Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 25



Mimi "Nashukuru sana kaka"

Ally Mpemba "Usijali brother,haya ni maisha tu ila unapaswa uwe makini"

Aliendelea "Tatizo lako master huwa unajisahahu sana hadi kuepelekea kunisababishia matatizo,kuna muda napenda tufanye mambo makubwa sana ila naona bado una changamoto zako!"

Mimi "Lakini kaka nishajifunza na sitorudia kufanya makosa "

Ally Mpemba "Ngoja tuone "

Baada ya mazungumzo na Ally niliondoka zangu kuelekea maskani huku nikiwa nafuraha kwssababu jamaa alikuwa amenipatia laki tano.Mambo yalianza kurudi kwenye mstari baada ya kupitia matatizo ya kiuchumi kwa siku kadhaa.

Kila ulipokuwa ukifika mwisho wa mwezi kama kawaida ile bangiri niliyokuwa nimeivaa ilikuwa ikibana sana na damu zikinitoka lakini mwisho wa siku sikuwa napata fedha kabisa na nilipokuwa nikimuuliza Ally Mpemba yeye aliniambia ni kwasababu nimekiuka masharti,sasa ile hali kiukweli iliendelea kunitesa sana na nisingeweza kuishi na kitu ambacho kinaendelea kunitesa na manufaa siyaoni.

Nilimuomba sana Ally Mpemba aweze kuniombea kwa Sheikh yule wa Chumbe kama kuna jambo lolote niweze kufanya ili ikiwezekana nitolewe ile bangiri ambayo iliendelea kunitesa,Ally Mpemba alionekana kama kuwa mbishi lakini alipoona nakomaa sana aliniambia atanirudisha tena kwa mzee lakini ni baada ya Mwezi utakaofatia.Sikuelewa ni kwanini jamaa alikuwa anakomalia mimi kuendelea kuivaa bangiri ambayo ilikuwa ikiendelea kuniumiza na haikunipa chochote zaidi ya kunitoa damu zangu.

Sasa nakumbuka jamaa aliniambia kabla ya kunipeleka kwa Mzee inapaswa kwanza nianze kutafuta wafanyakazi wa ile hotel/mgahawa wake.Kweli,sikutaka kabisa kupoteza muda kwasababu alikuwa ameniahidi atakuwa ananilipa kila mwezi kama msimamizi,yeye alijiweka kando kabisa ingawaje watu walikuwa wakifahamu ni mgahawa wa jamaa.

Niliwashirikisha mademu na washikaji tuliokuwa tukifanya nao kazi ya usajili wa line kila nilipokuwa nikienda ofisini pale buguruni,niliwapata mademu 3 na mshikaji mmoja ambao wao walikubali,kikichofanya wakubali pia ni kwasababu mauzo ya line kwa wakati huo yalianza kupungua,pia wale mademu ni kama walikuwa wamechoka na ishu za kusajili line maana waliona ni kama ilikuwa ikiwadharirisha.Pamoja na hao lakini nakumbuka jamaa aliongea na yule Mama aliyekuwa mpishi wa ile Catering yake akawa amemtafutia wafanyakazi wengine.Jumla mara ya kwanza kulikuwa na wafanyakazi 6,wakike 4 na wakiume wawili.

Baada ya kuanza kazi kwa ule mgahawa mimi pia nikawa nimeacha kazi rasmi ya usajili wa line nikaanza kusimamia ule mgahawa,mimi nilikuwa nakusanya mauzo yote kwa siku na ndiye nilikuwa msimamizi mkuu wa ule mgahawa.Mgahawa huu ulikuwa mtaa wa mkunguni nyuma ya Big bon jirani kabisa na Soko kuu la Kkoo.

Kiukweli tulikuwa tunauza sana na hatukuuza kama ujuavyo wewe bali ilikuwa ni nguvu za kishirikina.Nakumbuka kuna siku Ally Mpemba alipoona mgahawa unachanganyia sana aliinita nyumbani kwake,nilipofika tukawa tumejadili namna ya utoaji wa kafara maana alikuwa ameniambia tangu mwanzo ni kazi ambayo ningekuwa naifanya mimi.

Mimi "Niambie kaka namna ya kufanya"

Ally Mpemba "Kabla ya kufanya chochote orodhesha majina ya wafanyakazi wote kisha mimi nitayatuma kwa Sheikh Unguja"


Nilianza kumuorodheshea majina ya wafanyakazi wote wa ule mgahawa na kweli nilipompatia aliwasiliana na Sheikh akawa anamtajia,sasa baada ya muda kupita kuna majina Sheikh akawa ameyataja pale ambayo yote yalikuwa ya wanawake,walikuwa takribani 3,sasa wale wengine waliobaki hawakuwa na maana,Ally Mpemba aliniambia ikiwezekana niwafukuze waondoke kwasababu hawakuwa na umuhimu wowote kwenye ule mgahawa.

Kiukweli ilinipatia taabu sana kuwafukuza kwasababu hakukuwa na sababu maalumu ambayo ningewaeleza,nilianza kuwafanyia visa na nilikuwa mkali sana,niliamua kufanya uaminifu kwa Ally Mpemba ili kumridhisha kwasababu hapo nyuma nilikuwa nimemkwaza,sasa nilichokifanya ni kuwatafutia sababu wale wafanyakazi ambao Ally Mpemba aliniambia hawakuwa na faida na niliwalipa fedha zao na kuwaondoa,japo walinisihi sana nisiwafukuze lakini kiukweli sikuwa na namna,nilikuwa naumia sana lakini ndugu zangu sikuwa na jinsi.Sasa wale waliobaki nilijaribu kuwapeti peti kwa marupurupu na kuwasifia ya kwamba wao wanapiga sana kazi kuliko wale niliowaondoa,kiukqeli hawakuelewa jambo lolote na wao walifurahi wakawa wanajipa kichwa kama kweli walikuwa wanafanya kazi kumbe ilikuwa ni mtego wa panya,kupitia wale wale wafanyakazi niliwaomba wanitafutie wafanyakazi waliokuwa wanajituma kama wao ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi.Walifurahia sana na wakasema watawashitua ndugu zao ili waje wapambane.
Lile zoezi la kuwatimua halikuchukua siku moja bali ilikuwa ni prosesi ambayo ilichukua muda kwa takribani majuma mawili ili kuwatafutia sababu,hivyo nilivyomaliza hilo zoezi nilimwambia Ally Mpemba ya kwamba nimemaliza na nilikuwa natafuta wafanyakazi wengine wa kujaza nafasi,Ally Mpemba alinipongeza sana kwakupiga kazi na akaniambia mwisho wa Mwezi tutaondoka kulekea Unguja mara moja halafu tuwahi kugeuka.

Kweli,mwisho wa mwezi baada ya kuwa nimetoa damu kupitia bangiri langu la mkononi tukawa tumeondoka kuelekea Unguja kwa Sheikh,tulivyofika nakumbuka yule mzee alimwambia Ally Mpemba wale wafanyakazi itabidi kila baada ya miezi 6 awe anakufa mmoja kwasababu akisema iwe kila mwaka itakuwa mbali sana na majini yake aliyokuwa akiyafuga hayakutaka iwe mwaka,ndipo nikaja kugundua kwamba kumbe jamaa alikuwa akifuga majini na ndiyo yalikuwa yakimpa utajiri ule wote.
Yule mzee alimwambia Ally Mpemba ampatie shilingi milioni moja na Ally alifanya hivyo,baada ya kuipokea ile hela alianza kuifanyia dawa na baada ya kumaliza alimrudishia ile hela Ally Mpemba kisha akawa amemwambia ya kwamba.

Mzee "Hiyo hela hakikisha utakapokuwa unataka kuwalipa mshahara,utakuwa unachukuwa elfu kumi hapa na kisha unachanganya na fedha nyingine ndiyo unawalipa"

Ally Mpemba "Sawa Sheikh"

Mzee "Usiwalipe wewe,huyu kijana ndiye anapaswa kulifanya hilo jukumu"

Ally Mpemba "Hizi pesa anapaswa kukaa nazo yeye?"

