Utafanyaje mkeo au mumeo au mzazi wako akiwa na mambo ya Kishirikina? Hivi ñdivyo utakavyofañya

Utafanyaje mkeo au mumeo au mzazi wako akiwa na mambo ya Kishirikina? Hivi ñdivyo utakavyofañya

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
UTAFANYAJE MKEO AU MUMEO AU MZAZI WAKO AKIWA NA MAMBO YA KISHIRIKINA? Hivi ÑDIVYO UTAKAVYOFAÑYA.

Anaandika, Robért Heriel
Mtibeli.

Mtu yeyote ambaye haamini nguvu za Mungu huyo ni mshirikina.

Mtu yeyote ambaye anaamini nusu kwa nusu ñguvu za Mungu huyo ni Mshirikina.

Inaweza ikatokea kwenye maisha yako moja ya Watu wako wa karibu wakawa wanajihusisha na mambo ya kichawi au ushirikina.
Yaweza kuwa ni Mumeo au mkeo au wazazi au wazazi wa mumeo au mkeo.

Ikitokea ukajua kuwa moja ya Watu wako wa karibu ni wachawi au washirikina iwe kwa wao kujionyesha waziwazi au kwa kificho.
Au wanakushauri mambo ya kishirikina au uchawi wakisema kuwa huenda mambo yako hayaendi sawasawa kwa sababu kuna vitu haujafanya. Na vitu hivyo ambavyo haujafanya wàkakuambia ni kwenda kwa waganga wa kienyeji, kwenda kufanya mambo ya kishirikina iwe ya kimila au kiutamaduni.

Ikiwa ni Baba au Mama ndiye anayekushauri mambo hayo jitenge naye. Wala usiwe karibu na yeye. Tena asije nyumbani kwako akakaa kwa muda mrefu asije akawafundisha familia yako elimu yake ya kipumbavu.

Nawe usiende kwa baba au mama yako ukakaa kwa siku nyingi zizidizo siku saba. Na mkeo asikae kwa wazazi wako ikiwa unajua ni washirikina na wanamawazo ya giza.
Na watoto wako wasikae kwa wazazi wako(Bibi na Babu zao) ambao ni washirikina na wachawi.
Watakapokuuliza kwa nini unafanya hayo. Waambie ni kwa sababu wao ni washirikina na wachawi ndio maana unafanya hayo.

Kwa sababu mshirikina hana elimu nyingine ya kumpa mwanao wala binti yako au mkeo zaidi ya kumpotosha.

Ikiwa mkweo ni mshirikina au mchawi usiruhusu wanao wakakae huko. Wala wao wasijekukaa hapo kwenu kwa muda mrefu usiozidi siku saba.

Elewa, mzazi wako anaweza kumpotosha mkeo na kumfundisha mambo ya kishirikina.
Anaweza kumfundisha kwenda kwa waganga ili wakudhibiti wewe au kukupa sumu ambazo hawazijui wao wenyewe.

Hakuna mafanikio ya maana yanayotokana na ushirikina na uchawi. Ni akheri uwe maskini na wakuone hauna muelekeo kuliko kufuata njia zao.
Ni akheri ufe kuliko kupata msaada wowote, nasisitiza wowote kutoka kwenye uchawi na ushirikina.

Waambie wewe hutaki mafanikio kutoka kwenye uchawi na ushirikina.
Waambie wao wakifanikiwa kwa njia hiyo inatosha. Wafanikiwe wao kwa mambo hayo na sio wewe.

Ikiwa mkeo au mumeo anamambo ya kishirikina au kichawi vunja hiyo ndoa na familia siku hiyohiyo usisubiri. Wala usiweke mjadala wa kumbadilisha.

Kabla hujaoa wala kuolewa, hakikisha unamwambia mwenza wako kuwa siku utakayojihusisha na ushirikina na uchawi ndio siku ambayo mahusiano haya yatafika mwisho na hakutakuwa na mjadala na hakuna atakayesikilizwa.

Ikiwa mtoto wako ulimfundisha kutojihusisha na mambo ya ushirikina au uchawi lakini kwa hiyari yake akakaidi na kufuata maamuzi yake. Waeleze Ndio siku hiyohiyo hautakuwa mzazi wao, hautakuwa Baba yao, hautakuwa Mama yao.

Wasitajwe kwa jina lako. Na wala usiwape urithi wowote ule.
Na wala wasije ukajihisi vibaya kuona wengine watakuwa wamefanikiwa na hawategemei urithi au chochote cha kuwapa.
Wasije nyumbani kwako wala wewe usiende kwao.
Usichukue chochote kutoka kwao wala wao wasichukue chochote kutoka kwako.
Kwa maana waliamua kukudharau na kukaidi.

Hivyo ndivyo Watibeli walivyo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
UTAFANYAJE MKEO AU MUMEO AU MZAZI WAKO AKIWA NA MAMBO YA KISHIRIKINA? Hivi ÑDIVYO UTAKAVYOFAÑYA.

Anaandika, Robért Heriel
Mtibeli.

Mtu yeyote ambaye haamini nguvu za Mungu huyo ni mshirikina.

Mtu yeyote ambaye anaamini nusu kwa nusu ñguvu za Mungu huyo ni Mshirikina.

Inaweza ikatokea kwenye maisha yako moja ya Watu wako wa karibu wakawa wanajihusisha na mambo ya kichawi au ushirikina.
Yaweza kuwa ni Mumeo au mkeo au wazazi au wazazi wa mumeo au mkeo.

Ikitokea ukajua kuwa moja ya Watu wako wa karibu ni wachawi au washirikina iwe kwa wao kujionyesha waziwazi au kwa kificho.
Au wanakushauri mambo ya kishirikina au uchawi wakisema kuwa huenda mambo yako hayaendi sawasawa kwa sababu kuna vitu haujafanya. Na vitu hivyo ambavyo haujafanya wàkakuambia ni kwenda kwa waganga wa kienyeji, kwenda kufanya mambo ya kishirikina iwe ya kimila au kiutamaduni.

Ikiwa ni Baba au Mama ndiye anayekushauri mambo hayo jitenge naye. Wala usiwe karibu na yeye. Tena asije nyumbani kwako akakaa kwa muda mrefu asije akawafundisha familia yako elimu yake ya kipumbavu.

Nawe usiende kwa baba au mama yako ukakaa kwa siku nyingi zizidizo siku saba. Na mkeo asikae kwa wazazi wako ikiwa unajua ni washirikina na wanamawazo ya giza.
Na watoto wako wasikae kwa wazazi wako(Bibi na Babu zao) ambao ni washirikina na wachawi.
Watakapokuuliza kwa nini unafanya hayo. Waambie ni kwa sababu wao ni washirikina na wachawi ndio maana unafanya hayo.

Kwa sababu mshirikina hana elimu nyingine ya kumpa mwanao wala binti yako au mkeo zaidi ya kumpotosha.

Ikiwa mkweo ni mshirikina au mchawi usiruhusu wanao wakakae huko. Wala wao wasijekukaa hapo kwenu kwa muda mrefu usiozidi siku saba.

Elewa, mzazi wako anaweza kumpotosha mkeo na kumfundisha mambo ya kishirikina.
Anaweza kumfundisha kwenda kwa waganga ili wakudhibiti wewe au kukupa sumu ambazo hawazijui wao wenyewe.

Hakuna mafanikio ya maana yanayotokana na ushirikina na uchawi. Ni akheri uwe maskini na wakuone hauna muelekeo kuliko kufuata njia zao.
Ni akheri ufe kuliko kupata msaada wowote, nasisitiza wowote kutoka kwenye uchawi na ushirikina.

Waambie wewe hutaki mafanikio kutoka kwenye uchawi na ushirikina.
Waambie wao wakifanikiwa kwa njia hiyo inatosha. Wafanikiwe wao kwa mambo hayo na sio wewe.

Ikiwa mkeo au mumeo anamambo ya kishirikina au kichawi vunja hiyo ndoa na familia siku hiyohiyo usisubiri. Wala usiweke mjadala wa kumbadilisha.

Kabla hujaoa wala kuolewa, hakikisha unamwambia mwenza wako kuwa siku utakayojihusisha na ushirikina na uchawi ndio siku ambayo mahusiano haya yatafika mwisho na hakutakuwa na mjadala na hakuna atakayesikilizwa.

Ikiwa mtoto wako ulimfundisha kutojihusisha na mambo ya ushirikina au uchawi lakini kwa hiyari yake akakaidi na kufuata maamuzi yake. Waeleze Ndio siku hiyohiyo hautakuwa mzazi wao, hautakuwa Baba yao, hautakuwa Mama yao.

