Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 04.




Sasa muda ambao mke wa anko anafika pale nyumbani mimi nilikuwa nyuma ya nyumba ambapo kulikuwa kuna kama kibustani kidogo ndani yake kulikuwa kumepandwa miwa ambayo ilikuwa imekuwa mikubwa na hakukuwa na walaji,niliona nikate zangu muwa nikaa chini nikaanza kutafuna,kumbe aliingia chumbani anakolala yule mzee ambaye ni baba yake na akakuta amejisaidia kitandani na hakukuwa na mtu aliyemwangalia na kumjali,kwa mawazo yake yeye alidhani mimi nimemuona yule mzee na nikamuacha kama alivyo ili aendelee kuteseka!.
Akili na mawazo yake yalimtuma vibaya kwasababu sikuwa nimeingia mle chumbani tangia mchana,pia yule mzee alikuwaga kama na kakiburi fulani hivi ambako kalikuwa ka kijinga,anaweza kuwa amebanwa na haja kubwa wala asiite mtu yeyote,utakuta ameinyanyuka ameingia chooni na amechafua vibaya bila hata kuflashi.Inawezekana alifanya makusudi siku ile ili kunikomoa.

Kumbe muda huo Anko anapewa makavu laivu ilikuwa ni hiyo ishu na bahati mbaya sana Anko wangu alikuwaga akoromi kwa yule mwanamke bali hasira za kugombezwa na mkewe zilikuwaga zinaishia kwa wanae au mimi kwa wakati ule nipo kwake.

Muda huo ambao nipo zangu natafuna miwa sina habari,kumbe alimwambia yule mfanyakazi akaingia mle ndani akatoa yale mashuka akawa amemnyanyua mzee akampeleka bafuni mzee akajisafisha kisha akatandika shuka safi na kuweka mazingira ya chumba poa.

Mimi sikufahamu chochote kwasababu nilipomaliza kula miwa nikazunguka kule mbele ya nyumba ndipo nikakuta gari ya mke wa anko ikiwa imepaki nikajua atakuwa amerudi,sikutaka kuingia ndani kwasababu ilikuwa bado mapema,niliingia stoo nikachukua fagio la nje nikaanza kufagia pale nje.

Nilipomaliza niliingia ndani kuoga na kubadili nguo ili nije nikae sebuleni nitazame luninga,wakati naingia mle ndani nilikuta mzee amelala na kitandani kukiwa na shuka nyingine,sikufahamu kumbe dakika chache zilizopita hali ya mle ndani haikuwa nzuri,sasa huo usiku anko alivyorudi ndipo mkewe akamuamshia mtiti!.


Baada ya hayo malumbano Anko alivyorudi sebuleni alikuwa amebadirika na sikutaka kusema chochote mimi niliendelea kutazama luninga,chakula kilipotengwa alielekea kula na alipomaliza aliingia chumbani kwake!.Mkewe yeye sikuonana nae kwa siku hiyo.

Asubuhi kama kawaida wao waliondoka wakawa wamelekee kazini,pale nyumbani nikawa nimebaki mimi,yule binti wa kazi pamoja na mtoto mkubwa wa anko ambaye naye aliondoka ilipofika mida ya saa 3 asubuhi.Sasa baada ya yule mtoto wa Anko kuondoka,yule binti wa kazi alikuja kuniita nikanywe chai,muda huo nilikuwa nje napambana kungolea nyasi kwenye maua yaliyokuwa kando ya fensi.

Binti wa kazi " Hivi jana ulikuwa wapi?"

Mimi "Jana?,Jana saa ngapi?"

Binti wa kazi " Aliporudi Mama"

Mimi "Nilikuwa kule Bustanini"

Binti wa Kazi "Jana mama kagomba"

Mimi "Alikuwa anagomba kuhusu nini?"

Binti wa kazi "Aliporudi aliingia chumbani kwa babu akakuta babu kajinyea,alikuwa anakuulizia mi nikajua labda umetoka!"