Mzee "Siyo lazima akae nazo huyu,ila kama yakiwa yanafanyika malipo hakikisha ni lazima elfu kumi moja inatoka hapa kwenye hizo hela nilizokupatia"

Aliendelea "Na itakuwa kwa mmoja wapo wa mfanyakazi mliyemkusudia"

Ally Mpemba "Sawa nimekuelewa vema"


Kilichokuwa kinafanyika ni kwamba,kama kuna mfanyakazi ambaye tulikusudia afe baada ya miezi sita kutimia,nilikuwa nachukua elfu kumi moja kwenye ile milioni nachanganya na mshahara wake kisha nampatia,kwa mfano kama mshahara ilikuwa laki tatu basi ilikuwa namuandalia mfanyakazi laki mbili na tisini ambayo ilikuwa fedha ya kawaida na baada ya hapo nachukua na elfu kumi kutoka kwenye ile milioni moja kisha inakuwa laki tatu halafu ndipo namlipa mfanyakazi tuliyekusudia.

Baada ya maelekezo yale,Ally Mpemba alimwambia yule mzee afanye namna sasa ile bangiri iweze kunipatia fedha kwasababu tayari nishakuwa mwema kwake,lakini nilimuomba pia yule mzee anibadilishie ile bangiri kwasababu haikuwa na muonekano mzuri hata kidogo,kuna muda nilikuwa naonekana kama mganga wa kienyeji kwasababu tu ya mbangiri ule.

Yule mzee alinipatia Pete ndogo sana ambayo aliniambia niivae kwenye kidole cha kati na akasisitiza itafanya shughuli kama iliyokuwa ikifanya ile bangiri;kiukweli niliipenda sana ile pete kimuonekano kwasababu ilikuwa nzuri na ndogo pia,ingekuwa ngumu sana mtu kugundua,sasa lakini yule mzee akasisitiza sana ya kwamba nisije nikathubutu kuivua ile Pete kama ilivyokuwa kwa bangiri tu.

Baada ya kupata kilichotupeleka hatimaye tukarudi Dar es salaam,tulipofika Dar es salaam Ally Mpemba aliniambia zile fedha atakaa nazo na itakapofika mwisho wa mwezi ule wa sita atanipatia elfu kumi ili nijumlishe na fedha ya malipo ya mfanyakazi tutakayemkusudia.

Kiukweli ile Pete ilipokuwa ikifika mwisho wa mwezi ilikuwa ikibana kama ilivyokuwa bangiri na nilikuwa nikifanya kuituliza kama mwanzo,baada ya damu kumwagika nilikuwa nikipata fedha kama kawaida na zilikuwa nyingi kushinda mara ya kwanza,baada ya kupata zile fedha nilikuwa nikizihifadhi benki nikiwa na lengo la kuanza tena ujenzi upya.Niliendelea kupiga kazi kwenye mgahawa wa Ally Mpemba kwa uaminifu mkubwa na wale wafanyakazi wakawa wamewaleta wafanyakazi wengine,lakini kabla ya kuwaajiri Ally Mpemba akapendekeza kwanza majina yatumwe kwa Sheikh kule Unguja na majibu yakitoka vizuri tuwaajiri,majina yalirudi na kuonekana baadhi wanafaa na wengine hawafai(Hii ilikuwa inahusisha nyota ya bahati) wale waliofaa tuliwaajiri na wale ambao hawakufaa niliwatafutia sababu.

Ilipofika mwezi wa sita mwishoni kuna mdada ndiye tukawa tumekubaliana na Ally Mpemba nilimlipe pesa kupitia ile prosesi na kiukweli majibu yalikuwa mazuri,baada ya kumlipa ile fedha mkononi yule mdada aliipokea na mambo mengine ya kawaida yaliendelea,ingawa wote niliwalipa mkononi kila mmoja na fedha yake lakini yule mdada yeye ndiye tulikubaliana mwisho wa mwezi huo wa sita awe kitoweo kwa biashara ya Ally Mpemba.Taarifa tulizopata ni kwamba alipofika kwao aliugua ghafla na wakati anakimbizwa hospitali alifia njiani,ilikuwa ni huzuni kwa wafanyakazi wenzake waliokuwa wamezoeana lakini hakuna aliyefahamu ule mchezo,mambo yalikaa sawa hatimaye wakasahau na kazi ikaendelea kama kawaida.

Ally Mpemba yeye aliendelea kuingiza fedha nyingi sana na kwakuwa nilikuwa mshirika wake mkubwa nilikuwa naelewa kila kitu.
Baada ya muda kuwa umepita nakumbuka mwanamke wangu Rehema alipata likizo akawa amekuja kwao kisha akawa amekuja kunisalimu.


