Uspika wa Dkt. Tulia Ackson umedhihirisha yeye ni mtu wa namna gani

Uspika wa Dkt. Tulia Ackson umedhihirisha yeye ni mtu wa namna gani

Siku ndugai alipo jiuzulu tu kwa pressure kutoka serikalini nikajuq amna kitu hapa
 
Ukipewa nafasi ya uongozi iwe kwa kuchaguliwa, kuteuliwa au kwa kudra za Mwenyezi Mungu, inatoa nafasi nzuri na halisia ya watu unaowaongoza kukufahamu kiuhalisia wewe ni mtu wa namna gani. Nafasi utakayokuwa nayo inaweza kukuinua au kukuporomosha.

Tukirudi kwa kilichotokea baada ya Spika Ndugai kujiuzulu, na kisha wabunge kumchagua mwenzao mmoja, Dr. Tulia kuwa Spika, matarajio ya wengi ilikuwa pengine mabadiliko haya ya kumleta spika mpya, pamoja na Bunge kujaa wabunge wengi batili kwa mujibu wa katiba na sheria, kulikuwa na matarajio kuwa huenda Dr. Tulia angekuwa bora zaidi kuliko mtangulizi wake, kwa maana binadamu siku zote, kwenye mabadiliko, hutarajia kupata kilicho bora zaidi.

Bahati mbaya, nchi ilikuwa kwenye ubaya, kisha ikaenda kwenye ubaya zaidi.

Dr. Tulia, akiwa spika akatangaza wazi kuwa Bunge linapofanya kazi ni lazima lifuate matakwa ya Serikali. Na akatamka wazi kuwa Rais na Serikali ndiyo maboss wa Bunge.

Kama vile ilikuwa imepangwa, naye Jaji mkuu akawaambia majaji kuwa wakati wote wanapotoa hukumu wazingatie matakwa ya Serikali. Kauli hizi za wakubwa wa mihimili miwili, zikaufanya mhimili wa mahakama na mhimili wa Bunge kuwa idara za Serikali.

Kilichofuatia wote tumeshuhudia kazi ya Bunge na kazi ya kila mbunge akiwa bungeni ikawa ni kumsifu tu Rais na Serikali. Serikali na Rais iwe wametenda mema au mambo ya hovyo, Bunge chini ya Dr. Tulia kazi yake kubwa ikawa ni kusifu na kupitisha kila kitu kinacholetwa na Serikali Bungeni; na Dr. Tulia akizuia hoja zinazoonekana zinahoji utendaji wa Serikali. Wananchi wanakumbuka jinsi Spika Tulia, hivi karibuni, wakati watu wakitekwa na kupotezwa, alivyozuia Bunge lisijadili jambo hilo.

Na hiyo ilifuatia baada ya Rais Samia kudai kuwa utekaji haupo, na wanaotekwa ni drama. Hivyo Dr. Tulia kama mtu ambaye kazi yake ni kulifanya Bunge kuwa kama idara tu Serikali, alichokifanya ni kuisistiza kauli ya mkuu wake, hivyo naye akarudia maneno ya mkuu wake kwa lugha tofauti kuwa, kusiwe na hisia kuwa kila anayepotea ametekwa na Serikali. Baada ya kauli hiyo akazuia mjadala juu ya Watanzania wanaoikosoa serikali kutekwa na kupotezwa.

Lakini hayo yalifuatia tukio baya kabisa kwenye historia ya nchi yetu ambapo, Bunge chini ya Tulia, lilipitisha mkataba wa hovyo kabisa wa IGA unaopora sovereignity ya nchi. Mkataba ambao hata mtu asiyejua sheria, aliona wazi kabisa ni mkataba mbaya.

Mkataba huo ambao taasisi mbalimbali independent kuanzia TLS, watu binafsi wataalam waliobobea katika masuala ya kisheria na mikataba, taasisi za dini, baadhi ya viongozi wa kitaifa wastaafu, wote walitamka kwa uwazi kuwa IGA ile ilikuwa ya hovyo kabisa. Lakini Tulia, bila ya kujali maoni ya na hisia za wananchi, alihakikisha mkataba huo unapita, na mpaka sasa ni janga ambalo Taifa linaisha nalo, kwa sababu IGA hiyo haijabadilishwa hata nukta moja.

