Utajiri / ujasiriamali unavyopatikana

Utajiri / ujasiriamali unavyopatikana

CONSULT

Senior Member
Joined
May 8, 2011
Posts
194
Reaction score
204
NAMNA MOJAWAPO WAJASIRIAMALI WANAVYOPATIKANA
Palikuwapo na nchi tajiri pia na mfalme wake tajiri sana na alikuwa mzee sana kwa bahati mbaya hakujaliwa kupata mtoto wa kiume ila alikuwa na binti mmoja tu na mrembo sana,

Mila na desturi za kabila hilo hazikuruhusu nchi hiyo kutawaliwa na mwanamke, ila ililazimu atakayekuwa mume wa huyo binti mfalme ndie atakae rithi ufalme (kingdom) hali hiyo ilimfadhaisha sana mfalme pia na jamii yote ya hiyo nchi, moja ya maswali mazito waliokuwa wakijiuliza ni namna gani vijana wa kijijini hapo watakavyo posa huyo binti mrembo na tajiri sana wa mfalme ? ?

Kwa upande mwingine Mfalme alijiuliza ni kwa namna ipi atapata mkwe shupavu, hodari, mwenye karama ya uongozi atakaye mkabidhi mwanae pekee pia ufalme wa nchi yake yenye neema na utajiri na amani ? ? Lakini aligundua kuwa kwa tabia zote "ujasiri na ushupavu" ni muhimu sana katita utawala wa falme yeyote ile (risk taking) na lazima atoke hapo hapo.

Mfalme akaandaa namna ya kumpata mrithi wake/ mkwe wake/ mfalme mpya, akaamua kuchimba swimming pool kubwa nyembamba ndefu na yenye kina kirefu pia ndani yake akafuga mamba wengi sana wakilishwa mbuzi wazima wazima kila kukicha, penbeni kushoto na kulia kumejengwa kingo ndefu na uzio wa waya isipokua tu mwanzo wakuingilia na mwisho ng'ambo ya pili pa kutokea na mamba ni wengi na wakubwa sana.

Siku ya siku ilipowadia mfalme akawambia wafuasi wake kugonga kengele kwa ajili ya watu wote wakusanyike pale penye swimming pool vijana wa kiume waliokuwa tayari na umri wa kuoa ndio wawe mbele akawatangazia watu wote kama ifuatavyo " Nadhani mnaniona umri wangu umeenda sana kuendelea kuwa mfalme wenu , na mnajua kuwa sina kijana wa kiume ila nina binti pekee , na atakaye muoa ndie atakuwa mfalme wa nchi yenu hii, pia ni lazima awe jasiri hakika, na lazima atoke kati yenu nyie vijana,

Kwa maana hiyo bwawa hili nimeliandaa ili kumpata mfalme jasiri na hodari na ndani ya bwawa hili mnawaona hao mamba, (wakati huo mfanyakazi mmoja akatupa mbuzi mmoja wakanyakuana kwa fujo sana walikuwa na njaa) Mimi nasema kijana jasiri ni yule atakaye jitosa kupambana na hawa mamba kwa kuogelea kutoka ng'ambo hii na kuvuka hadi ng'ambo ya pili atakuwa amefaulu na huyo ndie ntakaye mkabidhi mwanangu pekee na ufalme wa nchi hii SASA HIVI"

Basi baada ya kumaliza usemi huo minonyono na miguno ikawa mingi sana baadaye pakapitwa na ukimya wa dakika kadhaa watu wakitafakari mtihani mzito sana wa mfalme, vijana wakitaniana wao kwa wao, wengine wakirudi nyuma la kufanya hawana na pia binti mfalme yupo akiduwaa ! !

HHHHEEEIIIIII Mungu wangu Ghafla bila kutarajia akatokea kijana mmoja akaruka ndani ya maji nayo yakaruka duuubwiiii watu wakapiga makelele jamani analiwa huyo o o o na mamba wakaruka kila mmoja kumng'ata wengine wakigongana midomo juu kwa juu na kumwacha chini na yeye kila akitokeza na kuwaona walipo anazama kupiga mbizi chini kwa chini, ilikuwa pata shika watu wengine wakishika vichwa wengine walisha anza kupiga mayowe na kulia, kumbuka mungu sio athmani hatimaye ghafla kijana anatokeza ng'ambo ya pili na mikwaruzo ya kucha za mamba damu zinavuja bila shati wala kaptura, na kuhema kwa wingi sana na kuaguka ukingoni papo hapo huku mfalme akiruka kumpokea na akishangilia na kuwahamasisha watu kumpokea mfalme mpya kwa shangwe sana,,, HAPANA ! ! HAPANA ! ! ! SITAKI ! ! ! SITAKI ! ! ! Ningekufa je ? ? ningekufa je ? ? Watu waka shangaa tena waka pigwa na butwaa ,,, kijana akaendelea kutoa maneno huku akihema ovyo NANI KANISUKUMA ? ? NANI AMENISUKUMAA ? ? watu wakaendelea kustaajabu , kasukumwaa ? amesukumwa na nani tena ?

Kumbe kilichotokea ni hivi, kama ilivyo mzaha mzaha na utani wa vijana na hasa kwa wale wanaojiona ni bora kuliko wenzao kilitokea kikundi kimoja kikala njama ya kumsukuma kijana wa watu hajui lile wala hili wakijuwa wazi kuwa lazima ataliwa na mamba awe jaribio la kupima hiyo hatari ( sijui ni chambo ?) (wale wasoni mtasema ? RISK ASSESSMENT)
Lakini Mfalme hakuwa na muda tena wa kusikiliza hayo kwani alikuwa na furaha sana sana kwa kumpata mwanae wa kiume /mrithi wake/ mkwe wake/ na akamkumbatia kwa furaha kuu na wanachi wote pia ngoma na vigelegele sherehe ikaendelea hatimaye si kijana ni MFALME MKUU wale vijana waliomsukuma wakazubaa na kustaajabu wengine wakakimbia kwa kuogopa kukamatwa na mfalme mkuu aliwasamehe.

Ndg zangu mfano huu ni namna mmojawapo wanavyopatikana wajasiriamali maarufu sana na kufaulu sana kimaisha kijana mfalme alijikuta yuko kwenye maisha HATARI SANA - KUFA AU KUPONA alichokifanya ni kuokoa roho yake/maisha yake na sio ufalme na pengine hakuwahi hata kidogo kuwaza ufalme ghafla akipigania roho yake ghafla anaibuka na Ufalme, Utajiri, Mke binti Mrembo sana mwana wa mfalme,

Ni hivyo hivyo inavyotokea kwa baadhi ya wajasiriamali unakuta amezaliwa kwenye lindi kubwa la umaskini au namna ya tabu kubwa sana ambayo inatishia uhai wake hivyo anakuwa anapigania kuokoa uhai/maisha yake hatimaye anapata ka-mwanga ka-maisha/ka-unafuu na kumtia moyo nae kukandamizia hapo hapo kwa mbinu hizo hizo za kufa na kupona mwisho anajikuta inakuwa ndio tabia yake na ndio raha yake mwisho watu wanashangaa yuko hatua kubwa na mbali sana TAJIRI HUYO.

ILI KUBORESHA ZAIDI HADITHI HII TUNAOMBA MAONI YENU HASA HEADING , MAIN STORY, etc
 
HONGERA HONGERA Sana mkuu CONSULT ni kweli kabisa wengi wao wanaganga njaa hatimaye utajiri

Hadithi hii ni fundisho zuri sana, ubarikiwe
 
Mkuu CONSULT, kwa mimi nilivyoilewa hii hadithi kuwa the main point uliyotaka kueleza hapo ni kuwa kwenye ujasiliamali kuna"Risk Taking" lakini kwenye contemporary entrepreneurship, wajasiliamali wengi wanasisitiza "Calculated Risk" na sifa kubwa ya mjasiliamali ni kuamka, kujifuta vumbi na kuanza upya pale anapoangukia "resilience". Pili maudhui ya hii hadithi mbona hayaendani na main point uliyotaka kueleza sababu huyu kijana alisukumwa na mtu na hakushurutishwa na mazingira yaliyomzungua kwa maana hakutaka kuingia kuogelea kwenye lile bwawa kwa ridhaa yake mwenyewe. Maudhui ya hadithi hii na kwa uelewa wangu ni kwamba binaadamu anauwezo kufanya mambo ambayo yanaweza hata kumstaabisha yeye binafsi pale panapokuwa hakuna njia mbadala. Kwa maana hiyo basi, kila kitu kinawezekana kwa mwanadamu kama tutatumia uwezo wetu wa juu kabisa tuliopewa na mwenyezi Mungu katika kujiokoa kimaisha au na shida zetu . Hata hivyo unahitaji pongezi nyingi sababu ni hadithi nzuri.
 