Itaendelea..............
Hii inanikumbusha tupatapo tu mshahara tutoe (zaka) fungu la kumi, ila naona hamkumpa hata muda wakutafakari na mshahara wake.
 
Kweli nimeamini, tembea kwingi uone mengi. Usione magari ya kushine barabarani kumbe ni mijoka mikubwa, sasa ichubue uone gharama yake ya malipo. Ukikosa kazi pahali, mshukuru tu muumba, usianze kulalama, huwenda amekuepusha na jambo kubwa mbeleni. Tunaishi kwa nguvu za Mungu, wenyewe hatujui wala hatuwezi kitu bila yeye.
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 07.




Kwakuwa Mwakisaka ndiye aliyekuwa mwenyeji wangu sikuwa na hofu kabisa kwasababu ni mtu ambaye tulifanya nae kazi kwa muda mfupi na alikiwa mtu mwema,baada ya kufika kivukoni(feri)tulikata tiketi za kivuko na tukawa tumefanikiwa kuvuka ng'ambo ya pili,baada ya kufika upande wa pili yaani Kigambo,jamaa aliniambia inapaswa tupande gari zilizokuwa zinaelekea Kibada kwa kuwa ndiyo njia yenyewe hiyo.

Tulifanikiwa kufika hapo kwenye mradi mkubwa kabisa uliofahamika kama DEGE ECO VILLAGE,kiukweli nilikuwa nashangaa sana namna ambavyo watu wanatumia fedha,ule mradi ndugu zangu ulikuwa mkubwa mno,na kwa waliobahatika kufika huko au wanaotokea huko watakubaliana nami.

Hatukutaka kupoteza muda kabisa ilibidi Mwakisaka aniambie tuulizie namna ya kupata kibarua kwasababu tulikuta watu wakiwa wanachakalika kinoma.Kuna jamaa tulimfuata tukaanza kumuulizia namna ya kupata kibarua siku hiyo.

Jamaa "Hapa kwetu yupo foreman ambaye ndiye msimamizi wetu,ukienda kule mbele pia wanae foreman wao"

Mwakisaka "Foreman wenu yuko wapi tujaribu kuongea nae?"

Jamaa "Nadhani atakuwa anazungukia maeneo anayosimamia,subirini tu hapa atakuja"

Tulisogea kando tukawa tunaendelea kuushangaa ule mradi wakati huo tunamsubiri mtu tuliyeambiwa ndiye foreman wa hapo tulipofikia.Baada ya muda wa nusu saa jamaa mmoja mweusi aliyekuwa mnene na kitambi cha kutosha akawa amekuja na ndipo yule jamaa alitukonyeza ya kwamba jamaa ndiye foreman wa lile eneo.Tulimfuata na kumjulia hali jamaa kisha Mwakisaka akaanzisha maongezi nae.


Mwakisaka "Kaka tunatafuta kazi ya kibarua "

Foreman "Aliyewaambia hapa tunaajili vibarua nani?"

Mwakisaka "Hakuna mtu aliyetuambia kaka tumekuja kuona kama tutapata"

Foreman "Hapa hatuajiri kwa sasa,siku tukiajiri vibarua mtapata taarifa"

Baada ya yale majibu ya kukatisha tamaa Mwakisaka aliamua akae kimya kisha jamaa akaanza kuondoka kuzunguka nyuma ya yale majengo yaliyokuwa mbele yetu.Sasa yule jamaa aliyekuwa kibarua pale akawa amemuita Mwakisaka akamwambia bila pesa ni ngumu sana kupata kibarua kwasababu hata wao walihonga ndipo kupata kibarua,jamaa akasema twende tukaongee nae kikubwa.Nilimwambia Mwakisaka hiyo kazi ya kuongea na jamaa aniachie mimi,akikataa basi tungerudi zetu kwa Mushi kule kivule kuendelea na ufyatuaji wa tofali.

Niliamua kuzunguka ule upande alokuwa amekwenda yule foreman na bahati nzuri nilimuona akiwa anaingia kwenye jengo moja,nilitembea kwa haraka ili kumuwahi kabla hajafika kwa watu wengi ikawa shida kuzungumza nae.

Mimi "Kaka kakaa"

Foreman "mmmh nambie"

Mimi "Kaka tusaidie ndugu yangu na kama ni chochote tutakupatia"

Foreman "Wewe si ndo upo na yule mwenzio nimewaambia hamna kazi!"

Mimi "Kaka tusaidie ndugu yangu!"

Foreman "Nyie mnatokea wapi?"

Mimi "Wote tunatokea kivule"

Foreman "Kivule?,sasa kivule hadi kuja kufanya kazi huku hamuoni tutasumbuana?"

Aliendelea "Ni bora hata mngekuwa hapa maeneo ya jirani"

Mimi "Tutaweka kambi maeneo haya kaka wala hilo lisikupe taabu"

Foreman "Hapa jirani haturuhusu watu kukaa kwasababu za kiusalama"

Mimi "Sijamaanisha hapa kwenye mradi kaka,tuta tafuta eneo maeneo ya jirani tutaweka kambi"

Foreman "Tukubaliane,mtanipa elfu tano tano kila siku kwa muda wa wiki moja"

Aliendelea "Na iwe siri,ikiwa vinginevyo mi nitawaruka na kuwageuka"

Mimi "Hakuna tazizo kaka"

Foreman "Kamuite mwenzio mje niwakabidhi huku juu!"


Niliondoka kumfuata Mwakisaka na kumueleza kila kitu jamaa alichosema na jamaa akaniambia hakuna tatizo;Tuliondoka kumfuata yule foreman ambaye alituchukua mpaka kwa jamaa wengine akamuacha hapo Mwakisaka kisha akaniambia tena nifuatane nae,mimi pia akawa amenipeleka kwenye kikosi kingine.
Tukaanza kuifanya kazi ya kibarua rasmi na kwa siku tukawa tunapewa elfu 15,ishu ya kula pamoja na maji ya kunywa ilikuwa ni juu ya yako wewe kibarua uzuri ni kwamba,kwenye kundi ambalo mimi nilikuwepo walikuwa wamejitolea kuchanga fedha na kununua vyakula kisha kuna mtu walikuwa wanamlipa anakuja kuwapikia,hivyo na mimi baada ya kuingia kwenye kundi la wale jamaa niliamua kuchangia elfu 10 kwa kila wiki kwa ajili ya huo mpango.

Miongoni mwa wale jamaa pia walikuwa wametengeneza matenti ya maturubai kuishi hapo maeneo ya jirani,niliamua kichangia fedha na mimi ili kukaa hapo,sasa bahati nzuri ni kwamba wikiendi tulikuwaga tunapumzika na hiyo niliitumia kwenda kufata virago vyangu kwa kaka Kileri na kurudi kambini,sikutaka kabisa kuhangaika na mambo ya jiji la Dar es salaam,fokasi yangu ilikuwa ni kwenye kufanya kazi na kutunza malipo yangu kwenye simu.

Nilipopambana ndani ya miezi mitano kwenye ule mradi nilipata kiasi kisichopungua Tsh milioni 1.3,sasa nilimuomba Mwakisaka aniambie ni eneo gani ni zuri kwa kupanga chumba na angalau linakuwa na maisha nafuu kwa hapa Dar es salaam.

Mwakisaka "Mwanangu mimi nakaa Gongo la mboto na nikuzuri sana"

Mimi "Kwahiyo kipindi kile ulikuwa unatoka Gongo la Mboto mpaka Kwa Mushi?"


Mwakisaka " Nilikuwa nakaa kulekule kivule kwa ndugu yangu mmoja"

Aliendelea "Kama unataka chumba we sema nimpigie simu jamaa mmoja pale kitaa akutafutie chumba"

Mimi "Nahitaji kaka"

Mwakisaka "Basi ngoja nitamcheki mshikaji"

Kweli,baada ya Mwakisaka kuwasiliana na jamaa yake na kumjulisha nilikuwa nahitaji chumba jamaa alianza kutafuta na akasema endapo angepata basi angetujulisha.
Baada ya siku tatu yule jamaa aliyepewa kazi na Mwakisaka ya kutafuta chumba akawa amesema nyumba imepatikana maeneo ya mwisho wa lami lakini ni vyumba viwili ambavyo malipo ilikuwa ni elfu 45 kwa kila chumba na ilipaswa kulipwa kwa miezi 6.

Mwakisaka "Jamaa anasema nyumba imepatikana Gongo la mboto mwisho wa lami"

Mimi "Mwisho wa lami ni maeneo ya wapi?"

Mwakisaka "Hapo hapo Gongo la mboto sema ni mbele kidogo"

Mimi "Sawa,na wewe ndiyo unaishi huko?"

Mwakisaka "Hapana,mimi naishi Mzambarauni"

Mwakisaka "Ila jamaa anasema amepata chumba na sebule kwa elfu 45 kwa kila kimoja na inalipwa miezi 6,vp?"

Mimi "Sawa,hakuna tazizo"

Mwakisaka "Ngoja nimwambie amwambie mwenye nyumba atulie kesho kutwa tukakicheki"

Mwakisaka aliwasiliana na yule jamaa akawa amemwambia amwambie mwenye nyumba jumapili tungeenda kukitazama ikiwezekana nilipie kabisa.

Namshukuru Mungu baada ya kwenda kuingalia ile nyumba niliipenda na nikawa nimelipia miezi sita,hela iliyobaki nikanunua godoro na mashuka nikawa nimeyaweka na mimi kufunga chumba kisha kurudi Kigamboni kuendelea na kibarua.

Kila nilipokuwa ninapata hela nilikuwa nikinunua kitu kimoja baada ya kingine na kuweka ndani na hatimaye vyumba vikawa na muonekano mzuri,kiukweli pamoja na mateso ya kushinda juani niliyokuwa nayapitia kule kigamboni lakini nilihakikisha najinyima kiasi kwamba hadi malengo yangu yatimie.

Ule mradi wa Dege kuna muda ukawa umesimama kidogo hivyo kwa muda ule nikaenda kukaa kwangu nilikokuwa nimepanga,sasa pale nilipokuwa naishi kulikuwa na geti na tulikuwa wapangaji kadhaa na kila mtu alikuwa na ishu zake.

Sasa kuna jamaa mmoja alikuwa akiitwa Steve yeye tulitokea kushibana sana na tukawa marafiki,jamaa alikuwa akifanya kazi kampuni ya Tigo kama msajili line za simu,kwakuwa ule mradi ulikuwa umesimama kwa muda usiojulikana,jamaa aliniambia kama vipi aniunganishe na timu leader wake anipatie kodi ya kusajili line za simu nami nianze kuwa msajili laini.Jamaa aliniambia ni kazi ambayo ilikuwa na pesa sana ila watu walikuwa wakiichukulia poa.

Steve "Ngoja kesho nitamueleza team leader kama vipi akupe kodi ili uanze kufanya kazi"

Mimi "Kazi inafanyikaje kaka"

Steve "Kazi ni nyepesi sana kaka utaelekezwa namna ya kuifanya"

Kwakuwa kwa muda huo sikuwa na kazi baada ya kusimama kwa mradi,niliona jamaa atakuwa amenisaidia sana ili kuweza kujinasua na ukata ambao ulikuwa ukininyemelea baada kuwa nakula hela nilizokuwa nimezitunza bila kuzizalisha.



Itaendelea.........

Muendelezo Soma Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani
......[emoji3578]
 
Nakumbuka kuna SINTOSAHAU moja hivi ya RFA majuz kati tu I think ni huu mwaka ulioisha kuna mjamaa goes by the name LwandaMagere alikuwa anasimulia kisa chake cha utajiri kama tu ilivyo kwa UMUGHAKA hapa, jamaa alifata masharti kama yalivohitajika akatajirika vibaya sana lakini alipoanza kulewa utajiri na kusahau kutimiza masharti wakaanza kumpora kila alichonacho hadi akabaki mweupe kama kima.

Sasa jamaa alidokeza siri moja kwamba kumbe fedha zozote zinatoka kwa hao jamaa huwa tayari Zina mihuri au alama zao na kitu kingine alisema kuwa ikitokea umezingua kwenye masharti yao na mkatofautiana basi huchukua kila kitu Chao walichokupa yani hata kama ni nyumba uliijenga kwa hela zao basi huwa wanaichukua chochote kile hata kiwe ni kidogo vipi lazima wa take back to their empire ili wakuache kapuku uliyechakaa ndipo uanze kutafta from 0 mali za kwako mwenyewe
Huyu jamaa story yake ilikuwa nzuri alihangaika sana kuupata utajiri
 
Back
Top Bottom