Utapeli tiGOPesa!

mbna unakuwa mbumbumbu wewe ataitumaje direct? Lazma akuingizie wewe na uisikie imeingia ili kuondoa mikanganyko
Acha uswahili bana!!!!!! kwani wewe umeshawahi kuingiziwa ukaisikia na kuondoa mkanganyiko? tumia lugha nyepesi bana.
 
Acha uswahili bana!!!!!! kwani wewe umeshawahi kuingiziwa ukaisikia na kuondoa mkanganyiko? tumia lugha nyepesi bana.
Ahahahahahaah!! Kumbe kiswahili kina utata namna hii...
 
Wakuu hackers wamefanikiwa kuingia kaatika mtandao wa tigo pesa na kusababisha matatizo mbali mbali kwa mfano wanunuzi wa vocha kupitia mfumo wa tigo pesa wataliwa ....kuweni waangalifu security system ya tigo pesa hiko chini sana kuweza kudhibiti wataalamu wa kuingilia mifumo na kuchukua fedha za watu
 
Wataalamu wa software na kuingilia mitandao ya mifumo mbali mbali leo wameingilia mifumo ya tigo pesa so leo natoa taarifa kuwa wataotumia mtandao huu watakuwa wanahatarisha usalama wa amana zao kwa leo kwani hackers wanaweza kunasa mpaka password za account za watu
 

HAYO ni majungu

Kwanini sahack VODA ambao hawalipi kodi?
 
na kwa watanzania walivyo dhahifu password ya tigo pesa ndio hiyo hiyo ya ATM zao so kuweni macho
 

taarifa nzuri lakini
mbona haijitoshelezi?
Mfano kuna tukio lolote
ambalo linathibitisha
ama kunani kilichotokea mpaka
useme tumevamiwa
mi ni mmoja wa watumiaji wa huduma hii,samahani km nimekukwaza
 
Tueleze incidency yoyote iliyotokea ili kujua hiyo hacking ilivyofanyika,otherwise taarifa hii itakuwa siyo warranted,TIGO pia watatoa taarifa kwa wateja wao kama kitu kama hicho.Isije ukawa unatumiwa na M-PESA kudemolarise tigo users.
 
Asante mkuu japo umechelewa kidogo.Nishaliwa 2,000 kupitia airtime recharge.Nilikuwa nahangaika tangu jana kununua airtime ikawa inashindwa kukamilisha na kunipa ujumbe "application is down".Leo majira ya saa saba mchana huu nikapata ujumbe kuwa nimefinikiwa kununua 2,000 ya airtime lakini nikicheki salio langu kwenye simu halioneshi hilo ongezeko la 2,000 kwa hiyo nimeshaliwa!!Hadi sasa hivi ninavyoandika hiyo 2,000 sijarudishiwa.tiGO!!!Na sijui kama hawa jamaa wana customer care au wakuu kuna mtu ameshawahi kuongea na tiGO customer care? huwa najaribu kupiga 713800800 ipo kwenye "automation" lakini pindi unapopokelewa na hiyo "computer" wanaanza kukukata hela
 
Tueleze incidency yoyote iliyotokea ili kujua hiyo hacking ilivyofanyika,otherwise taarifa hii itakuwa siyo warranted,TIGO pia watatoa taarifa kwa wateja wao kama kitu kama hicho.Isije ukawa unatumiwa na M-PESA kudemolarise tigo users.

nadhani ngoja official notification kwani ni kawaida ya watanzania kutoamini mpaka tatizo lishindikane, hivi ninavyokwambia tayari tigo wanaendelea kukabiliana na tatizo hili na wameomba msaada wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa mifumo,
wewe kama huna imani tafuta wahusika wa TIGO waulize suala hili,
 
Ahsante kwa taarifa Mheshimiwa!! Sasa tunafanyeje? Mimi leo asubuhi nimepatwa na mkasa huo,nimeliwa hela yangu Sh.6000 ambayo nilikuwa nanunua (vocha) kwa tigo-pesa. Je,nifanyeje ili niwe refunded??
 
Asante kwa taarifa yani huu mtandao unazingua kupita kiasi sasa imefika mpaka kwenye tigo pesa tena,na hiyo customer care wala hakuna unawekwa hewan zaidi ya lisaa,labda uende oficn kwao fizikali,mie nishaamua kuhamia zangu maisha burdannii!
 
...tunafanyeje sasa wandugu? Na mimi leo asubuhi nimeshaliwa elfu-6 na haohao wanaojiita tigo-pesa. Tunafanyeje sasa ili tuweze kuwa refunded? Inaniuma sana hii 6000,kwa maisha yenyewe ya "kasi mpya" haya,elfu sita si mchezo!!
 
Ahsante kwa taarifa Mheshimiwa!! Sasa tunafanyeje? Mimi leo asubuhi nimepatwa na mkasa huo,nimeliwa hela yangu Sh.6000 ambayo nilikuwa nanunua (vocha) kwa tigo-pesa. Je,nifanyeje ili niwe refunded??


nadhani ni tatizo kubwa kuliko uwezo wao wanaendelea na juhudi za kutafuta wajuzi wa mambo haya nadhani mambo yakienda sawa watatatua matatizo yote .....

Kwa mtu mmoja mmoja huwezi kutatua tatizo ili kwani wao wamepenya kwenye mfumo mzima wa TIGO PESA ....
 
Kabla ya kuwahukumu Tigo ingekuwa vizuri kama mkipata uhakika wa kilichotokea. Inaweza kuwa ni tatizo la mitambo yao which means baada ya kurekebisha mambo yatarudi kuwa sawa na pesa au credit zenu mtapewa. Ila kwa upande mwingine watu wengi watakuwa wameathirika sana na hili tatizo na sio ajabu wakapoteza wateja wengi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…