Utafiti: Wana JF na Avatar zao

Utafiti: Wana JF na Avatar zao

Ha ha ha !!! Afu akisema labda itokee tu anaweka pozi flani hivi.
Ha ha ngoja niende tena you tube nikamcheki sheikhe
Namkubali sana sheikh yule... hasa pale anapokuambia utapewa mizigo 60 lakini ukiwa na nguvu ya kuhudumia mizigo mia... hiyo mizigo 60 kazi inayo wallah
 
Hahahaaa kaazi kweli kweli.

Humu ndani huwa kuna imaginations za kuchekesha sana.

Wengine huwa wakisoma mwandiko wa mtu tu eti wanajua na umri wake😀😀😀😀.
Hahahahaaa

Wewe zari limekuangukia zaidi. Maana inaelekea watu wengi wanakufahamu. Hawajui tumesoma wote VETA pale Chang'ombe mwaka 1979.
 
Nafikiri kupitia maandishi utaweza kukisia tabia ya mtu kwa uhakika kuliko username au avatar.
Username na avatar zitasetiwa siku moja ila maandishi yatatolewa kila siku, mood ya siku ya kuseti avatar na username itapotea kidogo kidogo na uhalisia wako utahamia kwenye maandishi yako ya kila siku. Mfano attention seekers.
 
Nakubaliana na utafiti wako kwa 75%
Na nyongeza ID anayotumia mtu inaendana kwa kiasi kikubwa na maisha yake halisi au vile alivyo.
Nadhani hili suala la ID na Avatar lipo kisaikolojia zaidi.
Bila shaka nawe utakuwa mrembo sawa na avatar yako....natamani nione angalau picha yako halisi tu
[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji85]
 
Nafikiri kupitia maandishi utaweza kukisia tabia ya mtu kwa uhakika kuliko username au avatar.
Username na avatar zitasetiwa siku moja ila maandishi yatatolewa kila siku, mood ya siku ya kuseti avatar na username itapotea kidogo kidogo na uhalisia wako utahamia kwenye maandishi yako ya kila siku. Mfano attention seekers.
You are right... very right!
Nimekugongea like, kakague kama huamini.
 
Nimekuwa nikifanya utafiti kwa miaka miwili sasa juu ya tabia za wana JF kwa kutumia aina za avatar wanazotumia. Mpaka sasa nimekutana na members zaidi ya 30 humu.

Kiukweli avatar wanazopendelea kuweka zinafana sana na maisha yao halisi au vile walivyo nk. Au kwa lugha nyingine zinatoa preliminary background ya jinsi walivyo. Ukiona member kaweka avatar ya mrembo mkali, asee ni mrembo kweli si mchezo. Ukiona member kaweka picha la jamaa lina hasira, basi ujue yuko hivyo. Ukiona jamaa kaweka picha ya ya kiroho-mbaya ujue anakaribiana na sifa hiyo. Ukiona kaweka avatar ya kituko fulani hivi, naye ni kituko. Kadhalika na wenye avatar za ki hekima hekima, ni kweli kabisa wapo hivyo. Walioweka picha za wanyama, relatively wana maamuzi na matendo kama ya wanyama. Na wale wasioweka picha means they don't care, na kweli wenyewe wako laissez-faire tu.

Huu utafiti unatoa mwangaza mpya wa aina ya wana JF unaopanga ima kukutana nao au unapochat nao kuwajua japo kwa uchache tabia na mwonekano wao (imaginary). Awamu ya pili ya utafiti huu inaendelea...

NB: sitaanika members niliokutana nao wala "derived indicators" for privacy.
Kwahiyo wewe ni "don care"??? Nauliza tu
 
Back
Top Bottom