Mimi "Alijenyea saa ngapi?,mbona mchana nilipotoka ndani alikuwa tu vizuri"

Binti wa kazi "Alikusema maneno mabaya sana,we acha tu"

Mimi "Mimi siyo mjinga nimuone huyo mzee akiwa anashida niache kumsaidia,mbona siku zote namuosha na kumpeleka chooni na mpira nambadilishia!"

Mimi "Jana nilikuwa bustanini na sikutoka nje kabisa"

Mimi "Kwani kabla sijaja hapa nani alikuwa akimuangalia mzee?"

Binti wa kazi "Nani zaidi yangu?wanae tu wala hawana time na babu yao"

Baada ya mazungumzo ya muda kadhaa nilinoti kitu kwa yule dada wa kazi ambacho hakutaka kabisa kuniambia,kwa kifupi yule mke wa anko inaonekana alitoa shiti nyingi dhidi yangu,niliamua kutulia na kutafakari.
Sikwenda kwa Anko uenda kwakusema nimepigwa na maisha ili anifadhili la hasha,nilienda pale kwasababu wakati nafika mjini mwenyeji wangu alikuwa hapatikani,sasa kuna muda nilikuwa nashangaa wanavyonichukulia ni kana kwamba nimepigwa na maisha!.

Baada ya kupata kifungua kinywa niliamua nimsubiri Anko akitoka kazini ile jioni nimuage na kesho yake nisepe niwaache wapambane na matatizo yao na roho zao mbaya.Kweli,usiku ule kabla ya kula tukiwa pale sebuleni tukiangalia taarifa ya habari,nilimwambia kesho mimi nitaondoka.

Anko Nico " Utaondoka kwenda wapi?"

Mimi "Nitaenda kwa yule mtoto wa baba mkubwa"

Anko Nico " sawa siye tupo"

Baada ya hayo mazungumzo niliona kabisa nilikuwa sitakiwi.Ukiachilia Anko,lakini mkewe na watoto wa Anko walikuwa ni watu ambao hawana time na mtu,tangia nimefika hapo hawakuwahi hata kusema na mimi wala kujua hali ya maisha ya shangazi yao,walikuwa ni watu ambao hawakuwa na muda kabisa,pengine uzungu uliwaharibu au walilithi tabia za kwao mama yao.

Kesho yake nilimuaga yule mzee pamoja na yule binti wa kazi nikaondoka zangu,nilipotoka nje nilitembea hadi kituo cha daladala nikapanda kuelekea tegeta.

Kwakuwa nilikuwa nimeshawasiliana na Kileri akawa ameniambia anakaa Kivule na hivyo ilipaswa nipande magari yatakayonifikisha ubungo stendi ya daladala na nikifika hapo nipande za gongo la mboto nikashukie banana kisha nichukue za kivule.

Namshukuru Mungu nikawa nimefika na jamaa akaja kunichukua tukaelekea kwake.Nilipofika kwa jamaa nilikuta anakaa kwenye nyumba ambayo bado haijaisha na nilikuta mafundi wakiwa wanaweka vigae kwenye vyumba baadhi.


Kileri "Karibu wa kwetu,hapa mimi ndipo naishi na familia yangu"

Mimi "Hongera kaka umejitahidi"

Kileri "Kawaida tu,naipeleka mdogo mdogo mpaka itaisha,mjini hapa ukiwa na kwako unaepuka usumbufu wa kodi"


Baada ya mazungumzo ya hapa na pale,jamaa akawa ameniambia kesho yake tungeenda Tandika ambako alidai ndiko anakofanyia biashara ili nikajionee namna biashara ilivyo shamiri.

Ilipofika asubuhi tuliondoka kuelekea huko Tandika kama alivyokuwa ameniambia.Tulipofika hapo Tandika kuna duka moja la vyombo tuliingia lakini kuna kitu kikanishangaza.


Itaendelea......

Muendelezo Soma Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani
Kuna vitu nimeanza kuviamini kwa wale mnaosema jamaa anacopy na kupaste...

1. Scenario ya ugonjwa wa Babu ,
Iko hivi, babu yangu alishawahi kuugua ugonjwa Kama huo na aliwekewa mpira hivo hivo...
Huwezi amini alikuwa na ukorofi uliopitiliza.. saa zingine Kama hivo anajisaidia kitandani , yaani alikuwa na kiburi Cha hali ya juu.. jamaa nimekuelewa Sana hapo...!
Lakini pia Mjomba wako Niko sio kwamba alikuwa hakupendi..la hasha ni vile tu alikuwa amewekwa kwenye kiganya na mkewe! ...
Na umesema ni marehemu kwasasa... , na umesema mkewe ni MTU wa kaskazini... Najaribu kuwaza beyond the scene [emoji848][emoji855]

2. Jamaa yako kuishi Kivule...
This is true, Wakurya wengi Sana wanaishi ukanda huu wa kuanzia Banana , kwenda Mbele huko Kivule, Bombambili, Kwa mwanagati, na maeneo mengine ya Gongo la mboto...

Story yako naanza kuiamini japo wengine wanaibeza...Kuna vitu vya kujifunza pia...
Tuendelee
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 18.



Nilifanikiwa kufika Mbeya na kuanza kuzunguka kukusanya viazi huku nikiendelea kuwatumia madalali ili kufanikisha kwa haraka niweze kurudi mjini kuuza mzigo.

Nilitumia takribani wiki 1 kununua mzigo na kupakia kwenye fuso kisha kuuleta mjini Dar es salaam,nilipofikisha mzigo mjini hali haikuwa kama nilivyodhani mwanzo,wale madalali ambao niliongea nao tangu mwanzo nilipokutana nao walianza kuniambia mzigo kwasasa umekuwa mwingi na umeshuka bei,niliamua mwenyewe kupita na kufanya utafiti kwenye masoko ya Ilala,Buguruni na Mabibo na kugundua ya kwamba wale madalali walikuwa na nia ya kunipiga kwasababu hakukuwa na mzigo mwingi wala nini!,nilichoamua ni kuanza kuuza ule mzigo mwenyewe,ule mzigo kiukweli ulinikata sana na namshukuru Mungu niliambulia kiasi kidogo cha pesa kwasababu kuna magunia mengine ya viazi yalioza kwasababu ya kukaa chini muda mrefu bila kuuzwa,nilichogundua ni kwamba wale madalali mwanzo walikuwa wakinipanga ili nilete mzigo mjini na nikiisha ufikisha wao ndiyo wanipangie bei ya kuuza,wao wajipatie pesa nyingi kupitia mzigo wangu halafu mimi nipate faida kidogo,sasa nilipowakataa wakasambaza maneno kichini chini kwamba mzigo wangu haufai hivyo kila mteja akawa anaupita tu kama anaaga maiti kiukweli ile hali ilinifedhehesha sana hadi kuna watu ambao ni wema walinishauri niuuze wote kwa jamaa mmoja pale Mabibo ambaye alikuwa ni dalali na alinipatia fedha nusu ya mtaji,kiukweli kwasababu ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kuifanya ile biashara sikutaka kabisa kuendelea nayo kwasababu ilikuwa na fitina kubwa mno,na mpaka leo sielewi watu wengine wanawezaje kufanya biashara ya viazi.

Baada ya kuona hiyo biashara imenishinda kwasababu ya fitina ya mswahili,niliamua kurudi zangu kwenye usajili wa laini za simu huku nikiendelea na majukumu mengine ya usimamizi wa miradi ya Brother Ally Mpemba.

Baadae nilichokuja kugundua ni kwamba,hakukuwa na fitina za mswahili wala nini,ile hela ambayo nilikuwa nikiipata kila ijumaa ya mwisho wa mwezi kiukweli kila nilipojaribu kuifungulia biashara iligoma kabisa kwasababu ukiachilia mbali biashara hiyo ya viazi,nilifungua duka la nguo za kike pale Tandika na kuna jamaa mmoja kutoka Iringa nilimuajiri aniuzie,ilikuwa ni siri sana na sikutaka mtu yeyote ajue kuhusu hilo,lile duka halikufikisha hata miezi 6 likawa linaporomoka,mtaji na faida havikujulikana vinapotelea wapi,nikajaribu kumchunguza yule bwana mdogo nikadhani uenda akawa ananipiga kumbe haikuwa hivyo,lile duka nikaamua kuliuza na bidhaa baadhi zilizokuwa zimebaki,kwakuwa mwanzo nilipata ugumu kuelewa ila kadiri siku zilivyosonga ndipo akili na ufahamu vikanijia nikafahamu ya kwamba ile hela ilikuwa na matatizo,sasa nilichoamua ni kwamba ile hela niingize kwenye ujenzi wa nyumba yangu nitakayokaa huko Chanika kwenye uwanja wangu(Nitakuja kueleza kilichotokea maana hali ilikuwa mbaya kuliko nilivyodhani).

