Ustaadh akamatwa!!!

Ustaadh akamatwa!!!

Status
Not open for further replies.

MaxShimba

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2008
Posts
35,771
Reaction score
4,065

Imeripotiwa na gazeti la Mwananchi:

Date::12/29/2008
Ustaadh akamatwa akidaiwa kujaribu kubaka mwanafunzi
Na Samuel Msuya,Morogoro

JESHI la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia ustaadh wa madrasa, Dadi Ramadhani, 35, ambaye ni mkazi wa Mafiga mkoani hapa kwa tuhuma za kujaribu kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita wa Shule ya Msingi Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Thobias Andingenye alisema mwalimu huyo wa dini alikamatwa Desemba 24 majira ya saa 6:00 mchana kwenye nyumba ya kulala wageni ya Bembea iliyo maeneo ya Kiwanja cha Ndege mkoani hapa.

Kamanda Andingenye alisema awali wazazi wa binti huyo mara baada ya mtoto wao kurudi likizo walimuomba ustaadh huyo amsaidie masuala ya kidini katika madrasa yake na ndipo ustaadh huyo alipoanza kushikwa na tamaa na kuanza kumlaghai ili afanye mapenzi na mwanafunzi huyo.

Akisimulia tukio hilo, Andingenye alisema kutokana na mtoto huyo kuchoshwa na kusumbuliwa na ustaadh huyo aliamua kumshtaki kwa wazazi wake, ambao kwanza walimuonya, lakini mwalimu huyo wa dini alikana kufanya kitendo hicho.

Alisema pamoja na ustaadh huyo kuonywa na wazazi, aliendelea na ushawishi wake na safari hii akaamua kutumia mbinu ya kumnunulia binti huyo nguo kwa ajili ya sikukuu ya Krismasi.

Kamanda Andingenye alisema baadaye wazazi wa binti huyo waliamua kuweka mtego kwa kushirikiana na binti yao na ndipo walipomnasa Desemba 24 kwenye chumba namba 10 cha nyumba ya wageni ya Bembea akifanya jaribio la kumbaka.

Alisema kabla ya kumfikisha binti huyo katika nyumba ya wageni, ustaadh huyo alimpeleka kwenye duka la nguo na kumchagulia nguo za sikukuu na kisha kuziacha dukani huku akiahidi kuzifuata baadaye.

Kamanda Andingenye alisema mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baaada ya uchunguzi wa tuhuma hizo kukamilika.

Katika tukio jingine jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia wanafunzi wawili wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kiislam, Sadi Ayubu, 23, na Joseph Mwinjake, 27, kwa kuwashambulia na kuwajeruhi Abdul Mhanga, 22, na Mussa Rajabu wakiwatuhumu kuwa ni vibaka.

Kamanda Andingenye alisema tukio hilo lilitokea Desemba 26 saa 4:00 usiku katika maeneo ya karibu na chuo hicho.

Tuma maoni kwa Mhariri

 
Kuna watakaoanza kupinga,ngoja mtawaona
 

Jamaa wa hii dini, kaaazi kweli kweli. Mawazo yao ni ..!@#$%^&*?.

Jamaa badala ya kufundisha Mwamadi, anafundisha uroda.
 
Hapo suala sio dini yake ni yeye mwenyewe kaamua kufanya hivyo kutenda kitendo hicho na unaweza kukuta huyo ni ustadh jina kama watu wanavyotaniana mitaani
 
Hapo suala sio dini yake ni yeye mwenyewe kaamua kufanya hivyo kutenda kitendo hicho na unaweza kukuta huyo ni ustadh jina kama watu wanavyotaniana mitaani


Hivi wewe umeisoma hii habari au unataka kubisha kama utamaduni wenu. Mwandishi kasema jamaa ni USTAADH WA MADRASA. Wewe unapinga kama nani?

Hapa dini inahusika. Yoyo kweli umesema jamaa wataanza kupinga. Wakwanza huyoooo SHY.

Haya tusubiri mwingine.
 
Basi ipelekwe sehemu ya malalamiko haifai kuwa hapa sipingi kwa sababu ya dini wala nini huyo amefanya hivyo kama yeye sio kama mwanachama wa dini fulani tunaelewana ?
 
Basi ipelekwe sehemu ya malalamiko haifai kuwa hapa sipingi kwa sababu ya dini wala nini huyo amefanya hivyo kama yeye sio kama mwanachama wa dini fulani tunaelewana ?


Hii thread ni habari.

Acha kuchemsha. Waache watu wajuwe ukweli wa WASTAADH na tabia yao chafu waliyo ificha kwa miaka mingi.

Majuzi juzi tulisoma kuhusu Shehe. Kivipi dini ya Uislam isihusike? Hii nitabia ndani ya dini ya uislam.
 

