Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 14.




Mimi "Nishafika"

Warda "Umesimama wapi?"

Aliendelea "Ooh ok nishakuona"


Baaada ya nusu dakika alikuja mwanamke mmoja mwenye asili ya uarabuni akiwa amevaa hijab nyeusi ikiwa imempendeza sana kutokana na rangi ya ngozi yake.

Warda "Bila shaka wewe ndiye uliyetumwa na Ally"

Mimi "Yes ndiye mimi "

Warda "Unaitwa nani?"

Mimi "Naitwa Umughaka"

Warda "Mhh mbona Ally hakunitajia jina hilo!"

Mimi "Kaka Ally amezoea kuniita Master,Umughaka ndiyo jina langu halisi"

Warda "Ooh sawa nimekuelewa"

Aliendelea "Ngoja kwanza nimpigie simu halafu nikupe uongee nae"

Alichukua simu yake akaanza kumpigia simu Ally Mpemba na wakaanza kuongea,baada ya kuongea akanipatia na mimi simu ili niongee na Ally,baada ya kujiridhisha aliniambia nifuatane nae.Tulitembea kama hatua kumi kisha tukaingia kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa ni ghorofa,ile ghorofa ilikuwa ni Apartment ya watu kuishi na haikuwa kwa ajili ya ofisi.

Baada ya kufika ndani tuliingia kwenye lift nikaona yule dada anabonyeza batani ambayo ilionyesha namba 4,ile lift iling'oa nanga na baada ya sekunde kadhaa tukawa tumefika kwenye floor namba 4,tulipofika tulitembea hatua 3 tukawa tumefika kwenye chumba ambacho baada ya kukifungua tuliingia ndani.

Warda "Nisubiri hapo "


Aliingia chumbani ambako hakutumia muda mwingi akawa ametoka na pochi kubwa ambayo ilikuwa imetuna.

Warda "Hizi ni pesa ambazo Ally amesema nikukabidhi sasa kabla ya kuondoka inapaswa uzihesabu ndipo uondoke"

Alizitoa zile hela kwenye ile pochi kubwa ya kike,kiukweli zilikuwa ni pesa nyingi sana.Nilianza kuzihesabu na kuzipanga ndipo nilipata jumla yake milioni 40.Wakati nazihesabu alikuwa amekaa akiniangalia huku akiendelea kuchezea simu yake.

Mimi "Tayari"

Warda "Umepata bei gani?"

Mimi "Milioni 40"

Warda "Ok uko makini"

Alichukua karatasi pamoja na wino akawa ameweka pale juu ya meza na kuniambia.

Warda "Shika hii"

Aliendelea "Utasaini hapa na hapo chini utaweka dole gumba "

Basi nikafanya kama alivyoniambia na nilipomaliza alichukua simu yake kisha akampigia simu Ally Mpemba.


Warda "Haya nishamkabidhi pesa yako,huyu hapa ongea nae"

Ally Mpemba "Master,huo mzigo nenda kaniwekee benki,nakutumia sasa hivi vielelezo"

Mimi "Sawa kaka"


Warda "Ngoja nikupatie kibegi kidogo,huo mkoba nina kazi nao"

Sasa baada ya kupewa kibegi kidogo,niliziweka zile hela kwenye kile kibegi huku akili yangu ikiwa imechanganyikiwa kabisa,nilipanga nitoroke na zile hela,baada ya kushuka ghorofani nilianza kutembea mdogo mdogo kuelekea mnazi mmoja.

Nilikuwa najisemea uenda ndiyo wakati ambao Mungu aliamua kunitoa kwenye umasikini kupitia zile hela za Ally Mpemba kwa maana hata kama ningeondoka zangu kurudi Mwanza asingepata kwasababu ni mtu tu ambaye nilikutana nae kkoo na halikuwa hanijui kiundani wala haifahamu familia yangu,kiukweli nilikuwa kwenye vita nzito kuhusu zile fedha lakini niliamua nizipelekea Benki ili kuendelea kuonyesha uaminifu wangu kwa Ally,nilisema kama ni umasikini niliandikiwa basi ningekufa masikini tu hata kama ningekimbia na zile hela,pengine ni heri kufa masikini kuliko kuiba cha mtu ambaye ufahamu kakipata vipi,Uaminifu kwangu hata kama usingenilipa lakini ungenijengea heshima kubwa miongoni mwa marafiki na watu wa karibu,hivyo niliamua kuwa muaminifu ingawa nilikuwa nahitaji sana fedha.

Nilitembea kwa haraka sana hadi katikati ya jiji mtaa wa Azikiwe ambapo kwa mujibu wa maelekezo ya Ally Mpemba ilipaswa niende hapo ilipo benki ya Crdb kuziweka hizo fedha.

