Usiyoyajua kuhusu Senegal

Usiyoyajua kuhusu Senegal

Mziki wao ni mzuri sana ukichagizwa na namna wanavyocheza....

Mji wa Dakar una matajiri haswa. Barabara zao zimejaa magari ya kifahari latest. Majumba ni ya kifahari kwenye sehemu za kishua....

Wasenegal wanapenda kuendeleza vya kwao.
Wawekezaji wengi ni wazawa.
Jamii za wahindi, wachina si wengi kama Tanzania.
Wasenegal hawapendi kulipwa kidogo. Wao kazi ndogo hela nyingi....
Sasa mkuu unasema magari ya umma Ni Yale kuuu kuu na huku unasema watu Wana magari latest mbna hatari

Kuna documentary nimeonaga offcoz magar karibia yote Ni kuu kuu tu pia ya kizamani Sana [emoji38]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Sasa mkuu unasema magari ya umma Ni Yale kuuu kuu na huku unasema watu Wana magari latest mbna hatari

Kuna documentary nimeonaga offcoz magar karibia yote Ni kuu kuu tu pia ya kizamani Sana [emoji38]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Hapana mkuu.

Magari binafsi ni mazuri sana. Na brand tofauti.
USafiri wa uma ndio kisanga...
 
nchi nyingi zenye waislam wengi uhalifu ni mchache sana,, Somalia huko wanakosema kuna vita unaweza kulala hata mlango wazi,, kifupi panya road wakutafuta kwa tochi kama si hakuna kabisa
VIP Zanzibar inamaana hao 2 parcent Ni wakristo ndio panya rod

Mbona magerezani na police kote nchini kumejaha waislamu tupu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hali ya hewa ni mchanganyiko...
January mpaka march kuna baridi kiasi.

April - July joto linapanda

July - October ni mvua hivyo vipindi huchanganyika.

Dec ni joto....

Kiwango cha umasikini si sawa na Tanzania. Wametuzidi kiasi kidogo kwenye uhalisia wa maisha sijui kwenye makaratasi.

Mpangilio wa nyumba inategemea na maeneo lakini kwa kiasi wametuzidi.
Tunachowazidi kwao mji mkuu Dakar umejaa. Hvyo ukimiliki kiwanja ni unajenga chote hakuna cha parking wala eneo la kupumzikia. Nyumba zimeungana kabsa. Ila mitaa ipo vyema.

Ni taifa lenye waislamu wengi ila si taifa la kiislamu. Dini kwao ni tamaduni yao. Utaratibu ni wa mfaransa kama mkoloni wao aliyepita. Kumpuzika weekend.

Hawa watu kwa rangi tu ni weusi. Weupe wachache sana ila wapo....
Huyo rais wao Mack Sally Ni muislamu au mkiristo

Nae nasikia wanamtakaa asitawake kwa temu ya tatu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hahaha mkuu....

Simba wanaijua kwa sababu kuna wachezaji wa Senegal wamepita hapo. No less no more.....

Hawa hawafuatilii hata mpira kivile.
Nimevaa jezi ya Yanga sana na wengi husema ni jezi ya Brazili.

Ila ya Simba wanaijua.
Acha uongo mkuu na jesi wee inamaana umeenda na jesi za timu mbili mbna ubaanda kuwa muongo muongo acha hzo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Acha uongo mkuu na jesi wee inamaana umeenda na jesi za timu mbili mbna ubaanda kuwa muongo muongo acha hzo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mkuu nidanganye nipate nini?

Wapi nimesema mimi nimevaa jezi ya simba? Siwezi kuvaa na sitavaa.

Nimesema jezi ya simba wanaifahamu.....
 
Habari,
Nchi nyingi zina utaratibu, mila na desturi za maisha. Kutokana na kuzunguka sehemu mbali mbali leo nmeonelea nikuambie yale yahusuyo Senegal ambayo ni tofauti kidogo na nchi yetu ya Tanzania.....

VISA ya Senegal kwa Mtanzania ni on arrival. Ukishaingia Senegal hamna anayekufuatilia ilimradi uwe na passport yako. Visa ikiexpire haubugudhiwi na yeyote. Labda uchokoze mamlaka....
Ila ni vyema kugonga VISA ikiisha.