Hii thread ni habari.
Acha kuchemsha. Waache watu wajuwe ukweli wa WASTAADH na tabia yao chafu waliyo ificha kwa miaka mingi.
Majuzi juzi tulisoma kuhusu Shehe. Kivipi dini ya Uislam isihusike? Hii nitabia ndani ya dini ya uislam.

"Tabia za watu binafsi sio sahihi kuzioanisha moja kwa moja na Imani zao, ukisema ustaadh kataka kubaka kwa sababu ni Muislamu utasema pia mapadri wanaodaiwa kulawiti wanafanya hivyo kwa sababu ni Wakristo? Maovu yapo kwa imani zote"
 
Zile ndoa maarufu kwa jina la "ndoa za mkeka"vipi hapa tena! Mimi sijiui vizuri, ila nasikia ukibambwa unakabidhiwa demu moja kwa moja. Ustaadh si alikuwa anananihii.. kule gesti. Hajakabidhiwa mke wake aondoke naye! Wote ni waislamu, si angekabidhiwa mke, au? Na mahakama ya kadhi ikiundwa kwa gharama ya kodi zetu itakuwa inashughulikia mambo haya, au?
 

Jamaa wa hii dini, kaaazi kweli kweli. Mawazo yao ni ..!@#$%^&*?.

Jamaa badala ya kufundisha Mwamadi, anafundisha uroda
Hapa sio dini bali ni tabia ya mtu kama dini basi zile dini zinazofungisha ndoa mashoga ni zaidi.au zile dini ambazo viongozi wake huwa dhalilisha watoto kwa kuwanajisi basi zaid.hapa ni mtu mmoja lakini marekani mapadre wangapi.inaelekea katika JF wanaochemsha ni wengi kuliko nilivyodhani
 
Zile ndoa maarufu kwa jina la "ndoa za mkeka"vipi hapa tena! Mimi sijiui vizuri, ila nasikia ukibambwa unakabidhiwa demu moja kwa moja. Ustaadh si alikuwa anananihii.. kule gesti. Hajakabidhiwa mke wake aondoke naye! Wote ni waislamu, si angekabidhiwa mke, au? Na mahakama ya kadhi ikiundwa kwa gharama ya kodi zetu itakuwa inashughulikia mambo haya, au?


Mkuu umenena. Inaonekana Shehe alikuwa mbali au na yeye alisha kaonja.
 
Zile ndoa maarufu kwa jina la "ndoa za mkeka"vipi hapa tena! Mimi sijiui vizuri, ila nasikia ukibambwa unakabidhiwa demu moja kwa moja. Ustaadh si alikuwa anananihii.. kule gesti. Hajakabidhiwa mke wake aondoke naye! Wote ni waislamu, si angekabidhiwa mke, au? Na mahakama ya kadhi ikiundwa kwa gharama ya kodi zetu itakuwa inashughulikia mambo haya, au?
Nadhani hapa mnakosea kuhukumu ya kwamba dini ya kiislamu inahusika na kama Mkuu share ulivyosema "ndoa za mkeka" hii ndoa kwenye uislamu haipo na ni uzushi.Hivyo cha muhimu tuangalie kulirekebisha matatizo yanayoikabili jamii yetu na si kushutumu imani za watu.
 
Kazi ipo hapo naona kama kuna kiji tabia fulani ambacho sitaki kuamini kuwa wanacho wote hao maana mmm balaa mara misikitikini tumesikia mara madrasa...wote ma ustaadhi mmm acha sheria................
 
Zile ndoa maarufu kwa jina la "ndoa za mkeka"vipi hapa tena! Mimi sijiui vizuri, ila nasikia ukibambwa unakabidhiwa demu moja kwa moja. Ustaadh si alikuwa anananihii.. kule gesti. Hajakabidhiwa mke wake aondoke naye! Wote ni waislamu, si angekabidhiwa mke, au? Na mahakama ya kadhi ikiundwa kwa gharama ya kodi zetu itakuwa inashughulikia mambo haya, au?
...Soma katikati ya mistari, mwanafunzi wa darasa la sita afungishwe ndoa ya mkeka, angekuwa nduguyo au mwanao ungeruhusu aolewe??? Ni usingizi au mning'inio???!!!
 
kuna watu mawazo yao ni katika kuupaka matope Uislam, yaani akiona jambo limemhusu mtu mmoja ambaye ni Muislam basi yeye kapatia mahala pa kuukashifu na kuufanya uonekane kama ni Uislam ndio unaofundisha hayo. Mmomonyoka wa kimaadili upo kwa jamii nzima hapo imani hazihusiki kwani si kwa waislam na viongozi wao wala wakristo na viongozi wao na hata mabudha na viongozi wao achilia mbali wapagani na viongozi wao hakuna ambaye anaweza kusema kwa kinywa kipana kwamba wao wana nafuu ya mmomonyoko huu. sasa muhimu tujitizame kama jamii na kutafuta namna ya kuweza kurejesha maadili ndani ya jamii. na sio kukaa kutoa shutuma kana kwamba atoaye shutuma hizo yeye kaepukika na hili la kuvunjika kwa maadili.
 
Mara nyingi MaxShimba baada ya kuona akishindwa hoja na waislam kwanye jukwaa la dini hukimbilia kukashifu/kutukana waislam na Mtume, akijua wazi kuwa waislam tunawatukuza Mitume(A.S) wote wa Allah akiwemo Issa(A.S) ama Yesu kama ilivyo maarufu. na huwezi kusikia Muislam akitoa kauli isiyofaa kwa mtume wa haki yeyote yule. sasa yeye hujuona mshindi pale anapokashifu bila kupata kurejeshewa kashfa hiyo kwa mtume wake. Waislam tunaamini kwamba Yesu ama Issa(A.S) amekuja na Injili na ametimiliza kazi yake na baada ya kuondoka kwake kumetokea mafundisha ambayo ni ya nyonyeza na mengine ni tofauti kabisa na alichokifunza, hivyo ni wajibu wetu kuuelezea umma bila kashfa tena kwa hikma hayo yaliyotokea, hili haliwapendezi akina Maxshimba matokeo yake hutumia nafasi waipatayo kukashifu ama muchafua taswira ya Uislam.
Kwa kujua kwamba jukwa la dini watu wengi hawalitizami hivyo wamekuwa wakianzisha threads za kidini kwa njia nyingine ama ya Habari, Ucheshi ama vyovyote atakavyoona itatoa nafasi kwa yeye kutimiza nia yake ya kuuchafua Uislam.
 

Jamaa wa hii dini, kaaazi kweli kweli. Mawazo yao ni ..!@#$%^&*?.

Jamaa badala ya kufundisha Mwamadi, anafundisha uroda.

Your generalisation is clearly flawed! Kazi ipo!
 
Ama kweli nyani haoni kundule .. na Kimario alolawiti mtoto/kondoo alokabidhiwa kama mchungaji .. huyu atakuwa anarepresent kabila fulani .. ukooo au nasi tujitie wazimu tuseme wakristo bila kuchuja kwamba ni roman catholic, protestant, seventh day etc etc .. not fair

Hawa wanaojifanya watetezi sana wa nabii Issa (A.S) ... na kati ya msingi wa imani yao ni kwamba atarudi awamu ya pili kuja kuwachukua ... Wallahi nasema hivi .. watu kama nyinyi atawaacha maana mna tabia za uovu .. yeye hakutukana nyinyi mnatukana tena kwa kujifanya mnajua .. yeye hakuhumu watu .. nyinyi mnahukumu .. hamuoni kwamba tayari mnajizidishia madhambi tena kwa kulivaa joho lake .. nawapa pole na nawahurumia tena sana!!!!

KUWENI KAMA NABI ISSA (A.S) Mnyenyekevu, mtiifu, mwenye huruma .. hakika sifa zake ni nyingi .. Mwenyezi Mungu atujaalie kati ya sifa za nabii wake Issa (A.S)
 


Alisema pamoja na ustaadh huyo kuonywa na wazazi, aliendelea na ushawishi wake na safari hii akaamua kutumia mbinu ya kumnunulia binti huyo nguo kwa ajili ya sikukuu ya Krismasi.


Mukulu Max,

Maustadh wetu hapa JF na pro wao ktk kipindi hiki cha festive wametupigia makelele sana hapa JF kuwa X-mass ni sikukuu ya kipagani na makelele mengine kama hayo. Lakini kama wahenga wanavyosema ..Mungu hamfichi mnafiki, kumbe wakitoka hapa kujificha nyuma ya PC, wanaenda kimya kimya 'kusherehekea'..

Sasa hebu one huyu ustaadh alivyoumbuka..LOL..Bua ha ha ha..Tukianza kuwafuatilia hawa maustadh wetu hapa wasema chochote JF tutabaini mambo ni hayahaya!!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kujua kwamba jukwa la dini watu wengi hawalitizami hivyo wamekuwa wakianzisha threads za kidini kwa njia nyingine ama ya Habari, Ucheshi ama vyovyote atakavyoona itatoa nafasi kwa yeye kutimiza nia yake ya kuuchafua Uislam.

Nadhani ktk hii orodha ya kufungua thread za namna hii umesahau kwa kusudi kumuweka ndugu yako X-Matembele. Hii ni ktk kudhihirisha jinsi gani wewe ni mnafiki na mwongo..

Usidhani kuwa hatuna macho ya kuona na akili zinazofanya kazi 24/7.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom