kuenyeshwa na waekezaji wa migodi...kwa nini waipelekwe Zanzibar kwenye mijengo ya Karume?
 
Wamasai wanazaliana kama kuku, waondolewe wote kwa nguvu.
 
Masai marafiki zangu jiandaeni kisaikolojia hii nchi ina miardhi mingi yenye mamito na makonde ya kufugia ,mjadala uwe kuondoka kwa maslahi mapana ngorongoro ipewe maeneonyenu ya ibada na matambiko yalindwe vyema na kuheshimiwa ila mnahamishiwa handeni hakikisheni serikali inawajengea mabwawa ya maji visima vya mwaka mzima virefu,shule bora ,hospital,umeme etc lasivyo mtaondoka kwa kijinga ,hapo hakuna namna mtabaki HAIPOOO
 
Wamasai wanazaliana kama kuku, waondolewe wote kwa nguvu.
Weka ushahidi wa kuzaliana kama kuku. Nguvu watayotumia kuwaondoa kwa nguvu sikubaliani nayo, na Jeshi lelote litakalo husika na mchakato huo kutawapeleka kwenye historia za karne mpya kuwa wanahusika na 'Uangamizaji wa raia wao wenyewe' sidhani wenye akili timamu watapendezeshwa na hilo, ila kwa sababu wao ni wa kutii amri, mioyoni mwao hawawezi kuridhishwa na kuburuzwa, kuwafanyia binadamu wenzao uangamizaji.
 
Na Lukumay M.

Ufinyu wa taarifa sahihi ni janga jipya katika Dunia ya sasa. Wanasiasa wanautumia mwanya huu kubeba ajenda zao binafsi bila kuzingatia ukweli. Kwanza kabisa niweke wazi mimi ni mzaliwa wa kijiji cha Enduleni ndani ya NCA hivyo naandika ili kukupa uhalisia na si vinginevyo.

Kuanzia mwaka 2000 zimefanyika tafiti zaidi ya 94 kutoka Taasisi mbalimbali za elimu ya juu na mashirika ya ndani na nje ya nchi. Mara nyingi matokeo ya tafiti hizi yamekuwa yakishahabiana katika vipengele vya uhai wa NCA na ustawi wa wakaazi wa eneo hili.

Baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikijirudia mara nyingi na wakaazi wa Ngorongoro tunafahamu ni kama zifuatazo;

1. Ongezeko kubwa la idadi ya watu kwa mwaka. Mfano mpaka mwaka 2015 katika kijiji cha Nainokanoka ongezeko la watu lilikuwa karibu 40% kwa mwaka.

2. Uharibifu wa uoto wa asili (Nature vegetation). Hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na ongezeko la mifugo kama vile Ng'ombe kwa kiasi kisicho stahimilivu kwa eneo la NCA. Ukifika Enduleni leo hii si Enduleni ile ya mwaka 2002, hamna kabisa uto wa asili.

3. Kusambaa kwa magonjwa ya wanyama wa kufugwa na wale wa porini kutokana na muingiliano usio dhibitiwa. Hii ni moja ya mambo yaliyoonyeshwa na kila tafiti niliyowahi kuisoma hapa Ngorongoro na tunashukuru Mungu kuna jitihada zimefanyika lakin bado hali inaendelea kuwa mbaya siku hadi siku.

4. Wimbi kubwa la wahamiaji ndani ya NCA. Watu tunaofahamu historia ya NCA tunaweza kuwatambua wavamizi lakini kimsingi ni ngumu kuzuia watu wasihamie NCA, wengine wanakuja kama watumishi na na baada ya kustaafu wanaweka makazi yao hapa.

5. Ukosefu wa huduma bora za jamii. Binafsi natambua kuwa wazawa wa hapa Ngorongoro ni kama walivyo watanzania wengine hivyo haki ya huduma bora za Afya ni lazima lakini swali kubwa ni kwa namna gani miundombinu itajengwa ikiwa tunahitaji kutunza uasili wa eneo la NCA?

6. Mahitaji ya kisiasa na maslahi binafsi. Kati ya mambo yanayoondoa uhalali wa baadhi ya viongozi wetu hapa Ngorongoro ni kila mmoja kujaribu kuchukua changamoto za NCA kujijenga kisiasa, wapo watu wanajifanya wenye haki kuliko wengine ili mradi tu waweze kutimiza haja zao kisiasa.

