VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
UKUTA ulitangazwa na CHADEMA. Watangazaji wakajipanga kimaandalizi bila ajizi. Wanasiasa,viongozi wa dini,wa kiserikali na walinzi wa amani wakajitokeza na kukataza. Wengine wakafanya mazoezi ya kujiandaa kukata mizizi. Wengine leo ni birthday yao na wanashereheka kivyao.
UKUTA ukazua mjadala,ubishani na kuwekwa kwenye mizani. Kadiri ulivyokuwa ukisisitizwa kuwepo leo,mikwara ya kauli kalikali ilizidi. Ukaahirishwa kupisha mazungumzo ya kusaka suluhu kuzama kwenye Safina ya NUHU.
Difenda zimerandaranda kama vinanda mitaani bila utani. Bado zinaendelea. Kiintelijensia,huko ni kuhakiki bila mikiki. Kuhakiki kama kauli ya jana si kanyaboya au hewa. Wapinga UKUTA wakajikuta wanaujenga UKUTA kuupinga UKUTA. Mwisho,UKUTA ukafanyika. Watanzania tujipongeze kutunza amani yetu. Yote yanazungumzika!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
UKUTA ukazua mjadala,ubishani na kuwekwa kwenye mizani. Kadiri ulivyokuwa ukisisitizwa kuwepo leo,mikwara ya kauli kalikali ilizidi. Ukaahirishwa kupisha mazungumzo ya kusaka suluhu kuzama kwenye Safina ya NUHU.
Difenda zimerandaranda kama vinanda mitaani bila utani. Bado zinaendelea. Kiintelijensia,huko ni kuhakiki bila mikiki. Kuhakiki kama kauli ya jana si kanyaboya au hewa. Wapinga UKUTA wakajikuta wanaujenga UKUTA kuupinga UKUTA. Mwisho,UKUTA ukafanyika. Watanzania tujipongeze kutunza amani yetu. Yote yanazungumzika!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam