Utamuombaje simu mtu umfahamu?

Abbasfarudume

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2017
Posts
1,625
Reaction score
1,326
Wana jukwaa habari za saa hizi. Bila kupoteza muda jana mishale ya saa tisa alasiri nilikuwa maeneo ya Uchumi supermarket pale nyerere road kaja Jamaa simju anijui "namnukuu" Kaka naomba nikupe namba umpigie jamaa nataka kuongea nae. Mwisho wa kumnukuu mimi sasa nikamjibu Sitoi simu nishaibiwa simu kwa mtindo huo kama wako sitaki. Jamaa akastuka kwa mshangao eeeeeh[emoji15] [emoji15] nikaondoka zangu nikamuacha hapo hapo anashangaa
 
Hawachelewi kukutapeli au kukuingiza matatizoni hao watu mkuu.
 
Mkuu shida humkuta mtu yeyote...
Mimi kipindi niko F5 nimewahi kusaidiwa simu na stranger nilikuwa na shida kubwa sana..

Hivyo mimi kumsaidia mtu naangalia mazingira kama ni ya kitapeli au mtu ana shida kweli...
Kama ana shida namsaidia tu
 
Mkuu shida humkuta mtu yeyote...
Mimi kipindi niko F5 nimewahi kusaidiwa simu na stranger nilikuwa na shida kubwa sana..

Hivyo mimi kumsaidia mtu naangalia mazingira kama ni ya kitapeli au mtu ana shida kweli...
Kama ana shida namsaidia tu
Yule jamaa ungemuona sura yake kama kibaka
 
Unaweza omba kama umepata shiida, ila kuna wachache ambao wanatumia mbinu hiyo kuiba
 
Huyo jamaa bado anashangaa.


Huyo alikuwa hana maana angeacha matatizo tu heri umemuacha anashangaa.
 
Unaweza omba kama umepata shiida, ila kuna wachache ambao wanatumia mbinu hiyo kuiba
Dunia imekwisha uaminifu kwa mtu Usiomjua wala kumfahamu inakuwa ngumu sana kwa kweli mkuu
 
Alikuwa na shida sio wote matapeli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…