Nini kifanyike? Nashauri serikali iendelee kuchukua hatua za kina zenye kulenga kujenga ecosystem endelevu. Wanasiasa wapuuzwe kwa kuwa hawajui uhalisia bali wanafanya wanayoyafanya kwa maslahi yao. Wanaonufaika na NGO's tunawafahamu kwa majina na ukweli ni kwamba mipango yenu haina maslahi kwa Taifa letu.

Nawapongeza walioamua kuhama kwa hiari ndani ya Hifadhi ya NGORONGORO na pongezi kwa serikali kwa kutoa nyumba mpya na viwanja. Maeneo ya malisho ya kutosha, huduma za jamii ni baadhi ya mambo yanayoonyesha dhamira njema ya serikali.
Nilipita NCA niki elekea Serengeti.

Kwa kweli pale pana maisha duni kuwai kuyaona. Labda kinacho wafanya wang'ang'anie pale ni Marisho kwa ajili ya Mifugo yao.
 
Pole Lukumay, na unisamehe mimi pia kwa kukurupuka.

Kwa jina inawezekana wewe ni Mmmasai na kwa vile unatoka hapo katika maeneno ya umasaini, basi sina budi kukubali tu wewe ni Mmasai? Kama unavyodai.

Nitajibu kiunagaubaga kwa uliyo yaandika hapa, niseme tu kuwa mimi sio mwanasiasa, na sio mkazi wa maeneo hayo lakini ni Mtanzania mwenye kujali utu na Kilio cha Wamasai-sio Wanasiasa.

Lukumay,
=Unadai ng'ombe ni waharibifu wa uoto asilia, binafsi naelewa ng'ombe ni moja ya wanyama ambao ni wazuri katika "ecosystem' ya uoto asilia. Yaani uhusiano wa viumbe hawa na mazingira waishio huwa ni kinzani, sasa niulize ni ng'ombe tu? Je taka wanazotupa watalii? au Mvua zinazonyesha zinafikia mahitaji ya uoto asilia? Barabara zilizojengwa jebkwa sababu zinahitaji kila aina ya nguvu-petroli, oil n.k na ni uelewa wangu haya yanaweza dumaza "uoto asilia"au? ni ng'ombe peke yake?

Lukumay, Magonjwa ya wanyama
=Wakati naanza kupata uelewa wa dunia na mazingira yake nilipata kuelewa kuwa yamo magonjwa, na vile vile wapo watabibu, wamasai ni wabobezi wa nyanja hii ya utabibu wa kutumia njia asilia(nasikia hata viagara wanayo huko) yaani wamasai ni watunzi wazuri wa wanyama wao"ng'ombe" na vilevile ni watabibu au hujapata simulizi za kihistoria-eneway unauwezekano mkubwa kuwa wewe ni mmasai kwa hiyo nisije changanya mambo hapa. Najiuliza, miaka yote hiyo amabayo waliishi "NGORONGORO" waliishi vipi na wanyama pori pembezoni mwa maeneo yao bila kuathiri hayo Mazingira? " Watalii hawahesabiki kwenye hili la kusambaa kwa magonjwa, yaani hata waujumu uchwara(wanaolisha maplastiki wanyama pori) hawahesabiki na hili?


Lukumay,
binafsi sijui kumumunya na huwa nakurupuka sana tu na kama nilivyo teta huko juu, naandika kiunagaubaga.

Mosi- niwapongeze Wamasai wote huko kwa kusimama kidete kwenye mambo yao bila kuburuzwa buruzwa "SERIKALI" haitaji pongezi kwa kuburuza.
pili,sijawahi sikia wamasai wakilalamika kuwa hawana maeneno ya malisho au kupungukiwa na maeneno yao-i stand to be corrected.
...tatu huwezi ondoa uhusiano wa viumbe(wamasai ni viumbe) na mazingira yao na kudai hapo hapobkuna umuhimu wa "Ecosystem endelevu" au? Nimekosea?
nne ni mahitaji gani ya kisiasa, ni nani hasa hapa duniani ambaye hajui maslahi yake kwenye eneo analoishi? Hao wanasiasa ni wa chama kipi? CCM, ACT au? dhana unayoielezea hili ni potofu na ni yakuchanganya- deflection at best. Jee hiyo haki wanazodai zimefinywa ni za Wanyama tu? Wakati kenge wanauliwa msasani, mikocheni oysterbay mbona hao wakazi hawakuamishwa? au nazusha hili? mambo ya Ecosystem endelevu hayakuwepo?


