Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tanzania inatumia kati ya $40,000 & $60,000 kusomesha daktari mmoja (medical doctors), lakini madaktari wanne kati ya kumi wanaomaliza elimu hii wana achana na fani ya udaktari muda mfupi baada ya kuhitimu masomo yao. Hili tatizo (kama sio janga) kwa taifa, hasa ikizingatiwa pia kwamba Tanzania ni moja ya nchi zenye "Doctor to patient ratio" kubwa sana duniani – uwiano huu kwa Tanzania ni Wastani wa Daktari Mmoja Kwa Kila Watu 26,000. Kwa mujibu wa Shirika la Afya duniani (WHO), uwiano unaotakiwa ni Daktari Mmoja Kwa Kila Watu 1,000, au chini ya hapo. Kwa maana hii, wastani wa Tanzania umezidi kigezo cha WHO kwa mara ishirini na sita elfu, huku baadhi ya maeneo ya nchi yakiwa na uwiano ambao ni mkubwa na wa kutisha zaidi, kwa mfano:
Mikoa yenye uwiano ulio chini zaidi ya hiyo hapo juu ni pamoja na:
Lakini pamoja na mikoa hii kuwa na unafuu, bado uwiano huu ni mkubwa sana kwa vigezo vya WHO.
Kwa mujibu wa utafiti mwingine uliofanywa hivi karibuni, 42% ya watanzania wanaomaliza elimu zao za udaktari huwa wanachagua kufanya kazi katika miji michache kama ifuatavyo: Dar-es-salaam, Mwanza, Moshi, Mbeya na Arusha. Dar-es-salaam peke yake accounts for 32% ya medical doctors wote nchini, na hali hii ni ushahidi tosha kwamba kama taifa, tumeshindwa kuwapatia hudumu bora za kiafya wananchi walio wengi (hasa vijijini).
Katika karne ya ishirini na moja, ushindani wa nchi kiuchumi unapimwa na hazina ya rasilimali watu iliyoko (Human Capital), ambayo sehemu kubwa inajengwa na ubora wa Elimu na Afya miongoni mwa wananchi (hasa nguvu kazi). Kwa maana nyingine, Labour productivity ni zao la Elimu na Afya Bora ya labor force katika uchumi. Kwa vile ni dhahiri kwamba sekta zote hizi mbili (Elimu na Afya) zinakabiliwa na majanga, nadhani itakuwa sahihi kuhitimisha kwamba tunaendelea kujidanganya kwamba sisi kama taifa sasa tupo tayari in terms of "capabilities" kushiriki kikamilifu in today's competitive global economy.
Cc: Nguruvi3, Zakumi, Zinedine, gfsonwin, zumbemkuu, Kichuguu, JingalaFalsafa, HKigwangalla, EMT, Jasusi, JokaKuu, Ben Saanane, Bongolander et al.
- Kigoma – Daktari mmoja anahudumia watu 308,000
- Mara, Daktari mmoja anahudumia watu 167,000
- Tabora – Daktari mmoja anahudumia watu 132,000 (huu ni mkoa wa Dr. @hkigwangala).
Mikoa yenye uwiano ulio chini zaidi ya hiyo hapo juu ni pamoja na:
- Arusha (22,000);
- Dar-es-salaam (24,000) na
- Pwani (32,000);
Lakini pamoja na mikoa hii kuwa na unafuu, bado uwiano huu ni mkubwa sana kwa vigezo vya WHO.
Kwa mujibu wa utafiti mwingine uliofanywa hivi karibuni, 42% ya watanzania wanaomaliza elimu zao za udaktari huwa wanachagua kufanya kazi katika miji michache kama ifuatavyo: Dar-es-salaam, Mwanza, Moshi, Mbeya na Arusha. Dar-es-salaam peke yake accounts for 32% ya medical doctors wote nchini, na hali hii ni ushahidi tosha kwamba kama taifa, tumeshindwa kuwapatia hudumu bora za kiafya wananchi walio wengi (hasa vijijini).
Katika karne ya ishirini na moja, ushindani wa nchi kiuchumi unapimwa na hazina ya rasilimali watu iliyoko (Human Capital), ambayo sehemu kubwa inajengwa na ubora wa Elimu na Afya miongoni mwa wananchi (hasa nguvu kazi). Kwa maana nyingine, Labour productivity ni zao la Elimu na Afya Bora ya labor force katika uchumi. Kwa vile ni dhahiri kwamba sekta zote hizi mbili (Elimu na Afya) zinakabiliwa na majanga, nadhani itakuwa sahihi kuhitimisha kwamba tunaendelea kujidanganya kwamba sisi kama taifa sasa tupo tayari in terms of "capabilities" kushiriki kikamilifu in today's competitive global economy.
Cc: Nguruvi3, Zakumi, Zinedine, gfsonwin, zumbemkuu, Kichuguu, JingalaFalsafa, HKigwangalla, EMT, Jasusi, JokaKuu, Ben Saanane, Bongolander et al.
Last edited by a moderator: