Utapeli unaofanywa na baadhi ya "maajenti" wasio waaminifu pale Magufuli Bus Terminal ukomeshwe!

Utapeli unaofanywa na baadhi ya "maajenti" wasio waaminifu pale Magufuli Bus Terminal ukomeshwe!

Wabongo kukata tiketi mitandaoni wanaona ni usumbufu Bora atoke aende akatembee stand.
 
Vitambulisho na sare si matapeli wana forge vyao feki afu wanaendeleza utapeli kama kawaida. Hii nchi hata ukitaka mhuri wa Ikulu unapata ndo sembuse vitambulisho vya maagent wa stand ya bus!

Kutapeliwa ni uzembe/ujinga wa victim serikali haiwezi suluhisha hilo.
 
hii yote ni kutokana na tatizo la Ajira nchini kwetu vijana hawataki kufanya kazi ngumu
Malizia vijana hawataki kufanya kazi ngumu kwa malipo uchwara yaan unafanyishwa kazi ngumu alafu unalipwa malipo kiduchu unafanya kazi more than 12hrs alafu unalipwa afutatu yaan afutatu tu unafanyishwa kazi ngumu kwa zaidi ya masaa 12 alafu unalipwa afutatu na unapigishwa kazi ngumu za kuhatarisha hata Uhai wako na hapo hapo bado haujadharauliwa na kuonekana huna akili haufikiri nje ya box kwanini usiwataperi watu kwa siku ukaingiza more than 10 G's or even 20 G's?
 
Pamoja na kwamba Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli kimetengeneza ajira kwa watu wengi, lakini kuna jambo moja linaloendelea pale na linaonekana kufumbiwa macho na mamlaka husika. Jambo hilo ni utapeli.

Juzi nikiwa kwenye pitapita zangu, nikaona watu wamemzingira mama mmoja wa makamu. Mama huyo alikuwa akiangua kilio kwamba yeye alikuwa ameteremka kwenye daladala za Kinyerezi na wakati yupo kwenye daraja la juu la watembea kwa miguu linalounganisha upande wa Kituo cha Daladala cha Mbezi Louis na Magufuli Bus Terminal, alikutana na “ajenti” wa mabasi ya mikoani.

“Ajenti” yule alimshawishi mama yule na kumuuzia tiketi ya kwenda Kondoa na akamuandikia na kukabidhi kisha alipoingia ndani ya stendi akamwambia asubiri kwenye moja ya mabenchi mpaka basi lake litakapofika dakika ishirini baadaye.

Kutokea hapo hakumuona tena bwana yule. Na tiketi aliyokuwa amepewa haikuwa halali. Kwanza haikuwa tiketi halali ya gari aliloahidiwa, na pili gari hilo halifanyi safari za huko alipokuwa anaenda. Basi mama yule akawa amepoteza fedha zake.

Lakini hiyo haikuwa mara ya kwanza kusikia kuhusu watu kutapeliwa pale Magufuli. Kuna taarifa nyingi kuwa wale wanaojiita “maajenti” baadhi yao wako pale kwaajili ya kuchungulia fursa za kuwatapeli abiria wanaoenda mikoani. Inaelezwa kuwa kuna watu wengi safari zao zimekomea pale baada ya “kupigwa” na matapeli.

Ni sawa kwamba kinachoendelea kinatoa ajira kwa watu wengi, lakini kunaweza kuwa na utaratibu mzuri tu. Ni muhimu hao “maajenti” kama wanatambulika na makampuni ya usafirishaji wavae vitambulisho au sare. Kuna baadhi huwa wanavaa hivyo, lakini wengi wao hawana sare wala vitambulisho. Wanauza maneno tu. Tena wanawadaka wateja wanaposhuka tu kwenye daladala. Yaani kabla hujashuka unaona watu wamejaa mlangoni wanakuwania kama mpira.

Mamlaka ziliangalie hili na ziweke msimamo thabiti dhidi ya jambo hilo. Kila ajenti awe na kitambulisho na sare fulani inayomtambulisha, au namba kwenye kizibao au utaratibu mwingine wowote ule utakaofanya hawa watu watambulike kirahisi.

Lakini pia, hata wale maajenti ambao wanatambulika basi wasaidie kuwatambua wale wanaowaharibia kazi kazi yao.
Wa kulaumiwa ni watendaji wa serikali wenye dhamana ya kusimamia kituo hiko walipaswa waweke utaratibu mzima wa abiria na wasafirishaji wenye kulinda pande zote mbili
tena uwe wa wazi
 
Hiv watu mnapigwaje s mkatie tiketi officin au online au shekilango
 
Malizia vijana hawataki kufanya kazi ngumu kwa malipo uchwara yaan unafanyishwa kazi ngumu alafu unalipwa malipo kiduchu unafanya kazi more than 12hrs alafu unalipwa afutatu yaan afutatu tu unafanyishwa kazi ngumu kwa zaidi ya masaa 12 alafu unalipwa afutatu na unapigishwa kazi ngumu za kuhatarisha hata Uhai wako na hapo hapo bado haujadharauliwa na kuonekana huna akili haufikiri nje ya box kwanini usiwataperi watu kwa siku ukaingiza more than 10 G's or even 20 G's?
Bora ya harali kuliko dhurma kaka
Dhurma hailipi kaka
 
Kuna dogo pale kitaa anafanya usalange Magufuli stand, kwa siku anakunja buku30 minimum na yeye sio agent wa bus lolote.
 