Baada ya kumaliza kila kitu pale benki,niliondoka zangu kurudi kkoo,nilipofika kwakuwa muda nao ulikuwa umeenda sana,nilimwambia Aunt Farah anipatie kile kiasi ambacho aliambiwa na Ally anipatie ili niondoke zangu kununua mahitaji ya siku hiyo kisha niondoke nikaandae mapema.

Aunt Farah alinikabidhi laki tatu ambazo kwa mujibu wa maelekezo ya Ally Mpemba ni kwamba,laki mbili ningeitumia kwa mahitaji ya vitu kwa siku zilizokuwa zimebaki hadi yeye kurudi na ile laki moja ingekuwa kwa ajili ya matumizi yangu ya kawaida.

Kweli,ile kazi niliifanya kwa uaminifu mkubwa mno hadi siku ambayo alirudi Ally mpemba alikuwa akinishangaa namna nilivyokuwa muaminifu kiasi kile na sikuwahi kumwambia mtu yeyote siri ile.


Ally Mpemba "Kaka kati ya watu na wewe ni mtu!"

Mimi "Kwanini kaka?"

Ally Mpemba "Ndugu zangu si waaminifu kama wewe ulivyo muaminifu"

Aliendelea " Sielewi hata nitakulipa nini!"

Mimi "Usijali kaka haya ni maisha tu!"


Kiukweli nilikuwa najiuliza mle ndani kwa Ally kulikuwa na kitu gani lakini nilikuwa nakosa jibu kwasababu ndani ya siku zote hizo nimekuwa nikiwinda nipate kukiona lakini nilikuwa naishia kusikia sauti tu,mimi sikutaka kuonyesha kama nina wasiwasi,nilichofanya ni kwamba nikiwa nazungumza nae yeye aelewe mimi sifahamu chochote na nilikuwa napotezea mambo mengine ili asije kunoti kitu kutoka kwangu.

Niendelea kupiga kazi yangu ya usajili wa line za simu huku na ile kazi ya usimamizi wa Catering ikiendelea,kiukweli kama kuna muda ambao nilitengeneza pesa ilikuwa ni kipindi hicho,baada ya kupata pesa ya kutosha,nilimtafuta dalali akanitafutia uwanja maeneo ya Chanika Zingiziwa chenye ukubwa wa 25 x 20 nikawa nimenunua Milioni 3.

Nikawa nimepanga nipambane sana ili nikusanye fedha nyinngine nianze ujenzi mdogo mdogo ili nitoke kwenye nyumba za kupanga na mimi niamie kwangu.

Kuna siku tulipata tenda ya kuhudumia chakula maeneo ya Mikocheni,sasa Ally akawa ameniambia siku iliyokuwa inafuata nisiingie kazini ili niende kuwasimamia wale kina mama na vijana kama kawaida yangu maana ndiyo ilikuwa kazi yangu,kiukweli Ally alikuwa akiniamini sana na ilifika kipindi fedha zake zote mimi ndiye nilikuwa nikizipeleka benki,mkurya mimi nikajiona ni mtu mwenye bahati ya kuaminika na na mtu mwenye asili ya uarabu kuliko wakurya wote kutoka Tarime;kweli,siku iliyofuata sikwenda kazini kama kawaida na nilimpigia simu Team leader wangu nikampanga kabisa ili asije akaona baada ya kushika shika vihela nimeanza kuwa na kiburi.

Baada ya maandalizi mimi na timu yangu ya Catering,tukawa tumefika maeneo ya mikocheni kama kawaida,tuliendelea na maandalizi hadi kuhakikisha vitu vyote viko sawa,sasa tukiwa kwenye hiyo shughuli mida ya 2 usiku,Ally akanipigia simu akiwa na kiwewe kisichokuwa cha kawaida.


Ally Mpemba "Master hebu fanya haraka njoo hapa Sinza Mori"

Mimi "Kaka Sinza Mori sipafahamu"

Ally Mpemba "Hebu mpelekee Jabir simu niongee nae"

Baada ya kumpa Jabir simu na kuzungumza nae inaonekana alimwambia Jabir anitafutie muda ule Taxi na akamuelekeza eneo ambalo ningemkuta,sasa baada ya kupata Taxi,Jabir alimpatia maelekezo yule dereva kisha akaniambia niingie kwenye gari tuondoke.

Tulipofika hilo eneo ambalo ambalo Ally alikuwa amesema nimkute pale,nilimpigia simu akaniambia niingie ndani,ilikuwa ni hotel kubwa tu ambayo pia ilikuwa ni bar,nilipoingia ndani nilimkuta jamaa yupo na watu kadhaa wakiwemo mademu wenye asili kama yake wakila na kunywa.