Mkuu CONSULT, kwa mimi nilivyoilewa hii hadithi kuwa the main point uliyotaka kueleza hapo ni kuwa kwenye ujasiliamali kuna"Risk Taking" lakini kwenye contemporary entrepreneurship, wajasiliamali wengi wanasisitiza "Calculated Risk" na sifa kubwa ya mjasiliamali ni kuamka, kujifuta vumbi na kuanza upya pale anapoangukia "resilience". Pili maudhui ya hii hadithi mbona hayaendani na main point uliyotaka kueleza sababu huyu kijana alisukumwa na mtu na hakushurutishwa na mazingira yaliyomzungua kwa maana hakutaka kuingia kuogelea kwenye lile bwawa kwa ridhaa yake mwenyewe. Maudhui ya hadithi hii na kwa uelewa wangu ni kwamba binaadamu anauwezo kufanya mambo ambayo yanaweza hata kumstaabisha yeye binafsi pale panapokuwa hakuna njia mbadala. Kwa maana hiyo basi, kila kitu kinawezekana kwa mwanadamu kama tutatumia uwezo wetu wa juu kabisa tuliopewa na mwenyezi Mungu katika kujiokoa kimaisha au na shida zetu . Hata hivyo unahitaji pongezi nyingi sababu ni hadithi nzuri.

Shukrani sana mkuu, ni kweli kabisa ulivyoielewa ndivyo ilivyo, tafadhali kama ni nzuri ntafutie kichwa cha habari kizuri kinacho ifaa hii hadithi kwa nia njema na kwa manufaa ya wenzetu kwa maana niko kwenye utafiti pia...
 
Shukrani sana mkuu, ni kweli kabisa ulivyoielewa ndivyo ilivyo, tafadhali kama ni nzuri ntafutie kichwa cha habari kizuri kinacho ifaa hii hadithi kwa nia njema na kwa manufaa ya wenzetu kwa maana niko kwenye utafiti pia...

Still Shukrani kubwa zinakuja kwako Mkuu CONSULT, sababu nimejifunza na hii hadithi. Kwa muono wangu mimi kichwa cha habari kizuri kingestahili kuwa kwenye hii habari ni " ni "KUWA MJASIRIAMALI NI LAZIMA UWE JASIRI" au "KUWA TAJIRI/MJASIRIAMALI KUNAHITAJI UJASILI "" ". Hapo kwenye ujasili ndipo unapojitofautisha na binaadamu wengine wenye muono mdogo ambao kwao "kujaribu si kufanya". Nahisi nimeeleweka kwa hapo, kama nitahitajika kufafanua zaidi kwa kuongeza maelezo zaidi basi nitakuwa sina budi. Ahsante tena sana mkuu kwa hadithi yenye mafunzo mazuri.
 
Still Shukrani kubwa zinakuja kwako Mkuu CONSULT, sababu nimejifunza na hii hadithi. Kwa muono wangu mimi kichwa cha habari kizuri kingestahili kuwa kwenye hii habari ni " ni "KUWA MJASIRIAMALI NI LAZIMA UWE JASIRI" au "KUWA TAJIRI/MJASIRIAMALI KUNAHITAJI UJASILI "" ". Hapo kwenye ujasili ndipo unapojitofautisha na binaadamu wengine wenye muono mdogo ambao kwao "kujaribu si kufanya". Nahisi nimeeleweka kwa hapo, kama nitahitajika kufafanua zaidi kwa kuongeza maelezo zaidi basi nitakuwa sina budi. Ahsante tena sana mkuu kwa hadithi yenye mafunzo mazuri.

Shukran tena kwa ushauri wako nzuri sn pengine pana wengine pia naomba maoni na ushauri wao
 
Kisa kizuri sana hiki mkuu CONSULT,kina mafundisho mazuri ya namna maisha yanavyoweza kumsukuma mtu kufanya maamuzi yenye manufaa kwake.Napendekeza kichwa chake kiwe UJASIRIAMALI NI USHUJAA!

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Shukrani sana mkuu, ni kweli kabisa ulivyoielewa ndivyo ilivyo, tafadhali kama ni nzuri ntafutie kichwa cha habari kizuri kinacho ifaa hii hadithi kwa nia njema na kwa manufaa ya wenzetu kwa maana niko kwenye utafiti pia...

risk adjusted to unknown portfolio!
 
Kichwa bora cha hii hadithi nafikiri kingekuwa ni "CHANGAMOTO ZA UJASIRIAMALI"
Ikiwa na maana ya kuna changamoto nyingi kuwa mjasiriamali pamoja na ujasiri,uoga wa kufanya(kama watu walivyokuwa nyuma) kuna kelele za watu wa nje na mengine mengi ila kubwa zaidi ni kipimo cha ujasiri.

Ila nnachelea kwa hii hadithi kama iko kwa mjasiriamali anaechipukia kwa nchi hii ,kwa sasa hivi watu wengi wanaokuwa wajasiriamali ni wale wanaopata elimu ya ujasiriamali au pesa za kuanzisha kitu sio wale wanaofanya kwa msukumo wa wengine,nahisi hadithi ungejaribu kuigeuza ili ilete maana halisi

Sent from brand expert
 
Kisa kizuri sana hiki mkuu CONSULT,kina mafundisho mazuri ya namna maisha yanavyoweza kumsukuma mtu kufanya maamuzi yenye manufaa kwake.Napendekeza kichwa chake kiwe UJASIRIAMALI NI USHUJAA!

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Fukara nakushukuru nadhani wewe pia ni mjasiriamali,, hilo jina tuu hujalizika na ulichonacho fukara hawezi kutumia Pc ?
 
Kichwa bora cha hii hadithi nafikiri kingekuwa ni "CHANGAMOTO ZA UJASIRIAMALI"
Ikiwa na maana ya kuna changamoto nyingi kuwa mjasiriamali pamoja na ujasiri,uoga wa kufanya(kama watu walivyokuwa nyuma) kuna kelele za watu wa nje na mengine mengi ila kubwa zaidi ni kipimo cha ujasiri.

Ila nnachelea kwa hii hadithi kama iko kwa mjasiriamali anaechipukia kwa nchi hii ,kwa sasa hivi watu wengi wanaokuwa wajasiriamali ni wale wanaopata elimu ya ujasiriamali au pesa za kuanzisha kitu sio wale wanaofanya kwa msukumo wa wengine,nahisi hadithi ungejaribu kuigeuza ili ilete maana halisi

Sent from brand expert

Asante sana Mkuu Elisha Chuma nadhani umekosa muda tu, inavyoonekana unayo mengi sana ya kuibadili hii Hadithi, Hicho pia ni aina moja ya mazingira yanayowapata baadhi ya wajasiriamali duniani lakini hautujafanya utafiti kujua kwa TZ ni kwa idadi na kwa nja ipi wanayopitia wajasiriamali wetu, Ombi ebu pata muda uiframe/ uigeuze kwa namna yako kuwa bora zaidi - Shukrani mkuu
 
Asante mkuu CONSULT nnafanya kazi na wajasiriamali wadogo wadogo wengi na wakubwa wachache kwa idadi isiyokuwa rasmi na siwezi kukataa kwa mtu kuipinga ila Tanzania asilimia kubwa ya wajasiriamali ni wa aina mbili.

1. Anaefanya kazi sehemu huku anatunza fedha kwa ajili ya kuanzisha kitu chake mwenyewe kwa muda mrefu hadi anapohisi sasa anahitaji kuanza kwa vile anapesa ndio anaanza ujasiriamali ( asilimia kubwa ya hawa huwa hawaendi mbali sana kiujasiriamali sababu huhisi fedha ndio tatizo katika biashara).

2.Mtu asiekuwa na kazi ila akapata semina au wazo la biashara akaanza nalo bila ya fedha, asilimia kubwa ya hawa hufanikiwa wakiwa gizani wakiingia kwenye soko au ushindani hukumbana na nguvu ya pesa huishia kurudi walikokuwa.


Huwa sipendi kulinganisha Tanzania na nchi nyingine duniani kwa sababu ukweli ni kwamba Tanzania sio kama nchi nyingine ina mifumo tofauti kuanzia utawala hadi biashara inanjia zake tofauti na zinazoeleweka kikawaida za kibiashara hadi kisiasa mfumo wote uko tofauti.

Kuhusu hadithi ( kwenye mabano ni mfano kwa tanzania)
nahisi ifanye iwe hivi baada ya mfalme kutoa donge nono kwa wananchi (mfano: Jk alivyotoa zile bilioni) ambalo lilikuwa ni binti yake watu, aliwapa watu mtihani wa kuvuka dimbwi lenye mamba (jk aliwapa watu mtihani wa kutengeneza vikundi vya kijasiliamali ili wakopeshwe bila riba),kutokana na uoga wa watu hakuna alietaka kuthubutu kuvuka hilo dimbwi japo wote walitamani kumuoa mtoto wa mfalme (watu walizitamani zile fedha za jk lakini hawakuwa na mawazo ya kibiashara watazitumiaje ili warudishe deni na waendelee na biashara zao), baada ya muda mrefu na mfalme kusimama anashangaa kwanini watu wanaogopa kuvuka dimbwi la mamba wakati kuna wavuvi wanaovua kwenye ziwa ambako ndiko mamba wanapatikana, ameshapata taarifa mara nyingi watu kuua mamba pembezoni mwa ziwa ndipo akatoa muda ukiisha basi hakuna tena mtu wa kumuoa watu kuona kuna mwisho wakaanza kutoka kwa kujitoa muhanga kwa vile walihitaji kumuoa binti wa mfalme( watu walianza kukopa zile fedha hadi pale jk aliposimama na kusema watu wanalalamika hakuna pesa lakini fedha ziko kwenye serikali zao za mitaa wanatakiwa kuunda vikundi tu ili wapewe ndipo watu wakaanza kuunda vikundi vingine vikundi hewa ilimradi tu wazipate zile pesa) kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kupambana au kuvuka sehemu yenye mamba watu walikuwa wanaliwa na wale mamba lakini kuna kijana alikuwa na akili yeye alijua mamba anaona zaidi kwa pembeni hivyo alijitahidi kupita juu ya migongo ya mamba na tena kwavile watu wa kujaribu walikuwa wengi hivyo kipindi anapita kila mamba alikuwa anamtu anamtafuna akapita hivyo hivyo hadi kufanikiwa kufika ng'ambo ya pili na watu kumshangilia ( kutokana na watu kutokuwa na uzoefu wa ujasiriamali walijikuta wanaanzisha biashara lakini biashara zao hazikufanikiwa kwa sababu walikurupuka sababu walihitaji pesa na sio mtaji, lakini wapo walio ona nafasi kwa hawa wanaojaribu wao wakazifanyia kazi zile fedha kwa kuwa biashara ni kufanyia kazi makosa ya mshindani hadi wakafanikiwa) baada ya kijana kufika kwa mfalme watu alikabidhiwa mke wake kwa furaha na shangwe kubwa lakini kuna watu waliohoji kwanini mfalme atoe jaribio kalihivyo hadi familia zimepoteza ndugu na vijana wao badala ya kushangilia familia ziliondoka zimenung'unika huku wakimlalamikia mfalme kwa sababu kawapa misiba.lakini kwa familia iliyoshinda wao waliendelea kushangilia ushindi wao.( baada ya watu kuona zile fedha zilikuwa za bure bure kweli na bahati mbaya zilikuwa sio za mtu kukamatwa iwapo hautarudisha kwa wakati, watu waianza kunung'unika kwa nini zimeisha na wengi kusema zimeliwa bila kufika chini kwa walengwa, lakini kwa wale wajasiriamali waliozitumia vizuri waliendelea kusifu na kushangilia mafanikio yao kupitia fedha zile). nahisi nimeelewa kama nimepatia usisahau kulike.
 
Asante mkuu CONSULT nnafanya kazi na wajasiriamali wadogo wadogo wengi na wakubwa wachache kwa idadi isiyokuwa rasmi na siwezi kukataa kwa mtu kuipinga ila Tanzania asilimia kubwa ya wajasiriamali ni wa aina mbili.

1. Anaefanya kazi sehemu huku anatunza fedha kwa ajili ya kuanzisha kitu chake mwenyewe kwa muda mrefu hadi anapohisi sasa anahitaji kuanza kwa vile anapesa ndio anaanza ujasiriamali ( asilimia kubwa ya hawa huwa hawaendi mbali sana kiujasiriamali sababu huhisi fedha ndio tatizo katika biashara).

2.Mtu asiekuwa na kazi ila akapata semina au wazo la biashara akaanza nalo bila ya fedha, asilimia kubwa ya hawa hufanikiwa wakiwa gizani wakiingia kwenye soko au ushindani hukumbana na nguvu ya pesa huishia kurudi walikokuwa.


Huwa sipendi kulinganisha Tanzania na nchi nyingine duniani kwa sababu ukweli ni kwamba Tanzania sio kama nchi nyingine ina mifumo tofauti kuanzia utawala hadi biashara inanjia zake tofauti na zinazoeleweka kikawaida za kibiashara hadi kisiasa mfumo wote uko tofauti.

