Steven Joel Ntamusano
JF-Expert Member
- Jun 17, 2023
- 5,203
- 3,913
Vilabu vikubwa vya Ulaya vinamtangaza Emirates kila kukicha. Mechi inachezwa uwanjani na ukitazama yale mabango ya umeme yanayokatiza pembeni ya mstari wa uwanja huwezi kulikosa bango lenye sura za kinadada wazuri weupe wanaotangaza shirika hilo la ndege.
Kabla mechi hazijaanza au kabla ya matukio makubwa yanayorushwa dunia nzima kwenye viwanja vya mpira vya Ulaya huwa wanajipanga kinadada wazuri warefu na weupe wakiwa na mavazi ya shirika hilo la ndege, ni kwa makusudi ili dunia nzima iweze kujua nini kinaendelea kwenye sekta ya anga.
Mwarabu kaikamata biashara ya ulaya baada ya kupigwa vita nzito kule Marekani akipewa kesi nyingi za uongo ili akate tamaa na kuondoka. Akatua ulaya kwenye bara lenye uendeshaji wa biashara wa haki, ukiwa na kitu chenye kuonekana ni lazima utoboe. Ameendelea mwarabu kunawiri katika uwanja wa biashara wa haki barani humo.
Ulimwengu tunaoishi una utamaduni mpya wa kibiashara na haukwepeki ni kama mvua mwezi wa April hazikwepeki ni lazima zitanyesha sehemu fulani ya dunia. Kwa kimombo inaitwa NEW WORLD ECONOMIC ORDER. Ni hali ambayo inamuongezea uzee Joe Biden kule USA, kila Akitazama takwimu za kibiashara anakuta Marekani inamiliki asilimia 40 tu za Market Shares kwenye masoko yote ya hisa, nani mpinzani wake mpya?, ni mwarabu anayeongozwa na Al Makhtoum kiongozi mkuu wa UAE.
Anamnyima usingizi Mmarekani na kumpunguzia ushawishi wake wote unaozidi kupungua siku baada ya siku. Huu ni mfumo mpya wa dunia mpya na sioni ni kwa namna gani Tanzania itaweza kuepuka ushawishi huu unaovuma kwa kasi. Mwarabu anamiliki sekta zote kubwa za dunia hii na kwa sasa kaingia kwenye misitu, kiasi cha mtu kushangaa inakuwaje misitu ya Dodoma inamilikiwa na mwarabu?. Kakamata kila mahali nyeti duniani.
Kwenye sekta ya usafiri wa majini ndio balaa, anamiliki meli 400 za iliyokuwa P & O Nedlloyd kampuni kubwa ya shipping miaka michache iliyopita, anao ushawishi huko DRC, Congo na kwenye madini ndani ndani ya Afrika. Pia anao umahiri wa kufanya end to end logistics kwa miundo mbinu ya kisasa aliyonayo. Anao umahiri katika biashara ya Bandari kiasi cha kuendesha akiwa ni vigezo vyote vya kuwa INVESTOR PORT yaani anamiliki bandari kule kwao na wakati huo huo anazikodisha kila kona ya dunia hii.
Anao uwezo wa kushusha bei za bidhaa nyingi pale Kariakoo kwa kutenga meli zake 10 zikawa zinahudumia bandari ya Dar pekee, na kupunguza kwa kiasi kikubwa bei za bidhaa mbalimbali. Kitaifa naona ni vigumu kupinga huu upepo wa mwarabu anaokuja nao katika pwani ya afrika mashariki.
Anapachikwa majina mengi na taasisi za kidini kwa kigezo cha asili yake kwani hao wanaojaribu kumchafua ni mawakala wa utamaduni wa magharibi na kwa sasa upo katika hali mbaya tukizingatia kuwa Market Shares za USA zinakwenda zikipungua, magharibi na utamaduni wake anao mtihani wa kupata chanzo cha uhakika cha gas, mfaransa anapambana kila kukicha amuue rais mpya wa Niger ili alinde maslahi mapana ya utamaduni wa magharibi.
Mwafrika na rasilimali zake nyingi anaendelea kufanana na msichana mzuri anayevutia wanaume wenye pesa nyingi, anatazama tu wanavyomuhangaikia kwa mitindo mbalimbali ya kutaka kuuvuta moyo wake.
Kabla mechi hazijaanza au kabla ya matukio makubwa yanayorushwa dunia nzima kwenye viwanja vya mpira vya Ulaya huwa wanajipanga kinadada wazuri warefu na weupe wakiwa na mavazi ya shirika hilo la ndege, ni kwa makusudi ili dunia nzima iweze kujua nini kinaendelea kwenye sekta ya anga.
Mwarabu kaikamata biashara ya ulaya baada ya kupigwa vita nzito kule Marekani akipewa kesi nyingi za uongo ili akate tamaa na kuondoka. Akatua ulaya kwenye bara lenye uendeshaji wa biashara wa haki, ukiwa na kitu chenye kuonekana ni lazima utoboe. Ameendelea mwarabu kunawiri katika uwanja wa biashara wa haki barani humo.
Ulimwengu tunaoishi una utamaduni mpya wa kibiashara na haukwepeki ni kama mvua mwezi wa April hazikwepeki ni lazima zitanyesha sehemu fulani ya dunia. Kwa kimombo inaitwa NEW WORLD ECONOMIC ORDER. Ni hali ambayo inamuongezea uzee Joe Biden kule USA, kila Akitazama takwimu za kibiashara anakuta Marekani inamiliki asilimia 40 tu za Market Shares kwenye masoko yote ya hisa, nani mpinzani wake mpya?, ni mwarabu anayeongozwa na Al Makhtoum kiongozi mkuu wa UAE.
Anamnyima usingizi Mmarekani na kumpunguzia ushawishi wake wote unaozidi kupungua siku baada ya siku. Huu ni mfumo mpya wa dunia mpya na sioni ni kwa namna gani Tanzania itaweza kuepuka ushawishi huu unaovuma kwa kasi. Mwarabu anamiliki sekta zote kubwa za dunia hii na kwa sasa kaingia kwenye misitu, kiasi cha mtu kushangaa inakuwaje misitu ya Dodoma inamilikiwa na mwarabu?. Kakamata kila mahali nyeti duniani.
Kwenye sekta ya usafiri wa majini ndio balaa, anamiliki meli 400 za iliyokuwa P & O Nedlloyd kampuni kubwa ya shipping miaka michache iliyopita, anao ushawishi huko DRC, Congo na kwenye madini ndani ndani ya Afrika. Pia anao umahiri wa kufanya end to end logistics kwa miundo mbinu ya kisasa aliyonayo. Anao umahiri katika biashara ya Bandari kiasi cha kuendesha akiwa ni vigezo vyote vya kuwa INVESTOR PORT yaani anamiliki bandari kule kwao na wakati huo huo anazikodisha kila kona ya dunia hii.
Anao uwezo wa kushusha bei za bidhaa nyingi pale Kariakoo kwa kutenga meli zake 10 zikawa zinahudumia bandari ya Dar pekee, na kupunguza kwa kiasi kikubwa bei za bidhaa mbalimbali. Kitaifa naona ni vigumu kupinga huu upepo wa mwarabu anaokuja nao katika pwani ya afrika mashariki.
Anapachikwa majina mengi na taasisi za kidini kwa kigezo cha asili yake kwani hao wanaojaribu kumchafua ni mawakala wa utamaduni wa magharibi na kwa sasa upo katika hali mbaya tukizingatia kuwa Market Shares za USA zinakwenda zikipungua, magharibi na utamaduni wake anao mtihani wa kupata chanzo cha uhakika cha gas, mfaransa anapambana kila kukicha amuue rais mpya wa Niger ili alinde maslahi mapana ya utamaduni wa magharibi.
Mwafrika na rasilimali zake nyingi anaendelea kufanana na msichana mzuri anayevutia wanaume wenye pesa nyingi, anatazama tu wanavyomuhangaikia kwa mitindo mbalimbali ya kutaka kuuvuta moyo wake.