UTAPELI WA FOREX: Francisco Magnetics adaiwa kuhama nchi, anadaiwa pesa nyingi. Polisi wamsaka!

Watetezi wa sajefuh
huyo sirjeff kasababisha kupotea kwa mitaji mingi ya vijana wabongo alichokiandika jamiiforum ni tofauti kabisa alichozungumza YouTube channel yake jamii kaandika ni pesa za kudownload YouTube kasema ameunguza akaunti mara Mia na ngapi sijui? jamani tukitaka kujua ukweli twendeni quora kwa watu ambako forex imeanzia kwao
 
Huyo dogo inaonesha forex anaijua kinadharia, haja practise forex ndio maana anatumia nguvu nyingi kupata watu wa kuwafundisha, hata kipindi cha Jangid Plaza alileta wasouth ambao walikuwa hawajui chochote kuhusu forex wakaishia kuchoma akaunti za mamia ya watu.
 
Nafundisha fx kwa Siku moja tu unaelewa unaanza kudownload mapesa njoo DM
 
Siku zote wajinga ndio waliwao.

Kivipi?

Kuingia kichwa kichwa kwenye suala ambalo hauna maarifa nalo.
FOREX sio utapeli sema kuna matepeli wanaotumia FOREX kutapeli wasiokuwa na uelewa mzuri na biashara hiyo. Just imagine unashauriwa kufanya studying na research for at least mwaka mmoja au miezi sita kama una kichwa chepesi kabla haujaanza kufanya trading tena demo sio live. Na ukifanikiwa kufanya study hiyo pia unashauriwa kutrade Demo account for not less than 6 month, baada ya hapo kama utajiona upo confident enough ndipo ufungue live akaunti kwa broker ambaye ni Regulated.

Hivyo ukitazama kiundani hapo inakuchukua zaidi ya mwaka mmoja na nusu kama sio miwili ili kuweza kufanya trade kwa kujiamini, lakini wengi wanaotapeliwa huwa wanaruka hizi stage wakitaka kuget rich quick hivyo wanaongozwa na mihemko, na watu wa design hii ni wengi sana ndio maana wanafanya scammers nao kuwepo kuwawinda watu hao.

Uwepo wa matapeli katika biashara ya FOREX hakuifanyi FOREX kuwa utapeli, bali uwepo wa wajinga wenye tamaa ya pesa za chapchap ndio wanawavutia matapeli kuwepo katika biashara hii.
Mwisho kabisa FOREX its all about experience JIFUNZE - ELEWA - FANYA MAZOEZI - PATA FAIDA - PATA HASARA - RUDIA TENA = PATA UZOEFU ANZA KUINGIZA FAIDA ZAIDI YA HASARA UNAYOPATA maana hasara haiepukiki kamwe hata Professional Traders wanapata hasara ila wanaicompensate na Ukubwa wa faida ukilinganisha na udogo wa hasara.

Ila ukitaka kumpatia mtu pesa yako akufanyie trade jiandae kisaikolojia.
 
Kuna mwingine naye hapa hapa bongo kachukua usd laki moja na nusu kwa watu toka January mpaka leo kapotea pasipo julikana, kibaya zaidi aliwasainisha watu mikataba hata pesa isipo rudi he is not liable
It is the risk you take! Sometimes you win and sometimes you lose; it is the name of the game!
 
Mkuu huwa inachukua karibia 5-10 years kujua kuwa unafanya Nini ndani ya trading.sio ishu nyepesi. It's simple but not easy. Wala usidanganye watu mkuu.
Lete mtu Aliye consistent profitable years after years or months after months aliyeianza below five years.
Trading and investment is a career like any other careers i.e Md , Engineering, lawyers,mhasibu. Wafikirie hao wanasoma miaka mingapi afu wanakuja kupata take home less or equal to 1000$ ambayo wewe waweza ipata ndani ya dakika moja,but if only if you know what are you doing, you've experience, you've right mindset, you've enough capital minimum let say 50k $. Ni hayo tu
 
Umeniquote vibaya mkuu nimesema at least miaka miwili unaweza kujiamini kuanza kutrade live account ila kuwa consistent profitable hilo ni swala lingine halina kipimo cha muda.
 
Umeniquote vibaya mkuu nimesema at least miaka miwili unaweza kujiamini kuanza kutrade live account ila kuwa consistent profitable hilo ni swala lingine halina kipimo cha muda.
Pamoja. Yes miaka miwili utakuwa umejua margin, leverage,pips,lots, turns and continuation of trends.
Pamoja hii ni career Kama career zingine mkuu sema watu hatupo tayari ku sacrifice our efforts,time, energy and money. Yaani watu wanapenda uwape formula basi wapakue hela Ila life sio simple kiivyo
 
Nikiwaambia vijana tuache kupenda vitu rahisi wanakuwa wakali "MTU MWENYE UCHU WA MAFANIKIO YA HARAKA NDIO MTU RAHISI KUTAPELEWA".
Kuna dada anajifanya mjanja akataka aniingize mkenge akajua wakuja nilichomfanya yeye ndio akanitumia izo bitcoin badala ya mimi kumtumia.

Sent from my 601SO using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…