1. DINI
Upande wa dini waislamu ni asilimia 90 na wakristo ni asilimia 10.
Hii kwa kiasi kikubwa ni nchi iliyojaaliwa kuwa na waislam wengi pamoja na kuwa ilitawaliwa na wafaransa.
Tamaduni za waislam hapa ni tofauti sana na kwetu.
●Wana mji wao mtakatifu unaitwa Touba. Huko asilimia kubwa ya huduma ni bure na ni mji unaojitawala. Huko wanapatikana masheikh wakubwa na watu wanaoitwa Marabuuu... Wanamiliki madrasa ambazo watoto kuanzia wadogo wanalelewa huko.
●Uislam ni mtindo wa maisha kwao ni utamaduni wao. Wanauishi uislamu na uislamu unaishi ndani yao.
●Wanaswali sehemu yoyote muda wa kuswali utakapomkutia. Si barabarani, beach, kituo cha daladala au sehemu yoyote. Usishangae kukuta sehemu wanawake wanajiuza halafu kuna mtu katandika mswala wake anaswali bila bugudha.
●Wanawake waislamu hawavai hijab, nkabu wala chochote wao vazi lolote twende. Ikifika muda wa swala atatoa mtandio wake na kanga atajisitiri anaswali.... Same kwa wanaume. Senegal mpaka wahuni wanaswali....
●Asilimia kubwa hamna ubaguzi wa dini.

2. AMANI
Ni nchi yenye amani kwa kiasi kikubwa na utulivu siasa zao za kistaarabu ingawa kwa sasa Rais aliyepo anamtia kashkashi mpinzani wake Osuman Sonko kashapewa kesi za kutosha.... Siku wakiandamana wapinzani ujue shughuli zinafungwa town....

3. UHALIFU
Kuna asilimia ndogo sana ya uhalifu unaweza kusahau simu yako maeneo kama kariakoo au club au gym na ukaikuta pale pale. Sisemi hakuna wizi ila ni asilimia chache sana.

4. MAKAZI
Mji mkuu Dakar ni mji wa gharama kubwa sana. Bei ya ardhi haikamatiki. Mji umejaa wote na nyumba zinazojengwa ni maghorofa tu. Ukiwa na kiwanja unajenga chote mpaka kwenye mpaka na mwingine anakuja kuunga nyumba yake. Asilimia 95 ya nyumba hazina fense wala parking. Kiwanja kinajaa nyumba.

Kukodi nyumba ni gharama sana kwa Senegal ukifananisha na TZ.

5. VYOMBO VYA USALAMA NA ULINZI.
Askari wapo kwa ajili ya kulinda amani na raia. Hawana shida na yeyote. Ukikosea wanakurekebisha. Usipowagusa hawana habari na yeyote. Unaweza kukaa miezi hata kusimamishwa na traffic usisimamishwe. Unaweza safiri Dar to Mbeya hakuna wa kukusimamisha.
Usishangae kukuta mwanajeshi na raia wote wamevaa gwanda wanapiga story.
Au konda kavaa gwanda za jeshi (si za nchi yao) na hakuna shida.
6. MIUNDOMBINU.
Barabara za mjini zimejengeka vilivyo. Kuanzia flyover, bypass n.k ujenzi unafanyika kila sehemu.

Umeme na maji ni nadra kukatika.

7. MICHEZO
Wananchi wa Senegal wanapenda kufanya mazoezi sana. Usishangae beach zao kujaa watu wanafanya mazoezi. Barabara zimejaa watu wanafanya mazoezi. Wao ni mazoezi na mazoezi na wao.
Tofauti yao ni kwamba hawaendi viwanjani kuangalia michezo. Pamoja na kuwa na viwanja vingi. Wachezaji wengi wanatoka kwny academies... Hata ligi zao si maarufu kwa wasenegal wengi...
Ndio maana timu ya taifa inafanya vyema kuliko klabu....

8. VYAKULA
Bora umnyime chochote msenegal kuliko mkate. Ukienda mgahawani cha kwanza ni mkate kabla ya kula. Mkate ni deal...

Wana vyakula vingi maarufu kama Chepujam n.k.
Hakuna ugali na wanaushangaa

Kitunguu kwao kipo kwenye kila mlo.
Wanapenda kahawa sana na sukari.

9. STAREHE NA POMBE
Hivi vinapatikana sehemu zinazokaliwa na watu wa nje. Sehemu kama almadies, mji wa St. LUOIS.
Sehemu kubwa ya Senegal hawauzi pombe.... Klabu zao zinafunguliwa saa 6-9 jumatatu asubuhi saa 1 unakutana na makundi ya vijana wanatoka klabu.

sigara zake makasha yana picha za kutisha sana .