Kuhusu hadithi ( kwenye mabano ni mfano kwa tanzania)
nahisi ifanye iwe hivi baada ya mfalme kutoa donge nono kwa wananchi (mfano: Jk alivyotoa zile bilioni) ambalo lilikuwa ni binti yake watu, aliwapa watu mtihani wa kuvuka dimbwi lenye mamba (jk aliwapa watu mtihani wa kutengeneza vikundi vya kijasiliamali ili wakopeshwe bila riba),kutokana na uoga wa watu hakuna alietaka kuthubutu kuvuka hilo dimbwi japo wote walitamani kumuoa mtoto wa mfalme (watu walizitamani zile fedha za jk lakini hawakuwa na mawazo ya kibiashara watazitumiaje ili warudishe deni na waendelee na biashara zao), baada ya muda mrefu na mfalme kusimama anashangaa kwanini watu wanaogopa kuvuka dimbwi la mamba wakati kuna wavuvi wanaovua kwenye ziwa ambako ndiko mamba wanapatikana, ameshapata taarifa mara nyingi watu kuua mamba pembezoni mwa ziwa ndipo akatoa muda ukiisha basi hakuna tena mtu wa kumuoa watu kuona kuna mwisho wakaanza kutoka kwa kujitoa muhanga kwa vile walihitaji kumuoa binti wa mfalme( watu walianza kukopa zile fedha hadi pale jk aliposimama na kusema watu wanalalamika hakuna pesa lakini fedha ziko kwenye serikali zao za mitaa wanatakiwa kuunda vikundi tu ili wapewe ndipo watu wakaanza kuunda vikundi vingine vikundi hewa ilimradi tu wazipate zile pesa) kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kupambana au kuvuka sehemu yenye mamba watu walikuwa wanaliwa na wale mamba lakini kuna kijana alikuwa na akili yeye alijua mamba anaona zaidi kwa pembeni hivyo alijitahidi kupita juu ya migongo ya mamba na tena kwavile watu wa kujaribu walikuwa wengi hivyo kipindi anapita kila mamba alikuwa anamtu anamtafuna akapita hivyo hivyo hadi kufanikiwa kufika ng'ambo ya pili na watu kumshangilia ( kutokana na watu kutokuwa na uzoefu wa ujasiriamali walijikuta wanaanzisha biashara lakini biashara zao hazikufanikiwa kwa sababu walikurupuka sababu walihitaji pesa na sio mtaji, lakini wapo walio ona nafasi kwa hawa wanaojaribu wao wakazifanyia kazi zile fedha kwa kuwa biashara ni kufanyia kazi makosa ya mshindani hadi wakafanikiwa) baada ya kijana kufika kwa mfalme watu alikabidhiwa mke wake kwa furaha na shangwe kubwa lakini kuna watu waliohoji kwanini mfalme atoe jaribio kalihivyo hadi familia zimepoteza ndugu na vijana wao badala ya kushangilia familia ziliondoka zimenung'unika huku wakimlalamikia mfalme kwa sababu kawapa misiba.lakini kwa familia iliyoshinda wao waliendelea kushangilia ushindi wao.( baada ya watu kuona zile fedha zilikuwa za bure bure kweli na bahati mbaya zilikuwa sio za mtu kukamatwa iwapo hautarudisha kwa wakati, watu waianza kunung'unika kwa nini zimeisha na wengi kusema zimeliwa bila kufika chini kwa walengwa, lakini kwa wale wajasiriamali waliozitumia vizuri waliendelea kusifu na kushangilia mafanikio yao kupitia fedha zile). nahisi nimeelewa kama nimepatia usisahau kulike.


Mchango mzuri Elisha Chuma, mimi nataka kuchangia au kuongeza kwenye point zako #1 na 2 pale juu. Kwenye point ya kwanza (#1) mara nyingi watu wa namna hii huwa wanajiita wajasiliamali lakini kusema kweli ni wafanyabiashara. Mjasiriamali wa kweli hasubiri apate mtaji ndiyo atimize maono au ndoto yake. Mjasiriamali huwa anaanzisha kitu cha ubunifu na cha kipekee kufuatana na mahitaji ya wananchi au kutokana na mabadiliko ya mazingira yanayomzunguka kwa wakati ule. Kitu hiki huwa ni kipya kabisa hivyo huthubutu kuchasiri jambo ambalo hana uhakika nalo kama litakubalika na kuwa biashara ni kama kamari vile anacheza. Kwa upande mwingine na ni walio wengi ni wafanyabiashara ila wanaamua tu kujiita wajasiriamali. Mfanyabiashara ni yule anayetafuta mtaji kwa kuwa anapenzi na biashara fulani mfano ya duka la nguo au anataka kujiajili mwenye huwa anaweza kuwa hawana biashara maalum na ndiyo maana unawaona wengi anasema nina Milioni kumi na anauliza biashara gani naweza kufanya? Hivyo wanaingia kwenye jambo ambalo hajalifanyia utafiti, hajui changamoto zake na huwa hawadumu kwa muda mrefu anaangukia pua na kuamua kurudi kwenye mzingo wake wa faraja, kuajiliwa. Kwa kuongezea pia mjasiriamali muda ni muhimu mno huwezi kusema nifanye kazi nikusanye hela ndiyo nianzishe mradi au kitu fulani. Mradi wa mjasiriamali ni lazima uanze au usubiri mwingine auone na aanzishe. Ukiwa mjasiriamali utafanya kila njia inayowezekana kwenye ulimwengu huu ili ndoto yako itimie kwenye muda muafaka. Kunahitji ujasili wa kuthubutu na ukianguka unajifunza unaanza tena na mpango au azimio jipya. Lazima uvishinde viunzi kuna wakati inafikia utengano ndani ya nyumba ili mradi atimize ndoto yake sababu mwenye ndoa mwenza anakuwa kikwazo cha ndoto yake.

