Usumbufu TRA bandarini, tunaweza kufanya nini?

I just hate dealing with any Govt official!!!

Wala siyo Govt officials tu! Ni WaTZ kwa ujumla wetu tuna matatizo tena makubwa tu! Yaani ukichunguza kwa undani ni kila sekta palipo na M-TZ ni matatizo tu sijui nani aliyeturoga! "Nakubaliana na VOR kweli Bongo sekta zote zimeoza kuanzia juu mpaka chini!" Hapa tunamaanisha hata mkulu naye yumo.

Kwa kweli kama tungekuwa na viongozi wenye uchu na maisha ya waTZ tungekuwa mbali. Yaani tunataka kuzidiwa na Rwanda??? HII NI AIBU KIKWETE!!!!
 
Pamoja na kukubali kuna uzembe wa kiuongozi pale TRA, THA na ofisi zingine nyingi tu, ila
Sababu nyingine ni wafanyakazi tena wadogo tu, hawataki kufanya kazi zao mpaka akuzungushe ushinde hapo.
Wengine hawafanyi kazi wako kwenye internet.
Tuweni wa kweli, naamini wengi humu JF tunaacha kazi na kuanza kujibu hoja za humu JF wakati wa kazi.
Mods wakitoa takwimu traffic kubwa JF ni wakati wa kazi, weekend watu ni wachache, hii inaonyesha kuwa na sisi wafanyakazi wa chini inabidi tuache mizaa tufanye kazi, tuache kulalamikia wakubwa tu tutimize wajibu wetu.
 
Umewahi kujiuliza, hizo bandari zingekuwa zinamilikiwa na Wazungu hata kwa miaka 20 tu, zingekuwaje? Mimi naamini zingekuwa nzuri zaidi na huduma bora. Ni kweli tuna matatizo fulani.

Mkuu sio sahihi kufikiri hivyo(penye red) kwanza ni kujizarau na kutokutambua uwepo na utambuzi wako, hata sisi tunaweza ni suala la kuamua, na kuamua ni kuwa na viongozi ambao wapo kwa ajili ya hii nchi. Hakika tunaweza kama we ulivyoweza kutambua tatizo pia jaribu kufikiri na kufanyia kazi mawazo yako, umefika muda wa fikiri na kukutenda kwa ajili yetu mkuu, Mwingereza atafikiri Kiingeraza na kuja kutenda Kiingereza kazi yetu, nasi tutegemea outcome kwa ajili yetu?
 
Tatizo la bandari / TRA ni sugu, na chanzo cha kuzozota shughuli zote za ujasiriamali kwa wananchi na chanzo cha mapato kwa serikali. Suluhisho inabidi kwanza serikali na wenye madaraka liwaguse na kisha wakubali hivyo. Hadi hivi sasa, sioni dalili ya yoye hayo mawili niliyoyataja!
 
Kwa kuwa sasa hivi karibu mikoa yote ya TRA iko katika system, nashauri mizigo yote ambayo ni ya mikoani iruhusiwe kutolewa bandarini halafu ukadiriaji na malipo yote ya kodi yafanyike katika mikoa husika ili kuondoa mnsongamano wa mizigo hapo bandarini. Haingii akilini gari limeagizwa na ngosha mmoja pale Mwanza, anwani na kila kitu viko wazi halafu eti mzigo unazuiliwa bandarini ulipiwe kodi kwanza wakati TRA wako hata huko Mwanza. Tubadilike kwa maendeleo ya nchi yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…