Huduma bora za kijamii mmhh takwimu zipo wapi hapa? wimbi gani hilo? 40%? watumishi gani hao? Wangapi? wapi? watumishi gani hao wasiokuwa na huduma za kijamii? waliburuzwa Kutumikia? bila huduma.

Lukumay, wataje hao wanasiasa, tupatie hizo ripoti za"vyuo vikuu" na takwimu nasi tuone kama tutafikia ulipofika kuwapa pongezi serikali pamoja na kuwaponda ng'ombe na watu uanoishi nao huko.

Wacha porojo za kuhalilisha uangamizaji wa kabila la Wamasai na kutuletea umuhimu wa kuuzwa vitalu vya biashara kwa manufaa na maslahi ya hao wanasiasa ambao ni CCM na mamlaka wanayohodhi.

Usiku mwema.
Naomba kutoa ufafanuzi kwa baadhi ya mambo ulio andika

1.Wanyama wa porini hawatibiwi wanapo ugua isipo kua wale walio katika list ya kupotea kama Akina Faru john au kwa shida zinazo sababishwa na binaadamu(Majangiri)

2.Watalii hawaruhusiwi kuwapa chakula wala maji wanyama. Ni kosa kisheria kutupa hata ganda la pipi maeneo ya hifadhi.

3. Barabara za hifadhi hazna rami, zinarekebishwa kwa kiwango cha vumbi peke ake ili kutunza uhalisia wa eneo husika.

Mwisho, Binafsi naamini tatizo kubwa la NCA sio wamasai bali Ongezeko lisilo zuilika la Watu na Mifugo lazma lita athiri ecosystem ya NCA.
 
Nilipita NCA niki elekea Serengeti.

Kwa kweli pale pana maisha duni kuwai kuyaona. Labda kinacho wafanya wang'ang'anie pale ni Marisho kwa ajili ya Mifugo yao.
Usisahahu kuna "Oludonyu Lungai" au oldonyo longai ni kama mount temple la wa israeli kama kama sikosei
Kwanini wasing'ang'anie?
au ndio turudi kusema ni "watu wa sudan"?
 
handeni hakikisheni serikali inawajengea mabwawa ya maji visima vya mwaka mzima virefu,shule bora ,hospital,umeme etc lasivyo mtaondoka kwa kijinga ,hapo hakuna namna mtabaki HAIPOOO
handeni ni jangwa... maji toka enzi za wakoloni, ni jangwa. Unaukbuka mradi wa maji wa Handeni Trunk Main??? Wanakwenda kuumia pumbavu zao
 
Naomba kutoa ufafanuzi kwa baadhi ya mambo ulio andika

1.Wanyama wa porini hawatibiwi wanapo ugua isipo kua wale walio katika list ya kupotea kama Akina Faru john au kwa shida zinazo sababishwa na binaadamu(Majangiri)

Kuna tofauti ya kutibiwa na kulindwa.
Kweli wanyama pori huwa mara nyingi hawatibiwi mpaka pale kunapotokea "pandemic" ambayo unaweza kuathiri wanyama wengine na hususan kama binadamu anaweza kuathirika nalo.
Lukumay ametumia hilo la magonjwa au maambukizi kama kigezo mmoja wapo wa kuwaondoa hao wamasai.
2.Watalii hawaruhusiwi kuwapa chakula wala maji wanyama. Ni kosa kisheria kutupa hata ganda la pipi maeneo ya hifadhi.
Ni kweli ni kosa kisheria, lakini sheria zimewekwa kupunguza makali pamoja na kupunguza ari yakuwa na ukaribu wa wanyama-inatia hofu kwa anayetaka fanya hivyo na ndio sababu yangu kusema "watalii uchwara"...kuna yutubu video ambazo zinaonyeasha watalii wakifanya hivyo na kuna uwezekano yamefanyika mbugani huko, yanatokea mbugani ndio maana kuna sheria.
3. Barabara za hifadhi hazna rami, zinarekebishwa kwa kiwango cha vumbi peke ake ili kutunza uhalisia wa eneo husika.
Kweli barabara hazina Lami zipo karibu -tarime musoma? ilichanja maeneo. hata hizo za vumbi lazima upeleke magreda, yanatumia dizeli na nguvu kazi za watu mara nyingi mradi ukiisha wanatupa huko huko haya.
Mwisho, Binafsi naamini tatizo kubwa la NCA sio wamasai bali Ongezeko lisilo zuilika la Watu na Mifugo lazma lita athiri ecosystem ya NCA.
Naam ninakubaliana nawewe tatizo kubwa sio la wamasai peke yao hata hao anaodai Lakamay wenye "maslahi" za kisiasa mimi najua wenye kuhodhi mamlaka na wanaorusiwa kuendesha siasa ni CCM peke yao. Je na wao wana maslahi mengine nje ya siasa?

Lukumay amedai kuna ufinyubwa Taarifa 'sahihi' sina uhakika taarifa yake ndio sahihi. Lakini amesema katokea huko kijijini kwa hiyo nimchukulie an first hand information amesema "ili kukupa uhasilia" litakuwa na maana gani au nakosea?

Ameongeza kuwa mwaka 2000 kulikuwa na tafiti 94 kutoka Taasisi mbali mbali za juu za elimu ndani na nje-yakuwa kuna mamlaka ya anayosema/andika lakini huko juu amesema kuna ufinyu wa Taarifa sahihi. Sasa sijui niamini lipi, la taarifa za Taasisi mbali mbali au la Uhalisia wake alipotoka huko kijijini?

Mo, leo ni 2022 naamini kutakuwa na taarifa(information au report) au studies zaidi ya hizo 94 za mwaka 2000 labda 940 kwa uwiano lakini kuna "ufinyu" anaficha nini? Je anaficha ukweli wa kuwa kunataka kuuzwa? sio siri tenabkwani wakisema ukweli bila ya dhihaki na uangamizaji hilo la kuuzika haliwezi kufanyika?

Mo, huyo amedai kuna changamoto la ongezeko la watu kwa taarifa zake za 2015 wakati yeye kasoma na kuridhia 94 za mwaka 2000 sasa nichukue lipi? au ni mie ndiye najichanganya

Kutoka 2000 naamini kuna tafiti nyingi pamoja na kuwa kuna ufinyu lakini zipo kwa manufaa ya nani? Wanyama peke yao? Mbuga peke yake? Wamasai peke yao au Jumuisho la wote wahusika?

Nakataa kupokea vigezo ambavyo ni hasi kwa wamasai na nakataa Uangamizaji wa Utamaduni wao. Wananchi wasilgahiwe na vigezo visivyo na mantiki.
Ahsante
 
Wacha porojo za kuhalilisha uangamizaji wa kabila la Wamasai na kutuletea umuhimu wa kuuzwa vitalu vya biashara kwa manufaa na maslahi ya hao wanasiasa ambao ni CCM na mamlaka wanayohodhi.
Ngorongoro haiuzwi
 
Hai unaodai waondolewe ndio walikuwa wanapigwa picha ili kuleta watalii, ili watu waje kutoka nje na kufika maeneo yao-wamehujumiwa sana sana-pale walipostukia na kudai maafa yao- wakapewa na masharti-moja yapo ambao bado mimi nitaita GENOCIDAL ni lile la kuacha kuwinda simba wakati vijana wao wanabalehe-

Vitabu, majarida, magazeti yameuza mbuga kwa sura ya MMasai. yeroo!
Mnataka waendelee kuishi huko porini kama wanyama huku wakikosa huduma bora kwa faida zenu wenyewe hii sio sawa.

Mnawatumia kama vyanzo vyenu vya mapato ya kitalii huku nyie mkinufaika na sio wao, hamna huruma kabisa nyie.

Ni lazima waondoke huko ili Ngorongoro ibaki hai na wao wapate huduma muhimu kama Watanzania wengine.
 
Back
Top Bottom