Utajuaje kama sehemu uliyopo ni Bush?

Utajuaje kama sehemu uliyopo ni Bush?

1.Watu wengi wanajishughulisha na kilimo wanaamka saa 10 alfajiri kwenda mashambani.Pia ng'ombe zinatumika kulima

2.Ni kawaida kukutana na wazee mababu na mabibi

3.Watu wengi wanaongea lugha za makabila

4.Wanawake/wamama wengi wanavaa khanga

5.Ukipanda daladala kwenda Town mfano ahsubuhi unapanda na watu wanaopakia matenga ya mazao wanayotoka kuyanunua ili wakayauze huko waendako

6.Kujaa kwa nyumba za tope

7. Wenyeviti wa mitaa,vitongoji/ vijiji wanaogopeka kana kwamba ndio Marais

8.Kukitokea Msiba wanatangaza na vipaza sauti

9.Wasichana wengi wadogo kuwa na watoto pia wanawake wengi kubeba watoto migongoni

10.Watoto wengi kutomaliza la saba au wakimaliza hawaendelei.

11.Vikosi vya ng'ombe vinapita kwa wingi vikipelekwa machungani hasa ile ming'ombe yenye nundu

12.Nyumba kuwa na vyoo vya nje hasa vile vya shimo

Nitaongezea mengine kadri nitakavyokuwa nayasoma mazingira ya huku bushi nawe waweza kuongezea yako unayoyafahamu kuhusu mbwinde.
Umeoatia zote mkuu kula bia nakuja kulipa
 
Back
Top Bottom