Ustawi Wa Jamii vs Mahakama

Ustawi Wa Jamii vs Mahakama

Yohana Kilimba

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
8,105
Reaction score
5,629
Kati ya taasisi hizo mbili hapo juu,nani ana mamlaka ya kuamuru mdai na mdaiwa wakapime DNA?

Kuna mwanamke ana claim mimi ni baba wa mtoto wake na ameshapeleka shauri Ustawi wa Jamii,na wamenipa muda wa kujifikiria,

Nataka tukapime DNA ila ofisa wa Ustawi amekula mlungula ili atu force tukapime BLOOD GROUPS,

Naomba msaada
 
Kati ya taasisi hizo mbili hapo juu,nani ana mamlaka ya kuamuru mdai na mdaiwa wakapime DNA?


Kuna mwanamke ana claim mimi ni baba wa mtoto wake na ameshapeleka shauri Ustawi wa Jamii,na wamenipa muda wa kujifikiria,

Nataka tukapime DNA ila ofisa wa Ustawi amekula mlungula ili atu force tukapime BLOOD GROUPS,

Naomba msaada

Hiyo afisa ni mbumbumbu, Blood group haina chochote cha kukuthibitishia huyo ni mtoto wako. wewe unaweza kuwa na O na mtoto wako anaweza kuwa na group nyingine. Sisitiza DNA akikataa nenda kwa wanasheria na umweleze wazi kuwa unamshtaki kwa kung'ang'ania jambo lisilo na jibu sahihi
 
Kati ya taasisi hizo mbili hapo juu,nani ana mamlaka ya kuamuru mdai na mdaiwa wakapime DNA?


Kuna mwanamke ana claim mimi ni baba wa mtoto wake na ameshapeleka shauri Ustawi wa Jamii,na wamenipa muda wa kujifikiria,

Nataka tukapime DNA ila ofisa wa Ustawi amekula mlungula ili atu force tukapime BLOOD GROUPS,

Naomba msaada

Kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Kifungu cha 36(1) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1) iwapo ushahidi wa mama au ushahidi huru hautapewa nguvu na ushahidi mwingine kwa kiasi cha kuifanya mahakama ijiridhishe, mahakama yaweza kwa maombi au bila maombi, kuamuru kipimo cha Vinasaba vya Binadamu kifanywe kwa lengo la kumthibitisha Baba mzazi wa mtoto.

Angalizo;
Katika Sheria hii inazumgumzia hatua endapo Kesi iko Mahakamani, sina uhakika kama kuna Sheria ambayo inampa Afisa Ustawi mamlaka au uwezo wa Amri/Agizo la kupima vinasaba, labda kama akiutoa kama ushauri tu.
 
Kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Kifungu cha 36(1) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1) iwapo ushahidi wa mama au ushahidi huru hautapewa nguvu na ushahidi mwingine kwa kiasi cha kuifanya mahakama ijiridhishe, mahakama yaweza kwa maombi au bila maombi, kuamuru kipimo cha Vinasaba vya Binadamu kifanywe kwa lengo la kumthibitisha Baba mzazi wa mtoto.

Angalizo;
Katika Sheria hii inazumgumzia hatua endapo Kesi iko Mahakamani, sina uhakika kama kuna Sheria ambayo inampa Afisa Ustawi mamlaka au uwezo wa Amri/Agizo la kupima vinasaba, labda kama akiutoa kama ushauri tu.

asante,samahani kuna kipengele cha ktk sheria ya vinasaba ya 2009,ukurasa wa 16 sijaielewa kdogo(am nt a lawyer) sijakielewa...naomba ufafanuzi

Kwa io hata ku ienforce upimaji wa vinasaba ofisa anaweza kuamulu?
 
Hiyo afisa ni mbumbumbu, Blood group haina chochote cha kukuthibitishia huyo ni mtoto wako. wewe unaweza kuwa na O na mtoto wako anaweza kuwa na group nyingine. Sisitiza DNA akikataa nenda kwa wanasheria na umweleze wazi kuwa unamshtaki kwa kung'ang'ania jambo lisilo na jibu sahihi

asante,kulingana na sheria ya vinasaba ya 2009,nani anaweza enforce upimaji wa DNA?
 
Kati ya taasisi hizo mbili hapo juu,nani ana mamlaka ya kuamuru mdai na mdaiwa wakapime DNA?

Kuna mwanamke ana claim mimi ni baba wa mtoto wake na ameshapeleka shauri Ustawi wa Jamii,na wamenipa muda wa kujifikiria,

Nataka tukapime DNA ila ofisa wa Ustawi amekula mlungula ili atu force tukapime BLOOD GROUPS,

Naomba msaada

Huwa nawaza na kukosa jibu ni kwanini watu tuliopo duniani tupo jinsi tulivyo! Kweli huwa sipati jibu
Najaribu kutafakari na kujiuliza ni nini kinatokokea mpenzi uliyekuwa unampigia simu kwa bashasha na maneno matamu kama asali ya nyuki wadogo (wale wasiouma) leo hii mnaishia kulumbana na kutokuelewana?
Mpenzi uliekuwa unamvua nguo hata wakati mwingine bila ridhaa yake anakubali ili tu amridhishe mpenzi wake!! Kweli dunia haina huruma!! Leo hii ni mpaka Mahakamani na DNA Test?

Nikiwa kama kaka yako na ninaekutakia maisha mema huko mbeleni, kama utapenda naomba nikushauri!
Maisha sio yale tunayo yaona kwa macho au kuyagusa kwa mikono yetu, yale tuyaonayo ni asilimia ndogo sana hata 10% ya maisha halisi haifiki.

Najua kabisa utakuwa unaye mpenzi mwingine! ambaye kwa sasa amechukua nafasi kubwa katika mawazo yako! na ndio maana huyo wa zamani "Unaemuita mwanamke" unaona si lolote, lakini naomba utambue kuwa yeye ni kiumbe hai na anayo nafsi kama wewe na kuwaza na kuumia, kama wewe unavyoumia alivyokwambia ana mtoto wako!!
Najaribu kujiuliza ni mara ngapi umemvua nguo? ni mara ngapi amefanya mema sana kwako? Tafakari

Omba hekima ya mwenyezi Mungu ikutawale, na kaa na huyo mwanamke uongee nae kwa urafiki kabisa huwezi kuamini atakwambia ukweli wote kama mtoto ni wako au la,(Wanawake ni warahisi sana kujieleza ukijua wapi pa kushika) Naomba ukipenda unijibu (Je ulikuwa na mpando wa kumuoa? kama ni hapana je yeye alikuwa anajua hilo kabla hajaingia kwenye mahusiano na wewe? ningependa unijibu hapa JF kwa manufaa ya wote au unipm kama hutataka nikujibu hapa upenuni!

Naamini kabisa DNA hata ikisema huyo mtoto ni wako kwa sababu dhamira yako ni kuyakwepa majukumu hutakubaliana na matokeo yake. utaishia kusema mashine yenyewe feki!

bado natafakari kwa nini dunia haina huruma!!
 
Huwa nawaza na kukosa jibu ni kwanini watu tuliopo duniani tupo jinsi tulivyo! Kweli huwa sipati jibu
Najaribu kutafakari na kujiuliza ni nini kinatokokea mpenzi uliyekuwa unampigia simu kwa bashasha na maneno matamu kama asali ya nyuki wadogo (wale wasiouma) leo hii mnaishia kulumbana na kutokuelewana?
Mpenzi uliekuwa unamvua nguo hata wakati mwingine bila ridhaa yake anakubali ili tu amridhishe mpenzi wake!! Kweli dunia haina huruma!! Leo hii ni mpaka Mahakamani na DNA Test?

Nikiwa kama kaka yako na ninaekutakia maisha mema huko mbeleni, kama utapenda naomba nikushauri!
Maisha sio yale tunayo yaona kwa macho au kuyagusa kwa mikono yetu, yale tuyaonayo ni asilimia ndogo sana hata 10% ya maisha halisi haifiki.

Najua kabisa utakuwa unaye mpenzi mwingine! ambaye kwa sasa amechukua nafasi kubwa katika mawazo yako! na ndio maana huyo wa zamani "Unaemuita mwanamke" unaona si lolote, lakini naomba utambue kuwa yeye ni kiumbe hai na anayo nafsi kama wewe na kuwaza na kuumia, kama wewe unavyoumia alivyokwambia ana mtoto wako!!
Najaribu kujiuliza ni mara ngapi umemvua nguo? ni mara ngapi amefanya mema sana kwako? Tafakari

Omba hekima ya mwenyezi Mungu ikutawale, na kaa na huyo mwanamke uongee nae kwa urafiki kabisa huwezi kuamini atakwambia ukweli wote kama mtoto ni wako au la,(Wanawake ni warahisi sana kujieleza ukijua wapi pa kushika) Naomba ukipenda unijibu (Je ulikuwa na mpando wa kumuoa? kama ni hapana je yeye alikuwa anajua hilo kabla hajaingia kwenye mahusiano na wewe? ningependa unijibu hapa JF kwa manufaa ya wote au unipm kama hutataka nikujibu hapa upenuni!

Naamini kabisa DNA hata ikisema huyo mtoto ni wako kwa sababu dhamira yako ni kuyakwepa majukumu hutakubaliana na matokeo yake. utaishia kusema mashine yenyewe feki!

bado natafakari kwa nini dunia haina huruma!!

asante.uyu mwanamke alikuwa mpenzi,hakukuwa na mpango wa kuona kwani yy aliolewa nami nikaoa

usumbufu wa kudai uhusika wangu kwa mtoto wake ulianza baada ya kutoroka kutoka kwa mume wake

just tell me is it fair?
 
asante,kulingana na sheria ya vinasaba ya 2009,nani anaweza enforce upimaji wa DNA?

mamlaka yoyote na kijamii, kisheria na kijamii. kimsingi kipimo cha kundi la damu hakiainishi vinasaba.
 
asante.uyu mwanamke alikuwa mpenzi,hakukuwa na mpango wa kuona kwani yy aliolewa nami nikaoa

usumbufu wa kudai uhusika wangu kwa mtoto wake ulianza baada ya kutoroka kutoka kwa mume wake

just tell me is it fair?

Pole sana Al Mkubwa
Nitaomba unirekebishe kama nitakuwa sijakuelewa vizuri.
Kwa maelezo yako ni kwamba mmeshaachana muda mrefu na yeye kuolewa na mtu mwinginine na wewe kuoa,
je uliendelea kukutana kimwili nae baada ya yeye kuolewa? na je mara yako ya mwisho kukutana kimwili ilikuwa mwezi wa ngapi? na je mtoto aliye nae ana miezi mingapi?
Tukiweza kufumbua hilo fumbo hapo naamini kabisa tutamaliza mzozo?
Sitaweza kuongeza zaidi mpaka nipate jibu lako
 
Back
Top Bottom