Utajiri wa Magofu ya Rapta

Too selfish, lack of appreciation, too biased, negative minded. Shame on you idiot!!
Verry well to tell him. Wazee wa raphta tumekuja .tuone ni nini jamaa atasema kuhusu raphta tuangalie na chami amesema nini tujue wadau tunasoma. .ila kwa vile muandish ameanzia mbali na sisi tunavuta subira kuiendea raphta.navutiwa na stor za jamaa na ving anavosema mfano majina ya sehem kweli yapo.
 
Umetisha Sana mzee, uandishi ulotukuka hakika. Kila la kheir
 
Duuuh
Hii ndio shida kubwa ya simulizi za Jamii forums. Huwa zina chelewa hadi mzuka wa kuifatilia tena unakata[emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]
 
Siku hiyo kwangu ilikua ni kama orientation tu Kwani kama nilienda kujifunza ni kwa namna gani nitakua naifanya kazi hiyo. Ilikua tofauti kabisa na wenzangu ambao nilipishana nao njian wakati naludi camp, wao walionekana kuchoka zaidi kulingana na nature ya kazi walizokutana nazo.

Tukiwa njiani nilikua na mengi sana ya kumuuliza Javier hivyo nilisubiri tufike room na kutulia ndipo nimshushie mvua ya maswali. Maswali mengi yalihusu maisha ya Manuela na Catarina, lakini pia yalihusu malipo yetu maana toka tunafika hapo sikuona dalili ya cashier wala accountant ambaye anaweza kushughulika na malipo yetu.

Maswali mengine yalihusu huduma za msingi hususani huduma ya afya na mwisho kabisa ilikua inamuhusu yeye ni kwa namna gani ata nisaidia na mimi kupata share ya msosi kama anaopata yeye.

Tukiwa njiani tunatembea Javier hakua muongeaji kabisa hivyo tulikua kimya njia nzima huku speed ya Javier ya kutembea ilinifanye niwe kama na kimbia wakati ye anatembea.

Ilikua ngumu sana kukuta gari eneo hilo na kiukweli sikuona gari kabisa, wageni na wamiliki wa shamba hilo hufika apo kwa helicopter kwani hata njia ya maji ilikua haipitiki kwa sababu mto haullaga haukua navigable river ( mto ambao hauwezi kutumika kwa usafiri). Mto huu wenye urefu wa zaidi ya miles 700 kwa sehemu kubwa sio navigable kwa sababu ya uwepo wa makorongo kwenye baadhi ya sehemu

Asilimia kubwa ya wafanyakazi wa eneo hili walikua ni waraibu wa either pombe au cocaine hivyo inapofika mida ya jioni. Wengi huwa wapo bize kwenye vilevi vyao au starehe zao wakijisahaulisha shurba zote za mchana.


Hivyo basi jioni hiyo ilikua kila kona ya kambi hiyo kuna watu au mtu mmoja akipata either pombe au unga. Uzuri wa mashamba haya kila mtu anapata huduma ya msingi kutoka kwa mkubwa wake wa kazi, kila kitengo kilikua na supervisor ambaye alihakikisha anaowasimamia wanapata haki zote za msingi.

Jamaa ambao nili report nao mashambani hapo walionekana kama wananionea wivu kwa position niliyowekwa. Na mimi nilishindwa kuelewa, je! Pale nilipopangwa ndio sehemu nilitakiwa kufikia au ni favour tu kutoka kwa baba yake na Miguel.

Tulifika room kwa ajili ya kupumzika kutokana na kauchovu ka siku nzima lakini ilikua tofauti kidogo kwa Javier. Yeye hakukaa kabisa hivyo aliniaga anatoka atarudi baada ya muda hivyo mimi naweza kupumzika tu.


Hapo niliona kabisa yale maswali yangu niliyopanga kumuuliza yanaweza yasijibiwe kabisa, na yeye nadhani alilijua hilo na wakati anaondoka alisema kama atarudi nikiwa sijalala nitauliza chochote ambacho nahisi hakipo sawa.

Aliondoka na kuniacha peke yangu ndani ya room ile ambayo ilikua juu kabisa kwenye ki ghorofa cha mbao. Nilijitahidi nisilale ili anaporudi niweze kuongea nae mambo kadhaa ambayo mpaka wakati huo yalikua yanasumbua sana akili yangu.

Sikuweza kufahamu anaelekea wapi na wala sikutaka kumuuliza swali la kipumbavu kama hilo kwa mtu mzima kaka yeye ambaye alikua ni mwenyeji wangu maeneo hayo. Nikiwa nimejipumzisha nilitafuta kitu cha kunisaidia kupoteza muda ilinisipotelee kwenye usingizi kwakua nilihitaji kuongea na Javier.


Nilikumbuka kwenye kitanda cha Javier niliwahi kuona bible, nilijisogeza kwenye kitanda hicho iliniichikue kwa dhumuni la kupitisha macho kwenye baadhi ya chapter. Nilikua na miaka kadhaa sijawahi kushika bible, last time ilikua kwenye mafunzo ya kipaimara 2004 baada ya hapo sikumbuki kama niliwahi kushika bible au kwenda tena kanisani.

Sikuhiyo nimeishika ata sikujua nianzie wapi lakini pia nilijiuliza imekuaje Javier anasoma bible akiwa eneo lenye kila aina ya ouvu ama lile. Hapo niliamini kuna mengi yanamuhusu Javier ambayo siyajui na napaswa kuyajua taratibu.

Ndani ya bible nilikuta passports ( hati za kusafiria) na passport zile zilikua mbili huku zikiwa na majina tofauti moja ya Iran na nyingine Ilikua ya German citizenship. Hapo niligundua kuwa javier alikua na uraia wa ujanja ujanja wa nchi mbili lakini kimuonekano hakufanana na wajermani kabisa alikua na muonekano wa ki-Asia.

Wakati nanyanyua bible ile kwenye kitanda nilikuta message pia chini ya ile bible, message ile ilikua ni karatasi iliyoandikwa kwa peni nyeusi maandishi ya herufi kubwa MEET ME BY SHARMAHD.

Kwa haraka nilijua Javier safari yake hiyo ya dharula alienda kukutana na mtu anayeitwa sharmahd. Lakini pia nilijiuliza imekuaje Javier akawa pale na passport zake wakati sisi wengine tuliziacha Cabo de la vela.

Huyu sharmahd ni nani? Nilijiuliza pia kwanini Javier ana free entry na exit kwenye maeneo yote kuzunguka camp. Nikaongezea na swala la Javier kua na misosi mizuri yaani anakula anachokitaka.

Kuna muda niliwaza au na yeye ni moja ya supervisors wa eneo hilo lakini hajaamua kutuweka wazi, niliwaza hivyo kwani ata utendaji wake wa kazi ni wa kivivu nikirejea maneno ya Catarina.

Akili akaniambia Kama nahitaji kutoka apo basi natakiwa kuishi vizuri na Javier lakini pia kuwa loyal sana kwa kila maelekezo anayonipa. Niliamini kama nitaanza kuelezea ni namna gani sijaridhika kuwepo hapo anaweza kunipa msaada wowote wa namna ya kutoka.

Kilichonishangaza zaidi Kuhusu Javier hakufanana kabisa na viongozi wengine wa eneo hilo kama Miguel, baba yake Miguel na Daniel. Hawa walikua na muonekano wa kihuni wakiwa na tattoos nyingi lakini pia wakatili na watumiaji wa mihadarati.

Niliamua kurudisha kilakitu kama kilivyokua na kujilaza kitandani nikiendelea kutafakari mambo mengi. Sana sana niliwaza kuhusu pesa ambayo ndio ilinipelekea mimi kufika hapo, niliwaza kuhusu pesa kwa sababu sikuona dalili yoyote ya kulipwa kwa wafanyakazi wa eneo hilo hivyo nilipania sana kumuuliza Javier Kuhusu hilo.

Javier alirudi baada ya masaa matatu hii ilionesha ni kwa namna gani alikua na maongezi marefu na sharmahd ambaye sikuweza kumfahamu ni nani. Niligundua amerudi baada ya kuniamsha na kunipa chakula ambacho kilikua ni samaki mkubwa aliyeokwa.

Alisisitiza tu kama naweza kuendelea kula, kwani yeye ameshapata chakula alipotoka. Nilitamani kumuuliza alienda wapi lakini niliona ni swali ambalo halina maana.

Wakati naendelea na msosi sikutaka kumwambia chochote kama niliona nini kwenye bible yake. Sikutaka ajue kama nilichunguza vitu vyake baada ya yeye kutoka.

Javier aliuliza kama nina lolote nahitaji kujua mpaka muda huo kwani aligundua sura yangu inaonyesha nina mengi sana nahitaji kuyajua mpaka muda ule.

Swali la kwanza lilikua ni tunalipwaje kwa hizi kazi tunazofanya, kwani sijaona sehemu yoyote nikiulizwa account number au nikifanya bargain ya mshahara. Niliuliza hivyo lakini pia nilimuuliza yeye toka afike hapo analipwaje?

Javier aliuliza na yeye kwa kurudisha swali tena kwangu, aliuliza kama nimeona dalili yoyote ya wafanyakazi wale wa pale kulipwa.

Kwakweli hakukua na dalili yoyote ya kuonyesha kama wafanyakazi wale wanalipwa kwa kufanya kazi eneo lile.

Basi Javier aliniambia hakuna malipo ya kazi ninapo kua eneo lile, zaidi ni kwamba aliyelipwa ni wakala aliyenifikisha pale.

Hapa niliuliza wakala wangu ni nani kati ya McKenzie na Miguel.

Kwa mujibu wa Javier, wakala wangu alikua ni McKenzie kwani yeye ndio mara nyingi anahusika na kuhakikisha kwenye mashamba hayo kunakua na constant supply of labour.

Hivyo alieyelipwa ni McKenzie na timu yake, aliendelea kusema wale wote tulio report jana yake lilikua ni deal la McKenzie na mpunga wote umeingia kwenye account ya McKenzie.

Aliendelea kusisitiza hakuna namna naweza kutoka hapo kwani kuna ulinzi mkali na bado hakuna kiongozi yoyote mkubwa eneo hilo zaidi ya vibaraka tu ambao ni kina Miguel na Daniel.

Wamiliki wa mashamba hayo wapo mji Lima na wengine wapo united states na hakuna anaewajua ata wao kina Miguel hawana link na uongozi wa juu wa hapo.

Kwa upande wake na yeye alisema hakuwahi kulipwa chochote na wakati anajibu hili swali la Upande wake alikua anajikunja kuingia kwenye shuka. Hii ilimaanisha hayupo tayari kuendelea kuongea zaidi, lakini alisema kama nahitaji kutoka hapo basi niendelee kuwa positive.

Asubuhi ya siku hiyo tuliamka mapema sana na Javier kama kawaida yeye ndiye alikua wa kwanza kuamka. Tuliamka mapema zaidi kuliko ilivyokua jana yake, na na kulingana na javier ni kwamba sikuhiyo kulikua na kazi nyingi kwani walitarajia kuanza kuzalisha siku hiyo.

Hivyo tulitoka mapema zaidi kuliko wengine wote, na siku hii nilipewa koti kubwa alilokua analitumia Gatkuoth kwenye nyakati za baridi kali kama hizo. Tulitembea kwa speed sana kama ilivyokawaida ya bwana Javier alikua na hatua kubwa mno kama sio mtu wa Asia vile.

Tukiwa njiani nilimuuliza vipi kuhusu Catarina na Manuela wao wanaweza kuwa wameamka muda huo kwani ilikua mapema sana.

Javier alinijibu kuwa wale ndio huamka mapema zaidi kwani wao ndio engine ya ile maabara yaani yeye ata akiwahi vipi hawezi fanya lolote zaidi ya kusubiri maelekezo yao.

Aliendelea kusema kwa anavyoniona mda si mrefu nitakua pro au nitakua bingwa kwa upande wa maabara kitu ambacho Catarina amefurahi sana kupata mtu wa kusaidiana nae majukumu.

Javier alisisitiza pia nisijaribu kuweka mazoea yoyote na Manuela kama nataka kuendelea kufanya kazi kwa amani nikiwa eneo hilo. Apo nilikumbuka jana yake wakati manuela anakagua ile copper bracelet ambayo alihisi ni ya Gatkuoth na Javier akaingilia maongezi.

Javier alisema kuna kila sababu ya kuamini kuwa Catarina na Manuela wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Hivyo akijitokeza mwanaume yoyote kuweka mazoea na Manuela lazima atajijengea chuki ya hali ya juu na Catarina.

Javier aliendelea kusema inaonekana dhahiri kuwa Catarina Alikua na tabia hiyo kabla hajafika eneo hili la haullaga valley. Lakini kwa upande wa Manuela hakua tayari na wala hakuwahi kujihusisha na tabia hizo hapo awali.

Hivyo kinachomfanya Manuela kuvumilia au kuendelea kushiriki mapenzi hayo ni kwa vile hana namna ya kujitoa kwani Catarina ndio amekua msaada wake.

Ilionekana Manuela alikua ana kesi kubwa ya uhalifu uko mjini Rio de Janeiro na alikimbilia huko kama mafichoni hivyo hakua na chakufanya Zaid ya kumsikiliza Catarina tu.

Hata Javier alipogundua hilo alianza kuweka umbali na kuacha mazoea na Manuela ambaye anaonekana kua na shida sana ya mwanaume kwani hakua akiridhika na alichokua akifanya na Catarina.

Aliendelea kwa kusema kuna uwezekano mkubwa kwamba Catarina alihusika na kifo cha Gatkuoth, japo Gatkuoth alikua mraibu mkubwa wa unga na aliyepitiliza. Hivyo wengi waliamini Gatkuoth kafa kwa ku overdose cocaine lakin Javier baada ya kuuchunguza mwili wa Gatkuoth aligundua alipewa sumu aina ya strychnine.

Strychnine ni sumu inayotoka kwenye mmea wa strychnos nux-vomica ambao hupatikana sana maeneo ya kusini mwa Asia kwa vile India, Sri Lanka, East indies pamoja na Australia.

Mara nyingi watumiaji wa cocaine husababishiwa kifo kwa kuchanganyiwa sumu hii ndani ya unga. Lakini pia Javier aligundua uwepo wa sumu hiyo kwenye maiti ya Gatkuoth kwa sababu, mwili wa marehemu ulikua na viashiria kama vile taya kukaza sana, miguu na mikono kuwa migumu kuliko kawaida.

mtu pekee anaeweza kuipata sumu hiyo alikua ni Catarina Kwani yeye alikua ndio mmiliki wa kila chemical iliyokuwepo ndani ya maabara. Hivyo Catarina alihusika na kifo cha Gatkuoth Kwa sababu tu ya wivu wa mapenzi Kwa mantiki hiyo natakiwa kuwa mbali na Manuela ambaye anaonekana kua horn sana.

Kwa maelezo ya javier Catarina alifika hapo mwaka 2008 akitokea kwenye kundi moja maarufu nchini Colombia linalojulikana kama NORTE DEL VALLE CARTEL (north valley cartel).

Catarina alifika hapo baada ya kukamatwa kwa kiongozi wao aliejulikana kama JUAN CARLOS RAMIREZ ABADIA ambaye alikamatwa august 7 2007 huko jijini Sao Paulo Brazil. Kukamatwa kwa Juan Carlos kulifanya shughuli nyingi kusimama na hapo ndipo Catarina akatimkia haullaga.

Mwanzo alifika maabara kama mfanyakazi wa kawaida akisaidia shughuli za maabara kama mimi. Lakini baada ya uzoefu aliyekua mtaalamu wa mwanzo alihamishiwa Colombia na yeye rasmi akawa ndio lab technician.

Baadae nakuja na historia fupi ya JUAN CARLOS RAMIREZ ABADIA
 
Siku ile asubuhi asubuhi tukielekea lab (maabara) nilipata historia fupi iliyomuhusu Catarina. Hapo sasa nilipata picha japo kwa uchache nimeweza kuijua background ya Catarina.

Lakini kwa upande wa Manuela ilikua ngumu kwani ilionekana kabisa ata Javier mwenyewe hakujua chochote kuhusu background ya Manuela.

Tulipofika lab (maabara) ilikua ni asubuhi sana lakini Catarina na mwenzie walishafika hapo mapema sana wakiendelea na maandalizi mengine. Na sisi bila kuchelewa tulijiunga kuendelea na majukumu ili kuhakikisha tunata products kwa wakati.

Mimi na Javier tulianza kwa kusafisha zile drums au mapipa yaliyokua yamekatwa eneo la mfuniko. Mapipa haya yalikua muhimu sana kwenye hizi hatua za mwanzo za kuchakata koka.
Zoezi letu lilianza kwa kutoa yale mapipa yote na kuyapeleka eneo la nje kwa ajili ya kuyafanyia usafi. Wakati huu Catarina na mwenzie wao walikua ndani ya lab wakiendelea na shughuli nyingine.

Nikiwa nje na javier Catarina aliniita kisha akasema yupo kwenye stage muhimu sana ya maandalizi hivyo napaswa kuwa hapo ili nijifunze. Kwa maana hiyo hakutaka niendelee kukaa na Javier kule nje bali niingie ndani ili kujifunza cha kufanya wakati wa maandalizi.

Niliingia ndani na kukaa karibu na meza ile kubwa tayari kwa kutuzama mkemia Catarina akifanya mambo. Tukiwa hapo aliomba atoke anaenda kuchukua baking soda, hii ilikua very important kwenye hizi stages za mwanzo wakati unaandaa coca paste ili baadae kupata cocaine hydrochloride.


Baada ya Catarina kuondoka, Manuela alisogea nilipo na kuanza kuniongelesha. Hapa nilikumbuka kauli ya javier, kwamba kama nahitaji kuwepo pale maabara na kuendelea kufanya kazi kwa Amani basi nijiwekee mipaka kwa binti huyo.

Nilikumbuka maneno ya Javier kuhusu kifo cha Gatkuoth ambacho anadai Catarina alihusika kwa kutumia strychnine.

Wakati huu nilitamani ata kumfukuza Manuela asinisogelee kabisa, kwanza hakua na mvuto ata kidogo kimoyomoyo nilijiambia ata akinivulia nguo siwezi fanya chochote.

MANUELA: How was your first night at camp?
Did you enjoy sleep?
( Usiku wako wa kwanza kambini ulikuaje? Vipi ulifurahia usingizi)

MIMI: I couldn't
( Hapana sikufurahia kabisa)

MANUELA: what was the problem? Did javier left
You alone
(Tatizo lilikua nini? Au Javier alikuacha peke ako)

MIMI: no!!! it was cold and cold, Sorry can I find a way to escape here?
( Hapana baridi lilikua kali sana, Samahani hivi naweza pata njia ya kutoroka hapa)

MANUELA: why so early
(Mbona mapema sana)
MANUELA: Don't worry I'll help you, we'll talk later
( Usijali nitakusaidia nitafute baadae)

Kwa mbali nilimuona catarina akija na container ndogo ya chemicals, Ndani ya container ile kulikua na alkaline material (baking soda) wakati huu Manuela alibadirisha maongezi ghafla.
Manuela aliniagiza nikachukua benzol na maji nivilete maeneo ya karibu kwani vyote hivi vilihusika kwenye mchanganyo wa kwanza.

Hapo Manuela alinifurahisha kwani aliigiza as if hatukuongea chochote na tulikua bize na kazi. Lakini wakati naongea na Manuela niligundua kitu cha tofauti kabisa.

Manuela alikua serious sana na hakuonyesha dalili ya uteja kabisa alinihoji kama mtu mwenye akili timamu huku macho yake yakiniangalia kwa namna kama anatafuta kitu kwenye akili yangu.

Nilijiambia lazima nimtafute baadae, anaweza kunisaidia kujua namna gani naweza kuondoka ndani ya eneo hili sitakiwi kumzalau kabisa.

Lakini kingine watu hawa walizidi kunichanganya sana, mpaka wakati huo nilishindwa kumuelewa Javier na sasa hivi nashindwa kumuelewa manuela.

Kwenye hatua ya kwanza ya kutengeneza paste hua tunachanganya majani hayo yaliyopondwa pamoja na alkaline material ambayo Catarina alikuja na baking soda.

Lakini ukikosa baking soda unaweza kutumia sodium bicarbonate kwenye mchanganyo huo wa kwanza.

Baada ya hapo unachanganya na maji pia, wakati huu yale mapipa yaliyokatwa kwenye mfuniko ndio yalikua yanafanya kazi sasa.

Hatua hii ya kwanza hua haifanywi kwa haraka kwani zipo maabara zinazotumia mpaka siku tatu na wengine masaa kadhaa kuandaa paste. Hapa inategemea technology ya maabara husika lakini pia kiwango cha majani kilichopo.
Zoezi lilikua gumu kwani niliona kabisa idadi yetu kama ilikua haitoshi kulingana na energy tunayotumia pale. Maana kwenye kazi za nguvu sana sana ni mimi na javier ndio tulikua nguvu na kidogo Catarina lakini Manuela hakuweza kazi ngumu kabisa.

Baadae Catarina alikuja na mafuta ya taa, watu wa chemistry tunajua kama mafuta ya taa ni organic solvents. Sasa hapa zile alkaline material zinafanya cocaine alkaloids zilizopo kwenye majani ya koka kuwa extracted kwenye mafuta ya taa.

Daaaaah!!!! Tutasameheana najitahidi sana pia najaribu kutumia lugha rahisi Lakini bado naona wanangu wa HKL nawavuruga. Na sio wa HKL ata wale waliosoma chemistry kwa kukalili Nadhani mnatoka patupu.

Twendeni mdogo mdogo, ni hivi apa tunadili na alkaline material ( kiswahili chake sijui) pia tunadili na organic solvents ( pia kiswahili chake sijui) mwisho tunaweka na maji. Dhumuni la kufanya hivi ni ku extract ile cocaine ambayo ipo kwenye majani.

Kama tunakumbuka nilisema kiwango cha alkaloids cocaine kwenye majani ndio huthibitisha ubora wa majani hayo.

Sasa hii alkaloids cocaine hupatikan kwenye mimea inayoitwa erythroxylon plants, hii mimea ipo mingi lakini species kuu mbili ndio hutoa cocaine alkaloids nyingi nayo ni:-

I)erythroxylon coca na
II)erythroxylon novogranatense --

Hizi zote hupatikan sana maeneo ya chini kuzunguka safu za Andes principally in Peru, Bolivia, and Colombia.


Ukitaka kujua changamoto ya lugha ya kiswahili jaribu kuelezea matukio ya kisayansi ambayo hayana tafiri ya kiswahili.

Ndio maana wengi husema kiswahili ni lugha changa sana inahitaji kukua zaidi kuendana na technology. Mfano maneno mengi ya kitechnolojia hayapo kwa kiswahili. Mara nyingi BAKITA wanajitahidi kubumba bumba tu, utaskia oooh!!! Kimemeshi, mara tarakirishi mara tarairishi mpakato. Ebu tuyaache hayo.

Naomba nijaribu kwa kiswanglish tuone kama Hatua mambo yataenda
Hatua inayofata baada ya ile pale juu,
Cocaine alkaloids are extracted from the kerosene (mafuta ya taa) into a dilute acid solution.

Alkaline material (sodium carbonate) is added to the remaining solution which causes a precipitate to form. An acid and the water are drained off and the precipitate is filtered and dried to produce coca paste, off-white to light brown,

Hii coca paste ipo kama puti kwa wale walipita pita kwenye ufundi tutaelewana apa

Baada ya hapo tunakua tumemalizana na coca paste kinachofata hatua nyingine ni ku convert coca paste kwenda kwenye cocaine base.

Hapa tuliona tupate break kidogo hivyo tulienda zetu nje kwa ajili ya misosi. Catarina na Manuela waliongoza kwenye nyumba yao huku mimi na Javier tulibaki nje tunapunga hewa safi ya mto haullaga.

Wakati tunatoka Manuela alinisogelea na kutamka maneno mawili tu " keep promise".

Hapo nilijiuliza mimi ndio mwenye shida na nimemuomba anisaidie namna ya kutoroka kwenye maeneo haya. Lakini yeye ambae anahitajika kutoa msaada ndie anasisitiza nitimize ahadi ni wazi na yeye anajambo lake.

Na jambo lake si lingine litakua lile lile aliloniambia javier napaswa kua makini yote hayo yalikua ni mawazo yangu wakati huo.

Tukiwa nje tunasubiri, nilimuuliza javier kuhusu kisa cha JUAN CARLOS RAMIREZ ABADIA kwani hakua amenisimulia nilitaka afanye hivyo ili at least tusogeze muda.

Ila javier alionekana kuwa na njaa sana so mpaka muda huo hakuwa tayari kunieleza chochote mpaka atakapo shiba. Aliniambia kama ana njaa hawezi fanya lolote wala hatoweza kunisimulia vizuri na nikamuelewa.

Hapo nilikumbukua maneno ya Catarina kwamba Javier yupo punctual sana wakati wa misosi kuliko chochote kile.

Javier aliomba tusimame twende kulekule kwenye nyumba anayoishi Catarina na Manuela kwani wanakawaida ya kuchelewa sana wakiingia ndani humo. Hivyo wa kuwasubiri pale wanaweza kutuweka mda mrefu na njaa.

Kwa utani javier alisema wale wadada wakiingiaga ndani lazima wapige ata kimoja kwanza ndio wanaandaa msosi.
Wakati tunatembea Javier alihoji kwanini natamani sana kujua kuhusu Juan Carlos.

Nilimjibu kuwa binafsi napenda wapambanaji na ma hustlers wanaotafuta hela au utajiri kwa namna yoyote.

Javier aliuliza je nahitaji kuwa tajiri??
Bila shaka nilijibu ata kilicho nipeleka huko ni hizohizo harakati za kutafuta utajiri.

Javier alicheka sana na kisha akaniambia mbona utajiri umeuacha East Africa, nilimuuliza kivipi akasema atanipa story ya babu yake ambae aliniambia kuwa babu huyo aliishi mkoa wa Lindi.

Nilimsisitiza Javier kuwa namdai mambo mawili, jambo la kwanza ni kuhusu mzee wake ambae anadai aliishi bongo kabla ya uhuru na jambo lingine kuhusu Juan Carlos.

Kwa hakika javier alikua na mambo mengi anayoyajua hivyo kukaa naye nikinufaika na mengi.

Kuhusu juan Carlos na cartel yake ya kuuza madawa
Javier alinieleza kwa ufupi sana kuhusu jamaa huyo ambae ndie alipelekea Catarina kufika hapo.
Kilichonifurahisha kwenye story ya Juan Carlos ni namna alivyofanya plastic surgery na kubadili muonekano wake.


JUAN CARLOS RAMIREZ ABADIA
Picha ya Kabla na baada ya plastic surgery alivyofanya juan ili kubadili muonekano wake.

 
Ebwana kwa wale ambao wanahitaji simulizi ikimbilie rapta naomba tuwe na subira, kuna mengi ya kujifunza kabla ya kufika rapta.

Simulizi imepewa title ya rapta kwakua huko ndiko lengo letu kuu lilipo na tutaona mengi yanayohusu rapta apo baadae. Kwasasa tuyajue machache ili tupunguze maswali hapo baadae.

Wale wanaotumiwa PDF WhatsApp Nadhani wameanza kusikia machache yanayohusu mji wa rapta

(0623 329512 Whatsapp)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…