Wasitajwe kwa jina lako. Na wala usiwape urithi wowote ule.
Na wala wasije ukajihisi vibaya kuona wengine watakuwa wamefanikiwa na hawategemei urithi au chochote cha kuwapa.
Wasije nyumbani kwako wala wewe usiende kwao.
Usichukue chochote kutoka kwao wala wao wasichukue chochote kutoka kwako.
Kwa maana waliamua kukudharau na kukaidi.

Hivyo ndivyo Watibeli walivyo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
so msimamo wako ndo uwe wetu
basi sawa
 
Mungu hayupo wala shetani hayupo zaidi ya kichwani kwa muumini tu , mimi na wewe pia ni washirikina kwa sababu tunashiriki mambo mengi kwa pamoja ikiwa kuvuta pumzi, kuchangia humo jf kwa pamoja na hata kulisukuma gurudumu la maendeleo .
 
Mungu hayupo wala shetani hayupo zaidi ya kichwani kwa muumini tu , mimi na wewe pia ni washirikina kwa sababu tunashiriki mambo mengi kwa pamoja ikiwa kuvuta pumzi, kuchangia humo jf kwa pamoja na hata kulisukuma gurudumu la maendeleo .

Mungu hayupo kwa wale vipofu wa rohoni.

Ni kama Kipofu aseme Mwezi Haupo kwa sababu hawezi kutumia mlango wowote wa fahamu kuthibitisha uwepo wake.
 
Hauwezi kuamini Mungu ukaacha kuamini uchawi na mambo yake.


Uchawi ni uongo
Uwepo wa uongo haukufanyi uuamini.
Unaweza kujua kitu fulani kipo na ukakiamini
Na unaweza ukajua kipo na usikiamini.

Na unaweza kujua hakipo lakini ukauamua kukiamini.
Na unaweza usijue kipo lakini usikiamini au kukiamini.

Imani ni tofauti na Kujua.
Ingawaje kujua kwa sehemu kubwa hujenga Imani
 
Nadharia ili kuthibitisha nadharia nyingne tu.

Miaka elfu ijayo kuna kizazi kikiambiwa ulikuwepo hata kikipewa ushahidi kitasema haukuwepo na ni nadharia tuu.

Sasa hivi ukiambiwa kulikuwa na Mnyama aitwaye Dragon útakataa.

Imani inahusu Kitu kilichopita au kijacho kisichothibitishwa kwa njia ya mwili.

Zamani walioona maisha ya mbeleni kutakuwa na Ndege zinazopaa angani walikataa wakasema hicho ni nadharia

Lakini vipi sasa hivi?

Mungu yupo.
Sema bado sayansi na akili zetu ni ndogo kuthibitisha jambo hilo.
Kusema hayupo kwa sababu ya kushindwa kuthibitisha ni dalili ya kutokufikiri vizuri
 
Uchawi ni uongo
Uwepo wa uongo haukufanyi uuamini.
Unaweza kujua kitu fulani kipo na ukakiamini
Na unaweza ukajua kipo na usikiamini.

Na unaweza kujua hakipo lakini ukauamua kukiamini.
Na unaweza usijue kipo lakini usikiamini au kukiamini.

Imani ni tofauti na Kujua.
Ingawaje kujua kwa sehemu kubwa hujenga Imani
Kujua ni hatua ya mwisho kabisa mbele ya kuamini, watu wanaamini kwa sababu hawajui ,ukishajua hauna sababu ya kuamini .
 
Miaka elfu ijayo kuna kizazi kikiambiwa ulikuwepo hata kikipewa ushahidi kitasema haukuwepo na ni nadharia tuu.

Sasa hivi ukiambiwa kulikuwa na Mnyama aitwaye Dragon útakataa.

Imani inahusu Kitu kilichopita au kijacho kisichothibitishwa kwa njia ya mwili.

Zamani walioona maisha ya mbeleni kutakuwa na Ndege zinazopaa angani walikataa wakasema hicho ni nadharia

Lakini vipi sasa hivi?

Mungu yupo.
Sema bado sayansi na akili zetu ni ndogo kuthibitisha jambo hilo.
Kusema hayupo kwa sababu ya kushindwa kuthibitisha ni dalili ya kutokufikiri vizuri
Dah , ukishaona akili yako ni ndogo kuthibitisha hilo tambua kabisa Mungu hayupo labda tu ni wewe ulishindwa kuelewa walio leta hiyo nadharia ya Mungu walimaanisha nini.
 
Back
Top Bottom