Walichofanya ni kwenda kutengeneza HIGA ambayo inaweza kumpumbaza mtu kuona mambo ni mazuri, wakati IGA imesimama vile vile, na wakati wowote DPW inaweza kuitumia. Kufuatia IGA hiyo, kuna kila dalili, huko mbeleni, Tanzania ikapatwa na yale yaliyoipata nchi ya Djibout, ambayo viongozi wake baada ya kupewa rushwa, nchi ikaingia kwenye mkataba wa kishenzi na DPW, baadaye wazalendo wakachachamaa, wakaamua kuvunja mkataba, DPW wakaenda mahakama za UK, kulingana na mkataba waliousaini, Djibout ikahukumiwa kuilipa DPW zaidi ya dola za Marekani milioni 700.

Hata sisi kwa ubaya wa IGA iliyopo, kuna siku tutafika huko. Na hilo likitokea, mmoja wa wahusika muhimu watakaokuwa wameliletea hasara hiyo Taifa, ni Spika wa Bunge Dr. Tulia.

Matukio haya mabaya, ambayo yamelifanya Bunge kuwa chawa wa Rais na Serikali, yametupatia nafsi ya kufahamu kwa ukaribu na usahihi kuwa tuna Spika wa Bunge wa namna gani.

Na kwa haya aliyoyafanya Spika kwa Taifa hili, kuna haja kweli kuendelea na mtu huyu kwenye nafasi hiyo? Au kwa vile anaoenda sana kazi ya upambe, ingefaa akawa huku ikulu ambako kazi yake kubwa ingekuwa ni kumteyea Rais na Serikali?

Pia soma: Tulia Ackson awataka viongozi wa magharibi kumheshimu. Ni baada ya kushambuliwa kuhusu kukutana na Vladmir Putin
Bandiko refu mno, ulipaswa kuandika hata kwa aya moja tu na ukaeleweka.
 
Kuna kitu watu nadhani wanakichanganya sana. Kufanya Tafsiri ya Kingereza ya neno Governement kuwa ni Serikali

Governement ipo na Pillars tatu:
1. Executive = Kwetu tunaita Serikari
2. Legislature = Bunge
3. Judiciary = Mahakama

Mkuu wa Gorvernment ni Rais wa Jamhuri ya muungana

Huu hapa mchoro unaonesha Three Pillars of the Givernement

View attachment 3131274
Pascal Mayalla Ukiusoma mchoro huu na kuuelewa hautakuwa na shida sana. Mkuu wa nchi yeye ndiye kiongozi wa Serikali. Lakini Bunge na Mahakama zipo chini yake. Bams
hiki ulichoandika umetoa kwenye reference gani. Mbona unapotosha
 
Ukipewa nafasi ya uongozi iwe kwa kuchaguliwa, kuteuliwa au kwa kudra za Mwenyezi Mungu, inatoa nafasi nzuri na halisia ya watu unaowaongoza kukufahamu kiuhalisia wewe ni mtu wa namna gani. Nafasi utakayokuwa nayo inaweza kukuinua au kukuporomosha.

Tukirudi kwa kilichotokea baada ya Spika Ndugai kujiuzulu, na kisha wabunge kumchagua mwenzao mmoja, Dr. Tulia kuwa Spika, matarajio ya wengi ilikuwa pengine mabadiliko haya ya kumleta spika mpya, pamoja na Bunge kujaa wabunge wengi batili kwa mujibu wa katiba na sheria, kulikuwa na matarajio kuwa huenda Dr. Tulia angekuwa bora zaidi kuliko mtangulizi wake, kwa maana binadamu siku zote, kwenye mabadiliko, hutarajia kupata kilicho bora zaidi.

Bahati mbaya, nchi ilikuwa kwenye ubaya, kisha ikaenda kwenye ubaya zaidi.

Dr. Tulia, akiwa spika akatangaza wazi kuwa Bunge linapofanya kazi ni lazima lifuate matakwa ya Serikali. Na akatamka wazi kuwa Rais na Serikali ndiyo maboss wa Bunge.