Nilipigwa hela na dada wa tumbo moja kabisa tangu hapo sijawahi kumuamini mtu yoyote linapokuja suala la hela. Inakuaje unatoa hela kulipia tiketi na basi haulioni tena sio ofisini? Majuzi nilikua nauza simu nikaongea na winga wa mjini akaniambia nimuachie simu ndani ya siku mbili atakua ashapata mteja nikasema thubutuuuuuu
 
Bora ya harali kuliko dhurma kaka
Dhurma hailipi kaka
Hujaumwa na njaa wewe yaan njaa haijakukaba alafu watu wanakuona km kiazi mdomo wa kuingiza watu King unao kwanini unashindwa kuutumia?
 
Bora ya harali kuliko dhurma kaka
Dhurma hailipi kaka
Kuongea ni rahisi sana mkuu sio ajabu unaandika comment yako ukiwa na goli linalokuingizia maokoto ya kuishi vizuri. Ufanye kazi masaa 12 unalipwa 4k toa nauli na kodi ya tumbo haubakiwi na chochote hivi unafanya mchezo
 
Kuongea ni rahisi sana mkuu sio ajabu unaandika comment yako ukiwa na goli linalokuingizia maokoto ya kuishi vizuri. Ufanye kazi masaa 12 unalipwa 4k toa nauli na kodi ya tumbo haubakiwi na chochote hivi unafanya mchezo
Kijijini si kuna mashamba kaka! Ukilima heka zako tano za mahindi ushakua millionaire. Hakuna aliyekushika shati kubaki mjini...
 
Pamoja na kwamba Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli kimetengeneza ajira kwa watu wengi, lakini kuna jambo moja linaloendelea pale na linaonekana kufumbiwa macho na mamlaka husika. Jambo hilo ni utapeli.

Juzi nikiwa kwenye pitapita zangu, nikaona watu wamemzingira mama mmoja wa makamu. Mama huyo alikuwa akiangua kilio kwamba yeye alikuwa ameteremka kwenye daladala za Kinyerezi na wakati yupo kwenye daraja la juu la watembea kwa miguu linalounganisha upande wa Kituo cha Daladala cha Mbezi Louis na Magufuli Bus Terminal, alikutana na “ajenti” wa mabasi ya mikoani.

“Ajenti” yule alimshawishi mama yule na kumuuzia tiketi ya kwenda Kondoa na akamuandikia na kukabidhi kisha alipoingia ndani ya stendi akamwambia asubiri kwenye moja ya mabenchi mpaka basi lake litakapofika dakika ishirini baadaye.

Kutokea hapo hakumuona tena bwana yule. Na tiketi aliyokuwa amepewa haikuwa halali. Kwanza haikuwa tiketi halali ya gari aliloahidiwa, na pili gari hilo halifanyi safari za huko alipokuwa anaenda. Basi mama yule akawa amepoteza fedha zake.

Lakini hiyo haikuwa mara ya kwanza kusikia kuhusu watu kutapeliwa pale Magufuli. Kuna taarifa nyingi kuwa wale wanaojiita “maajenti” baadhi yao wako pale kwaajili ya kuchungulia fursa za kuwatapeli abiria wanaoenda mikoani. Inaelezwa kuwa kuna watu wengi safari zao zimekomea pale baada ya “kupigwa” na matapeli.

Ni sawa kwamba kinachoendelea kinatoa ajira kwa watu wengi, lakini kunaweza kuwa na utaratibu mzuri tu. Ni muhimu hao “maajenti” kama wanatambulika na makampuni ya usafirishaji wavae vitambulisho au sare. Kuna baadhi huwa wanavaa hivyo, lakini wengi wao hawana sare wala vitambulisho. Wanauza maneno tu. Tena wanawadaka wateja wanaposhuka tu kwenye daladala. Yaani kabla hujashuka unaona watu wamejaa mlangoni wanakuwania kama mpira.

Mamlaka ziliangalie hili na ziweke msimamo thabiti dhidi ya jambo hilo. Kila ajenti awe na kitambulisho na sare fulani inayomtambulisha, au namba kwenye kizibao au utaratibu mwingine wowote ule utakaofanya hawa watu watambulike kirahisi.

Lakini pia, hata wale maajenti ambao wanatambulika basi wasaidie kuwatambua wale wanaowaharibia kazi kazi yao.
Ujinga tu, kwanini usikate kwenye basi moja kwa moja au ofisini?
 
Kijijini si kuna mashamba kaka! Ukilima heka zako tano za mahindi ushakua millionaire. Hakuna aliyekushika shati kubaki mjini...
Nenda kalime wewe au fungua kanisa ubiri matendo mema wengine waache wapambane kwa mbinu wanazoweza
 
Dawa pakee ukifika pale ni kuingia ndani ya stendi na kuhakikisha unakata tiketi nje ya basi husika, na baada ya hapo unaingia kwenye basi.

Ukiingia tu mkenge na kuwapa hela wale wahuni wa pale nje, unaweza ukajikuta umepigwa! Au hata kupakizwa kwenye basi tofauti kabisa na lile ambalo unataka.
Pia,siku hizi kampuni zinazojielewa hukatisha tiket online. Mimi huwa ninajilipua online tu. Nikifika stend sina taim na mtu.
 
Back
Top Bottom