Utakiona cha mtema kuni!, Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....

Utakiona cha mtema kuni!, Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....

Dah......Kwa hisani ya Google..... C & P
UTAKIONA CHA MTEMA KUNI!" Nimeambiwa msemo huu wahenga waliupata katika kisa kimoja cha zama za kale.
Wanasema kulikuwa na msitu jirani na kijiji, ndani ya msitu kulikuwa na miti mingi sana. Ilitokea kuwa katika msitu ule, kulikuwa na miti inapishana sana kwa uzuri, na kati yao ulikuwepo ule ambao ni mzuri sana!
Mtema kuni (Mtemakuni maana yake ni Mkatakuni) alienda katika msitu ule katika shughuli zake za kila siku za kukata kuni!
Alipofika jirani na ule mti mzuri, huku akiwa na shoka mkononi, ule mti zuri sana ulikuwa jirani na mti mbaya sana!
Katika hali ya kufedhehesha (kwa nyodo na maringo) ule mti mzuri sana ukawa unamcheka na kumdhihaki ule mti mbaya, kwamba hauna mvuto na ndio maana kuanzia mbali kabisa, Mtemakuni amaonyesha kuvutiwa na (yeye) Mti mzuri! Huku Mtemakuni akizidi kuusogelea mti mzuri, mti mbaya sana ukajifariji kwa kumwambia mti mzuri basi subiri "utakiona cha mtema kuni"


Kilichofuata ni kweli, Mtema kuni aliukata na kuucharanga Mti mzuri sana kiasi cha kuugeuza kuni za kumfaa kubeba na kuondoka nazo, huku akiuacha ule mti mbaya salama salmini pale msituni!
Yakawa ni majuto kwa Mti mzuri na furaha kwa Mti mbaya!
Hivo ndio nilivyopokea kisa cha "mtema kuni"



UJUMBE WAKE KWA JAMII
1f447_1f3fd.png
👇🏽
mnaodhani mna uzuri wa sura punguzeni maringo na nyodo!
wanasema utakipata cha mtema kuni hapo iaonyesha victim alikuwa mtema kuni
 
Aman iwe nanyi wapendwa
Ni siku nyingi sana huwa nasikia kisa cha mtema kuni

Je mtema kuni ni nani?
Je aliwahi kuwepo au tu ni story za kutunga?
Kitu gan kilimpata huyu mtema kuni?
Kwa kifupi naomba kujua kisa na mkasa mzima wa mtema

Maana huwa naona mtu ukifanya kosa unaambiwa utakiona cha mtema kuni hivyo bas naomba kujua mkasa huu

Nawasilisha

London boy

Sent using Jamii Forums mobile app
Siku hizi umekuwa unashirikisha ubongo kuleta uzi wako umeacha zile takataka ulizotoka nazo fb
 
Alikuwa anachanja kuni akafunga mzigo kuunyanyua akauona mzito akaushusha chini akaufungua lakini badala ya kupunguza kuni akaogeza akaufunga tena kisha kaunyanyua auweke kichwani. Loh mbona uzito unazidi akafanya hivyo hivyo mara ya tatu akashindwa hata kuunyanyua. Akasema siubebi huu mzigo hata kifo kikija. Mara akakiona kifo kinakuja kilipokaribia kama hatua 20 na kilivyokuwa kinatisha mtema kuni alisalimu amri akasema kama kifo ndio kiko hivi basi mzigo wangu naubeba. Mtema kuni aliona kifo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii simulizi imetungwa na mtu asiyejua kabisa kilichotokea. Kwa taarifa yako ''mtema kuni'' ndiye aliyepatwa na kisa na si mti. Kwa kifupi hadithi inasema mtema kuni alienda porini na alipokuwa anakata mti kuna kitu kilimtokea, akatupa shoka lake na kuanza kutimua mbio. Kuna baadhi wanasema lilitokea joka kubwa likaanza kumfukuza na wengine wanasema mti ulianza kuzungumza ukimlaani mtema kuni hivyo akakimbia kwa kihoro cha ule muujiza. Miaka ya nyuma wakati gazeti la Uhuru likiwika hasa kwenye safu ya Ushairi hili swali liliwahi kuulizwa na mshairi mmoja gwiji na magwiji wenzake walimjibu. Kuna mshairi mmoja mlemavu asiyeoona akiitwa Andanenga (Sauti ya Kiza) naye alikuwepo kwenye mjadala! Ulikuwa ni mjadala mzuri sana ila sikuweza kufuatilia ili nijue jibu lililokubaliwa na wengi. Ila la msingi ni kuwa mtema kuni ndiye aliyepatwa na masaibu na siyo mti kama simulizi yako inavyosema.
Amri Sudi mzee wa 'Nyege ni kunyegezana'
 
Habari wana JF

Tangu nikiwa mdogo nimepata kuambiwa habari za MTEMA KUNI, pale nilipokua naghafirika na kukosea basi naelezwa nitakiona cha MTEMA KUNI. Sasa basi, umri umeenda sana na sijawahi kubahatika kusoma wala kusikia habari za huyo mtema kuni. Hivyo basi, kwa yeyote anayejua habari za mtema kuni tafadhali naomba kujuzwa.
 