10. LUGHA
Waliosoma wanajua kifaransa, wananchi wengi wanaongea WOLOF ingawa si wote.
Lugha ya ofisini ni kifaransa...

11. UWEPO WA WATU KUTOKA EAST AFRICA.
Jamii ya watu kutoka East Afrika ni wachache sana. Unaweza kukaa miezi 6 ukakutana na mmoja. Watanzania almost hakuna bora wakenya...

msanii maarufu wa East Afrika ni Diamond Platnum. Na watu wanamjua Shilole na nyimbo yake ya Chura kuliko hata Ali Kiba.

Wanamkubali sana Magufuli.
Zanzibar ni maarufu sana.

Sheikh Sharif anajulikana sana na ni maarufu mno.

Simba inajulikana kuliko Yanga kwanza Yanga hawaijui kabsa... Big up kwa Simba wanawakilisha.
12. UVAAJI WA HIRIZI,SHANGA VIUNONI WAZIWAZI NI KAWAIDA.

Usishangae kukutana na mtu kajitwisha hirizi yake na hana muda na mtu. Hii inanikumbusha yule mchezaji wa Simba Pape N'daw kutoka Senwgal alikutwa na hirizi kwenye moja ya mechi. Kwao ni kawaida kama bangili.
Au mwanamke kavaa shanga zake kiunoni na top na wala hamna muda na watu hawashangai.
Pia ni nadra kuona mwanaume anapishana na mwanamke na kumuangalia.

13. KAZI MWISHO IJUMAA
Ni nadra sana kukuta ofisi imefunguliwa jumamosi yani hata kwa ofisi za madalali weekend wanafunga tofauti na kwenye real state agencies wao weekend ndio biashara inanoga.
14. SHULE
Wanafunzi wa shule nyingi hawavai uniform ni mara chache sana.
Shule hufungwa kipindi cha mvua. Yani kuanzia july mpaka September.
Sijawahi ona watu wanaogopa maji kama wasenegal. Dereva akiona kadimbwi anageuza na hawapiti hapo. Sijui nini kiliwahi wakumba...
N.k n.k n.k

15. USAFIRI WA UMA NA BINAFSI.
USafiri wa uma kwa Senegal yani daladala na Tax ni magari yaliyochoka. Unaweza kushuka airport pale ukakuta Tax zimechoka hatari usifikiri utatafuta na kupata mpya hizo ndio zilizopo, atleast sikuhizi uber yao (YANGO) wanaingiza gari mpya.
Daladala ndio usiseme.
Wanatumia pia farasi kama usafiri anafungwa tela.
Magari binafsi huwezi kuingiza gari kuu kuu mwisho miaka mitano.
Brand za magari ni EUROPEAN. Toyota ni za kutafuta na pia ni ghali kwa kuwa zinatoka Japan Mbali.

Magari yao ni LHD.

AJALI
Senegal hata ukinunua gari leo kesho unaweza kuwa umechubuliwa. Raia hawajali kuhusu magari wao magari kuchubuana ni kawaida na sio kesi. Watu wanaweza gongana magari waaishia kusem INSHALLAH. Hao wanasepa hakuna kesi....

Madereva wa Senegal wanapenda kukimbiza sana magari. Sijui wanawahi wapi speed 120 kwao ni kawaida.

*************************************

Dakar na omba omba ni kama chanda na pete....

Nikiendelea kukumbuka nitaendelea kujazia kadri ya uwezo maana ni muda umepita tangu nipite pale.
Nauli ni kama Bei gan Kwa chopa
 
Vipi kuhusu fursa za kiuchumi zipo,
Yaan Kwa wasomi na sie Watumia nguvu.
Uhakika WA kutusua upoo.
Fursa za kiuchumi zipo nyingi....

1. Kilimo wapo chini sana. Asilimia kubwa ya mazao wana import kutoka nje.
2. Biashara mbali mbali kuanzia vyakula, vifaa vya umeme, vipuri vya magari, hardware....
3. Kazi za wasomi zipo kikwazo ni lugha. Usipojua kifaransa na lugha yao kufanya kazi ni ngumu. Wachache wanaongea kingereza.
4. Nchi hii inajengwa kila sehemu. Vibarua vya kazi ngumu vipo na wenyeji hawapendi. So wengi wanatoka Guinea, Gambia n.k
 
VIP Zanzibar inamaana hao 2 parcent Ni wakristo ndio panya rod

Mbona magerezani na police kote nchini kumejaha waislamu tupu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Sasa kwa akili yako zanzibar kuna panya road??? Na hiyo Tanzania uliyoutolea mfano kwani nchi ya kiislam??
Umekurupuka!!
 
_20230322_053702.JPG

Naona miamvuli ya tigo
 
Back
Top Bottom