Kundi la pili (#2) hawa wajisirimali wanaoanguka ni wale wanaoshindwa kujitambua kuwa kitu kinapoanza kukua kinahitaji msaada na nguvu za ziada kutoka kwenye fani mbalimbali na watu wenye weredi tofauti. Hakuna binaadamu aliye mkamilifu utakuwa na mawazo yenyewe miono ya kibiashara lakini huna pesa hivyo huna budi kutafuta pesa. Ni lazima kujifanyia tathimini binafsi kujua unataka nini na mapungufu yako? Kwa mfano mtafute mwenye pesa pia utahitaji msaada wa mwanasheria kuunda uhusiano wenu au makubaliano yenu. Utahitaji mshauri wa watu wenye weredi wa mambo ya biashara wakina sisi hapo sasa. Usilale kwenye mawazo hasi kwa mfano kuwa mwenye pesa ataniibia sasa utakaposhindwa kuafikiana na pesa inabidi ujiulize nini njia mbadala. Kama hakuna njia mbadala basi huna budi kuthubutu kumchukua mwenye pesa hata kama unajua atakubadilishia kibao mbeleni. Ila hakikisha hata kabla hajakuibia unameshatengeneza pesa ya kutosha na wewe kutoka kwake. Hata ikaja siku amekuibia basi na kwakuwa wewe ni mjasiriamali hutaishiwi na fikra mpya. Kumbuka yeye ni tajiri wa pesa wewe ni tajiri wa mawazo ya miradi. Pia kwenye hatua ya pili ya mradi mpya utakuwa na pesa na mradi mpya na ndivyo unavyozidi kusonga mbele. Kumbuka siku zote kwenye biashara kuna kupata na kukosa songa mbele usiangalie nyuma jifunze kwenye kila hatua unayopiga. Kuna mengi nadhani haya ni makosa ya wengi wanakuwa wanafanya kwa wale wanaoingia kwenye soko la ushindani.
 
wakuu nawashukuru sana wote ELISHA CHUMA na EWGM's kumbe humu jf tuna wataalam wazuri sana na wazoefu na ujuzi/maarifa yanayoweza kujenga mtu kifedha na pia elimu kwa haraka sana, imefikia wakati natamani sana tufahamiane zaidi kwani nahisi tukiwa watatu au zaidi kwa pamoja tunaweza kufanya kitu cha nguvu sana ok naomba tuendelee kuwasiliana zaidi, mm binafsi ni Mjasiriamali/Mfanyabiashara 20 yrs +
 
Hadithi yako haina tofauti na mkasa wa Ben Carson, M.D. aliekuwa akipata zero na kuchukiwa darasani na nyumbani ila alisukumwa na mama yake [Sonya] na kuwa Mtu wa ajabu kabisa ulimwenguni.
namfananisha na avatar yako.
 
Hadithi yako haina tofauti na mkasa wa Ben Carson, M.D. aliekuwa akipata zero na kuchukiwa darasani na nyumbani ila alisukumwa na mama yake [Sonya] na kuwa Mtu wa ajabu kabisa ulimwenguni.
namfananisha na avatar yako.

Shukrani mkuu kwa utafiti wako wa kina, je nini unapunguza au kuongeza ? ?
 
Jamani ndugu zangu mimi nina fremu duka kubwa lkn sijui niweke biashara gani msaada wenu plz
 
Asante mkuu CONSULT nnafanya kazi na wajasiriamali wadogo wadogo wengi na wakubwa wachache kwa idadi isiyokuwa rasmi na siwezi kukataa kwa mtu kuipinga ila Tanzania asilimia kubwa ya wajasiriamali ni wa aina mbili.