Kama vile ilikuwa imepangwa, naye Jaji mkuu akawaambia majaji kuwa wakati wote wanapotoa hukumu wazingatie matakwa ya Serikali. Kauli hizi za wakubwa wa mihimili miwili, zikaufanya mhimili wa mahakama na mhimili wa Bunge kuwa idara za Serikali.

Kilichofuatia wote tumeshuhudia kazi ya Bunge na kazi ya kila mbunge akiwa bungeni ikawa ni kumsifu tu Rais na Serikali. Serikali na Rais iwe wametenda mema au mambo ya hovyo, Bunge chini ya Dr. Tulia kazi yake kubwa ikawa ni kusifu na kupitisha kila kitu kinacholetwa na Serikali Bungeni; na Dr. Tulia akizuia hoja zinazoonekana zinahoji utendaji wa Serikali. Wananchi wanakumbuka jinsi Spika Tulia, hivi karibuni, wakati watu wakitekwa na kupotezwa, alivyozuia Bunge lisijadili jambo hilo.

Na hiyo ilifuatia baada ya Rais Samia kudai kuwa utekaji haupo, na wanaotekwa ni drama. Hivyo Dr. Tulia kama mtu ambaye kazi yake ni kulifanya Bunge kuwa kama idara tu Serikali, alichokifanya ni kuisistiza kauli ya mkuu wake, hivyo naye akarudia maneno ya mkuu wake kwa lugha tofauti kuwa, kusiwe na hisia kuwa kila anayepotea ametekwa na Serikali. Baada ya kauli hiyo akazuia mjadala juu ya Watanzania wanaoikosoa serikali kutekwa na kupotezwa.

Lakini hayo yalifuatia tukio baya kabisa kwenye historia ya nchi yetu ambapo, Bunge chini ya Tulia, lilipitisha mkataba wa hovyo kabisa wa IGA unaopora sovereignity ya nchi. Mkataba ambao hata mtu asiyejua sheria, aliona wazi kabisa ni mkataba mbaya.

Mkataba huo ambao taasisi mbalimbali independent kuanzia TLS, watu binafsi wataalam waliobobea katika masuala ya kisheria na mikataba, taasisi za dini, baadhi ya viongozi wa kitaifa wastaafu, wote walitamka kwa uwazi kuwa IGA ile ilikuwa ya hovyo kabisa. Lakini Tulia, bila ya kujali maoni ya na hisia za wananchi, alihakikisha mkataba huo unapita, na mpaka sasa ni janga ambalo Taifa linaisha nalo, kwa sababu IGA hiyo haijabadilishwa hata nukta moja.

Walichofanya ni kwenda kutengeneza HIGA ambayo inaweza kumpumbaza mtu kuona mambo ni mazuri, wakati IGA imesimama vile vile, na wakati wowote DPW inaweza kuitumia. Kufuatia IGA hiyo, kuna kila dalili, huko mbeleni, Tanzania ikapatwa na yale yaliyoipata nchi ya Djibout, ambayo viongozi wake baada ya kupewa rushwa, nchi ikaingia kwenye mkataba wa kishenzi na DPW, baadaye wazalendo wakachachamaa, wakaamua kuvunja mkataba, DPW wakaenda mahakama za UK, kulingana na mkataba waliousaini, Djibout ikahukumiwa kuilipa DPW zaidi ya dola za Marekani milioni 700.

Hata sisi kwa ubaya wa IGA iliyopo, kuna siku tutafika huko. Na hilo likitokea, mmoja wa wahusika muhimu watakaokuwa wameliletea hasara hiyo Taifa, ni Spika wa Bunge Dr. Tulia.

Matukio haya mabaya, ambayo yamelifanya Bunge kuwa chawa wa Rais na Serikali, yametupatia nafsi ya kufahamu kwa ukaribu na usahihi kuwa tuna Spika wa Bunge wa namna gani.

Na kwa haya aliyoyafanya Spika kwa Taifa hili, kuna haja kweli kuendelea na mtu huyu kwenye nafasi hiyo? Au kwa vile anaoenda sana kazi ya upambe, ingefaa akawa huku ikulu ambako kazi yake kubwa ingekuwa ni kumteyea Rais na Serikali?

