Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Zanzibar kuna Chumbe mbili.... moja ni kisiwa kabla ya kufika Unguja na Chumbe ya pili ipo karibu na Mbweni katika barabara ya kwenda Entebbe.

Master naona kashindwa kabisa kuelezea ni Chumbe ipi alikwenda! Kama ni Chumbe ya barabara ya kwenda Entebbe, hiyo haina msitu na bahari ipo mbali kidogo aidha eneo lote toka Chumbe hadi ufukweni kumejengwa, hivyo basi hakuna msitu wa aina ya simulizi ilivyosema.

Kwa upande wa kisiwa cha Chumbe, ni kisiwa kisichokaliwa na wenyeji, zamani wavuvi walipita hapo baada ya shughuli zao za uvuvi na ndio sababu kuna msikiti kisiwani hapo. Zaidi ya msikiti kuna mnara wa kuongezea meli na vibanda vya hoteli ya kitalii. Ni kisiwa ambacho kipo chini ya uangalizi na kinasimamiwa na kampuni binafsi!

Sijui Master alikwenda Chumbe ipi! Kama kuna mtu anajua ni vema akatufahamisha.
Kwenye mambo ya kichawi unaweza ona msitu mnene posta... so relax and enjoy broh
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 07.




Kwakuwa Mwakisaka ndiye aliyekuwa mwenyeji wangu sikuwa na hofu kabisa kwasababu ni mtu ambaye tulifanya nae kazi kwa muda mfupi na alikiwa mtu mwema,baada ya kufika kivukoni(feri)tulikata tiketi za kivuko na tukawa tumefanikiwa kuvuka ng'ambo ya pili,baada ya kufika upande wa pili yaani Kigambo,jamaa aliniambia inapaswa tupande gari zilizokuwa zinaelekea Kibada kwa kuwa ndiyo njia yenyewe hiyo.

Tulifanikiwa kufika hapo kwenye mradi mkubwa kabisa uliofahamika kama DEGE ECO VILLAGE,kiukweli nilikuwa nashangaa sana namna ambavyo watu wanatumia fedha,ule mradi ndugu zangu ulikuwa mkubwa mno,na kwa waliobahatika kufika huko au wanaotokea huko watakubaliana nami.

Hatukutaka kupoteza muda kabisa ilibidi Mwakisaka aniambie tuulizie namna ya kupata kibarua kwasababu tulikuta watu wakiwa wanachakalika kinoma.Kuna jamaa tulimfuata tukaanza kumuulizia namna ya kupata kibarua siku hiyo.

Jamaa "Hapa kwetu yupo foreman ambaye ndiye msimamizi wetu,ukienda kule mbele pia wanae foreman wao"

Mwakisaka "Foreman wenu yuko wapi tujaribu kuongea nae?"

Jamaa "Nadhani atakuwa anazungukia maeneo anayosimamia,subirini tu hapa atakuja"

Tulisogea kando tukawa tunaendelea kuushangaa ule mradi wakati huo tunamsubiri mtu tuliyeambiwa ndiye foreman wa hapo tulipofikia.Baada ya muda wa nusu saa jamaa mmoja mweusi aliyekuwa mnene na kitambi cha kutosha akawa amekuja na ndipo yule jamaa alitukonyeza ya kwamba jamaa ndiye foreman wa lile eneo.Tulimfuata na kumjulia hali jamaa kisha Mwakisaka akaanzisha maongezi nae.


Mwakisaka "Kaka tunatafuta kazi ya kibarua "

Foreman "Aliyewaambia hapa tunaajili vibarua nani?"

Mwakisaka "Hakuna mtu aliyetuambia kaka tumekuja kuona kama tutapata"

Foreman "Hapa hatuajiri kwa sasa,siku tukiajiri vibarua mtapata taarifa"

Baada ya yale majibu ya kukatisha tamaa Mwakisaka aliamua akae kimya kisha jamaa akaanza kuondoka kuzunguka nyuma ya yale majengo yaliyokuwa mbele yetu.Sasa yule jamaa aliyekuwa kibarua pale akawa amemuita Mwakisaka akamwambia bila pesa ni ngumu sana kupata kibarua kwasababu hata wao walihonga ndipo kupata kibarua,jamaa akasema twende tukaongee nae kikubwa.Nilimwambia Mwakisaka hiyo kazi ya kuongea na jamaa aniachie mimi,akikataa basi tungerudi zetu kwa Mushi kule kivule kuendelea na ufyatuaji wa tofali.

Niliamua kuzunguka ule upande alokuwa amekwenda yule foreman na bahati nzuri nilimuona akiwa anaingia kwenye jengo moja,nilitembea kwa haraka ili kumuwahi kabla hajafika kwa watu wengi ikawa shida kuzungumza nae.

Mimi "Kaka kakaa"

Foreman "mmmh nambie"

Mimi "Kaka tusaidie ndugu yangu na kama ni chochote tutakupatia"

Foreman "Wewe si ndo upo na yule mwenzio nimewaambia hamna kazi!"

Mimi "Kaka tusaidie ndugu yangu!"

Foreman "Nyie mnatokea wapi?"

Mimi "Wote tunatokea kivule"

Foreman "Kivule?,sasa kivule hadi kuja kufanya kazi huku hamuoni tutasumbuana?"

Aliendelea "Ni bora hata mngekuwa hapa maeneo ya jirani"

Mimi "Tutaweka kambi maeneo haya kaka wala hilo lisikupe taabu"

Foreman "Hapa jirani haturuhusu watu kukaa kwasababu za kiusalama"

Mimi "Sijamaanisha hapa kwenye mradi kaka,tuta tafuta eneo maeneo ya jirani tutaweka kambi"

Foreman "Tukubaliane,mtanipa elfu tano tano kila siku kwa muda wa wiki moja"

Aliendelea "Na iwe siri,ikiwa vinginevyo mi nitawaruka na kuwageuka"

Mimi "Hakuna tazizo kaka"

Foreman "Kamuite mwenzio mje niwakabidhi huku juu!"


Niliondoka kumfuata Mwakisaka na kumueleza kila kitu jamaa alichosema na jamaa akaniambia hakuna tatizo;Tuliondoka kumfuata yule foreman ambaye alituchukua mpaka kwa jamaa wengine akamuacha hapo Mwakisaka kisha akaniambia tena nifuatane nae,mimi pia akawa amenipeleka kwenye kikosi kingine.
Tukaanza kuifanya kazi ya kibarua rasmi na kwa siku tukawa tunapewa elfu 15,ishu ya kula pamoja na maji ya kunywa ilikuwa ni juu ya yako wewe kibarua uzuri ni kwamba,kwenye kundi ambalo mimi nilikuwepo walikuwa wamejitolea kuchanga fedha na kununua vyakula kisha kuna mtu walikuwa wanamlipa anakuja kuwapikia,hivyo na mimi baada ya kuingia kwenye kundi la wale jamaa niliamua kuchangia elfu 10 kwa kila wiki kwa ajili ya huo mpango.

Miongoni mwa wale jamaa pia walikuwa wametengeneza matenti ya maturubai kuishi hapo maeneo ya jirani,niliamua kichangia fedha na mimi ili kukaa hapo,sasa bahati nzuri ni kwamba wikiendi tulikuwaga tunapumzika na hiyo niliitumia kwenda kufata virago vyangu kwa kaka Kileri na kurudi kambini,sikutaka kabisa kuhangaika na mambo ya jiji la Dar es salaam,fokasi yangu ilikuwa ni kwenye kufanya kazi na kutunza malipo yangu kwenye simu.

Nilipopambana ndani ya miezi mitano kwenye ule mradi nilipata kiasi kisichopungua Tsh milioni 1.3,sasa nilimuomba Mwakisaka aniambie ni eneo gani ni zuri kwa kupanga chumba na angalau linakuwa na maisha nafuu kwa hapa Dar es salaam.

Mwakisaka "Mwanangu mimi nakaa Gongo la mboto na nikuzuri sana"

Mimi "Kwahiyo kipindi kile ulikuwa unatoka Gongo la Mboto mpaka Kwa Mushi?"