Ally Mpemba "Kaka kanisaidie kufungua chumba,siunajua nimejisahau "

Aliendelea "Aiseee yaani hata sielewi nimejisahau vipi!"


Mimi "Sawa kaka ngoja sasa niwahi!"

Ally Mpemba "Ukishafungua utanirudishia hapa funguo utanikuta hapa hapa "


Mimi "Sawa kaka"

Niliondoka kuelekea kwenye Taxi tukaondoka zetu kuelekea Magomeni,nilipofika nilimwambia dereva Taxi anisubili nje ya geti.Nilifungua mlango kisha nikaingia ndani nikawasha taa,sasa nilipowasha taa sikuona kitambaa cheupe pale kwenye ile meza ya kioo ndipo nilielekea jikoni kwenye kabati nikakikuta ikabidi niende nikitandike kisha nikachukua kabeji na mboga mboga nikaziweka juu ya ile meza,baada ya kumaliza niliondoka zangu nikaenda kufungua ule mlango wa kile chumba.

Sasa nilipomaliza kuufungua ule mlango nikiwa nimegeuza mgongo naondoka ili nitoke ndani nifunge mlango niondoke,aisee nilisikia nimesukumwa na nguvu isiyokuwa ya kawaida,ile nataka kuanguka chini nilimuona kiumbe wa ajabu ananipita kwa kasi ya ajabu akiwa uchi kama alivyozaliwa akikimbilia sebuleni na kuanza kuyafakamia yale makabeji kwa spidi kali mno,nilipokuwa bado naendelea kushangaa na kuhamaki yeye hakuwa kabisa na muda na mimi.

Ndipo nilimshuhudia mwanamke aliyekuwa na asili ya kiarabu lakini akiwa na manywele mengi si kichwani tu hadi kwenye makwapa na sehemu za siri,alikuwa anatoa harufu kali sana ambayo haikuwa ya kawaida.Niliogopa sana na ikabidi nikimbilie nje na kufunga mlango kisha nikaelekea kwenye lile bomba la nje kunawa,baada ya kumaliza kunawa nikatoka nje nikafunga geti nikapanda Taxi kurudi Sinza kumrudishia jamaa funguo,kiukweli roho ilichafukwa sana na niliogopa sana na hata ujasiri niliokuwa nao wote uliyeyuka.

Huruma,majuto na masikitiko vyote kwa pamoja vilinisumbua sana kwa usiku ule;Sasa wakati nikiwa kwenye gari narudi Sinza,Ally Mpemba alinipigia simu akiwa kama mtu aliyepagawa.



Itaendelea................
YAANI MTU ANAFUGA MAJINI UONDOKE NA HELA YAKE!![emoji1][emoji1] HILO JINI LINALOTOA HARUFU KALI LINGEKUFATA MPAKA HUKO KWENU KYABAKARI.

"Kwa maana hata kama ningeondoka zangu kurudi Mwanza asingepata kwasababu ni mtu tu ambaye nilikutana nae kkoo na halikuwa hanijui kiundani wala haifahamu familia yangu"
 
YAANI MTU ANAFUGA MAJINI UONDOKE NA HELA YAKE!![emoji1][emoji1] HILO JINI LINALOTOA HARUFU KALI LINGEKUFATA MPAKA HUKO KWENU KYABAKARI.

"Kwa maana hata kama ningeondoka zangu kurudi Mwanza asingepata kwasababu ni mtu tu ambaye nilikutana nae kkoo na halikuwa hanijui kiundani wala haifahamu familia yangu"
Ndio akili zake Sasa alichokuwa anafikiria kusepa kirahis na pesa za majini " no gain without pain"

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hiki kipande mwili umesisimka kwa kwl ....pongezi kwako UMUGHAKA
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 14.




Mimi "Nishafika"

Warda "Umesimama wapi?"

Aliendelea "Ooh ok nishakuona"


Baaada ya nusu dakika alikuja mwanamke mmoja mwenye asili ya uarabuni akiwa amevaa hijab nyeusi ikiwa imempendeza sana kutokana na rangi ya ngozi yake.

Warda "Bila shaka wewe ndiye uliyetumwa na Ally"

Mimi "Yes ndiye mimi "

Warda "Unaitwa nani?"

Mimi "Naitwa Umughaka"

Warda "Mhh mbona Ally hakunitajia jina hilo!"

Mimi "Kaka Ally amezoea kuniita Master,Umughaka ndiyo jina langu halisi"

Warda "Ooh sawa nimekuelewa"

Aliendelea "Ngoja kwanza nimpigie simu halafu nikupe uongee nae"

Alichukua simu yake akaanza kumpigia simu Ally Mpemba na wakaanza kuongea,baada ya kuongea akanipatia na mimi simu ili niongee na Ally,baada ya kujiridhisha aliniambia nifuatane nae.Tulitembea kama hatua kumi kisha tukaingia kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa ni ghorofa,ile ghorofa ilikuwa ni Apartment ya watu kuishi na haikuwa kwa ajili ya ofisi.

