Utafiti: Madaktari Tanzania Wanatelekeza Wananchi Vijijini

Utafiti: Madaktari Tanzania Wanatelekeza Wananchi Vijijini

Mchambuzi;

Mchambuzi;
Hapa tunazungumzia madaktari na huduma wanazotoa vijijini. Ukweli wa mambo, hili daktari wafanye kazi vizuri ni lazima sekta zingine za jamii ziwe nzuri. Na hili daktari afanye kazi vizuri ni lazima awe karibu anaofanana nao kiutaalamu. Na hii sio kwa daktari bali kwa watu wa fani zingine pia.

Hili nakubaliana na wewe ndio maana hapo juu kuna sehemu nimejadili juu ya umuhimu wa mikakati kuwa more holistic, sio kuangalia tu kwamba solution ni good salaries as a motivation of performance;sina maana kwamba good salaries sio kigezo muhimu, bali yapo masuala mengine nje ya good pay yanayochangia motivation;

Kwanini msanii wa bongo flava aishi DSM na sio Mpindimbi. Kwa sababu atakuwa karibu watu wa fani yake. Kwa sababu wagonjwa wengi wako vijijini haina sababu madaktari waende vijijini. Kwanini wanasiasa hawahamii Dodoma?

Katika hili, ina maana tunakubaliana kwamba huduma ya afya imepewa zaidi market value kuliko social value katika nyakazi hizi tofauti na kipindi cha nyuma;Katika hili nikahoji, je kwanini liberalisation, marketization and privatization haven't delivered to the poor in the post 1985 period? Tufanye nini ili hali ibadilike?

Kuhusu swali lako kwanini wanasiasa hawakai dodoma, sidhani kama ni kosa lao bali la serikali hasa in the post ujamaa period;kwa mfano, nchi nyingi zinazoendelea ziliweka jitiada za dhati kuhamisha makao makuu ya nchi na uamuzi huo trickled down kwenye kila taasisi ya ndani na ya nje kwani governments had political will; Kwetu Tanzania, nilipoona tu balozi mpya za marekani, EU, UAE etc zinajengwa DSM nikajua kwamba serikali haina mpango wa dhati wa kuhamia dodoma, vinginevyo tungeona balozi hizi zikihamia dodoma, tazama miji mikuu mingi mipya ya nchi zinazoendelea, balozi nyingi zimefuata serikali;

Siasa za Tanzania ni kufikiri kuwa unaweza kum-train miracle worker ambaye anaweza kwenda kuleta maendeleo vijijini. Nchi imejaribu hivyo kwa miaka 50 na haiwezekani.

Kwanini tuseme madaktari wanatelekeza wananchi vijijini? Kwanini hatusemi wabunge wanatelekeza wananchi vijijini?


Kutofanikiwa kwa miaka 50 haina maana kwamba haiwezekani;and in actual semse, jitiada hazijawa kwa miaka 50 but less (wakati wa nyerere);mimi nakumbuka wakati ule, mzazi wangu alikuwa anafanya kazi mikoani kama RDD, na katika mikoa yote tuliyoishi, nakumbuka maafisa mbalimbali walikuwa wanafurahia kabisa maisha ya kuishi nje ya Dar-es-salaam;nadhani dhana ya decentralisation kimaamuzi na kifedha ikihimizwa, itabadilisha mambo mengi;vinginevyo katika hali ya sasa, dhana ya decentralisation ni nadharia zaidi, maamuzi ya kifedha yanashikiliwa dar-es-salaam, na hata bungeni kila siku tunasikia kwamba hata nusu ya fedha za bajeti hazijafika huko chini wakati ni miezi michache tu imebakia kabla ya ujio wa mwaka mpya wa fedha;

Fani yako Mchambuzi inatakiwa kuleta maendeleo vijijini. Kwanini husemi unatelekeza wananchi vijijini? To single out madaktari ni kuwa wanafiki.

Kwa ufupi wa kamba yangu mkuu Zakumi, najitahidi sana kuelewa matatizo ya msingi ya wanavijiji kwani ni jadi yangu kwenda maeneo mbalimbali kwa gharama zangu mwenyewe kwenda fanya tafiti ndogo ndogo, hasa kuishi na wananchi na kujionea first hand;nimeenda sana singida, arusha, mbeya, na nikifanikiwa zaidi, nitaenda maeneo mengine zaidi;

Chuo cha kilimo cha Sokoine kinatoa wataalamu wengi tu. Je wanakwenda vijijini? Hapana. Je wanawatelekeza wanavijiji kama madaktari? Ndio.

Katika mjadala wetu mwingine nadhani unakumbuka kwamba Nguruvi3 alilijadili hili la SUA vizuri sana;hoja yake ya msingi ni kwamba serikali ikiamua kwa mfano kuondoa porojo za kilimo kwanza na kuzipeleka SUA na pakawekwa performance indicators na targets, mabadiliko sekta ya kilimo yatakuja;vinginevyo sio kwamba wataalam wa kilimo nchini hawajui tatizo nini, wanajua, na wameandika volumes and volumes of reports, lakini zinaishia kuliwa na mende kwenye makabati serikalini;

Sekta ya afya invokes political emotions. Lakini wanachofanya madaktari kinachangiwa na movement of labour.
Kama kila mkoa wa Tanzania utakuwa na angalau urban center moja au mbili ambazo zitavutia top talents kukaa katika centers hizo, madaktari na talents zingine zitavutiwa kwenda kwenye miji hiyo na kufanya huduma kuwa karibu na wananchi.
Definition yako ya urban center ni nini? Eneo husika kufikia hadhi ya manispaa?kama jibu ni ndio, mbona zipo nyingi tu leo?
Kama jibu ni hapana, what's your definition?
Urbanization sio inayochangia umalaya, ujambazi, and political unrests. Kinachochangia ni miundo mibaya ya uchumi.


haukunisoma vizuri katika hili kwani unachosema ndicho nilichosema;

Ukikataa kufanya urbanization na kuwapelekea watu huduma nzuri za afya, utaongeza wastani wa maisha na idadi ya watu. Hii pekee yake ni chanzo cha urbanization. Kuna vijiji vingi Tanzania watu wanaishi kimjini lakini hawana mazingira ya kimji.

Nadhani hapa ukifafanua zaidi utanisaidia majibu kwa swali langu kwako hapo juu kuhusiana na your definition of "an urban center"

Vilevile huwezi kukwepa urbanization. Mabadiliko ya hali ya hewa yamefanya vijana wengi kuacha shughuli za vijijini na kuanza kutafuta kazi kuajiriwa. Chukua mfano kazi za ulinzi. Miaka ya zamani wamasai wengi walikuwa wachungaji. Sasa hivi vijana wengi wako happy kufanya kazi za ulinzi.

Ni kweli, urbanisation ni phenomenon ambayo ni unavoidable, kwani hata China hili ni tatizo, na halitokani na mabadiliko ya tabia nchi tu bali pia structural transformation;je sisi Tanzania, is there a structural transformation taking place?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hili nakubaliana na wewe ndio maana hapo juu kuna sehemu nimejadili juu ya umuhimu wa mikakati kuwa more holistic, sio kuangalia tu kwamba solution ni good salaries as a motivation of performance;sina maana kwamba good salaries sio kigezo muhimu, bali yapo masuala mengine nje ya good pay yanayochangia motivation;



Katika hili, ina maana tunakubaliana kwamba huduma ya afya imepewa zaidi market value kuliko social value katika nyakazi hizi tofauti na kipindi cha nyuma;Katika hili nikahoji, je kwanini liberalisation, marketization and privatization haven't delivered to the poor in the post 1985 period? Tufanye nini ili hali ibadilike?

Kuhusu swali lako kwanini wanasiasa hawakai dodoma, sidhani kama ni kosa lao bali la serikali hasa in the post ujamaa period;kwa mfano, nchi nyingi zinazoendelea ziliweka jitiada za dhati kuhamisha makao makuu ya nchi na uamuzi huo trickled down kwenye kila taasisi ya ndani na ya nje kwani governments had political will; Kwetu Tanzania, nilipoona tu balozi mpya za marekani, EU, UAE etc zinajengwa DSM nikajua kwamba serikali haina mpango wa dhati wa kuhamia dodoma, vinginevyo tungeona balozi hizi zikihamia dodoma, tazama miji mikuu mingi mipya ya nchi zinazoendelea, balozi nyingi zimefuata serikali;



Kutofanikiwa kwa miaka 50 haina maana kwamba haiwezekani;and in actual semse, jitiada hazijawa kwa miaka 50 but less (wakati wa nyerere);mimi nakumbuka wakati ule, mzazi wangu alikuwa anafanya kazi mikoani kama RDD, na katika mikoa yote tuliyoishi, nakumbuka maafisa mbalimbali walikuwa wanafurahia kabisa maisha ya kuishi nje ya Dar-es-salaam;nadhani dhana ya decentralisation kimaamuzi na kifedha ikihimizwa, itabadilisha mambo mengi;vinginevyo katika hali ya sasa, dhana ya decentralisation ni nadharia zaidi, maamuzi ya kifedha yanashikiliwa dar-es-salaam, na hata bungeni kila siku tunasikia kwamba hata nusu ya fedha za bajeti hazijafika huko chini wakati ni miezi michache tu imebakia kabla ya ujio wa mwaka mpya wa fedha;



Kwa ufupi wa kamba yangu mkuu Zakumi, najitahidi sana kuelewa matatizo ya msingi ya wanavijiji kwani ni jadi yangu kwenda maeneo mbalimbali kwa gharama zangu mwenyewe kwenda fanya tafiti ndogo ndogo, hasa kuishi na wananchi na kujionea first hand;nimeenda sana singida, arusha, mbeya, na nikifanikiwa zaidi, nitaenda maeneo mengine zaidi;



Katika mjadala wetu mwingine nadhani unakumbuka kwamba Nguruvi3 alilijadili hili la SUA vizuri sana;hoja yake ya msingi ni kwamba serikali ikiamua kwa mfano kuondoa porojo za kilimo kwanza na kuzipeleka SUA na pakawekwa performance indicators na targets, mabadiliko sekta ya kilimo yatakuja;vinginevyo sio kwamba wataalam wa kilimo nchini hawajui tatizo nini, wanajua, na wameandika volumes and volumes of reports, lakini zinaishia kuliwa na mende kwenye makabati serikalini;


Definition yako ya urban center ni nini? Eneo husika kufikia hadhi ya manispaa?kama jibu ni ndio, mbona zipo nyingi tu leo?
Kama jibu ni hapana, what's your definition?


haukunisoma vizuri katika hili kwani unachosema ndicho nilichosema;



Nadhani hapa ukifafanua zaidi utanisaidia majibu kwa swali langu kwako hapo juu kuhusiana na your definition of "an urban center"



Ni kweli, urbanisation ni phenomenon ambayo ni unavoidable, kwani hata China hili ni tatizo, na halitokani na mabadiliko ya tabia nchi tu bali pia structural transformation;je sisi Tanzania, is there a structural transformation taking place?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums


Mchambuzi;

Kwanza nianze na urban centers. Kwa Tanzania definition tunayotumia inatokana zaidi na idadi ya watu. Mji ukifisha idadi fulani ya watu itaitwa manispaa. Ikifikisha watu zaidi ya laki saba kwenda milioni itapewa hadhi ya city (Jiji).

Watu wanapoongezeka katika eneo fulani, ongezeko lao linatalajiwa kuongeza economic activities, social services, innovation na mambo mengine. Je public policies zinaambatana au kusaidia maongezako hayo? Ukweli wa mambo haziambatani. Viongozi katika mikoa na wilaya wanachofanya ni kuwa viranja wa rais. Hawana innovations zozote kusaidia mikoa wanayoongoza.

Kwa maelezo yangu, urban centers ni centers za utawala na uzalishaji. Ambazo zina sera zinaongeza economic activites, social services, innovation na mambo mengine. Sera hizi ziwe uniquely defined kutokana na mazingira ya centers husika. Na cha muhimu wananchi wa karibu na centers hizi wawe na wajibu wa kuongoza centers hizo. Kwa mfano mkuu wa mkoa wa Tabora awe ametoka mkoa wa Tabora.

Miaka ya nyuma kuna shule na taasisi mbalimbali zilizojengwa mbali na wananchi. Taasisi hizi zingejengwa kwenye urban areas zingechangia sana maendeleo ya miji. Ukiwa na mashule, taasisi mbalimbali za kijamii katika eneo moja unavutia talents mbalimbali.

Umefika wakati Tanzania iwe ina-tie economic activities and social services.
 
Mkuu Zakumi:

Nakubaliana na hoja zako za msingi bandiko #22 ; Lakini nabakia na maswali kadhaa ya kujiuliza, kwa mfano:

Je kuna haja ya ku balance baina ya rural and urban development, hasa ikizingatiwa kwamba sehemu muhimu ya afya ya mwananchi ni lishe?

Binafsi naamini kwamba rural development ina mchango kwa taifa lenye afya bora kupitia LISHE kwani wanaozalisha mazao ya chakula ni wananchi wanaioshi kwenye rural sector; Bila ya kuongeza uzalishaji wa chakula vijijini tutakuwa ni taifa la namna gani, kwani ina maana itabidi hata chakula tuanze kuagiza kwa wingi sana kutoka nje;

Suala lingine ni kwamba - kwa mtazamo wangu pengine finyu, a country stops to be underdeveloped pale wananchi wake wa mijini na vijijini wanapokuwa na access to all basic amenities; Pamoja na nchi kama marekani na uingereza kwa mfano kuendelea, bado kuna maeneo ambayo yapo categorized as rural areas, hayajatoweka, lakini maeneo haya yanapata huduma zote za msingi, je sisi tunashindwa nini?

Kwa jinsi navyoelewa, changamoto kubwa kwetu inahusiana na suala lile lile ambalo tumekuwa tunajadili kule kwenye uzi wetu wa "uchumi wa tanzania" ambapo wengi wetu tumekuwa tunahimiza kwamba industrialization was a necessary policy mara baada ya uhuru, suala ambalo umekuwa unapingana nalo; Nitafafanua:

Kinachopelekea urbanization Tanzania (na nchi nyingi za Afrika) ni tofauti na ilivyotokea katika nchi za Asia, Europe na Marekani; Tofauti na hawa wenzetu, urbanization kwetu inatokea bila significant industrial expansion; Kwetu, urbanization ni matokeo ya market forces and failures za serikali katika kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye rural sector; Watanzania wanakimbilia mijini kutafuta ajira/riziki kwenye sekta zisizo rasmi (tofauti na nchi za wenzetu ilivyotokea huko karne za nyuma), watanzania wanakimbilia mijini kutafuta running water, electricity, na modernity kwa ujumla (tofauti na process iliyojiri katika nchi za wenzetu); Wakifika mijini what do they find?

-Run down neighborhoods overwhelmed na idadi kubwa ya watu vis a vis services and infrastructure (kama vile zinazohusiana na huduma za afya);
-Shacks/Slums zenye uchafu wa mazingira yanayotishia hali zao za kiafya kuliko hata Vijijini;
-Monetary economy ambayo inahitaji kila mtu kuwa na fedha za kulipia huduma zote hata zile muhimu kama za afya (mind you, suala la ajira/kipato bado ni changamoto kubwa kwa migrants wengi);

Mwisho wa siku, badala ya urbanization kuja na package nzuri kuchangia maendeleo, kutokana na structural weaknesses za uchumi, urbanization inapunguza kasi ya maendeleo katika taifa kwani nguvu kazi ambayo ilikuwa under utilized vijijini, ikija mjini, sio tu kwamba inaendelea kuwa under utilized bali pia inakabiliwa na matatizo mengine mengi hasa yanayohusiana na suala la afya duni za potential labour force kutokana na vipato duni; kunazuka magonjwa ya mlipuko kutokana na uchafuzi wa mazingira na pia kutokana na ukosefu wa maji safi n.k;

Swali:

  • Je tunahitaji a balance approach baina ya urban and rural development au tuachana na rural development na badala yake tuhamishie scarce resources towards urban development?
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin
Kwanza kabisa napenda niseme kuna bias katika kuliangalia tatizo. Kwanini uzalendo uwe kwa daktari na si mtumishim mwingine yoyote. Mfano, wabunge wanakula milioni 11 kwa mwezi.

Wamo katika kamati za bunge ambako ni sehemu yao ya kazi na wanakula posho.
Wannalipwa lakini mbili kwa siku kwa kukaa katika kiti kama anavyokaa daktari tena akiwa na mgonjwa wa TB mbele yake. Wabunge wana viyoyozi.

Kamati ya bunge ya Chenge inalipwa 430,000 kwa siku. Kwa maana kuwa katika siku 5 chenge ana pesa zaidi ya daktari anayefanya kazi usiku na mchana kwa siku 30. Kwanini tudai uzalendo kwa daktari na si hawa ambao katika nchi masikini kama Tanzania kwa mwezi mbunge anakomba milioni zaidi ya 15.

Maswali yako: Je hali hii itaendelea hadi lini.
Hali hii itaendelea hadi pale wananchi watakapouliza pesa za kulipa akina Chenge 430,000 zinatoka wapi na kwanini pesa za kununua ultrasound zisipatikane.

Hadi wananchi watakapouliza kwanini mbunge na waziri wakatibiwe Milpark ili hali tuna huduma 'bora' kabisa Muhimbili.

Hadi wananchi watakapouliza bilioni 7 zilitokaje kwenda kulipa kamisheni ya rada na iwe ngumu kutoa milioni 100 kununua CT scan

Hali itaendelea hadi pale wananchi watakapogundua kuwa madaktari wakidai mazingira mazuri ya kazi ni kwa faida yao na si ya wabunge ambao siku moja ya kukaa katika kiti ni zaidi ya mshahara wao.

Hadi pale wananachi watakapouliza kodi zao zinafanya nini katika huduma za afya na kwanini waendele kulipa ili hali wanawea kubeba magogoro hadi Muhimbili wakisubiri siku zao.

Kwanini manesi hawalalmiki?
Si kweli nao pia wana kilio kama hicho, wanachokifanya ni kitu 'kidogo' ama mgonjwa aachwe.
Wameamua mfumo huo ambao unakuumiza wewe na mimi badala ya mabomu.
In general kuna go slow katika sekata ya afya ambayo sisi wananchi tumechangia sana ikiwa ni pamoja na kushangilia wanasiasa diamond jubilee.

Kwanini madkatari wamekuwa ma admin
Jibu ni rahisi, wao kama raia wengine wanamahitaji sawa na wanahitaji fursa za kimaisha. Kuwa Dr hakumaanishi kuwa udhalilike au ushindwe kuhudumia jamii yako. Hakufanyi ushindwe kusomesha mtoto kwa uzalendo ambao wazalendo namba moja (wabunge) hawana.

Kwaninii walichagua fani hiyo kama hawataki
Well, inawezekana wanataka kwasababu wakienda Botswana na kwingine wanafanya. Kwanini wasisusie huko na kurudi kijijini. Kinachotokea ni kuwa mtu huishi kwa elimu yake na kama anaona njia ni kupitia udaktari basi na iwe hivyo. Sijaona kosa kwa wao kutumia taaluma zao kama Engineer anapokuwa na MBA na kufanya kazi za Admin. Kama mtu wa SUA napofanya kazi za benki. Na kama mhasibu anapoamua kuwa mfanyabiashara.

Nadhani suala la uzalendo tuliangalie kwa ujumla na si kwa kada. Haya ndiyo mambo yale ya Ualimu ni wito na sasa tunaona div 5 na 6 zinaongezwa ili watoto wafaulu na si kushindana na ulimwengu wa leo.
 
Last edited by a moderator:
ndugu yangu Nguruvi3, kwanza nashukuru sana kwa majibu yako yaliyo jibu maswali yangu kwa ufasaha sana.

nashukuru sana kwamba sasa umeona ule uzalendo ambao mie nimekuwa nausimulia ana nausemea hapa jamvini kwa muda mrefu sana.

tulipokuwa tunajadili maswala ya uchumi nilihoji hivi nani anayetoa vipaumabele katika maendeleo ya nchi yetu?? na je nani anayetolea ama anayepanga gharama za kila kinaqchofanywa katika jamii yetu?? na je nani anayehakikisha misaada tunayopewa ana mikopo tunayoomba inafanya kazi kusudiwa??

ningepeta jibu kwenye hili swala ungejua kwamba nani ambaye ni mzalendo ama nani ambaye si mzalendo. kiukweli tanzania hatuna uzalendo kabisa. sioni sababu ya wabunge wanaokaa kupiga domo tuu kujaziwa mihela ilihali madaktari, na waalimu wanalipwa pesa ndogo sana huku ndio wanaotumika kupita wenzao.

lakini pia sisi wanachin tumekuwa wazembe sana na tusiokuwa na uchungu kabisa wala hatuna umoja manake hakuna mtanzania ambaye yuko radhi kuona anaungana na madaktari ama hata waalimu kudai haki zao. sasa je hawa bila mass behind wafikiri wataweza kupata wanachokidai?

kimsingi suluhisho la haya mambo yote ni katiba yetu kwenye katiba tuweeke condition kwamba mbunge alipwe pesa sawa na mtumish yyte yule wa umma na wasiwe na privallege yyte ile.
 
Last edited by a moderator:
Wadau,

mimi nadhani kuliangalia tatizo hili kwamba chanzo kikubwa ni maslahi duni ya madaktari ni makosa kwani tunakuwa tunatumia an atomistic approach badala ya holistic approach kwani in my very uneducated view , miaka ya nyuma, kulikuwa na tatizo la poor performance miongoni mwa watumishi wa ushuru na forodha ambapo moja ya sababu kubwa kwanini kulikuwa na low motivation na pia rushwa nyingi ilitajwa kwamba ni maslahi kidogo; Reforms zilizofuatia ambazo ndio zikazaa TRA in the 1990s zilitarajiwa kutatua tatizo hili; Je, tunaweza sema kwamba TRA imebadilika sasa na inakidhi mahitaji yanayotarajiwa na watanzania walio wengi baada ya reforms kufanyika, hasa kuboresha maslahi ya watumishi wa TRA? Hoja yangu ya msingi ni kwamba kuna tatizo kubwa zaidi ya maslahi peke yake, but again, this is my very uneducated view, nasimama kupingwa kwa hoja;
MpigaKelele, Bongolander, gfsonwin, Nguruvi3, EMT

Mchambuzi, i beg to differ. This view of yours is not "un-educated" one as you think it is. If you see it that way fine, but to me it is very realistic and practical, sometimes we are too academic or too theoretical to the extend that we borrow theories which can not work on our land. Maslahi ni moja ya sababu lakini sio sababu pekee, ukijaribu kuchimba tatizo la rushwa Tanzania, bila shaka hatuwezi kusema kuwa per se umaskini ndio chanzo cha rushwa, kwa kuwa wezi wakubwa na mafisadi wakubwa hapa Tanzania sio maskini, ni wale wenye pesa nyingi. So there are people who have it in their genes, no matter how much they have they will need more.

Kwa upande wa madaktari tunazungumzia basic means of survival, we are talking about resources that can help them do their job in normal way, bila kupata profit. Waweze kwenda kazini vizuri, kufanya kazi vizuri na wakiwa kazini wasifikiri ya nyumbani, hasa njaa na shule kwa watoto wao. I do not this that is too much to ask for the ratio of doctor/patient of 1:300,000. Until otherwise, this atomistic view will remain valid and realistc.

We can also look at it holistically, that is why in my previous bandiko i said, it looks like those who have the mandate to manage the whole health care system in Tanzania, do not give a damn. The do so because they are not part of the system, whenever they catch a cold the go to best hospitals in Germany, UK, SA or India. To them health care is just a talking point or a political platform they use to play politics.

Kama kweli Tanzania tungekuwa serious kuhusu hili unalosema, hakuna mtanzania ambaye angekufa kwa Malaria tangu mwaka 2000. Kama afya ikiwa ni ajenda ya kweli ya uchaguzi ingeboreshwa sana. Unatakiwa kujiuliza ni kwanini wanganga wa kienyeji wanashamiri Tanzania na mabango kibao ya ajabu ajabu.
 
Mkuu Zakumi:

Nakubaliana na hoja zako za msingi bandiko #22 ; Lakini nabakia na maswali kadhaa ya kujiuliza, kwa mfano:

Je kuna haja ya ku balance baina ya rural and urban development, hasa ikizingatiwa kwamba sehemu muhimu ya afya ya mwananchi ni lishe?

Binafsi naamini kwamba rural development ina mchango kwa taifa lenye afya bora kupitia LISHE kwani wanaozalisha mazao ya chakula ni wananchi wanaioshi kwenye rural sector; Bila ya kuongeza uzalishaji wa chakula vijijini tutakuwa ni taifa la namna gani, kwani ina maana itabidi hata chakula tuanze kuagiza kwa wingi sana kutoka nje;

Suala lingine ni kwamba - kwa mtazamo wangu pengine finyu, a country stops to be underdeveloped pale wananchi wake wa mijini na vijijini wanapokuwa na access to all basic amenities; Pamoja na nchi kama marekani na uingereza kwa mfano kuendelea, bado kuna maeneo ambayo yapo categorized as rural areas, hayajatoweka, lakini maeneo haya yanapata huduma zote za msingi, je sisi tunashindwa nini?

Kwa jinsi navyoelewa, changamoto kubwa kwetu inahusiana na suala lile lile ambalo tumekuwa tunajadili kule kwenye uzi wetu wa "uchumi wa tanzania" ambapo wengi wetu tumekuwa tunahimiza kwamba industrialization was a necessary policy mara baada ya uhuru, suala ambalo umekuwa unapingana nalo; Nitafafanua:

Kinachopelekea urbanization Tanzania (na nchi nyingi za Afrika) ni tofauti na ilivyotokea katika nchi za Asia, Europe na Marekani; Tofauti na hawa wenzetu, urbanization kwetu inatokea bila significant industrial expansion; Kwetu, urbanization ni matokeo ya market forces and failures za serikali katika kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye rural sector; Watanzania wanakimbilia mijini kutafuta ajira/riziki kwenye sekta zisizo rasmi (tofauti na nchi za wenzetu ilivyotokea huko karne za nyuma), watanzania wanakimbilia mijini kutafuta running water, electricity, na modernity kwa ujumla (tofauti na process iliyojiri katika nchi za wenzetu); Wakifika mijini what do they find?

-Run down neighborhoods overwhelmed na idadi kubwa ya watu vis a vis services and infrastructure (kama vile zinazohusiana na huduma za afya);
-Shacks/Slums zenye uchafu wa mazingira yanayotishia hali zao za kiafya kuliko hata Vijijini;
-Monetary economy ambayo inahitaji kila mtu kuwa na fedha za kulipia huduma zote hata zile muhimu kama za afya (mind you, suala la ajira/kipato bado ni changamoto kubwa kwa migrants wengi);

Mwisho wa siku, badala ya urbanization kuja na package nzuri kuchangia maendeleo, kutokana na structural weaknesses za uchumi, urbanization inapunguza kasi ya maendeleo katika taifa kwani nguvu kazi ambayo ilikuwa under utilized vijijini, ikija mjini, sio tu kwamba inaendelea kuwa under utilized bali pia inakabiliwa na matatizo mengine mengi hasa yanayohusiana na suala la afya duni za potential labour force kutokana na vipato duni; kunazuka magonjwa ya mlipuko kutokana na uchafuzi wa mazingira na pia kutokana na ukosefu wa maji safi n.k;

Swali:

  • Je tunahitaji a balance approach baina ya urban and rural development au tuachana na rural development na badala yake tuhamishie scarce resources towards urban development?


First, let me start with industrialization and then I will move to urbanization. With regard to industrialization, it has come to my attention that whenever we have contentious discussions about Tanzanian economy, you tend to gravitate towards industrialization. Correct me if am wrong. You believe that through industrialization Tanzania can dig itself out of the abyss of backwardness.

To a greater extent, I agree with you. industrialization process will make a huge different economically and socially. The process will create decent jobs, will add values to our products, will improve and modernized our urban centers etc. etc. However, we have to keep it in mind that our process will not emerge in isolation or gradually as it happened in Europe and Northern America.

It can happen in isolation because we depend on others for our survival. It can’t emerge gradually because technology keep changing at a rapid pace, and the competition is fierce. To that end, we can’t use the same template of policies that Nyerere used in 1967-1985. He viewed our problems from a different perspective.

More than that we have to change the way we think. Nikisome posti nyingi za wale waliopenda siasa za 1967-1985, inaonyesha kuwa ujenzi wa viwanda peke yake ulitosha. Mpaka sasa hivi hawatoi hoja za msingi wa kuelezea uendeshaji wa viwanda hivyo na matatizo yaliokuwepo.

Tukirudi kwenye urbanization, the country is paying a heavy price for ignoring urbanization. Kama industrialization, orderly urbanization creates wealth and also improves quality of lives. Kwa mfano watu wenye pesa Tanzania wamejenga majumba ya kifahari lakini ujenzi wa majumba hayo haujaboresha maisha ya watanzania au kuongeza productivities ya wenye majumba hayo.

Tukirudi kwenye mada kamili. Kuna financial gain and job satisfaction. Madaktari na watu katika fani zote wanafanya kazi kwa ajili ya kipato na kuridhika kwa matumizi ya utaalamu wao katika maendeleo ya jamii. Kuhusiana na kipato naona imeshajadiliwa. Kuhusiana na matumizi ya utaalamu ni lazima jamii iwape nafasi madaktari kutoa mchango wa kwa jamii na kutambulika.

Kila siku jamii inataka kuwasifia wabunge au wanasiasa machachari. Kila kiongozi mashuhuri alikwenda kwa babu wa Loliondo. Lakini kuwa madaktari wanaofanya real medicine ambao hawasikiki.
 
ndugu yangu Nguruvi3, kwanza nashukuru sana kwa majibu yako yaliyo jibu maswali yangu kwa ufasaha sana.

nashukuru sana kwamba sasa umeona ule uzalendo ambao mie nimekuwa nausimulia ana nausemea hapa jamvini kwa muda mrefu sana.

tulipokuwa tunajadili maswala ya uchumi nilihoji hivi nani anayetoa vipaumabele katika maendeleo ya nchi yetu?? na je nani anayetolea ama anayepanga gharama za kila kinaqchofanywa katika jamii yetu?? na je nani anayehakikisha misaada tunayopewa ana mikopo tunayoomba inafanya kazi kusudiwa??

ningepeta jibu kwenye hili swala ungejua kwamba nani ambaye ni mzalendo ama nani ambaye si mzalendo. kiukweli tanzania hatuna uzalendo kabisa. sioni sababu ya wabunge wanaokaa kupiga domo tuu kujaziwa mihela ilihali madaktari, na waalimu wanalipwa pesa ndogo sana huku ndio wanaotumika kupita wenzao.

lakini pia sisi wanachin tumekuwa wazembe sana na tusiokuwa na uchungu kabisa wala hatuna umoja manake hakuna mtanzania ambaye yuko radhi kuona anaungana na madaktari ama hata waalimu kudai haki zao. sasa je hawa bila mass behind wafikiri wataweza kupata wanachokidai?

kimsingi suluhisho la haya mambo yote ni katiba yetu kwenye katiba tuweeke condition kwamba mbunge alipwe pesa sawa na mtumish yyte yule wa umma na wasiwe na privallege yyte ile.

Just to provoke the discussion. I believe that Uzalendo is a state of mind and isn’t measurable. So we can’t really say with conviction that watanzania hawana uzalendo.


Watanzania wengi wanaipenda nchi yao. Lakini inawezekana kuna vitu wanavyofanya ambavyo uvioni kuwa ni vya kizalendo. Je vitu hivyo vina characteristics ya kupima uzalendo wa mtu.


Chukua mfano mzazi wangu. Alifanya kazi serikalini, lakini mshahara wake haukutosha kupeleka watoto shule. Hivyo ilibidi aende kwenye seminars au atunge usafiri wa kikazi apate per diems za kusomesha watoto. Je ninaweza kusema sio mzalendo?
 
Back
Top Bottom