Tunarudi pale pale kwamba kama kafa siku si zake una maanisha unazijua siku zake za kuishi,ni sawa na kusema jamaa kachelewa ama kawahi ili hali hujui mda wake wa kufika.ni kama onyo tu..kukumbusha ulifanyalo si jema na linaweza kukusababishia kifo mapema.
kijana ana uwezo wa kuishi maisha halal ya haki na akaishi hata uzeeni....kaamua kuwa kibaka kadakwa kacharangwa mapanga.hapo si kafa kabla ya siku zake
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kumbuka hakuna aina moja ya kifo,wala hakuna anaejua atakufaje,na kama hujui utakufaje pia hujui mwenzako atakufaje sasa wawezaje mwambia mtu mwingine atakufa siku si zake??vifo vingine vya kujitakia ujue.. unaambiwa mke wa mtu sumu! wewe unasema geto lina maziwa, siku wakikubamba na mke wa mtu wakakuua.
hapo ndio tunarejea kwenye mada. "utakufa siku si zako"
Nakubaliana na wewe mkuu.
Dhambi?? yawezekana ikawa ni kweli lakini vipi kuhusu watoto wadogo wapotezao maisha,nao ni dhambi?Dhambi ndio huleta kifo kabla ya muda wako.yaani utajikuta ulienda sehemu ambayo sio sahihi na muda ambao sio sahihi ukakumbwa na kifo hivyo usiende na wadhalimu na watenda uovu
Sent using Jamii Forums mobile app
Kudos mkuu,Tundu Lissu's a vivid example.Tuko pamoja, kama siku haijafika utatwangwa risasi zaidi ya 30 hautakufa, ndege itapata ajali utapona peke yako, jengo litalipuliwa wakati huo unaweza hata ukawa na udhuru usiwepo eneo la tukio.
Lakini kama siku imefika, hata kama umelala utarudi mavumbini tu, utapita eneo lenye taharuki risasi itapinda kona na kukutafuta wewe tu, utapelekwa hospitali bora kuliko zote duniani na mauti itakufika tu.