Mshangazi dot com
JF-Expert Member
- Nov 19, 2011
- 1,345
- 3,503
Nimeulizwa sana kwenye nyuzi, ngoja leo niwasimulie.
Jan 16, 2025 alinipigia simu ndugu yangu mmoja akasema anataka tuonanae. Nikamkaribisha nyumbani, akaja na akaanza kunielezea shida yake. Kiufupi, alikuja kuniomba nimuazime pesa na atanirudishia baada ya wiki mbili. Nikamuuliza kulikoni? akanijibu, kuna fursa ambayo amekutana nayo ya LBL Tanzania. Yeye ameshatengeneza faida ya zaidi ya TZS 300,000 na sasa kuna special offer, akiweka milioni 4 atapata milioni moja ya faida ndani ya wiki mbili kwa hiyo atatoa milioni 5 na ushee.
Taa nyekundu ikawaka kichwani, nilikua sijawahi kusikia kuhusu hiyo kampuni ila kwa maelezo ya awali, nilijua tu ni Pyramid scheme. Akanionyesha group lao la WhatsApp ambalo wako watu 1,000 pamoja na kiongozi wao muwakilishi kutoka hiyo kampuni na app yao ya movie. Alivyoona natilia mashaka, akasema “bora hata nisingekuambia hiyo hela nataka kufanyia nini, maana ushaanza kuleta komplikesheni” Nikaignore hiyo kauli, nikamwambia nitamjibu jumatatu ngoja nimshirikishe Mr. (Wote mlio kwenye mahusiano mnajua hichi kisingizio kinavyotusevu kwenye upumbavu).
Alivyoondoka nikaendelea na utafiti wangu, nikagundua hao watu wa LBL ni matapeli. Kwa sababu sina mitandao ya kijamii, nikawa natafuta namna gani nitawaambia na watu wengine kuhusu hili janga. Ndiyo nikakumbuka kuna Jamii forums ya Maxence Melo , wakati najiunga 2011 nilikua binti mdogo na jamvi lilikua la moto sana kwa mambo ya kiasiasa. Sikuwahi kuthubutu kuchangia na baadaye maisha yalichanganya (watoto, kazi, familia etc.) sikukumbuka tena mambo ya JF wala mtandao wowote wa kijamii.
Nyuzi yangu ya kwanza kuandika ilikua Ijumaa Jan 17, 2025 na ilihusu utapeli wa hii kampuni na kuwaonya watu kutojiunga LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji. Pia nilimuonya huyo ndugu yangu na nikamwambia pesa ya kumuazima sina.
Japo lengo langu lilikua ni kuandika hii nyuzi ili kufikisha taarifa na kusign out after. Nilipoperuzi kidogo nilinogewa baada ya kukutana na nyuzi za mapishi za Mwachiluwi , nyuzi za siasa za Cute Wife , Waufukweni etc. nyuzi za picha za kushangaza za Mshana Jr , story za realMamy , Mallerina , Poor Brain , Eli Cohen , PSL god n.k bila kusahau replies za wanajamvi kama mzee Ushimen , Aaliyyah , Numbisa , ephen_ , Qashy Lilith , nakwede97 , Intelligent businessman na wengine wengi.
Asante kwa wote mnaoandika nyuzi za kufundisha, kutoa taarifa na kuburudisha.
Asanteni pia wote mnaochangia kwenye nyuzi zangu na mnaonichekesha kwenye replies kama Nomadix na wenzako.
Hakuna kipindi nimejifunza, nimefurahi na nimecheka kwa sauti mpaka nikaja kuulizwa kama niko sawa, kama baada ya kurudi JF last month. Haya tuliendeleze Jamvi 🫶!
Jan 16, 2025 alinipigia simu ndugu yangu mmoja akasema anataka tuonanae. Nikamkaribisha nyumbani, akaja na akaanza kunielezea shida yake. Kiufupi, alikuja kuniomba nimuazime pesa na atanirudishia baada ya wiki mbili. Nikamuuliza kulikoni? akanijibu, kuna fursa ambayo amekutana nayo ya LBL Tanzania. Yeye ameshatengeneza faida ya zaidi ya TZS 300,000 na sasa kuna special offer, akiweka milioni 4 atapata milioni moja ya faida ndani ya wiki mbili kwa hiyo atatoa milioni 5 na ushee.
Taa nyekundu ikawaka kichwani, nilikua sijawahi kusikia kuhusu hiyo kampuni ila kwa maelezo ya awali, nilijua tu ni Pyramid scheme. Akanionyesha group lao la WhatsApp ambalo wako watu 1,000 pamoja na kiongozi wao muwakilishi kutoka hiyo kampuni na app yao ya movie. Alivyoona natilia mashaka, akasema “bora hata nisingekuambia hiyo hela nataka kufanyia nini, maana ushaanza kuleta komplikesheni” Nikaignore hiyo kauli, nikamwambia nitamjibu jumatatu ngoja nimshirikishe Mr. (Wote mlio kwenye mahusiano mnajua hichi kisingizio kinavyotusevu kwenye upumbavu).
Alivyoondoka nikaendelea na utafiti wangu, nikagundua hao watu wa LBL ni matapeli. Kwa sababu sina mitandao ya kijamii, nikawa natafuta namna gani nitawaambia na watu wengine kuhusu hili janga. Ndiyo nikakumbuka kuna Jamii forums ya Maxence Melo , wakati najiunga 2011 nilikua binti mdogo na jamvi lilikua la moto sana kwa mambo ya kiasiasa. Sikuwahi kuthubutu kuchangia na baadaye maisha yalichanganya (watoto, kazi, familia etc.) sikukumbuka tena mambo ya JF wala mtandao wowote wa kijamii.
Nyuzi yangu ya kwanza kuandika ilikua Ijumaa Jan 17, 2025 na ilihusu utapeli wa hii kampuni na kuwaonya watu kutojiunga LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji. Pia nilimuonya huyo ndugu yangu na nikamwambia pesa ya kumuazima sina.
Japo lengo langu lilikua ni kuandika hii nyuzi ili kufikisha taarifa na kusign out after. Nilipoperuzi kidogo nilinogewa baada ya kukutana na nyuzi za mapishi za Mwachiluwi , nyuzi za siasa za Cute Wife , Waufukweni etc. nyuzi za picha za kushangaza za Mshana Jr , story za realMamy , Mallerina , Poor Brain , Eli Cohen , PSL god n.k bila kusahau replies za wanajamvi kama mzee Ushimen , Aaliyyah , Numbisa , ephen_ , Qashy Lilith , nakwede97 , Intelligent businessman na wengine wengi.
Asante kwa wote mnaoandika nyuzi za kufundisha, kutoa taarifa na kuburudisha.
Asanteni pia wote mnaochangia kwenye nyuzi zangu na mnaonichekesha kwenye replies kama Nomadix na wenzako.
Hakuna kipindi nimejifunza, nimefurahi na nimecheka kwa sauti mpaka nikaja kuulizwa kama niko sawa, kama baada ya kurudi JF last month. Haya tuliendeleze Jamvi 🫶!