Utafanyaje?!

Mkeshahoi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2009
Posts
2,469
Reaction score
284
Uko zako uraiani na ushamaliza mihangaiko yako ya kila siku...!!unaangalia taarifa ya khabari unaona rafiki yako, mfano classmate wako wa sekondari, anaonekana ktk TV akitafutwa na Polisi kama mhalifu sugu na mwenye mtandao mkubwa hadi polisi.. na zawadi nono kwa atakayefanikisha kukamatwa kwake!!

Siku chache, unakutana nae uso kwa uso ukiwa mihangaikoni... anakusabahi..anaonekana ni mtu mstaarabu na mwenye hela... mnabadilishana mawili matatu ila wewe huna amani naye anaonekana hana amani na wewe...!!

utamuuliza kuhusu habari zake ktk tv...utamsalimisha polisi(kumbuka kuna zawadi nono nawe umifulia)?!:A S 39:
 
Kwanza mbona umeileta hapa hii thread?

Pili hapo utaonesha busara zako kama ni skendo ya kawaida mpe habari tu, na kama ni mbaya basi ripoti lakini si kwa kutaka hela.
Hela zitakupeleka pabaya na ni za hivo hivo.

lakini mara nyingi inategemea na busara yako kumwokoa nduguyo maana hapo ndipo atabadilika vizuri kama nni wa kubadilika.
 
Binadam nowdaiz hawaaminiki hata kidogo,unaweza sema usimseme police kesho akakuvamia na kuiteketeza familia yako,to me as long as kashabadilisha maisha yake kawa mtu mwingine asie na maadili ntamripot police tu,dnt forget do the do before the do does u.
 
Nitamripoti polisi... sio kwasababu nataka pesa (huo utakuwa usaliti). Nitamripoti kwasababu ya uraia wema...
 

unafahamu maana ya urafiki chief?!:confused2:
 
Nitamripiti fasta polisi, Mwizi ni mwizi tu siku yoyote anaweza kukugeuzia kibao hata km ni classmate. Sio tu ili upate zawadi nono ila kuokoa maisha na mali za wavuja-jasho.
 
Nitamripoti polisi... sio kwasababu nataka pesa (huo utakuwa usaliti). Nitamripoti kwasababu ya uraia wema...

ni roho yako ndiyo imenena haya au just the fingers on the keyboard
 
Wakati huo huo familia yake inakufahamu na inatambua wewe ni mmoja wa marafiki!
 
Kirafiki zaidi....utamwambia/muuliza ili ajue jinsi yakujisaidia!Sidhani kama kuna mtu anapenda kuona rafiki yake akiingia matatizoni!
Kibinadamu zaidi....itabidi utoe taarifa kwasababu huwezi jua....vile umemuona anaweza akawa na wasiwasi na wewe ,akakudhuru ili usitoe taarifa!

Kutoa taarifa ni mantiki zaidi!!
 

U got it!!
 
Sijali pesa wala zawadi, nitamripoti kwa watu wa usalama hata akiwa ni ndugu yangu wa kuzaliwa kwa baba na mama.
 
Let the nature take place. I am not going to be the source of his problem. I will just leave it, unless he has shared the problem with me and ask for my advice. Otherwise its wise to stay cool. You better be a good listener than a good speaker.
 


Jiulize yafuatayo;

1. Wewe unaweza kuathirika kwa uhalifu huo kwa namna yoyote?

2. Je, zawadi nono hiyo kweli ipo? Na kama ipo, inatosha kuwa suluhisho la kufulia kwako?

3. Urafiki wenu utaathiri vipi maisha, jamii na nchi yako?

Lakini utambue yafuatayo pia;

1. Ni mtu anayekufahamu pengine hadi nyumbani...!

2. Anao mtandao mkubwa sana polisi, ukimripoti huenda umejipeleka kwake...!

3. Pia ni mtu ambaye tayari hana amani nawe, hivyo amekwisha tambua utofauti kati yenu...!

Cha kufanya;

1. Kaa kimya, na kamwe usizungumze naye kuhusu tuhuma hizo.

2. Kaa mbali naye na umkwepe kuongozana naye kabisa.

3. Kama utaripoti polisi, angalia usipelekwe na tamaa za zawadi nono, tembelea vituo mbalimbali na utumbukize maandishi yako kwenye masanduku ya maoni, then ishia zako kimyakimya. Wasipolifanyia kazi basi wewe umetimiza wajibu wako. Vinginevyo, kaa kimya na umuombe mungu akulinda na akuweke mbali naye...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…