1. Anaefanya kazi sehemu huku anatunza fedha kwa ajili ya kuanzisha kitu chake mwenyewe kwa muda mrefu hadi anapohisi sasa anahitaji kuanza kwa vile anapesa ndio anaanza ujasiriamali ( asilimia kubwa ya hawa huwa hawaendi mbali sana kiujasiriamali sababu huhisi fedha ndio tatizo katika biashara).

2.Mtu asiekuwa na kazi ila akapata semina au wazo la biashara akaanza nalo bila ya fedha, asilimia kubwa ya hawa hufanikiwa wakiwa gizani wakiingia kwenye soko au ushindani hukumbana na nguvu ya pesa huishia kurudi walikokuwa.


Huwa sipendi kulinganisha Tanzania na nchi nyingine duniani kwa sababu ukweli ni kwamba Tanzania sio kama nchi nyingine ina mifumo tofauti kuanzia utawala hadi biashara inanjia zake tofauti na zinazoeleweka kikawaida za kibiashara hadi kisiasa mfumo wote uko tofauti.

Kuhusu hadithi ( kwenye mabano ni mfano kwa tanzania)
nahisi ifanye iwe hivi baada ya mfalme kutoa donge nono kwa wananchi (mfano: Jk alivyotoa zile bilioni) ambalo lilikuwa ni binti yake watu, aliwapa watu mtihani wa kuvuka dimbwi lenye mamba (jk aliwapa watu mtihani wa kutengeneza vikundi vya kijasiliamali ili wakopeshwe bila riba),kutokana na uoga wa watu hakuna alietaka kuthubutu kuvuka hilo dimbwi japo wote walitamani kumuoa mtoto wa mfalme (watu walizitamani zile fedha za jk lakini hawakuwa na mawazo ya kibiashara watazitumiaje ili warudishe deni na waendelee na biashara zao), baada ya muda mrefu na mfalme kusimama anashangaa kwanini watu wanaogopa kuvuka dimbwi la mamba wakati kuna wavuvi wanaovua kwenye ziwa ambako ndiko mamba wanapatikana, ameshapata taarifa mara nyingi watu kuua mamba pembezoni mwa ziwa ndipo akatoa muda ukiisha basi hakuna tena mtu wa kumuoa watu kuona kuna mwisho wakaanza kutoka kwa kujitoa muhanga kwa vile walihitaji kumuoa binti wa mfalme( watu walianza kukopa zile fedha hadi pale jk aliposimama na kusema watu wanalalamika hakuna pesa lakini fedha ziko kwenye serikali zao za mitaa wanatakiwa kuunda vikundi tu ili wapewe ndipo watu wakaanza kuunda vikundi vingine vikundi hewa ilimradi tu wazipate zile pesa) kutokana na kutokuwa na uzoefu wa kupambana au kuvuka sehemu yenye mamba watu walikuwa wanaliwa na wale mamba lakini kuna kijana alikuwa na akili yeye alijua mamba anaona zaidi kwa pembeni hivyo alijitahidi kupita juu ya migongo ya mamba na tena kwavile watu wa kujaribu walikuwa wengi hivyo kipindi anapita kila mamba alikuwa anamtu anamtafuna akapita hivyo hivyo hadi kufanikiwa kufika ng'ambo ya pili na watu kumshangilia ( kutokana na watu kutokuwa na uzoefu wa ujasiriamali walijikuta wanaanzisha biashara lakini biashara zao hazikufanikiwa kwa sababu walikurupuka sababu walihitaji pesa na sio mtaji, lakini wapo walio ona nafasi kwa hawa wanaojaribu wao wakazifanyia kazi zile fedha kwa kuwa biashara ni kufanyia kazi makosa ya mshindani hadi wakafanikiwa) baada ya kijana kufika kwa mfalme watu alikabidhiwa mke wake kwa furaha na shangwe kubwa lakini kuna watu waliohoji kwanini mfalme atoe jaribio kalihivyo hadi familia zimepoteza ndugu na vijana wao badala ya kushangilia familia ziliondoka zimenung'unika huku wakimlalamikia mfalme kwa sababu kawapa misiba.lakini kwa familia iliyoshinda wao waliendelea kushangilia ushindi wao.( baada ya watu kuona zile fedha zilikuwa za bure bure kweli na bahati mbaya zilikuwa sio za mtu kukamatwa iwapo hautarudisha kwa wakati, watu waianza kunung'unika kwa nini zimeisha na wengi kusema zimeliwa bila kufika chini kwa walengwa, lakini kwa wale wajasiriamali waliozitumia vizuri waliendelea kusifu na kushangilia mafanikio yao kupitia fedha zile). nahisi nimeelewa kama nimepatia usisahau kulike.
Penda sana like eeh
 
Back
Top Bottom