Sasa kwakuwa nilikuwa na kiasi cha fedha ambacho nilibaki nacho,niliamua kununua ramani ya nyumba na kwenda kuanza ujenzi kwenye uwanja wangu kule Chanika ili ule uwanja usiendelee kuota nyasi,baada ya kupiga msingi na jamvi niliamua kuachia hapo ili niendelee kuvuta nguvu za kupandisha boma.

Sasa kuna siku Ally Mpemba alinipigia simu akawa amenitaka nionane nae pale kwake ili tupange mipango kadhaa kwasababu yeye alikuwa anahitaji kusafiri kama alivyokuwa ameniambia awali,tulikubaliana tungeonana jumapili ya wiki hiyo pale nyumbani kwake kwasababu pia hata mimi jumapili mara nyingi nilikuwa napumzika.

Niliondoka zangu kuelekea kwa Ally na bahati nzuri nilimkuta akiwa nyumbani.


Ally Mpemba "Salama?"

Mimi "Salama kaka"

Baada ya salamu na mazungumzo mafupi,jamaa aliingia ndani ambako alichukua muda mrefu kidogo ndipo akawa ametoka.

Ally Mpemba "Pika chakula ule master,hapa ni kama kwako wala usione taabu!"

Mimi "Kaka usijali niko vizuri"

Ally Mpemba "Ulikula muda gani?"

Mimi "Nimekula muda si mrefu!"

Ally Mpemba "Sawa kama ndivyo"

Aliendelea "Mimi nimekuita weye kwasababu hapo awali nilikueleza ya kwamba nina safari ya kwenda Oman,hivyo nikakuomba unisitiri master!"

Mimi "Sawa kaka"

Ally Mpemba "Kuna jambo nahitaji nikwambie na nakuomba Union unionyeshe uaminifu wako kama nilivyokuamini"

Mimi "Kaka ina maana huniamini tu!"

Ally Mpemba "Mimi nakuamini tangua siku ya kwanza ila nadhani unakumbuka nilikutahadharisha ya kwamba kuna mambo ukiyapayuka kwa watu wengine utakachokutana nacho basi utajua mwenyewe!"

Aliendelea "Ndugu zangu siwathamini kama ninavyo kuthamini weye,hivyo thamani ninayokupatia ni kubwa mno"

Aliendelea "Hivyo mimi naondoka na itanichukua takribani mwezi mmoja huko,nakuomba usimamie shughuli zangu hasa ile niliyokukabidhi huko kwengine Farah atasimamia!"

Mimi "Sawa kaka nimekuelewa!"

Ally Mpemba "Vipi mambo yako lakini yanakwenda?"

Mimi "Yanakwenda kaka"

Ally Mpemba "Sawa jitahidi ufanye vema kama ulivyoambiwa na nakuhakikishia wewe ukiwa mwaminifu hakika utakuwa mkubwa hapa Bara kote na hata huko pwani hakuna atakaye kugusa kwa utajiri!"


Niliendelea kumsikiliza Ally Mpemba namna alivyonitia moyo kuhusu ile bangiri lakini sikutaka kumwambia kabisa kuhusu biashara zangu zote mbili zilivyonipatia hasara ikabidi nikaushe.

Ally Mpemba "Kuna jambo ambalo kabla ya kuondoka naomba ulifahamu maana nilazima ndipo uweze kufanya maamuzi ya kunisitiri"

Aliendelea "Bila shaka Huyu kiumbe ninayeishi naye hapa kwangu unamfahamu!"

Mimi "Ndiyo kaka namfahamu"

Ally Mpemba "Sasa nadhani unaelewa huwa nisipokuwepo nakuomba unisaidie kumwandalia chakula"

Mimi "Ndiyo kaka"

Ally Mpemba "Naomba leo nikueleze ukweli na usije kujaribu kumueleza mtu,mimi na wewe tumekuwa wamoja na siri yako ni yangu na naomba siri yangu iwe yako,huwezi kufanikiwa kama hutaweza kutunza jambo!"

Aliendelea "Huyo unayemuona hapa she's my blood sister,na ndiye mwanamke ninaye mpenda kuliko wanawake wote duniani,jina lake si Maya kama unavyodhani,jina lake ni Zahra,hakuna mtu yeyote anayejua Zahra yuko hapa ila wewe,hivyo nakuomba uwe makini na siei hii na nakuomba sana!"

Kiukweli Ally Mpemba alionyesha hali fulani ya huruma na upole baada ya kumuongelea Maya,nilikuwa nikimuangalia Ally Mpemba alionyesha usoni ni mtu wa huruma sana lakini kiuhalisia hakuwa kama ulivyomdhania.

Ally Mpemba "Nikitoka Oman nitakuja kukueleza vizuri ila nachotaka ujifunze na unisitiri!"

Aliendelea "Oman sina mke kama nilivyokwambia hapo awali ila kuna jambo kubwa ambalo na wewe utalifanya siku moja,nikirudi nitakujuza ila kwasasa nakuomba unisitiri!"

Kiukweli hali haikuwa rahisi kama nilivyodhani ila kwakuwa nilikuwa tayari nishaingia kwenye mfumo wa Ally Mpemba sikuwa na jinsi ilibidi nitekeleze na kufanya nilichoambiwa ili kuendelea kujipatia pesa.


Ally Mpemba "Nitakapoondoka nakuomba kila ijumaa uwe unalala kwenye chumba changu hicho!"

Mimi " Sawa kaka nimekuelewa"

Ally Mpemba "Naomba usiwe unashituka kwasababu Zahra atakuwa anakuja mnalala naye na atakachokuwa anataka umfanyie naomba umfanyie usiogope!"

Mimi "Hawezi kuniletea fujo kaka?"
Ally Mpemba "Hawezi,yeye akishakula huwa hana shida,hakikisha kila ijumaa haufungi mlango wa chumba changu,yeye atakuwa anaingia na mnalala nae kisha akitaka chochote mpatie"

Aliendelea "Bila shaka master wewe ni rijali na kama huwezi kabisa basi mimi kuna dawa nitakupatia utakuwa unakunywa ili uweze kuwa imara kitandani!"

Mimi "Hapana kaka wala usijali niko Imara sana!"

Ally Mpemba "Sawa nitashukuru sana kama umeamua kunisitiri!"

Mimi "Kaka asije akajua mimi siyo wewe akaniletea vurugu!"

Ally Mpemba "Hapana hawezi kufanya hivyo,akishaingia chumbani atalala kitandani na wewe nakuomba usipoteze muda wala usione huruma,mshughulikie kikweli kweli,ikifika asubuhi ataamka mwenyewe ataondoka chumbani kwake!"

Mimi "Sawa kaka nimekuelewa!"

Ally Mpemba "Japo anayo harufu ila nakuomba usionyeshe hali ya kujuta maana hiyo harufu ndiyo pesa yenyewe!"

Aliendelea "Ukifanya vema utapata zaidi na utakuwa mkubwa sana"

Mimi "Sawa kaka nimekuelewa kabisa na sitokuangusha"

Ally Mpemba "Usije kuruhusu mtu yeyote kuingia humu ndani zaidi yako!"

Mimi "Sawa"


Ally Mpemba "Sasa jiandae kesho twende pale TRA ukachukue TIN,kuna jamaa pale nishampa hela nitamkabidhi kwako akufanyie mchakato wa leseni ya gari!"