Mtema kuni si mtu mzuri kwani hakuwa na bahati. Alipenda sana kukata miti hovyo. Siku moja alipokuwa akitembea kando ya mto, akaona mti mzuri sana. Kama kawaida hakuwa akiacha shoka. Akapanda juu ya mti ili aanze kukata matawi taratibu. Alipokuwa juu ya mti ghafla akaona joka kubwa likikenua ulimi, hajakaa sawa akaona nyuki wakiwa kwenye mzinga. Wakati anawaza kushuka, Hamadi! Akaona chini kuna simba amelala anamsubiri[emoji23][emoji4] akataka arukee mtoni, akakutana na mamba amefungua mdomo tayari kwa kitoweo. Sema alichokiona ndio kilibaki historia hadi leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kulikuwa na miti miwili mmoja ulikuwa mzuri sana ukamcheka na kumdharau mwenzake uliokuwa sio mzuri bahati mbaya mtema kuni alipita njia hiyo akakutana na hiyo miti akachagua ulio mzuri sana akaukata huo ndio msemo uliopatikana utakiona cha mtema kuni..
 
Nimeambiwa msemo huu wahenga waliupata katika kisa kimoja cha zama za kale. Wanasema kulikuwa na msitu jirani na kijiji, ndani ya msitu kulikuwa na miti mingi sana. Ilitokea kuwa katika msitu ule, kulikuwa na miti inapishana sana kwa uzuri, na kati yao ulikuwepo ule ambao ni mzuri sana!

Mtema kuni (Mtemakuni maana yake ni Mkatakuni) alienda katika msitu ule katika shughuli zake za kila siku za kukata kuni!

Alipofika jirani na ule mti mzuri, huku akiwa na shoka mkononi, ule mti zuri sana ulikuwa jirani na mti mbaya sana!
Katika hali ya kufedhehesha (kwa nyodo na maringo) ule mti mzuri sana ukawa unamcheka na kumdhihaki ule mti mbaya, kwamba hauna mvuto na ndio maana kuanzia mbali kabisa, Mtemakuni amaonyesha kuvutiwa na (yeye) Mti mzuri! Huku Mtemakuni akizidi kuusogelea mti mzuri, mti mbaya sana ukajifariji kwa kumwambia mti mzuri basi subiri “utakiona cha mtema kuni”

Kilichofuata ni kweli, Mtema kuni aliukata na kuucharanga Mti mzuri sana kiasi cha kuugeuza kuni za kumfaa kubeba na kuondoka nazo, huku akiuacha ule mti mbaya salama salmini pale msituni!
Yakawa ni majuto kwa Mti mzuri na furaha kwa Mti mbaya!
Hivo ndio nilivyopokea kisa cha “mtema kuni”

UJUMBE WAKE KWA JAMII
[https://z-p3-static][https://s]
1. Mliobarikiwa uzuri punguzeni maringo na nyodo!

2. Usijutie ubaya wa maumbile yako, Mungu anajua zaidi kuliko wewe

Jr[emoji769]
 
Mtema kuni si mtu mzuri kwani hakuwa na bahati. Alipenda sana kukata miti hovyo. Siku moja alipokuwa akitembea kando ya mto, akaona mti mzuri sana. Kama kawaida hakuwa akiacha shoka. Akapanda juu ya mti ili aanze kukata matawi taratibu. Alipokuwa juu ya mti ghafla akaona joka kubwa likikenua ulimi, hajakaa sawa akaona nyuki wakiwa kwenye mzinga. Wakati anawaza kushuka, Hamadi! Akaona chini kuna simba amelala anamsubiri[emoji23][emoji4] akataka arukee mtoni, akakutana na mamba amefungua mdomo tayari kwa kitoweo. Sema alichokiona ndio kilibaki historia hadi leo


Jr[emoji769]
 
😀 😀 😀 😀
Mtema kuni si mtu mzuri kwani hakuwa na bahati. Alipenda sana kukata miti hovyo. Siku moja alipokuwa akitembea kando ya mto, akaona mti mzuri sana. Kama kawaida hakuwa akiacha shoka. Akapanda juu ya mti ili aanze kukata matawi taratibu. Alipokuwa juu ya mti ghafla akaona joka kubwa likikenua ulimi, hajakaa sawa akaona nyuki wakiwa kwenye mzinga. Wakati anawaza kushuka, Hamadi! Akaona chini kuna simba amelala anamsubiri[emoji23][emoji4] akataka arukee mtoni, akakutana na mamba amefungua mdomo tayari kwa kitoweo. Sema alichokiona ndio kilibaki historia hadi leo


Jr[emoji769]
Ni nini kilimpata?
 
Back
Top Bottom