Pia soma: Tulia Ackson awataka viongozi wa magharibi kumheshimu. Ni baada ya kushambuliwa kuhusu kukutana na Vladmir Putin
Uzi umesheheni kila kitu, siongezi neno
 
naunga mkono hoja Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

Huu ni ukweli mchungu and this is not right, asante sana kulisemea hili, hili nami pia sio tuu nimelisemea, bali nimeliandikia Je, wajua kuwa Rais wa JMT ndie Serikali, Bunge na Mahakama? Yuko juu ya Mihimili yote 3. Je, kuna uwezekano Rais wa JMT pia yuko juu Katiba?

Hili la IGA, hatukunyamaza ,tumesema sana
Kilichotokea behind the closed doors, waligundua ile IGA
ni batili hivyo they abandoned it kimya kimya bila kutangaza,ile HGA ni safi nzuri na legit ila ni siri。Walitekeleza ushauri huu Wajua kuna ndoa halali, batili na batilifu? Ndoa ya TPA na DPW, ni Ubakaji? Wajua ubakaji unaweza kuwa alali? IGA batili yaweza kuzaa HGA halali?
Na hii sio mara ya kwanza Bunge letu kupitisha madudu ya ajabu wakiisha shtuliwa ni madudu, wanayasokomeza uvunguni kimya kimya
na kuyafuta kwenye hansard as if nothing happened !
baada ya kuwastua hapo waliufyata,azimio lao batili wakalisokomeza uvunguni kimya kimya wakaipokea ripoti ya CAG。
asante kwa hoja mujarab
P
Pascal, una uhakika ile IGA ya hovyo ilikuwa abandoned? Ina maana hakuna IGA kabisa au ilirekebishwa?
 
naunga mkono hoja Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!

Huu ni ukweli mchungu and this is not right, asante sana kulisemea hili, hili nami pia sio tuu nimelisemea, bali nimeliandikia Je, wajua kuwa Rais wa JMT ndie Serikali, Bunge na Mahakama? Yuko juu ya Mihimili yote 3. Je, kuna uwezekano Rais wa JMT pia yuko juu Katiba?

Hili la IGA, hatukunyamaza ,tumesema sana
Kilichotokea behind the closed doors, waligundua ile IGA
ni batili hivyo they abandoned it kimya kimya bila kutangaza,ile HGA ni safi nzuri na legit ila ni siri。Walitekeleza ushauri huu Wajua kuna ndoa halali, batili na batilifu? Ndoa ya TPA na DPW, ni Ubakaji? Wajua ubakaji unaweza kuwa alali? IGA batili yaweza kuzaa HGA halali?
Na hii sio mara ya kwanza Bunge letu kupitisha madudu ya ajabu wakiisha shtuliwa ni madudu, wanayasokomeza uvunguni kimya kimya
na kuyafuta kwenye hansard as if nothing happened !
baada ya kuwastua hapo waliufyata,azimio lao batili wakalisokomeza uvunguni kimya kimya wakaipokea ripoti ya CAG。
asante kwa hoja mujarab
P
Kaka Paschal IGA ni mkataba wa awali wa biashara ya pande mbili,, Tanzania na Dubai, mle ni kama skeleton tu hakuwekwi vipengele vizito vya kibiashara.

Mikataba iliyokuja kusainiwa mbele ya Rais SSH ndio yenye habari pana ya kibiashara, IGA hata hao waarabu walipogundua kuwa imevuja hawakujihangaisha kwa sababu mle hakuwekwi vifungu vizito vya kibiashara.

Sio kwamba IGA ilibadilishwa kwa sababu ya kelele zetu, hapana. Ni utaratibu wenyewe wa kimikataba ilibidi ufuate mkondo wake.
 
Pascal, una uhakika ile IGA ya hovyo ilikuwa abandoned? Ina maana hakuna IGA kabisa au ilirekebishwa?
IGA ni skeleton tu, mle hakuna financials zinazoandikwa. Ndio maana waarabu hawakuhangaika walipojua imevuja kwa umma.

Mkataba mkubwa ni ule uliosainiwa mbele ya Rais na kiongozi wa DPW, mle ndio kunawekwa siri za kibiashara.
 
Back
Top Bottom