Mwakisaka " Nilikuwa nakaa kulekule kivule kwa ndugu yangu mmoja"

Aliendelea "Kama unataka chumba we sema nimpigie simu jamaa mmoja pale kitaa akutafutie chumba"

Mimi "Nahitaji kaka"

Mwakisaka "Basi ngoja nitamcheki mshikaji"

Kweli,baada ya Mwakisaka kuwasiliana na jamaa yake na kumjulisha nilikuwa nahitaji chumba jamaa alianza kutafuta na akasema endapo angepata basi angetujulisha.
Baada ya siku tatu yule jamaa aliyepewa kazi na Mwakisaka ya kutafuta chumba akawa amesema nyumba imepatikana maeneo ya mwisho wa lami lakini ni vyumba viwili ambavyo malipo ilikuwa ni elfu 45 kwa kila chumba na ilipaswa kulipwa kwa miezi 6.

Mwakisaka "Jamaa anasema nyumba imepatikana Gongo la mboto mwisho wa lami"

Mimi "Mwisho wa lami ni maeneo ya wapi?"

Mwakisaka "Hapo hapo Gongo la mboto sema ni mbele kidogo"

Mimi "Sawa,na wewe ndiyo unaishi huko?"

Mwakisaka "Hapana,mimi naishi Mzambarauni"

Mwakisaka "Ila jamaa anasema amepata chumba na sebule kwa elfu 45 kwa kila kimoja na inalipwa miezi 6,vp?"

Mimi "Sawa,hakuna tazizo"

Mwakisaka "Ngoja nimwambie amwambie mwenye nyumba atulie kesho kutwa tukakicheki"

Mwakisaka aliwasiliana na yule jamaa akawa amemwambia amwambie mwenye nyumba jumapili tungeenda kukitazama ikiwezekana nilipie kabisa.

Namshukuru Mungu baada ya kwenda kuingalia ile nyumba niliipenda na nikawa nimelipia miezi sita,hela iliyobaki nikanunua godoro na mashuka nikawa nimeyaweka na mimi kufunga chumba kisha kurudi Kigamboni kuendelea na kibarua.

Kila nilipokuwa ninapata hela nilikuwa nikinunua kitu kimoja baada ya kingine na kuweka ndani na hatimaye vyumba vikawa na muonekano mzuri,kiukweli pamoja na mateso ya kushinda juani niliyokuwa nayapitia kule kigamboni lakini nilihakikisha najinyima kiasi kwamba hadi malengo yangu yatimie.

Ule mradi wa Dege kuna muda ukawa umesimama kidogo hivyo kwa muda ule nikaenda kukaa kwangu nilikokuwa nimepanga,sasa pale nilipokuwa naishi kulikuwa na geti na tulikuwa wapangaji kadhaa na kila mtu alikuwa na ishu zake.

Sasa kuna jamaa mmoja alikuwa akiitwa Steve yeye tulitokea kushibana sana na tukawa marafiki,jamaa alikuwa akifanya kazi kampuni ya Tigo kama msajili line za simu,kwakuwa ule mradi ulikuwa umesimama kwa muda usiojulikana,jamaa aliniambia kama vipi aniunganishe na timu leader wake anipatie kodi ya kusajili line za simu nami nianze kuwa msajili laini.Jamaa aliniambia ni kazi ambayo ilikuwa na pesa sana ila watu walikuwa wakiichukulia poa.

Steve "Ngoja kesho nitamueleza team leader kama vipi akupe kodi ili uanze kufanya kazi"

Mimi "Kazi inafanyikaje kaka"

Steve "Kazi ni nyepesi sana kaka utaelekezwa namna ya kuifanya"

Kwakuwa kwa muda huo sikuwa na kazi baada ya kusimama kwa mradi,niliona jamaa atakuwa amenisaidia sana ili kuweza kujinasua na ukata ambao ulikuwa ukininyemelea baada kuwa nakula hela nilizokuwa nimezitunza bila kuzizalisha.



Itaendelea.........

Muendelezo Soma Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Dope
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 10.





Nilishitushwa na sauti ya Steve akiwa ananiita na kunigongea akitaka nimfungulie mlango,nilipochukua simu na kutazama muda ilikuwa imefika saa 4.Niliamka nikaenda kumfungulia jamaa mlango,kiukweli alionekana hayuko kawaida na sikutaka kumpa presha,nilimwambia aingie alale atulize akili.

Namshukuru Mungu kulipokucha,mimi niliwahi kuondoka nikamuacha jamaa akiwa amelala,kabla ya kwenda Kariakoo ilikuwa ni lazima kila msajili line kupitia pale ofisini Buguruni kusikiliza kikao na mambo mapya kisha kuelekea kwenye kituo chake cha kazi,nami ndivyo nilivyofanya!.Nilipofika Kariakoo nilielekea eneo ambalo nilikuwa nikihifadhia vitu vyangu vya kazi na kuja kuanza kupiga kazi.

Sasa wakati nafika pale,lile duka la Ally mpemba lilikuwa bado halijafunguliwa,mi niliweka zangu meza nikaanza kupiga kazi kawa kawaida,kiukweli kwa kipindi kile kulikuwa na wateja wengi mno,yaani ilikuwa ukifungua tu ile saa 2 asubuhi wateja wanaanza.Ilipofika mida ya saa 3 asubuhi,kuna gari aina ya Range Sport nyeusi iliyokuwa na Private Number iliyoandikwa " SALIM " ilisimama pembeni yangu kisha ukafunguliwa mlango akawa ameshuka yule Aunt ndugu yake na Ally Mpemba.

Aunt "Leo umeniwahi"

Mimi "Leo nimekuwahi Aunt,salama lakini"

Aunt "Mie niko salama kabisa sijui wewe huko utokako"

Mimi "Salama kabisa"

Wakati nikiwa naendelea kuzungumza na Aunt ile gari ikawa imeondoka kuelekea Kamata.Yule Aunt pamoja na ndugu yake Ally Mpemba walikuwa wakizungumza kiswahili cha kipwani pwani kama ambavyo wazanzibar wakizungumza!.

Ilipofika mida ya 5 asubuhi,alinipigia simu Steve na akawa ananiambia ya kwamba,yule demu wake wamekubaliana arudi nyumbani na yeye amemsamehe ili mambo mengine yaendelee,mimi kwakuwa nilishamshauri sana kuonekana kama natwanga maji kwenye kinu nilimwambia sawa,hakuna tatizo,sikutaka kabisa kuwashauri kwasababu niliona ni kama nilikuwa napoteza muda.

Mimi "Kwahiyo vitu anarudisha?"

Steve "Ndo naenda kuvichukua kaka"

Mimi "Kwahiyo Leo hujaenda Tandika"

Steve "Leo siendi kaka ngoja kwanza nikamchukue huyu"

Mimi "Poa,kama ukitoka funguo utaniwekea juu ya mlango hapo"

Steve "Leo sina ratiba ya kutoka kaka"

Mimi "Sawa,baadae"

Safari hii niliamua nikae pembeni katika kushuri kwasababu nilichokuja kugundua ni kwamba,mambo yote ya msingi niliyokuwa nikimshauri jamaa kuhusu demu wake,yeye alikuwa akimwambia kila kitu na hivyo mimi kuonekana mchonganishi!,hivyo nikaamua sitokaa tena nimshauri na kama ni kufa yeye afe tu!.

Ilipofika mida ya saa 9 mchana,Ally Mpemba akawa amekuja akiwa ndani ya kanzu nyeupe,alipofika pale nje kabla ya kuingia ndani ya duka lake akawa amenisalimu.

Ally mpemba "Assalam aleykum"

Mimi "Alekom salam"

Ally mpemba "Kwema?"

Mimi "Kwema kaka"

Ally mpemba "Leo wafunga saa ngapi?"

Mimi "Kama kawaida kaka saa 12"

Ally mpemba "Basi utanipa muda wako kidogo Leo sheikh"

Mimi "Sawa kaka"

Sasa mida ya saa 10 alasiri alipokuwa anatoka pale dukani akawa ameniomba kama itawezekana tuondoke wote kuelekea Aggrey.

Mimi "Si hakuna haja ya kutoa vitu vyangu"

Ally mpemba "We viache tu,nishamwambia Farah atakuangalizia usijali"

Niliondoka na Ally kuelekea mtaa wa Aggrey ambako huko nako nilikuta kuna duka kubwa la simu na ndani yake kukiwa na wafanyakazi kama 4 wakisaidiana kuuza,sasa tofauti na kule ni kwamba lile la kule niliko lilikuwa dogo na la pale Aggrey lilikuwa kubwa.

Ally mpemba "Mi huwa nashinda hapa mara zote,nisipokuwa kule basi wanipata hapa"

Mimi "Ok sawa kaka lete maneno"

Ally mpemba "Kuna kazi nataka unisaidie Master"

Mimi "Kazi gani tena kaka?"

Ally Mpemba "Ni kazi ya kawaida tu!"

Aliendelea "Mimi ninahusika pia na mambo ya caterings na nimewaajiri ndugu wa familia na watu wengine lakini ndugu zangu ni watu wa ovyo sana huwa hawapendi kazi za kujishughulisha wao wanapenda kukaa kama hivi unavyowaona"

Ally Mpemba "Sasa kila ninapokutazama nakuona wewe ni mpambanaji mtu wa bara na ndiyo maana nakuita Master"

Aliendelea "Mimi nataka tu unisaidie kitu kimoja na offcouse siyo msaada bali nataka tufanye kazi"

Mimi "Sawa kaka"

Ally Mpemba "Kwani huko Tigo mnalipana shi ngapi?"

Mimi "Kaka kule ninalipwa kwa kamisheni"

Ally Mpemba "Sawa naelewa ni kamisheni lakini malipo yao huwa yapoje?"

Mimi "Inategemea na laini nilizosajili na matumizi ya wateja kwa mwezi husika"

Ally Mpemba "Doo kwahiyo mteja asipotumia laini hulipwi!"

Mimi "Ni mara chache mteja aje kusajili line na asiitumie,sema huwa malipo yanategemea,kuna muda yanapungua na kuna muda yanaongezeka"

Ally Mpemba "Ok sasa mimi nataka unisimamie kwenye mradi wangu hata kwa muda wa mwezi tu Master halafu nikipata mtu muaminifu nitamuweka halafu wewe utaendelea na shughuli zako:

Mimi "Kaka kwanini mimi?"

Allya Mpemba "Mi unajua nilikuwa sikutilii maanani sana,kuna siku Farah akaniambia wewe ni mtu poa sana hata namna unavyo behave,kwa maana nilipokuta umeweka meza yako kando ya duka langu nilimwambia Farah unapaswa utoke pale ila akaniambia wewe ni mtu poa sana"

Aliendelea "Ninachotaka mimi ni kwamba,wafanyakazi wapo ila wewe ukanisimamie tu maana alikuwa anasimamia mama yangu mdogo lakini yuko Unguja anamuuguza me wake!"

Aliendelea "Wewe niambie tu unataka niwe nakulipa shi ngapi?"

Mimi "Kaka unajua sijawa na uzoefu na kazi unayotaka niifanye,hivyo itakuwa ngumu kujua unilipeje kaka"

Ally Mpemba "Sasa fanya hivi,wewe nenda kahifadhi vitu vyako halafu uje twende nyumbani mara moja"

Basi niliondoka zangu kurudi gerezani nikachukua meza,kiti pamoja na mwamvuli nikawa nimerudisha mahali ambapo nilikuwa nahifadhia.Baada ya hapo nikawa nimeondoka hadi Aggrey kisha Ally Mpemba akanichukua kuelekea Msimbazi uelekeo wa kituo cha polisi,tulitembea hadi pale Big Bon ambapo nikaona anatoa funguo wa gari kwenye kanzu yake kisha akabonyeza ile gari ikawaka taa na milango ikafunguka,ilikuwa ni ile ile Range ambayo asubuhi niliona dada yake akiwa anashushwa ambayo ilikuwa na Private Number,sasa kwa mara ya kwanza mwanaume kutoka Kijiji cha Mogabiri huko Ukuryani Tarime nikapanda Range,aisee asikwambie mtu na ndiyo maana kuna watu wako tayari kufanya kila aina ya ovu ili kujipatia fedha wanunue magari,ile ilikuwa ni moja ya gari nzuri kuwahi kupanda katika maisha yangu ya umasikini!.

Tuliondoka lile eneo tukaikamata Morogoro Road kisha safari ikaanza kwa spidi ya wastani,baada ya muda tukawa mbele ya nyumba moja maeneo ya magomeni Mikumi,ile nyumba ilikuwa ya kawaida sana kwa muonekano wa nje ila nilipoingia ndani kiukweli ilikuwa nzuri mno na usingedhani kama muonekano wa nje unasadifu kilichomo ndani!.

Baada ya kupiga honi na kufunguliwa geti gari ikawa imeingia pale uani na kupaki,sasa tulipoteremka kuna vitoto vya kike viwili vya kiarabu(Kipemba) tulivikuta hapo ndani vikawa vinamkimbilia Ally na kumrukia kwa furaha!.

Ally Mpemba " Hawa ni watoto wa Farah "

Mimi "Ooh sawa kaka"

Sasa pale nje nilikuta kuna vyombo vingi sana vya kisasa na majiko makubwa ya Gesi na mkaa,na ndivyo vilikuwa vyombo vilivyokuwa vinatumika kwenye shughuli za catering.

Ally Mpemba "Nimekuleta hapa ili ujionee mwenyewe,na ukishajionea najua utaniambia nikulipe kiasi gani master"

Aliendelea "Sasa wewe kazi yako utakuwa unahakikisha vyombo vyote vinaondoka hadi kwenye events na baada ya hapo utakuwa unahakikisha vyombo vyote vinarudi kama vilivyokuwa,baada ya hapo utakuwa unasimamia ishu ya usafi wa vyombo"

Aliendelea "Kikubwa wewe utakuwa msimamizi"

Baada ya yale maelezo angalau sasa ndipo nikaanza kupata uelewa wa kazi nitakayoenda kuifanya.

Ally Mpemba "Na bahati nzuri ni kwamba,events siyo kila siku,kama kutakuwa hakuna events yeyote wewe utakuwa unaendelea na shughuli zako,mimi nahitaji tu msimazi hadi pale atakaporudi mama mdogo au nitakapompata mtu sahihi,ila nakuomba kwa sasa unisaidie kwenye hili"

Mimi "Sawa kaka nimekuelewa"

Ally Mpemba "Ok sasa niambie niwe nakulipaje!"

Mimi "Wewe nilipe utakavyoona kaka"

Ally Mpemba "Wewe niambie kiasi utakachoona kwako kinafaa maana hii siyo shughuli nyepesi kama unavyodhani!"

Mimi "Tufanye hivi kaka,tukianza kazi ndiyo nitajua,nadhani kwasasa tusubiri kwanza "

Ally mpemba "Ok hakuna tatizo maadamu umeamua hivyo!"

Baada ya mazungumzo yale tuliingia kwenye gari tukawa tumeondoka kuelekea Kariakoo,sasa wakati tunarudi tulipitia njia ya Kigogo na tulipofika pale Karume,jamaa alinipatia elfu 20 ya nauli mi nikashuka kwenye gari yeye akawa ameondoka.Nilienda upande wa pili kupanda gari za Gongo la mboto na kuondoka zangu maskani.



Itaendelea.......

Muendelezo soma Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Oky
 
Kuna watu ni wajuaji humu hadi kero!!! Kila mtu analazimisha kuwa great thinker. Someni story mkalale kha! Yaani mtu anajifanya anachambua hadi basi. Mara utaskia Znz ukifika hawavai viatu vyeusi wewe ulivaa viatu gani😏 yaani ujuajiii
Asiongeze chumvi tu! Mambo yatakuwa sawa!

Mfano hiyo safari yake ya kwenda Chumbe imejaa ukakasi..
 
Zanzibar kuna Chumbe mbili.... moja ni kisiwa kabla ya kufika Unguja na Chumbe ya pili ipo karibu na Mbweni katika barabara ya kwenda Entebbe.

Master naona kashindwa kabisa kuelezea ni Chumbe ipi alikwenda! Kama ni Chumbe ya barabara ya kwenda Entebbe, hiyo haina msitu na bahari ipo mbali kidogo aidha eneo lote toka Chumbe hadi ufukweni kumejengwa, hivyo basi hakuna msitu wa aina ya simulizi ilivyosema.

Kwa upande wa kisiwa cha Chumbe, ni kisiwa kisichokaliwa na wenyeji, zamani wavuvi walipita hapo baada ya shughuli zao za uvuvi na ndio sababu kuna msikiti kisiwani hapo. Zaidi ya msikiti kuna mnara wa kuongezea meli na vibanda vya hoteli ya kitalii. Ni kisiwa ambacho kipo chini ya uangalizi na kinasimamiwa na kampuni binafsi!

Sijui Master alikwenda Chumbe ipi! Kama kuna mtu anajua ni vema akatufahamisha.
Gambushi kuna magorofa na mataa kuliko dar,ni katika ulimwengu wa kufikirika lakini.
Hizi ni hekaya majina yq watu na vitu havina uhusiano na ukweli relax
 
Back
Top Bottom