Basi baada ya yale mazungumzo Ally Mpemba alinikabidhi laki 5 kisha akaniambia kesho asubuhi mida ya 2 tuonane ili tuelekee TRA kwa ajili ya ishu ya leseni.Kiukweli nilibaki kushangaa namna Ally Mpemba alivyokuwa na ujasiri wa kulala na dada yake kitanda kimoja na kumuingilia kimwili.Haikuwa kazi ndogo ila niliamua kupiga moyo konde kwasababu nilikuwa ninataka pesa na mimi niliamua kuwa na roho ngumu.

Baada ya siku tatu kufatilia masuala ya leseni,namshukuru Mungu nilijipatia leseni yangu ya kwanza kabisa kwa ajili ya uendeshaji wa gari.Nilipopata leseni Ally Mpemba alinipatia ile gari yake iliyokuwa mpya aina ya Aud A4,kiukweli nilipata kiburi sana kwa kujiona mimi ndiye mimi,sasa kabla Ally hajaondoka kuelekea Oman alinipatia maelekezo namna ya kuimiliki ile gari.

Ally Mpemba "Master nakuomba tu kwenye hii gari mpya ninayokukabidhi ukiamua kuwabeba marafiki zako basi wakae viti vya nyuma,hii siti ya mbele asije akaikalia mtu yeyote labda kama akitokea ndugu yangu,tafadhali sana nakuomba!"

Mimi "Ndugu zako siwafahamu kaka zaidi ya mama yako mdogo pamoja na Farah"

Ally Mpemba "Hao ndiyo ninao maanisha,kama Farah akikuona na akihitaji lift usiache kumbeba na asikae nyuma bali akae kiti cha mbele,wengine wote usithubutu kuwabeba mbele"

Mimi "Nimekuelewa kaka nitakuwa muangalifu!"

Ally Mpemba "Sawa mimi nadhani Alhamisi ijayo naondoka,hakikisha jumatano utakuja kulala hapa ili nikiwa naondoka kuna pesa nikukabidhi pia nikukabidhi na funguo"

Mimi "Utachukua muda mrefu huko?"

Ally Mpemba "Haitapungua mwezi!"

Mimi "Sawa kaka"

Baada ya kuniambia niwe muangalifu na ile siti ya mbele nilivuta picha lakini sikupata majibu,lakini nikakumbuka mara zote nimekuwa nikimuona na ile range akiwa amebeba mtu basi uishia kukaa nyuma na siti ya mbele hukaa bila mtu na mimi pia mara zote nimekuwa nikipanda ile Range ndivyo ilivyokuwa!.

Kweli,baada ya siku kufika Ally Mpemba aliondoka akawa amenikabidhi funguo za nyumba yake pamoja na kiasi cha shilingi milioni 3 na akawa ameniambia amempatia Farah maelekezo endapo zikiisha nimuone atanipatia nyingine,pesa aliyonipatia ilikuwa ya matumizi ya kawaida ya kununulia vyakula vya Maya pamoja na matumizi yangu.Nilifurahi sana maana niliona kila kitu sasa kipo mikononi mwangu na nilipanga kiukweli marafiki na ndugu wanitambue mimi ni nani kupitia lile Audi A4.

Baada ya Ally Mpemba Kuondoka hiyo Alhamisi,ilipofika ijumaa kama kawaida nilienda zangu kazini pale Kkoo kusajili line za simu,ilipofika mida ya saa 10 jioni nilimuaga Farah nikamwambia nitawahi kufunga kuna mahali nawahi.

Farah "Mbona mapema leo!"

Mimi "Kuna mahali nawahi Aunt!"

Farah "Sawa,siunarudi lakini au ndiyo hadi kesho!"

Mimi "Hiyo hadi kesho dada"

Niliondoka zangu nikaenda kununua vyakula vya maya kama kawaida kisha nikaelekea nyumbani kwa Ally Mpemba,nilipofika kama kawaida nilichukua kitambaa kile cheupe nikatandika pale mezani kisha nikaweka vile vyakula,baada ya kuweka vile vyakula nilifunga mlango kisha nikawasha mchuma nikatoka zangu kuelekea kupata chakula ili niwahi kurudi kufungua kile chumba cha Maya.

Nilipomaliza nilirudi mdogo mdogo na ile gari huku nikiendesha kwa madaha kama yangu vile,ilipofika mida ya saa 1 usiku niliwasha taa kisha nikawa nimetoka zangu nje,kiukweli sikutaka kabisa kumuangalia Maya,nilichoamua ni kwenda kuzurura na ikifika mida ya 3 usiku nirudi kulala.Kweli,niliporudi nyumbani kwa Ally Mpemba kama kawaida niliingia chumbani kwake nikawasha taa na sikufunga mlango,kile chumba kilikuwa ni kizuri na kisafi kupita mfano,sikutaka kabisa kuzima taa,niliingia bafuni kuoga kisha nikarudi kujitupa kitandani kulala huku nikiendelea kumsubiri Zahra(Maya)niliyeambiwa na Ally ya kwamba nikiacha chumba wazi ataingia mwenyewe.

Kweli,haikupita hata nusu saa nilimuona Zahra akiingia chumbani akiwa uchi kama ambavyo siku zote huwa.



Itaendelea................
@Queen Kan
 
Umughaka episode ifuatayo isimulie kwa details zaidi hasa kwenye tukio la kumla Maya. Ikiwezekana episode nzima simulia ya chumbani tu ukiwa na Maya achana na vipengele vya kwenda kula kiepe wala kwenda kusajili line.

Tunahitaji kujifunza kitu hapa mkuu
 
Umughaka episode ifuatayo isimulie kwa details zaidi hasa kwenye tukio la kumla Maya. Ikiwezekana episode nzima simulia ya chumbani tu ukiwa na Maya achana na vipengele vya kwenda kula kiepe wala kwenda kusajili line.

Tunahitaji kujifunza kitu hapa mkuu
Yaan iwe full kama kupapasa makalio ya maya na akawa anatoa milio ya kimahaba,akamgusa mbususu akakuta imelowa,basi akamgeuza mbuzi kagoma kachomeka mashine kaanza kupush taratibu huku maya akikata viuno kama feni,umughaka akaanza kupush kwa nguvu mara wazungu hao,akaunganisha na kumuweka maya kifo cha mende na kuanza kuzinyonya taratibu chuchu za maya zilizokuwa zimesimama huku maya anajinyonga nyonga kwa utamu,jamaa akaanza kumpeleka moto upya huku maya anatoa milio ya kimahaba tu

Baadae maya akaomba kuingiliwa kwenye jicho
 
Kuna vitu nimeanza kuviamini kwa wale mnaosema jamaa anacopy na kupaste...

1. Scenario ya ugonjwa wa Babu ,
Iko hivi, babu yangu alishawahi kuugua ugonjwa Kama huo na aliwekewa mpira hivo hivo...
Huwezi amini alikuwa na ukorofi uliopitiliza.. saa zingine Kama hivo anajisaidia kitandani , yaani alikuwa na kiburi Cha hali ya juu.. jamaa nimekuelewa Sana hapo...!
Lakini pia Mjomba wako Niko sio kwamba alikuwa hakupendi..la hasha ni vile tu alikuwa amewekwa kwenye kiganya na mkewe! ...
Na umesema ni marehemu kwasasa... , na umesema mkewe ni MTU wa kaskazini... Najaribu kuwaza beyond the scene [emoji848][emoji855]

2. Jamaa yako kuishi Kivule...
This is true, Wakurya wengi Sana wanaishi ukanda huu wa kuanzia Banana , kwenda Mbele huko Kivule, Bombambili, Kwa mwanagati, na maeneo mengine ya Gongo la mboto...

Story yako naanza kuiamini japo wengine wanaibeza...Kuna vitu vya kujifunza pia...
Tuendelee
Kaa Kwa kutulia endelea kufurahia
 
Gari ina mashariti hvyo na bado unataka kwenda nayo kwa ndugu zako

Ningekuwa mimi hilo gari nisingeliendesha kabisa,
Mfano trafik wamekumata wanakwambia twende kituoni utamwambia akae nyuma!?
Kisheria trafik haruhusiwi kupanda gari aliyoikamata. Usije ukaruhusu hili, unaweza ukawekewa vitu haramu kwenye siti.
 
Back
Top Bottom