Utapeli wa kampuni ya tigo wakishirikiana na bima mkononi (milvik)

Utapeli wa kampuni ya tigo wakishirikiana na bima mkononi (milvik)

Je serikali haioni jinsi kampuni ya Milvik ikishirikiana na Tigo wanavyofanya dhuluma kwa wananchi??

Kampunj ya tigo imekua ikifanya uhamasishaji wa wananchi kujiunga bima mkononi ambapo mnufaika hukatwa 5500 kila mwezi na endapo ataumwa yeye au wanufaika wengine wa familia yake kisha wakalazwa basi Tigo na Milvik watamlipa mwanachama elfu 40 kwa kila siku aliyolazwa.

Zikiwa pesa ndogo ndogo hizi wanalipa ila peleka madai makubwa hapo ndiyo utajuta. Mke wangu (mteja wao) mwaka 2021 alilazwa na mtoto MUHIMBILI zaidi ya miezi 3 na aliporuhusiwa aliwatumia Milvik document zote walizohitaji ili ku process malipo.

Shida ikaanza wakaanza kumsumbua mke wangu kwamba eti wameenda MNH ku verify hizo taarifa ila hawajaziona, tulipowaluzoa kwahiyo hizo document ni fake wakasema sio fake ila kule muhimbili hazipo, tukawaambia sasa kama sio fake kwanini hamtaki kulipa, tukataka watuambie sehemu walipoenda ku verify wakakataa, wakamtaka mke wangu (tunaishi Tabora) atoke Tabora arudi Muhimbili kuwaomba waandike medical report ingine yenye kuonyesha ile ya awali ni sahihi, tukawaambi suala la verification ni la kwenu sio mteja mbona huu ni usumbufu na hizi gharama za safari nani ata cover, kwanini nyie msitumie vyanzo zaidi ya kimoja ku verify, je mmefika kwa mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji ambaye yeye ndiye msimamizi na barua zinapitia kwake??

Je mmefika kwa madaktaribwa jengo la watoto kuwauliza , je mmeendea ku verify wapi??! Wakasema wao washaenda ku verify na hawawezi enda tena. Kwakua MILVIK walikuwa wanapaswa kulipa zaidi ya milion ilibidi tukope fedha kurudi hadi MNH kuwaelezea, majibu waliyotupa ni kwamba sisi sio wa kwanza hiyo kampuni inasumbua sana wananchi, wakasema tuwapigie pale simu ili waende MNH wakaonane na Mkurugenzi wa Huduma, Milvik wakakataa kwakusema madai yetu yalishafungwa, tulijaribu kuwasiliana na Tigo ila hakuna walichotusaidia ikabidi turudi Tabora bila kufanikisha na tukawa tumeingia hasara.

Tuliandika barua ya malalamiko TIRA na Muhimbili ila hadi leo miaka 3 hatujawahi kujibiwa!! Huu ni utapeli mkubwa unaofanywa na Tigo na Milvik kwa Watanzaia ambao unapaswa kuchukuliwa hatua. Tulitamani kuwafungulia mashtaka kwa hayo madai, hasara na usumbufu waliotusababishia ila gharama na kukosa msaada kisheria vikatufanya tukubali kudhulumiwa.

ILA NIMEONA NI BORA KULISEMA HILI JAMBO ili wengine yasije kuwakuta!!
Hii huduma ya bima mkononi sasa hivi ni kama mbinu mpya ya mapato kwa mitandao hata vodacom wanayo na wekuwa wanapigia wateja wao simu mara kwa mara nami pia nikiwa mmoja wao lakini huwa nakataa maana hainiingii akilini nichange 55000/= kwa mwezi halafu upate changamoto upewe 40000/= kwa siku.
 
Hii katika bitu nasikitika ni kua licha ya serikali ya chama cha kijani kutokubali kutoa walipo, hawataki hata kutetea maslahi ya wananchi wao kwenye huduma zinazofanywa na third parties, yani ukisoma comment watu wengi wanasema hayo malalamiko juu ya hizo kampuni ni mengi ila serikali haizibani hizo kampuni mwisho wake wananchi tunakua watu wa kupigwa tu kila sekta
 
Hizi huduma za mtandaoni muwe nazo makini sana maana huduma za bima Kwa Tanzania hata hizi zenye ofisi ni issue nzito yaani wanakuja na mambo mengi mazuri mazuri huku hawakuelezi process za kufanya unapopata shida.

Sasa Kwa mtandaoni si ndio balaa maana ukienda Tigo watakuruka watamwambia hao wanaofanya hiyo kazi ni mbia na lazima atakuwa ame-click vigezo na masharti ambavyo mkija kuvisoma baadae mtakuta vinampa haki mtoa huduma.

hao ni washenzi sana tena mkeo alijikuta amejaa akakubali maana wakikupigia simu ukiwaandekeza wanaweza wakaongea hata dakika 20 alafu unawakatalia wanakomaa wachukue tu details zako hata kama hujiungi ili ukitafakari baadae ujiunge
 
Nimekosea hapo kidogo huwezi kuchanga 5500/=kwa mwezi halafu mtu akulipie 40000/= kwa siku.
Mimi mwenyewe ndo nimeshangaa, haiingii akilini eti ukatwe elf tano Mia tano (5,500/=) alaf ulipiwe upasuaji kweli?? Inamaana kabla ya kujiunga hata hamkufikiria hilo??

Yaani itakuhitaji uchangie miezi isiyopungua 8 ndo ipatikane hela wanayokulipia wao siku moja? Hata kengele ya hatari haikulia kichwani seriously??

Hii serikali mbona mnaipa kazi ya kuchakata mambo ambayo yangepambanuliwa na kichwa chako tu
 
Kuna uzi nilisoma inaonekana wanatumia mbinu ya delay technique maana unatumia kwanza ela yako then unapeleka vielelezo kama ulivyosema na ukipeleka vielelezo Kuna uwezekano unaambiwa vina mapungufu mara hakuna muhuri mara hivi hivyo ulete vielelezo vyenye muhuri na ukirudi hospital utaambiwa utaratobu wetu huo na hatufanyi Kwa matakwa mgonjwa yaani document wanaziverify Kwa kugonga muhuri pale wanapoandika madai ya kuomba kulipwa mfano NHIF etc. Kimsingi wamekosa uhalali wa kutoa bima maana bima inatakiwa ifidie gharama zako pasipo kuweka wewe chochote labda Kwa zile huduma ambazo bima haihusiki. Kwa maana nyingine hao jamaa huduma yao haitambuliki kwenye hospitali zetu na ndio maana hata ushirikiano unakuwa mdogo.

Kama Wana Nia njema walipaswa kuingiza makubaliano na hospitali ili ukienda tu unawaambia hospitali Kwa kutoa vielelezo vyako na hospitali inawasiliana nao.

Soma uzi huo chini, comment namba 6

 
Mamlaka inayosimamia bima ambayo ni TIRA ipo lakini haishughulikii hizi changamoto, hawa jamaa wanatakiwa kufutiwa usajili na kuburuzwa mahakamani kabisa!!
Unakuwa kama mgeni na hizi mamlaka,hapo watu washakula chao
 
Mimi mwenyewe ndo nimeshangaa, haiingii akilini eti ukatwe elf tano Mia tano (5,500/=) alaf ulipiwe upasuaji kweli?? Inamaana kabla ya kujiunga hata hamkufikiria hilo??

Yaani itakuhitaji uchangie miezi isiyopungua 8 ndo ipatikane hela wanayokulipia wao siku moja? Hata kengele ya hatari haikulia kichwani seriously??

Hii serikali mbona mnaipa kazi ya kuchakata mambo ambayo yangepambanuliwa na kichwa chako tu
Mantiki nzima ya bima unaielewa lakini?? Hebu tuambie bima yoyote uliyojiunga na namna unanufaika. Bima kiufupi ni mchange wengi wanufaike wachache kwa kile walichochanga wengi, ndiyo maana unaweza tibiwa Upasuaji wa milioni 5 kwa NHIF na michango yako ikawa chini ya milioni 1.
 