Baada ya kufika ndani tuliingia kwenye lift nikaona yule dada anabonyeza batani ambayo ilionyesha namba 4,ile lift iling'oa nanga na baada ya sekunde kadhaa tukawa tumefika kwenye floor namba 4,tulipofika tulitembea hatua 3 tukawa tumefika kwenye chumba ambacho baada ya kukifungua tuliingia ndani.

Warda "Nisubiri hapo "


Aliingia chumbani ambako hakutumia muda mwingi akawa ametoka na pochi kubwa ambayo ilikuwa imetuna.

Warda "Hizi ni pesa ambazo Ally amesema nikukabidhi sasa kabla ya kuondoka inapaswa uzihesabu ndipo uondoke"

Alizitoa zile hela kwenye ile pochi kubwa ya kike,kiukweli zilikuwa ni pesa nyingi sana.Nilianza kuzihesabu na kuzipanga ndipo nilipata jumla yake milioni 40.Wakati nazihesabu alikuwa amekaa akiniangalia huku akiendelea kuchezea simu yake.

Mimi "Tayari"

Warda "Umepata bei gani?"

Mimi "Milioni 40"

Warda "Ok uko makini"

Alichukua karatasi pamoja na wino akawa ameweka pale juu ya meza na kuniambia.

Warda "Shika hii"

Aliendelea "Utasaini hapa na hapo chini utaweka dole gumba "

Basi nikafanya kama alivyoniambia na nilipomaliza alichukua simu yake kisha akampigia simu Ally Mpemba.


Warda "Haya nishamkabidhi pesa yako,huyu hapa ongea nae"

Ally Mpemba "Master,huo mzigo nenda kaniwekee benki,nakutumia sasa hivi vielelezo"

Mimi "Sawa kaka"


Warda "Ngoja nikupatie kibegi kidogo,huo mkoba nina kazi nao"

Sasa baada ya kupewa kibegi kidogo,niliziweka zile hela kwenye kile kibegi huku akili yangu ikiwa imechanganyikiwa kabisa,nilipanga nitoroke na zile hela,baada ya kushuka ghorofani nilianza kutembea mdogo mdogo kuelekea mnazi mmoja.

Nilikuwa najisemea uenda ndiyo wakati ambao Mungu aliamua kunitoa kwenye umasikini kupitia zile hela za Ally Mpemba kwa maana hata kama ningeondoka zangu kurudi Mwanza asingepata kwasababu ni mtu tu ambaye nilikutana nae kkoo na halikuwa hanijui kiundani wala haifahamu familia yangu,kiukweli nilikuwa kwenye vita nzito kuhusu zile fedha lakini niliamua nizipelekea Benki ili kuendelea kuonyesha uaminifu wangu kwa Ally,nilisema kama ni umasikini niliandikiwa basi ningekufa masikini tu hata kama ningekimbia na zile hela,pengine ni heri kufa masikini kuliko kuiba cha mtu ambaye ufahamu kakipata vipi,Uaminifu kwangu hata kama usingenilipa lakini ungenijengea heshima kubwa miongoni mwa marafiki na watu wa karibu,hivyo niliamua kuwa muaminifu ingawa nilikuwa nahitaji sana fedha.

Nilitembea kwa haraka sana hadi katikati ya jiji mtaa wa Azikiwe ambapo kwa mujibu wa maelekezo ya Ally Mpemba ilipaswa niende hapo ilipo benki ya Crdb kuziweka hizo fedha.

Baada ya kumaliza kila kitu pale benki,niliondoka zangu kurudi kkoo,nilipofika kwakuwa muda nao ulikuwa umeenda sana,nilimwambia Aunt Farah anipatie kile kiasi ambacho aliambiwa na Ally anipatie ili niondoke zangu kununua mahitaji ya siku hiyo kisha niondoke nikaandae mapema.

Aunt Farah alinikabidhi laki tatu ambazo kwa mujibu wa maelekezo ya Ally Mpemba ni kwamba,laki mbili ningeitumia kwa mahitaji ya vitu kwa siku zilizokuwa zimebaki hadi yeye kurudi na ile laki moja ingekuwa kwa ajili ya matumizi yangu ya kawaida.

Kweli,ile kazi niliifanya kwa uaminifu mkubwa mno hadi siku ambayo alirudi Ally mpemba alikuwa akinishangaa namna nilivyokuwa muaminifu kiasi kile na sikuwahi kumwambia mtu yeyote siri ile.


Ally Mpemba "Kaka kati ya watu na wewe ni mtu!"

Mimi "Kwanini kaka?"

Ally Mpemba "Ndugu zangu si waaminifu kama wewe ulivyo muaminifu"

Aliendelea " Sielewi hata nitakulipa nini!"

Mimi "Usijali kaka haya ni maisha tu!"


Kiukweli nilikuwa najiuliza mle ndani kwa Ally kulikuwa na kitu gani lakini nilikuwa nakosa jibu kwasababu ndani ya siku zote hizo nimekuwa nikiwinda nipate kukiona lakini nilikuwa naishia kusikia sauti tu,mimi sikutaka kuonyesha kama nina wasiwasi,nilichofanya ni kwamba nikiwa nazungumza nae yeye aelewe mimi sifahamu chochote na nilikuwa napotezea mambo mengine ili asije kunoti kitu kutoka kwangu.

Niendelea kupiga kazi yangu ya usajili wa line za simu huku na ile kazi ya usimamizi wa Catering ikiendelea,kiukweli kama kuna muda ambao nilitengeneza pesa ilikuwa ni kipindi hicho,baada ya kupata pesa ya kutosha,nilimtafuta dalali akanitafutia uwanja maeneo ya Chanika Zingiziwa chenye ukubwa wa 25 x 20 nikawa nimenunua Milioni 3.

Nikawa nimepanga nipambane sana ili nikusanye fedha nyinngine nianze ujenzi mdogo mdogo ili nitoke kwenye nyumba za kupanga na mimi niamie kwangu.

Kuna siku tulipata tenda ya kuhudumia chakula maeneo ya Mikocheni,sasa Ally akawa ameniambia siku iliyokuwa inafuata nisiingie kazini ili niende kuwasimamia wale kina mama na vijana kama kawaida yangu maana ndiyo ilikuwa kazi yangu,kiukweli Ally alikuwa akiniamini sana na ilifika kipindi fedha zake zote mimi ndiye nilikuwa nikizipeleka benki,mkurya mimi nikajiona ni mtu mwenye bahati ya kuaminika na na mtu mwenye asili ya uarabu kuliko wakurya wote kutoka Tarime;kweli,siku iliyofuata sikwenda kazini kama kawaida na nilimpigia simu Team leader wangu nikampanga kabisa ili asije akaona baada ya kushika shika vihela nimeanza kuwa na kiburi.

Baada ya maandalizi mimi na timu yangu ya Catering,tukawa tumefika maeneo ya mikocheni kama kawaida,tuliendelea na maandalizi hadi kuhakikisha vitu vyote viko sawa,sasa tukiwa kwenye hiyo shughuli mida ya 2 usiku,Ally akanipigia simu akiwa na kiwewe kisichokuwa cha kawaida.


Ally Mpemba "Master hebu fanya haraka njoo hapa Sinza Mori"

Mimi "Kaka Sinza Mori sipafahamu"

Ally Mpemba "Hebu mpelekee Jabir simu niongee nae"

Baada ya kumpa Jabir simu na kuzungumza nae inaonekana alimwambia Jabir anitafutie muda ule Taxi na akamuelekeza eneo ambalo ningemkuta,sasa baada ya kupata Taxi,Jabir alimpatia maelekezo yule dereva kisha akaniambia niingie kwenye gari tuondoke.

Tulipofika hilo eneo ambalo ambalo Ally alikuwa amesema nimkute pale,nilimpigia simu akaniambia niingie ndani,ilikuwa ni hotel kubwa tu ambayo pia ilikuwa ni bar,nilipoingia ndani nilimkuta jamaa yupo na watu kadhaa wakiwemo mademu wenye asili kama yake wakila na kunywa.


Ally Mpemba "Kaka kanisaidie kufungua chumba,siunajua nimejisahau "

Aliendelea "Aiseee yaani hata sielewi nimejisahau vipi!"


Mimi "Sawa kaka ngoja sasa niwahi!"

Ally Mpemba "Ukishafungua utanirudishia hapa funguo utanikuta hapa hapa "


Mimi "Sawa kaka"

Niliondoka kuelekea kwenye Taxi tukaondoka zetu kuelekea Magomeni,nilipofika nilimwambia dereva Taxi anisubili nje ya geti.Nilifungua mlango kisha nikaingia ndani nikawasha taa,sasa nilipowasha taa sikuona kitambaa cheupe pale kwenye ile meza ya kioo ndipo nilielekea jikoni kwenye kabati nikakikuta ikabidi niende nikitandike kisha nikachukua kabeji na mboga mboga nikaziweka juu ya ile meza,baada ya kumaliza niliondoka zangu nikaenda kufungua ule mlango wa kile chumba.

