Utajiri wa Magofu ya Rapta

Utajiri wa Magofu ya Rapta

Kuna mambo mengi sana yalinishangaza yanayomuhusu Javier, kwanza Javier alikua smart sana kwenye mambo kadhaa. Mfano, alikua smart kwenye maongezi yaani kila anachoongea kina maana na logic pia. Javier hakua muongeaji sana ila ni wale watu ambao wakianza kuongea huchoki kuwasikiliza.

Javier hakua mtumiaji wa mihadarati wala aina yoyote ya madawa ya kulevya. Kitanda anacholala Javier kilikua kimetandikwa muda wote tofauti na kile kitanda nilicholala kilikua rough sana.

Mtu Yoyote asinge gundua u smart wa Javier kwa kumuangalia mara moja tu, kwani kilichokua kinaficha utanashati wake ni zile nywele ndefu pamoja na ndevu zilizoonekana kuwa hazikuchanwa kwa zaidi ya miezi 12.


Kuhusu bwana Javier, Kwa maumbile ya nje ukimuona unaweza kuhisi ni mtu Fulani legelege au dhaifu na asiye na afya. lakini binafsi nilikanusha hilo baada ya kukaa nae muda usiopungua masaa matatu tukiongea mambo kadhaa.

Nilimuuliza swali Kuhusu uwepo wa baadhi ya vitu nilivyoviona juu ya kenchi eneo ambalo kitanda changu kilikuwepo.

Kwa mujibu wa maelezo yake vitu hivyo vilikua mali ya muafrika mwenzangu ambaye alikua anatumia kitanda hicho nilicholala kabla sijafika.

Nilimuuliza pia vipi kuhusu muafrika huyo je! Aliondoka eneo hilo?

Javier alitabasamu kidogo kisha akaniambia kwenye akili yangu nisahau kabisa kuhusu kutoka eneo hilo. Kwani kuna wengi walikuwepo hapo wakiwaza kurudi nyumbani baada ya ku accumulate kiasi fulani cha pesa lakini ilishindikana na wakafia hapo.

Hapo niliuliza je! Tunazuiliwa kutoka baada ya kuingia humu au inakuaje?
( binafsi Nilihisi tunazuiliwa kutoka baada ya kuingia, maana eneo hilo kulikua na ulinzi mkubwa japo haikua rahisi kuona kwa macho)

Kwa maelezo ya Javier ni kwamba hawakuzuii physically bali psychologically,
Sikumuelewa kabisa alimaanisha nini na yeye alisema nitaelewa baada ya muda. Kwakua nimefika hapo bado nina ugeni hivyo siwezi kuelewa kilakitu kwa wakati mmoja.

Aliendelea kwa kusema kuna kijana ye alimkuta hapo alikua akiitwa Gatkuoth, Gatkuoth kwa Miaka kadhaa alikua na ndoto ya kufika hapo kisha kukusanya pesa na kurudi nyumbani kwao lakin kwa bahati mbaya umauti ulimkuta akiwa hapohapo huku ndoto za kurudi nyumbani zikiishia hewani.

"Gatkuoth ndiye kijana wa kiafrika aliyekua anatumia kitanda hicho ulicholala" aliongea Javier
Alikua ni kijana mweusi sikuwahi kupata kuona mweusi wa rangi ile hapo kabla japo nimekutana na vijana weusi kadhaa kwenye maisha yangu ila Gatkuoth alizidi.

Nilikutana na vijana weusi maeneo tofauti tofauti ya dunia hii kama vile Quebec na wengine California ila hawakumfikia Gatkuoth. Ukiachana na rangi Gatkuoth pia alikua mrefu nadhani alifikia 7ft, tulithibisha hilo wakati tunajiandaa kuzika mwili wake.

Baada ya kukaa nae kwa muda mrefu nilipata kuyajua mengi kuhusu Gatkuoth, kwanza nilifanikiwa kujua kua Gatkuoth alikua anatokea South Sudan Western Bahrel Ghazal.

Javier aliendelea kusema "naomba nikueleze kila kitu kuhusu kijana mwenzio wa Africa ili na wewe yasije yakakukuta yaliyomkuta. Na kisha ndoto zako zikaishia hapa. Sababu unaonekana kua Innocent na umekuja bila kujua nini kinaendelea apa UHV"

Maisha ya Gatkuoth yalianza kua magumu alipofikia umri wa miaka 16 baada ya kupoteza wazazi wote wawili April mwaka 2003. Alipoteza wazazi kwenye machafuko huko magharibi mwa Sudan (Darfur) wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Kwakua hakua na msaada mwingine Gatkuoth alijiunga na kikundi cha waasi kilichoitwa janjaweed. Chenye makazi yake hukohuko Sudan na nchi nyingine jilani Chad, alidumu kwenye kikundi hicho kwa miaka isiyopungua 7 mpaka pale siku alipogundua ata mauaji ya wazazi wake yalifanywa na kikundi hicho hicho cha janjaweed.
Baada ya kugundua kuhusika kwa janjaweed kwenye mauaji ya wazazi wake ndipo alipojitoa kwenye kikundi hicho kwa kukimbilia nchini somaria ambapo alikutana na marafiki ambao walioshauriana kutimkia South America.

Akiwa Sudan hakuwahi kabisa kutumia dawa zozote za kulevya isipokua baada ya kufika somaria ndipo alipoanza kujiunga na vikundi hivyo ambavyo vilijihusisha pia na utumiaji wa dawa hizo.

Akiwa somaria ndipo alipata fursa ya kuja huku, target yake ilikua atafute pesa ili arudi tena nchini kwao.

Aliichukia sana siasa akiamini ndio chanzo cha vita kwenye nchi yake lakini pia ni chanzo cha kifo cha wazazi wake wote wawili. Hivyo ndoto yake ilikua ni kutamani kuimaliza vita hiyo kwa namna yoyote japo haikua kazi rahisi kwa mtu ambaye hajawahi kufika shule kabisa.
Mpaka hapo niliamini Gatkuoth alikua hajui kusoma wala kuandika.
Baada ya kusikia hakuwahi kufika shule kabisa kwenye maisha yake.

Gatkuoth alijikuta ameingia kwenye matumizi ya kupindukia ya madawa ya kulevya baada ya kua amekata tamaa kabisa ya maisha aliamini hana future. Alitamani sana kurudi kwenye kaburi la mama yake na baba yake lakini haikua rahisi tena.

Javier alimalizia kwa kusema "mwaka jana yaani 2011 Sudan kusini ilitambaulika rasmi kama nchi huru. Nilitamani sana kumuona Gatkuoth anarudi kwao kwani ndoto yake ilikua imetimia ya kuiona Sudan kusini inakua sehemu salama kwa raia wake.

Lakini ilishindikana kwa Gatkuoth kurudi kwani alikua kwenye hali mbaya huwezi mpeleka popote.

Mpaka sasa mwezi umepita tangu Gatkuoth afariki akiwa amelala kitandani hapo, ilituchua mpaka siku mbili kujua kama Gatkuoth alikua amefariki. Hakuna aliekua anamjali ata akiumwa kwani hakua na msaada kabisa, sababu hakua tena ata na uwezo wa kufanya shughuli yoyote hivyo alikua useless.

Gatkuoth nimemzika mi mwenyewe kwa mikono yangu nikisaidiana na watu wengine wawili waliokuja kunipa msaada baada ya kuona hakuna mtu anaejali msiba ule.

Umejifunza nini kwenye maisha ya Gatkuoth? Lilikua ni swali la Javier.

Wakati nataka kumjibu aliniambia kama kuna chochote nilichojifunza it's ok haina haja ya kumwambia.


Nilitamani kujua Javier anamda gani mashambani hapo ila niligundua kuna baadhi ya maswali hayupo tayari kuyajibu.

Nilimuuliza kwa namna gani naweza toka hapo, ila alichojibu ni maneno mawili tu STAY POSITIVE.

Apo niligundua Javier anajua mengi kuhusu eneo hilo lakini Javier pia anaweza asiwe mfanyakazi wa kawaida kama wengine hivyo natakiwa kumsikiliza sana.

Siku hiyo iliisha huku tukiwa free bila kufanya shughuli yoyote nadhani ile ilisababishwa na ugeni wetu hivyo tulipewa muda wa kupumzika.

Javier alipotea kwa zaidi ya masaa matano na nilikuja kumuona muda wa kulala, alirudi kulala na nilistuka kumkuta yupo ndani sikubahatika ata kusikia hatua zake akiwa anaingia.

Alishangaa kunikuta bado sijalala na nilimwambia kua nimeshindwa kupata usingizi muda huo kwa kua mchana wote niliutumia kwa kulala.

Alikuja akakaa juu ya kitanda chake na kunyanyua pillowcase (foronya ya mto) ambayo alikua anaitumia kama begi la kuhifadhia nguo zake na baadhi ya vitu vingine vikiwemo vitabu.

Kwenye pillowcase ile alitoa kitambaa cha sufi ambacho alikifungua na kutoa copper bracelet (bangili ya shaba).
Alinikabidhi mikononi niichunguze kwa makini kisha akauliza.



JAVIER: do you real know what is this
( Hivi unajua hiki ni nini)

MIMI: yes I do! It's copper bracelet
( Ndio najua ni bangili)

JAVIER: even myself I know that it's a copper bracelet but how does it work on human body?
( Ndio najua ni bangili ya shaba lakini inafanya kazi gani kwenye mwili kulingana na taratibu za kiafrika)

Javier alisema week kadhaa nyuma kabla ya kifo cha Gatkuoth, Gatkuoth mwenyewe alimuomba ikitokea amefariki na yeye yupo kiasi kwamba atahusika kwenye mazishi yake.
Basi anamuomba asikubali Gatkuoth azikwe na hiyo bangili, aivue then na kama atakua tayari aitumie yeye au ampe mtu yoyote ambaye atai value kama kinga na dawa.


Kwa maelezo ya Javier ni kwamba bangili hiyo aliitoa kwenye mwili wa Gatkuoth ambaye alimuomba ikitokea amekufa asizikwe na bangili hiyo kulingana na tamaduni za kwao.

Kwa taratibu na miiko ya koo zao marehemu hazikwi na aina yoyote ya mapambo au urembo kwenye mwili. Hivyo kwakua Javier alihusika moja kwa moja na mazishi hayo alikumbuka swala hilo, lakini hakujua umuhimu wa bracelet ile ndio maana aliponiona mimi aliamini nitajua chochote kulingana na uafrika wangu.

Kwa bahati mbaya na mimi sikua na taarifa za kutosha zinazohusu uvaaji wa bangili hizo. Kikubwa nilichokua najua ni kwamba niliwaona watu kadhaa mtaa wakivaa bangili hizo. Lakini pia mara kadhaa nimekutana na wamasai wakiuza bangili hizo japo sijawahi kuuliza zinamanufaa gani kwa mvaaji.
Nilimuuliza Javier kama yeye alijaribu kumuuliza Gatkuoth kuhusu matumizi ya bangili hiyo. Alisema alimuuliza na akampa majibu, alichotaka kujua kutoka kwangu ni je! Na mimi nafahamu chochote kuhusu bangili hiyo.

Nilipomwambia kwamba nimeona watu kadhaa wakivaa bangili hizo mtaani kwangu basi lilikua jibu tosha kwamba naifahamu.

Nilijaribu kuongea na Javier anielezee japo kwa uchache Kuhusu bangili hiyo na alisema kwakua imetokea kwenye tamaduni za kiafrika basi atanikabidhi kabisa nitumie.

Alisema Gatkuoth alipewa bangili hiyo na marehemu baba yake kabla kifo hakijawakuta huko Darfur akiwa na mama yake mzazi miaka hiyo ya 2003


Javier aliambiwa na Gatkuoth kwamba waafrika especially watu wa misri ya kale ndio waligundua uvaaji wa shaba (genuine copper) na wakasambaza ustaarabu huo duniani kote.

Uvaaji wa bangili ya shaba husaidia mambo mengi kwa mvaaji ikiwepo afya ya mvaaji na Mambo mengine ya kiroho yaani (physical and spiritual world).

Mara nyingi tiba hizi ni tiba zisizoonekana na ni tiba za kimaajabu lakini huleta matokeo chanya kwa mvaaji. Mfano:

Mvaaji wa bangili ya shaba huponywa taratibu maumivu ya misuli na viungo hivyo wavaaji wa bangili ya shaba (copper bracelet) huwa ni wenye nguvu, afya njema na wasio na woga na hujiamini sana hii ndio nguvu ya kiroho isiyoonekana ambayo inapatikana kwenye bangili ya shaba.


Kuimarisha afya ya mishipa na moyo, kukosa madini ya shaba hupelekea mtu kuugua magonjwa yanayohusisha mishipa na moyo Aortic aneurysm
Hivyo uvaaji wa bangili ya shaba huwalinda watu na magonjwa hatari kama moyo na kupooza ni mara chache sana kukuta mtu aliyevaa copper bracelet kwa mda mrefu kuugua magonjwa ya moyo.

Huimarisha mfumo wa kinga, Javier alitoa mfano kama ambavyo chuma cha shaba huchimbiwa ardhini kwa ajili ya kupambana na nguvu za umeme wa ziada. basi hivyo hivyo ikivaliwa shaba hufyonzwa taratibu kwenye mwili wa binadamu. Na kupambana na nguvu zote chafu zinazoweza kumshambulia mvaaji.

Hupunguza uzee (anti-aging) kwakua copper ina viua sumu viitwavyo antioxidant ambazo huzuia taka na sumu za mwili kuharibu cell na kuzilinda pia. Wavaaji wengi huonekana vijana ikiwa umri umeenda.
Kwenye mambo ya kiroho alizungumzia vitu kama channel spiritual vibrations na Spiritual Energy mwisho kabisa Positive Energy ambayo tutaizungumzia huko mbele.

Hapa sasa utafanya uchunguzi wako binafsi kuhusu hizi copper bracelet either kwa wavaaji au wauzaji na ina sisitizwa kama unavaa basi vaa genuine copper kwa matokeo chanya zaid.
Kuna zaidi ya 90+ spiritual benefits of copper bracelet
( Binafsi naamini uvaaji wa copper bracelet na ukihitaji genuine unaweza kuniona au watafute madereva wa maroli wanaoenda Congo wanazijua)

Binafsi bwana Javier alinipa ile bracelet ya Gatkuoth yeye hakutaka kukaa nayo aliamini ile ni tamaduni ya waafrika hivyo haiwezi kuwa na impacts au matokeo chanya kwa wazungu.

Je! Na sisi ni tamaduni ngapi za wazungu tumezishikiria na hatufikirii kama zinaweza kuleta matokeo chanya kwenye mazingira yetu.


Next episode tutaongelea spiritual benefits za uvaaji wa dhahabu especially Kwa wankina mama

0623329512 Whatsapp


Copper bracelet
images%20(34).jpg
 
THE WEALTH OF RAPTA RUINS
(Get Rich or Die Tryin)

Msimuliaji: LUDOVIC MASSAWE

NB: SIMULIZI HII IMEAMBATANISHWA NA BAADHI YA PICHA ZINAZOTUMIKA KUELEZEA MATUKIO, HURUSIWI KUTUMIA PICHA HIZO MAHALI POPOTE.

PROLOGUE/DIBAJI

Mji wa rapta ni mji uliozama baharini kisiwani mafia kwa zaidi ya miaka 2000. Unaweza kua mji mgeni Kwa baadhi ya watu, lakini wengi mnaweza kua mmepata kuusikia uwepo wa mji huu wa kale pembezoni mwa pwani ya Africa mashariki. Wapo wanaodai mji huu unapatikana maeneo ya rufiji kwa sasa na wapo wanaodai mji huu unapatikana pembezoni mwa kisiwa cha mafia. Je! ni nani yupo sahihi?

Mji huu ulipata kuwepo mwanzoni mwa karne ya 1 na imepita zaidi ya miaka 1600 mpaka 2000 tangu kuwepo kwa mji huu. Unaaminika kuwa mji wa kwanza tajiri barani Africa na pia ni miongoni mwa miji kumi na tano inayopatikana chini ya maji. ukiacha miji kama vile Thonis-Heracleion na Alexandria iliyopo Egypt, Yonaguni Jima (Japan), Port Royal (Jamaica) Dwarka (India), Pavlopetri iliyopo south-western Greece, Villa Epecuen (Argentina) nk.

Tofauti na ilivyo kwa watanzania na wakazi wa Africa mashariki wakiwemo wana archeologia. Wengi wamechelewa kuzipata habari za mji huu, mimi nilizipata habari hizi nje kabisa ya ukanda huu. Nilizipata habari hizi nikiwa jiji la Tehran uko inchini Iran (uajemi ya kale) ndani ya maktaba ya taifa (National Library of the Islamic Republic of Iran) iliyoanzishwa mwaka 1937 ikiwa na zaidi ya items milion 15 ndani yake.

Wakati nafika Iran nilikua nikitokea nchini Colombia na Peru kwenye mashamba ya koka (coca plantations). kwa wasiojua koka leaf ndio mmea unaotumika kutengeneza madawa ya kulevya aina ya Cocaine kupitia mchakato mrefu. Na ugumu wa ku control uzalishaji wa cocaine unasababishwa au unatokana na kushindwa kuthibiti chemicals zinazotumitumika kwenye mchakato huo kwani ni chemicals za kawaida zinazotumiwa kila siku kwenye matumizi ya binadamu.

Mfano; ku process coca leaf kuwa coca paste mpaka kupata cocaine base na HCI zinatumika chemicals kama, Sulfuric Acid, Sodium Bicarbonate, Sodium Hydroxide, benzene, Potassium Permanganate, Dichromate, Ammonia Hydroxide, Sodium Hydroxide, Methyl Ethyl Ketone na kerosene. Tutajuzana mengi kuhusu cocaine hapo mbele tukiendelea na simulizi.

Sasa basi Niliwezaje kufika Colombia, Peru kisha Iran na miji mingine mikubwa duniani? Niliwezaje kuzisikia habari za mji wa rapta? nani alinipa habari hizi? na mji huu wa rapta una utajiri kiasi gan ndani yake? Nilifikaje rapta na kwa msaada wa technologia gan nilifanikisha zoezi langu? Kipi kilisababisha mji huu kuzama baharini?

Swali lingine la msingi, wageni wa kwanza wa pwani ya Africa mashariki walikua ni warumi na wachina kabla ya waarabu na waajemi, sasa imekuaje details za rapta zilizoandaliwa na warumi zikafika Iran (Persian gulf) zilifikaje huko?

Najua baada ya kutaja wachina wengi mtajiuliza maswali lakini msijali tutaona ushahidi wa uwepo wa wachina ndani ya mji wa rapta. 90% ya wachunguzi wa mji huu wanatumia taarifa za warumi zilizoandaliwa na Claudius Ptolemaeus (Claudio Ptolemy). Je wana fahamu kua details hizo kabla ya kuwafikia zilishatumiwa na waajemi wa kale Na kuna uwezekano taarifa hizo zilichakachuliwa!?

Je! Mzungu bwana Alan Sutton (mzamiaji) aliyegundua kuta za rapta akiwa kwenye helicopter hivi karibuni, ilikua ni bahati mbaya tu au na yeye ni moja ya wale treasure hunters ila hajaliweka hili wazi?
Ungana nami kwenye simulizi hii ya kuvutia ili kupata majibu ya maswali yote na kwa hakika utajifunza mambo mengi ndani yake.

SEHEMU YA 01

Mgomo sengerema secondary

Wakati unajiuliza Niliwezaje kufika Colombia, Peru na kisha Iran unatakiwa kujua safari yangu ya jasho na damu pamoja na misukosuko mingi ilianzia shule ya sekondari ya sengerema nikiwa kidato cha sita. Kwa waliopata kupita shule hii wanaweza kua mashihidi kwa namna shule hii ilivyokua ya kikomando yaan wenyewe tulikua tunaita late-summer boot camp.

Kwa haraka haraka tu ni shule aliyowahi kufundisha hayati magufuli kabla hajawa waziri na kisha raisi. Nadhani umeanza kupata picha ilikua shule ya aina gani, Ni shule ambayo kila mtu alikua jeuri kuanzia headmaster mpaka mpishi wa jikoni. Wakati nikiwa hapo tuliwahi kushuhudia kesi nyingi ngumu na za ajabu kama wanafunzi kukutwa na kombati za jeshi full set. Kuna mengi kuhusu sengerema ambayo hatuyajui nitawaeleza machache tu na ni kwa namna gani safari yangu ilianzia hapo.

Nilifika hapo kwa mbinde huku o'level nikitokea Ngerengere kizuka sekondari baada ya kufukuzwa MAKOKO SEMINARY, kiukweli nilikua mtoto mtukutu na jeuri ilifika hatua mzee wangu mzee MASSAWE alisema hizi tabia nimeridhi kutoka kwa babu yangu. Ambae alikimbia nchi baada ya kuhusika kwenye matukio mawili, lile la utekaji wa ndege ya ATC mwaka 1982 February kwa makusudi ya kushinikiza mwalimu ajiuzulu na lile jaribio la kuangusha serikali ya mwalimu Nyerere la mwaka 1980's. Babu Yangu alikua ni miongoni mwa wale maafisa wakuu waliosuka ule mpango, Tuachane na babu na tuludi zetu sengerema.

Tukio la mgomo ndio lililoanzisha safari yangu Na lilipangwa usiku baada ya mlo wa jioni, vidume baada ya kushiba dona maharage pamoja na nchima boyo akili zikatutuma tufanye mgomo usiku wa siku hiyo. Sababu za mgomo zilikuwepo japokua hazikua na mashiko sana naweza sema ni ujana tu ndio ulikua unatusumbua ukiongeza na zile bangi zakuvutia maporini (chaka).
Kama kawaida mzee baba siku hiyo ya mgomo niliwekwa kitengo cha TANESCO, yani niliambiwa ikifika saa 2 kamili usiku ni hakikishe shule nzima umeme umezima. Hii ilitokana na ujuzi wangu wa mambo ya electronics na wiring za ujanja ujanja za mabwenini especially bweni la kimweri na sokoine.

Basi ilipotimu saa 2 kamili nilihakikisha Giza limetanda shule nzima kasoro nyumba za walimu tu, na kazi yangu iliishia hapo na Majukumu mengine yaliyobaki yalikua kwa wenzangu wahamisishaji kuhakikisha kila mmoja anashiriki. Lakini pia kuna jamaa mmoja wa mwananyamala yeye alikua na dumu la petrol lita 5 sijui alilitolea wapi usiku ule huyu bwana kazi yake ilikua kuhakikisha moto unawaka maeneo yote yaliyopangwa kuchomwa.

Mpaka kufika saa nne usiku stationary ya mwalimu wetu siwezi kumtaja jina ilikua haitamaniki na baadhi ya walimu walikimbiza familia zao mjini. 90% ya wanafunzi tulikua michepuo ya sayansi yani PCM, PCB na combination nyingine hivyo tulikubaliana kutokugusa maabara wala library wala darasa, wachache sana walikua arts na cha ajabu kwenye hii shule watu wa arts walikua wamestaarabika ukilinganisha na sayansi.

Shule imejengwa mlimani kabisa kiasi kwamba ilipofika saa 4 na nusu usiku defender ilionekana ikipandisha na wote tukapotelea maporini. Jambo la kufurahisha ni kwamba askari hawakufanikiwa kukamata ata mwanafunzi mmoja kati ya wanafunzi 800. Wengi waliishia kulala kwenye miembe na majaruba ya mpunga kwa usiku huo kwani shule ilizungukwa na makachero wakutosha. Lakini massawe nikasema siwezi lala juu ya mti Kama tumbili, usiku ule ule nikaanza safari ya kuelekea mjini mitaa ya soko mjinga.

Pale mjini kuna binti alikua anasoma shule ya jilani inaitwa NTUNDURU alikua amepanga ghetto. Can you imagine!!! Shule ya boarding na bado amepanga mtaani! asee!!... Merry alikua ni hatari sana mnyaturu yule wa singida.

Mishale ya saa tano usiku nilikua mlangoni kwa merry nabisha hodi, baada ya dikaka 3 alifungua mlango nikaingia. Walikua wawili yeye na mwenzie anaitwa jane. Ndani kulikua na chupa za safari na mzinga mkubwa wa konyagi, nilipoingia nilihisi uwepo wa mwanaume mule ndani na baadae niliona funguo za sun LG na vipisi vya sigara. Ila sikujali sana nilijitupa kitandani nikapitiwa na usingizi mzito uliotokana na uchovu wa mgomo na mbio za kuwakimbia field Force.

Nilikuja kustuka saa kumi alfajiri na mlio wa pikipiki uliokua unamrudisha merry ambae alikuja yupo hoi na kwa haraka niligundua jane amebaki na yule kidume wa jana.

Merry akilewa bia hua zinashuka chini, waliosoma cuba wamenielewa hapa. Hivyo baada ya kuingia ndani hakutaka story zaidi ya kutupa nguo kwenye kila kona ya chumba hicho kama mwehu. Na mimi kutokana na nilikua namjua vizuri haikusumbua kujua anataka nini zaidi ya kuanza mtanange wa kukata na shoka uliochukua zaidi dakika 90 kama finally ya Argentina vs France kule Qatar.

Tulikuja kuamshwa na mwanga mkali wa jua la saa 4 asubuh uliokua unapita dirishani Huku merry akiwaza supu. Ilituchukua muda mfupi kujiandaa kwenda maeneo ya stendi kupata supu, nilishangaa baada ya kufika stendi nilikutana na wanafunzi wenzangu wakiwa na mabegi wengine ma tranka. Nilipowauliza walijibu shule imefungwa kwa muda wa week 3 na tutapewa utaratibu wa jinsi ya kurud tukiwa nyumbani. Hapo nilianza kuwaza namna ya kurud nyumbani huku mizigo yangu yote imebaki shule na hakuna mwanafunzi anaeruhusiwa kwenda tena shule kwa muda huo.

Basi bwana tulipata supu na mrembo merry kisha tukarud zetu ghetto kupumzika, nakumbuka ilikua siku ya alhamisi hivyo merry hakuenda shule kutokana na hangover na tulishinda ndani siku nzima mpaka kesho yake asubuhi.

Siku ya pili akili ilivurugika zaidi baada ya kupata habari kwenye vituo vya habari viwili tofauti kuhusu mgomo wa sengerema, kituo cha kwanza ni redio sengerema ilitangaza wanafunzi kumi na tisa (19) wamefukuzwa na wengine kusimamishwa masomo kwa muda usiojulikana. Hivyo hivyo kwa redio free Africa na gazeti la mwananchi, gazeti hili lilitoa majina ya waliofukuzwa na mimi nilikua jina la kwanza kwenye ile list.

Niliwaza namwambia nini mzee massawe ambae alichoshwa na tabia zangu.

Akili ikanituma kuangalia upande wa pili wa maisha na sio kukomaa na shule, niliamini siku Moja nikiludi home na pesa nyingi mzee massawe atanikubali sana jembe lake.

Baada ya kupata wazo la kutoendelea na shule nikaanza kuwaza natakiwa nianzie wapi kutafuta pesa. Apo apo akili ikaniambia dar ndio sehemu pekee naweza tengeneza pesa nyingi, lakin kwa bahati mbaya sikua mzoefu wa mji huo na wala sikutakiwa kufikia kwa ndugu yoyote na bado sina nauli ya kufika huko. Niliamini nikifika Mwanza kwenda dar itakua rahisi hivyo nikaanza mchakato wa kufika mwanza (nyegezi).

Nilimshirikisha merry kwa makusudi ili anisaidie nauli ya kufika nyegezi kwani kutoka sengerema hadi nyegezi ni kiasi cha shilingi 4000 tu. Na kwa maelezo ya merry aliniomba tufike stendi kuna mtu atampatia tukifika hapo.tukiwa stendi Merry alimfuata jamaa mmoja bonge hivi anadeal na tickets pale stendi, Kwa haraka niligundua huyo ndio sponsor waliekua nae jana. Sikujua waliongea nini na merry ila merry aliniambia tusubiri kuna coaster inatokea katolo ndio tutaenda nayo mwanza.

Haikuchukua muda mrefu ile coaster ilifika na walipanda abiria kadhaa kisha bonge akamwambia konda hawa ndio wadogo zangu wanaoenda nyegezi. na sisi tulipanda tukaanza safari, nilishangazwa na uwepo wa Merry kwenye safari sikujua na yeye anaelekea wapi kwani hakua na sababu ya kutoka sengerema siku hiyo kwani masomo kwa upande wake yalikua yanaendelea. Merry alikua mwanafunzi wa kidato cha nne NTUNDURU sekondari na ile siku tumeshinda ote ndani nilitumia fursa kumfundisha almost topics tatu za msingi.

Sasa tukiwa ndani ya coaster kuelekea nyegezi nilimuuliza kwanini na yeye ameamua kusafiri, majibu yake yalikua ni kwamba ana muda mrefu hajafika mjini mwanza hivyo alitaka kwenda kuosha macho kwa muda kisha baadae ataludi sengerema.

Nilipata nafasi ya kupiga stories na konda ndipo niligundua wametokea geita walipeleka msiba na hapo wanarudi dar es salaam. Niliamini safari yangu kufika Dar es Salaam imerahisishwa nachotakiwa ni kuwaza namna gani naweza kushawishi jamaa ili aniruhusu nisafiri nae.

Majadiliano na konda yalikua hivi.

Konda:"dogo! we ni mwanafunzi Nini? Jana tukiwa na msiba tulibeba madogo kama watatu hivi wakiwa na suruali nyeusi na tishet za bluu kama ulivyovaa wewe"

Merry alijibu fasta kama ameulizwa yeye,

Merry: ndio sisi ni wanafunzi, ila tumerudishwa nyumbani ghafla sababu ya mgomo wa juzi usiku.
(konda hakujua kama sengerema ni shule ya wavulana pekee)

Konda: kama wanafunzi wenyewe ndio nyinyi hiyo shule kazi ipo. Kwaiyo nyumbani ni wapi??
Nilitumia swali hilo kama fursa ya kufanikisha misheni yangu.

Mimi: home dar na hatujatumiwa nauli sijui tunafikaje?

Konda: we mtoto wa kiume jitahidi upambane.

Jibu lile lilinikatisha tamaa ya kuendelea na maongezi yale.
Haikuchukua muda tulikua tumefika kivukoni busisi. Abiria wote tulishuka na kupanda kivuko, lakini nilifurahi baada ya kumuona konda anajisogeza kwa merry na kujiongeresha. nilijua kwa ujanja wa merry anaweza kufanikisha safari yangu kirahisi sana.

Baada ya kufika upande wa pili tulirudi ndani ya coaster na kuendelea na safari na wakati huu merry aliniambia ameshampanga konda hivyo tutafika wote dar es salaam.

Merry alikua binti mjanja sana na anamacho Fulani akikuangalia tu unajua atakua fundi, hahahahahaha kwa wale tuliopita sengerema miaka ile najua mtakua mnamkumbuka kwani alikua maarufu sana. Especially tukienda shuleni kwao kwa ajili ya michezo wengi walimtolea macho, nitakuja kueleza nilimpataje hapo baadae.

Baada ya kufika nyegezi tukijiandaa na safari ya kuanza kuitafuta dar es salaam nilishangaa konda aliniita na kunipa buku tano nikatafute msosi. Na kisha konda na merry walipotelea kusiko Julikana, Nilijua merry ameshafanya yake tayar niliishia kuitunza ile buku tano nikiamini itanisaidia mbele ya safari kwani sikua na chochote mfukoni.

Baada ya nusu saa merry na konda walirudi huku nikimuona merry na vifurushi vya kutosha bila shaka ilikua ni misosi na kimoyomoyo nikasema merry hajawahi kuniangusha ata siku moja. Tulikaa kwenye siti na kuendelea na safari Huku tukipiga msosi mzito nakumbuka ilikua ni Sato na chipsi kavu za kutosha.

Mimi: merry ulisema unaishia nyegezi vipi mbona unaendelea na safari???

Merry: sijawahi kufika Dar es Salaam, nadhani hii ni fursa ambayo sitakiwi kuichezea. Najua nipo na wewe hakuna kitachoharibika nitakaa week moja kisha nitarudi shule.

Daaaaah!!!!! Nilihisi mwili unakufa ganzi nilitaman kumwambia Mimi mwenyewe sina pa kufikia ila nikapiga moyo konde. tukaendelea na safari yetu huku stories zikiwa nyingi. Merry pekee ndio alikua na simu Mimi kilichokua mfukoni ni ile buku tano, kibiriti cha gesi na scientific calculator tu.

Baada ya safari ya muda mrefu wote tulipitiwa na usingizi, safari ile ni ya kutwa nzima kwani nakumbuka tuliingia morogoro usiku wa saa tano tena hiyo ilikua ni baada ya abiria kulalamikia speed ya gari ilikua kali mno. Tulipotoka moro baada ya kufika maeneo ya chalinze nilipitiwa tena na usingizi mzito. Nilikuja kushtuliwa na konda akidai alitusahau tumeshaingia mjini mda mrefu.

Konda: nyie mnashukia wapi tumeingia Dar es Salaam tayari.
Lile swali lilikua gumu kwangu kwani sikua ata najua tunapoelekea baada ya kufika dar. Kwa Dar es Salaam nachojua ni ubungo tu hivyo nilimjibu tunashuka ubungo.

Konda: ubungo tumepita tayari sisi tunaelekea mbagara, shukeni hapa mrudi vertinary mkapande gari za ubungo.

Kiukweli sikumuelewa konda ata kidogo kila alichonambia kilikua kipya ila sikutaka kuonyesha kutokujua mbele ya Merry hivyo tulishuka. Tulishushwa eneo moja lina mataa na ilikua saa saba na nusu usiku, nikiwa sijui cha kufanya Merry alianza kulalamika maumivu makali ya tumbo.
Nilijua tu itakua njaa kwani ni muda mrefu hatujapata chakula, baada ya kupepesa macho huku na kule niliona sehemu kwa mbaali kuna watu na mataa mengi yanawakawaka nikajua fika hapo patakua na bar hivyo hatuwez kosa msosi.

"Massawe hapa na kwenu kuna umbali gani?" Lilikua ni swali la Merry na mimi sikuona haja ya kuendelea kumficha ukweli, nilimueleza kila kitu kama nimeenda huko kutafuta maisha na nimeachana rasmi na masomo baada ya kufukuzwa shule na nilimueleza siwezi kurudi moshi kwa mzee massawe hatonielewa kabisa.

Kwa maumivu ya tumbo aliyokua anapitia Merry hakutaka kuendelea na mjadala nilimuona akiongoza kwenye lile eneo tuliloliona likiwa na watu wengi usiku ule.
Baada ya kufika eneo Hilo niliona maandishi makubwa yakiwakawaka yameandikwa SUGAR REY. Ni dhahiri ilikua ni bar, nilishangazwa na mavazi ya wadada wa eneo hilo na sio mimi tu ata merry pia.
"Hhhmmm kweli hii ndio dar es salaam ninayoisikia kila siku" yalikua ni maneno ya Merry. Tukiwa bado tumeduwaa alikuja bodaboda

Bodaboda: vipi mnaenda?

Mimi: hapana tumefika bro.

Bodaboda: punguzeni kushangaa basi.

Tulisogea mpaka eneo lile nikiamini hatuwezi kukosa chakula ukizingatia nilikua bado na lile buku tano la konda.

Tulipofika tu merry alimfuata Binti mmoja aliekua amekaa pembeni akiwa kwenye pozi Kama anamsubiri mtu na waliongea baadae wakafatana sikujua wameenda wapi. Nilijisogeza kwa jamaa wa bodaboda wakiwa na makoti makubwa nikajiunga kupiga nao story huku nikimsubiri Merry.

Mimi: bro samahan hawa wadada mbona wapo wengi na wana mishe gani apa mbona wamevaa kiasala asala?

Bodaboda: hao wanajiuza mjomba. We mgeni nini?

Mimi: ndio mi mgeni.

Bodaboda aliniangalia tu na hakuendelea kuongea chochote Zaidi ya kuwafata abiria wawili waliokua mbele yake.
Baada ya muda kidogo hivi nilimuona merry akiludi eneo nililokuwepo.

Mimi: merry punguza kujifanya unamjua kila mtu apa sio singida hii dar rafiki angu.

Merry: lile tumbo lilikua ni la siku zangu na sio njaa kama ulivyohisi hivyo nilienda kwa yule mdada kuona kama ata nipa msaada wowote si unajua sijatembea na chochote. Lakini pia nimemueleza changamoto niliyonayo kwamba hatuna pa kulala na ndio tumefika mjini.

Mimi: akasemaje?

Merry: kasema atanisaidia kwa leo sehemu ya kulala ila kuanzia kesho nitajua pa kwenda, lakini pia amenieleza kama sina ndugu kabisa atanionyesha kazi ya kufanya na tutakua tunachangia wote kulipa pango la nyumba hivyo mi nimeona niende nae tu.

Kiukweli sikutamani merry aondoke na yule dada lakini sikua na jinsi kwani hata hivyo sikua na sehemu yoyote ya kumpeleka. Merry alinikabidhi simu yake ili iwe rahisi kunipata siku inayofuata kwani alikua anajua sikua na simu. Tuliagana na merry na mimi nikabaki eneo hilo nikiwaza naelekea wapi kwa usiku huo wala sikutaka kujutia maamuzi yangu ata kidogo niliamini nipo sahihi kabisa.

Tunaendelea baadae usikae mbali.View attachment 2583318
Poor narration... umeweka mambo mengi sana un necessarily imeboa.
 
Aisee na wewe kidume umeweka picha ya miguu?? [emoji849][emoji849] hilo pozi tuwaachie Darlin na luckyline peke yao tafadhali na miguu yao mizuri ngozi nyororo, unayumba baharia ila kama we ni ke nisamehe mkuu itakua nimezoom vibaya mmhh [emoji23][emoji23]

Jokes
Hahahaha Aaya bhanaa,..nimekusoma mwamba
 
Asubuhi na mapema Javier aliniamsha tukatoka nje na kushuka chini ya ngazi za banda lile ambalo lilikua na vyumba kadhaa vya kulala. Watu wote walikua bize, ilionekana wageni wote tunapokea maelekezo kutoka kwa room mate ambaye umemkuta kwenye chumba ulichopangiwa.

Baridi lilikua kali sana asubuhi ile huku wenyeji walionekana kutokua na shida yoyote hivyo ni dhahiri jamaa walizoea mazingira hayo.

Kiukweli nilikua najivunia sana kupata mwenyeji kama Javier alionekana kutokua na makuu kabisa kwenye kambi ile.

Mgawanyo wa kazi ulikua kwenye sehemu kama tatu hivi, kulikua na wale wa mashambani hawa majukumu yao yalikua ni kulima na kupanda wakati mwingine kuvuna.
Kuna waliohusika na usafirishaji wa bidhaa kuanzia majani yenyewe, chemicals na baadhi ya vifaa.

Na wengine walikua Upande wa Lab (processing lab) huku kwa upande huu wa lab kulihitaji ideas za chemicals lakini pia na uzoefu wa kutosha.

Kwa asubuhi ile nikiwa na Javier tulitembea umbali wa zaidi ya mita 400 kushuka bonde lililokaribiana na mto haullaga ambao ulikua ni tributary ya mto Maranon. Kabla ya kufikia upande wa kulia kwa juu kwenye kamsitu kadogo kulikua na banda kubwa lenye urefu wa kama madarasa mawili.

Banda hili lilijengwa kwa mbao ngumu za porini likiwa na madirisha yaliyopitisha hewa ya kutosha. Kwa juu lilifunikwa au liliezekwa kwa turubai kubwa jeupe kwa ustadi wa hali ya juu, eneo hilo kulijengwa ngazi za magogo ilikupanda kufikia banda hilo.

Kwa haraka nikajua huko ndipo yatakua majukumu yangu kwani ilionekana ndio sehemu ambayo ata Javier nae hufanya shughuli zake.

Tulipanda ngazi zile na kuribia jengo lile (banda) ambalo naendelea kusisitiza lilijengwa kwa ustadi sana. Tulipolifikia banda lile ndipo nilipogundua ilikua ni maabara, hivyo mahala hapo ndipo wajuba huchakata coca paste na kupata cocaine hydrochloride.

Kwenye akili yangu niliamini hivyo Lakini sikutaka kujithibitishia hilo mpaka nitakapo tambulishwa na Javier ambae alikua mwenyeji wangu.

Tuliingia ndani ya lile banda, kiukweli kwa ndani lilikua na space kubwa sana tofauti na nilivyokua nikiwaza hapo awali.

Kwa ndani Upande wa kushoto kutoka mlango wa kuingilia ulipo, kulikua na meza kubwa pana na nzito kiasi kwamba ata ukiwa powerful kiasi gani huwezi tingisha meza ile. Mwishoni mwa banda lile upande wa kulia kulikua na drums au mapipa mengi yaliyokua wazi.

Katika kulikua na kabati pamoja na mashine ambayo sikuweza kuitambua kwa haraka lakini mashine ile ilikua kuukuu yaani imechoka na sikudhani kama inaweza kua nzima.

Eneo lile lilikua tulivu sana na haikua rahisi kila mtu kufika hapo kama huusiki kabisa, tukiwa ndani kabla Javier hajaongea chochote walifika wasichana wawili wote wana asili ya kibrazil.
" Hi Javier, is this the new guy"
(Habari Javier, huyu ndio kijana mpya)
JAVIER: Of course
(Bilashaka)

Javier alinitambulisha kwa wale wasichana wawili ambao mmoja wapo hakukua na haja ya kuuliza alionekana ni teja kabisa. Wasichana wale waliitwa Catarina na Manuela, Catarina hakua amechoka sana ukilinganisha na Manuela lakini Wote hawa walikua ni wenyeji wa Brazil kutoka mji mmoja unaitwa Rio de Janeiro.

Catarina na Manuela walielezwa kama naitwa mustapha kutokea East Africa, Javier alimalizia kwa kusema anajua machache sana kuhusu mimi hivyo tutaendelea kujuana taratibu kwakua tutakua pamoja kipindi chote.

Catarina alikua na element flani flani kama tom-boy japo wote miili yao ilijaa tatoo. Catarina alikua ni Chainsmokers (mvutaji wa sigara aliyepindukia) niligundua hilo kwani tangu afike hapo alishamaliza kama pisi mbili za CARIBE.

Jambo lingine lililonishangaza ni kwamba toka jana yake tunafika mpaka muda huo sikukutana na mtu mnene kabisa. Wengi walikua wembamba tena wembamba kweli kweli kiasi kwamba mi sikua na mwili mkubwa kiivyo ila nilionekana kibonge kwa maeneo hayo.

Na hapa ndipo nilipogundua watu wote au asilimia kubwa ya watumiaji wa cocaine na pombe kali hawanenepi kabisa kwa sababu zifuatazo:-
Kwanza kabisa matumizi ya dawa za kulevya na pombe kali hufanya watu kupoteza hamu ya kula kwa point hii unaanzaje kupata mwili.

Matumizi ya dawa za kulevya kwa wingi Hupunguza uwezo wa mwili kutunza fat ( reduce body ability to store fat)

Mwili hupoteza au huchoma calories nyingi kwa mvutaji wa dawa hizo na mtumiaji wa pombe kali.

All in all utumiaji uliokithiri wa dawa hizi especially cocaine, madhara makubwa huja kwenye ubongo na mwili kwa ujumla.

Kwa kuwaangalia tu, Catarina na Manuela walionekana ni watu ambao wapo huko kwa muda mrefu na maisha yao yote wataishi huko.
Wote kwa pamoja walivalia tshirts pana za mikono mifupi zilizofanya tattoo zao za mikononi kuonekana kirahisi sana.

Asilimia kubwa ya wafanyakazi wa eneo hilo ni wale watu ambao waliwahi pia kua na criminal cases kubwa hivyo kuwepo eneo hilo ilikua kama wapo mafichoni. Yaah ni mafichoni kwakua hakukua na serikali yoyote kule na haikua rahisi mtu yoyote kufika maeneo hayo.

Nilihisi hilo ata wale mabinti pia kwa mfano Manuela alionekana kuwa mrembo sana ila ni unga ndio ulimdhoofisha na kumuharibu. Mpaka anaenda huko lazima kuna sababu iliyompush kwenda huko, niliamini ninavyoendela kuwa nao karibu nitajua mengi.

Baada ya utambulisho, Javier aliwaambia kuwa mi ni mgeni kabisa kwenye tasnia husika na hakuna ninachofahamu hivyo nahitaji msaada wao ili kuanza kazi.
Catarina alikua wa kwanza kuniuliza kama nimewahi kutumia cocaine.

CATARINA: have you ever taste cocaine
( Umewahi kuonja cocaine)
MIMI: NO!!!!!
(Hapana sijawahi)
CATARINA: do you want to make a try
(Vipi unataka kujaribu)
MIMI: i don't
(Sitaki kabisa)
Walicheka sana baada ya jibu langu lile kwamba sitaki kujaribu kabisa, ni wazi kilichowachekesha ni kilekile alichokisema Javier kwamba vijana wa kiafrika hua tunakuja na mipango mingi lakini baadae inapotela hewani.

Manuela hakua muongeaji sana zaidi ya kuvuta sigara muda wote na wakati huu niliona ameshika chupa ambayo ni dhahiri ilikua ni chupa ya pombe. Mabinti hawa waliridhika na maisha ya hapo huwezi kudhania eti wanawaza maisha mengine mbali na hapo.

Catarina alinipa assignment moja ambayo kwangu ilikua simple sana kwani nilitumia idea zangu chemistry kujibu kila nilichoulizwa.

Catarina swali la kwanza kuniuliza ni alitaka kujua tokea nimeingia ndani ya jengo lile ni kitu gani nilichokiona na nakijua vizuri.

Lilikua swali rahisi sana,
Kwa kujiamini nilimjibu kuwa cha kwanza ndani umo niliona organic solvents ambazo zilikua ni benzol, gasoline na kerosene
(Apa kama hukuwahi kusoma chemistry kwakweli sina msaada kwako we kalili tu)
Kama huzijui ni nini organic solvents subiri wakati wa maelekezo ya kutengeneza cocaine hydrochloride nitaelezea kwa undani kila kitu.

Kwa kujiamini tena nilimwambia nimeona alkaline material (baking soda) lakini pia kulikua na sulfuric acid.

Kwa mara ya kwanza niliiskia sauti nzito ya Manuela akiuliza
MANUELA: you are a lab technician
(We ni mtaalam wa maabara)

MIMI: I'm not a lab technician anymore but I knew them when I was highschool
( Hapana mimi sio mtaalam wa maabara ila nimezijua nilipokua highschool)

Catarina alitabasamu na kusema sasa wamepata mtu sahihi kwani kama nimezijua chemicals hizo bila kuelekezwa basi ata kazi ya michanganyo haitokua ngumu wakinielekeza.

Sijisifu ila kwakweli nilikua na kichwa chepesi sana, namshukuru mwalimu wangu wa chemistry SENGEREMA alikua anaitwa dibro jina la utani, concept zake zilinifanya nionekane genius na specialist ambae nilikua moto wa kuotea mbali ndani ya muda mfupi sana kwenye maabara lie ya porini.

Mwanzoni Catarina alionyesha dalili ya kunidharau lakini baada ya kuzichambua chemicals zile sio tu kwa kutaja majina bali na kuzielezea sifa zake nyingine ambazo ata yeye hakua akizijua. Catarina alianza kua mpole na kuonyesha kutaka kujua vingi kutoka kwangu.

Muda huu Javier alikua pembeni anatuangalia niigundua ata yeye hakuamini alichoisikia kutoka kwangu.

Ni hivi kwenye lab zile za coca hazihitaji mkemi wa elimu kuuubwa bali zinahitaji ujue kwenye hatua ipi unatumia chemical ipi na kwa kiasi gan basi.

Hivyo ata hawa niliowakuta lab ni kama walikalilishwa tu chakufanya na sio kwamba walikua ni ma expert kiiivyo.

Manuela aliniangalia mkononi na kuona copper bracelet ambayo nilipewa na Javier. Alinishika mkono na kuingalia vizuri, Javier aligundua kama Manuela anaifananisha bracelet hiyo na ile ya Gatkuoth.

JAVIER: what are you wondering? I am the one who gave him
(Unashangaa nini Manuela, mimi ndio nilimpa)
Wakati Manuela amenikamata mkono anaishangaa ile copper bracelet, niligundua Catarina hakua comfortable kabisa na ata Javier aliligundua hilo hivyo alikuja kuingilia maongezi yale kwa makusudi.

Nilihisi kitu kati ya mabinti wale wawili hivyo niliamini baadae Javier atanieleza chochote kuhusu ukaribu wao. Kwani mmoja alikua na wivu sana especially huyu mwenye asili ya u tomboy hakupenda kabisa contact ya mimi na Manuela.

Niliamini amini kati yao mmoja ata kua mwanaume na mwingine mwanamke yaani wanashiriki mapenzi ya jinsia moja.

Javier baada ya kuingilia maongezi yale alianza kunipa maelekezo mengine yanayohusiana na vyombo especially yale mapipa makubwa yaliyokatwa kwa juu.

Kwenye ile meza kubwa kulikua na kitu mfano wa putty, Javier aliniambia ile haikua putty bali iliitwa coca paste au BASUCO.

Nchi nyingi za South America wanaivuta paste kama ilivyo bila hata kui process mpaka kufikia kua powder. Hii sasa ndio inaitwa cocaine crack, inavutwa sana maeneo ya temeke (mtongani mpaka kwa azizi ali). Wale wapiga deba wanaitumia sana ni cheap likija swala la gharama ukilinganisha na cocaine hydrochloride.

Huko united states uvutaji wa coca paste haupo kwa kiasi kikubwa wengi hawatumii kabisa hii coca paste kama ilivyo kwa America ya kusini na Africa.


MNAWEZA KWENDA WHATSAPP 0623329512 KWA PDF NA USOMAJI WA HARAKA
 
Kuna story nyingi.. mim binafsi sio mtu wa kufatilia story nyingi humu ila kwa chache nilizopitia nimegundua kuna aina mbili za uandishi

1- Uandishi wa kutumia Akili
2- Uandishi wa kutumia mihemko (Vibes)

Mara nyingi uandishi wa kutumia Akili unavutia sana, na aina hii ya uandishi ni mfno wa hii story hapa.

Kuna mambo mengi yanaguswa ya kitaalamu ambayo kwa mwandishi (Kilaza) si rahisi kufit in.

Nafatilia story.
 
Back
Top Bottom