Hii dhulma inafahamika, ila kwa kuwa waTz ni wajinga, wanaendelea kujiunga
 
Je serikali haioni jinsi kampuni ya Milvik ikishirikiana na Tigo wanavyofanya dhuluma kwa wananchi??

Kampunj ya tigo imekua ikifanya uhamasishaji wa wananchi kujiunga bima mkononi ambapo mnufaika hukatwa 5500 kila mwezi na endapo ataumwa yeye au wanufaika wengine wa familia yake kisha wakalazwa basi Tigo na Milvik watamlipa mwanachama elfu 40 kwa kila siku aliyolazwa.

Zikiwa pesa ndogo ndogo hizi wanalipa ila peleka madai makubwa hapo ndiyo utajuta. Mke wangu (mteja wao) mwaka 2021 alilazwa na mtoto MUHIMBILI zaidi ya miezi 3 na aliporuhusiwa aliwatumia Milvik document zote walizohitaji ili ku process malipo.

Shida ikaanza wakaanza kumsumbua mke wangu kwamba eti wameenda MNH ku verify hizo taarifa ila hawajaziona, tulipowaluzoa kwahiyo hizo document ni fake wakasema sio fake ila kule muhimbili hazipo, tukawaambia sasa kama sio fake kwanini hamtaki kulipa, tukataka watuambie sehemu walipoenda ku verify wakakataa, wakamtaka mke wangu (tunaishi Tabora) atoke Tabora arudi Muhimbili kuwaomba waandike medical report ingine yenye kuonyesha ile ya awali ni sahihi, tukawaambi suala la verification ni la kwenu sio mteja mbona huu ni usumbufu na hizi gharama za safari nani ata cover, kwanini nyie msitumie vyanzo zaidi ya kimoja ku verify, je mmefika kwa mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji ambaye yeye ndiye msimamizi na barua zinapitia kwake??

Je mmefika kwa madaktaribwa jengo la watoto kuwauliza , je mmeendea ku verify wapi??! Wakasema wao washaenda ku verify na hawawezi enda tena. Kwakua MILVIK walikuwa wanapaswa kulipa zaidi ya milion ilibidi tukope fedha kurudi hadi MNH kuwaelezea, majibu waliyotupa ni kwamba sisi sio wa kwanza hiyo kampuni inasumbua sana wananchi, wakasema tuwapigie pale simu ili waende MNH wakaonane na Mkurugenzi wa Huduma, Milvik wakakataa kwakusema madai yetu yalishafungwa, tulijaribu kuwasiliana na Tigo ila hakuna walichotusaidia ikabidi turudi Tabora bila kufanikisha na tukawa tumeingia hasara.

Tuliandika barua ya malalamiko TIRA na Muhimbili ila hadi leo miaka 3 hatujawahi kujibiwa!! Huu ni utapeli mkubwa unaofanywa na Tigo na Milvik kwa Watanzaia ambao unapaswa kuchukuliwa hatua. Tulitamani kuwafungulia mashtaka kwa hayo madai, hasara na usumbufu waliotusababishia ila gharama na kukosa msaada kisheria vikatufanya tukubali kudhulumiwa.

ILA NIMEONA NI BORA KULISEMA HILI JAMBO ili wengine yasije kuwakuta!!
Tigo waliigawa huduma ya Bima kwa jamaa wa kampuni moja inaitwa Proin kama sikosei. Waliitoa huduma hiyo, kwa malengo ya kufanya iwe na ufanisi.
Na baadhi ya wamiliki wa kampuni hiyo ni jamaa ambao ni miongoni mwa waliofanikiwa kuchota zile hela za EPA ambao JK aliamuru warudishe ili wasishtakiwe.

Hawa Proin ndiyo wanatakiwa kutoa majibu.

Ova
 
Back
Top Bottom