Sasa nilipomaliza kuufungua ule mlango nikiwa nimegeuza mgongo naondoka ili nitoke ndani nifunge mlango niondoke,aisee nilisikia nimesukumwa na nguvu isiyokuwa ya kawaida,ile nataka kuanguka chini nilimuona kiumbe wa ajabu ananipita kwa kasi ya ajabu akiwa uchi kama alivyozaliwa akikimbilia sebuleni na kuanza kuyafakamia yale makabeji kwa spidi kali mno,nilipokuwa bado naendelea kushangaa na kuhamaki yeye hakuwa kabisa na muda na mimi.

Ndipo nilimshuhudia mwanamke aliyekuwa na asili ya kiarabu lakini akiwa na manywele mengi si kichwani tu hadi kwenye makwapa na sehemu za siri,alikuwa anatoa harufu kali sana ambayo haikuwa ya kawaida.Niliogopa sana na ikabidi nikimbilie nje na kufunga mlango kisha nikaelekea kwenye lile bomba la nje kunawa,baada ya kumaliza kunawa nikatoka nje nikafunga geti nikapanda Taxi kurudi Sinza kumrudishia jamaa funguo,kiukweli roho ilichafukwa sana na niliogopa sana na hata ujasiri niliokuwa nao wote uliyeyuka.

Huruma,majuto na masikitiko vyote kwa pamoja vilinisumbua sana kwa usiku ule;Sasa wakati nikiwa kwenye gari narudi Sinza,Ally Mpemba alinipigia simu akiwa kama mtu aliyepagawa.



Itaendelea................
 
Kwa hiyo umughaka Hana kazi za kufanya siku hz ? Hadi aje kukufurashisha ww na genge lako ,embu acha ujinga ridhika na hicho kipande Cha leo inatosha kbsa kwa [emoji753]
yaani we jamaa,imenibidi nicheke tu,yaani pamoja na watu kukutukana wala wewe uko peace tu,na unaendelea kukoment bila wasiwasi😂😂😂😂
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 13.




Ile sauti ya mtetemo iliendelea sana kana kwamba hicho kitu kilichokuwa humo chumbani kilikuwa kimekasirishwa,nilisimama taratibu nikatembea kwa kunyata hadi kwenye mlango wa kile chumba,nilipofika kwakuwa muda wa kukifungua ulikuwa bado,nilitegea sikio kwa makini kusikiliza kilikuwa ni kitu gani,nilitulia kimya kabisa lakini ile sauti ya mtetemo ilikoma,niliamua tena kunyata na kurudi sebuleni.

Muda wa kufungua ule mlango ulipowadia nilinyanyuka na kwenda kuufungua,sasa nilipofungua ule mlango kama kawaida niliuacha wazi kisha nikawasha taa za nje nikatoka zangu ndani kuelekea nje.Siku hiyo sikutaka kabisa kutoka kwenda kula kwasababu nilikuwa nimekula muda siyo mrefu hivyo nikawa nimeshiba,kwakuwa bado ilikuwa mapema,niliona nifungue ile gari nikae ndani nitulie hadi nitakapopitiwa na usingizi,nilifungua vioo vya mbele vya ile gari upepo ukaanza kuingia ndani lakini nilipoona mbu wanazidi kuingia kwa kasi nilivifunga kisha nikawasha AC nikaendelea kula upepo.

Ilipofika mida ya saa 3 usiku kukiwa kumetulia,nilianza kusikia sauti ya kitu ambacho sikukielewa kilikuwa ni kitu gani kikiwa kinatafuna kwa sauti na miguno kama ya nguruwe,ile sauti ilikuwa inasikika kwa nguvu sana kiasi kwamba ikabidi nifungue mlango wa gari na kushuka,baada ya kutoka kwenye gari nilisimama kando ili niweze kuisikia ile sauti vizuri.Hali ile hakuna mwanadamu mwenye moyo ambaye asingeiogopa,mimi pamoja na ujasiri wangu wa kikurya lakini ilifika sehemu nikawa naogopa sana lakini niliendelea kuwa mvumilivu na kumdhibitishia Ally Mpemba ya kwamba mimi ni mwanaume na ni mwaminifu,hivyo mategemeo yangu yalikuwa ni ipo siku atanipa fedha au sehemu ya mali zake kutokana na uaminifu wangu kwake.

Ile sauti ilipozidi,nilisogea hadi pale mlangoni kwa kunyata kisha nikawa nasikiliza kilikuwa ni kiumbe wa aina gani aliyekuwa mle ndani,kiukweli ilikuwa ngumu kutambua kama alikuwa mwanadamu au mnyama,kwasababu nilichokuwa najiuliza,kama ni mwanadamu anawezaje kutafuna kwa kasi kiasi kile na miguno kama ya nguruwe?

Kwa watu mliofuga nguruwe au mlioishi na nguruwe nadhani hapa mtakuwa mnanielewa,kile kitu kilichokuwa humo ndani kilikuwa kinatafuna na kuguna kwa utamu kama nguruwe anapokuwa anakula.

Pia kama ni mnyama,Je alikuwa ni mnyama gani?,kiukweli niliendelea kujiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu,niliona nijiondokee zangu nirudi kwenye gari kutulia,nilipitiwa na usingizi nikajikuta naamka saa 12 baada ya kusikia milio ya magari huko nje,niliamka haraka na kwenda kuufungua ule mlango na kuzama ndani,nilipofika ndani niliwasha taa za pale sebuleni na kukuta kile kitambaa kilichokuwa pale juu ya meza kimetupwa chini na nilipoangalia chini nikakuta kuna ute ute mzito kama ambao hutoa ng'ombe akiwa anatafuna nyasi,zile kabeji pamoja na mboga za majani sikuzikuta hata kipande tu,kiukweli niliingiwa na hofu sana na sikutaka kusubiri nilielekea moja kwa moja mpaka kwenye kile chumba na kukifunga.Nilipokifunga kile chumba angalau sasa moyo wangu ulitulia,niliingia jikoni nikachukua dekio (Mop) nikaenda kusafisha ule ute mzito kisha kile kitambaa nikakirudisha jikoni kama kawaida.

Baada ya kumaliza lile zoezi,nilitoka nje nikafunga mlango kisha kuelekea bombani kunawa,nilipomaliza kunawa uso na kusukutua nilirudi kwenye gari kusikilizia hadi mida ya saa 2 ili niondoke niingie Kkoo kufanya kazi yangu ya usajili.Baada ya muda kufika niliondoka nikaelekea Buguruni ofisini ambako vikao vilikuwa vinafanyika kila siku na ilikuwa ni lazima kuhudhuria,baada ya kumaliza kikao nilichukua box la line kisha nikaondoka zangu Kkoo,sasa wakati nipo kariakoo napiga kazi,Ally Mpemba alinipigia simu na kutaka nimpatie taarifa za usiku.


Ally Mpemba "Assalam aleykum"

Mimi "Alekom salam "

Ally Mpemba "Wajionaje na hali?"

Mimi "Niko vema kabisa kaka"

Ally Mpemba "Mambo yalienda vyema?"

Mimi "Ndiyo kaka hakuna kilichoharibika"

Ally Mpemba "Hakukuwa na usumbufu kama wa jana?"

Mimi "Hapana kaka"

Nilitaka nimuulize jamaa ni kitu gani kilikuwa mle ndani lakini nilikuwa nasita sana na niliona ningemuuliza uenda ningeharibu uhusiano wetu ambao tayari ushaanza kuwa mkubwa,niliamua nipige kimya ili mambo mengine mazuri yaliyokuwa mbele yangu nisiyazibe.

Ally Mpemba "Sasa utamwambia Farah akupe elfu 50 na utafanya kama ambavyo ulifanya jana"

Mimi "Sawa kaka"

Baada ya mazungumzo jamaa akawa amekata ile simu.Ilipofika mida ya saa 10 Alasiri,niliamua nifunge nirudishe vifaa vyangu vya kazi mahali ambapo nimekuwa nikivihifadhi,nilirudi hadi dukani pale nikamwambia yule sister Farah anipatie kiasi cha fedha kama ambavyo Ally Mpemba alikuwa ameniambia.


Farah "Mbona sikuhizi wawahi sana kufunga!"


Mimi "Hata muda wa usajili umebaki mchache na kuna mahali inabidi niwahi"


Farah "Ooh ok nambie"

Mimi "Brother Ally aliniambia unipatie elfu 50"

Farah "Ally kaka yangu au Ally yupi!?"

Mimi "Yes,brother Ally"

Farah "Mbona hajaniambia "

Aliendelea "Ngoja nimtafute nithibitishe"

Baada ya kumpigia Ally Mpemba na kumpata hewani walikuwa wakiongea lakini yule demu nikama alikuwa akimuuliza Ally mimi na yeye tunabiashara gani kwasababu jana alitoa elfu 50 akanipa na leo tena anatoa elfu 50 kunipatia,sikujua Ally Mpemba alimjibu kitu gani,alichukua elfu 50 akanipatia kisha mimi nikaondoka kuelekea sokoni kununua bidhaa kama ambazo nilinunua jana,maelekezo yalikuwa ni yale yale.

Kiukweli kwa muda huo nilikuwa napata sana hela kwasababu kununua mahitaji yote yale nilikuwa natumia chini ya elfu 20 na elfu 30 iliyokuwa inabaki ilikuwa yangu na Ally Mpemba hakuwahi kuiulizia kabisa,kila siku nilikuwa napewa elfu 50 kwa ajili ya manunuzi.

Kama kawaida niponunua bidhaa nilirudi hadi nyumbani Kwa Ally Mpemba na kuyaweka kama ambavyo nilikuwa nimeelekezwa.Ilipofika jioni muda wa kufungua kile chumba,niliamua kufungua pazia la pale sebuleni kisha nikawasha taa,lengo langu ilikuwa ni kuhakikisha siku hiyo nakiona kile kiumbe ambacho sikukifahamu kilikuwa kiumbe cha aina gani!;baada ya kufungua pazia na kuwasha taa,nilienda kuufungua ule mlango na kuacha wazi kisha nikatoka nje.

Niliamua kukaa kando ya lile dirisha la pale sebuleni huku nikiwa na shauku kubwa ya kuona ni kitu gani kilikuwa mle ndani,ilipofika mida ya saa 2 usiku,nilitoka nje nikaelekea kununua chips na soda kisha nikawahi kurudi,nilipofika breki ya kwanza ilikuwa ni kwenye dirisha la pale sebuleni,niliangalia kwa umakini na ndipo niliona zile kabeji na mboga za majani uilikuwa hazijaliwa,hivyo nikaa pale pembeni nikaanza kula huku nikisubiri nione ni kitu gani kilikuwa mle ndani.

Nilikaa sana pale chini hadi mida ya saa 5 usiku lakini kila nikichungulia hakukuwa na dalili ya kitu chochote,niliamua kufungua mlango na kisha kuingia ndani ili nikafunge yale mapazia na kuzima taa,nilipomaliza nilitoka nje kisha nikakaa pale mlangoni na kusikiliza,ndipo haukupita muda nikaanza kusikia utafunaji wa ovyo na papara ukiendelea kama kawaida,niliondoka nikaingia kwenye gari kwenda kulala kama kawaida huku kile kiumbe kikiendelea na utafunaji wake wa sauti kama nguruwe.

Asubuhi kama kawaida niliingia ndani nikafunga ule mlango kisha nikaanza kufanya usafi pale sebuleni kama kawaida,nilipomaliza niliondoka kuelekea kazini kama kawaida.

Sasa ilipofika mida ya saa 3 asubuhi nikiwa tu ndo nimeanza kazi,alinipigia simu Ally Mpemba.

Ally Mpemba "Kaka salama?"

Mimi "Salama kabisa,vipi wewe huko?"

Ally Mpemba "Huku naendelea vema ila narudi wiki ijayo"

Mimi "Sawa kaka,nambie"

Ally Mpemba "Kuna mtu nimempa namba yako atakupigia simu ana mzigo wangu utaenda atakupatia"

Mimi "Sawa kaka ni mzigo gani?"

Ally Mpemba "Ni pesa,hakikisha akikupatia utanipelekea Benki Crdb,nitakutumia vielelezo"

Mimi "Sawa kaka hakuna tatizo"

Ally Mpemba "Pia nimemwambia Farah kuna pesa atakupatia,utachukua utanunua mahitaji yale kama kawaida na itakayobaki utatumia "

Mimi "Nashukuru sana Kaka Ally"

Ally Mpemba "wala huna haja ya kunishukuru,mimi ndiye ninapaswa kukushukuru "

Aliendelea "Nitakufanyia mambo makubwa sana kwa uaminifu wako"

Mimi "Sawa kaka nitashukuru sana"

Baada ya mazungumzo yale mafupi Ally Mpemba akawa amekata simu.

Ilipofika mida ya saa 7 mchana,kuna namba ngeni ikawa imenipigia simu,ilikuwa ni sauti ya mwanamke ambaye alijitambulisha kama Warda.


Mimi "Ndiye mimi"

Warda "Ally kaniambia kuna mzigo wake nikupatie,sijui nakupataje?"

Mimi "Wewe uko wapi?"

Warda "Njoo hapa mtaa wa mkunguni ukifika uniambie"

Mimi "Sawa nakuja muda si mrefu"

Mimi "Aunt Farah samahani naomba unitazamie hapo narudi mara moja"

Farah "Kwani ndo unafunga?"

Mimi "Hapana,kuna mahali nafika mara moja ila nawahi kurudi"

Farah "Ooh sawa kuna hela Ally ameniambia nikupatie,hivyo ukitaka kuondoka utaniambia"

Mimi "Sawa nawahi kurudi"


Itaendelea........
Mhhhh niwe mkweli kabisa siku ya kwanza tu ningetoka nduki si nduki yani sielewi kabisa
 
Back
Top Bottom