Utaratibu mpya wa Sumatra wasotesha abiria bandarini

Utaratibu mpya wa Sumatra wasotesha abiria bandarini

abdulahsaf

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
858
Reaction score
130
[h=2][/h]



Mamia ya abiria waliotarajiwa kusafiri jana kwenda visiwani Zanzibar, jana walikwama kuondoka kutokana na utaratibu mpya wa vitambulisho unaodaiwa kutolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini Nchini (Sumatra).

Kwa mujibu wa utaratibu, abiria haruhusiwi kukata tiketi ya kusafiri kwenda visiwani humo iwapo hatakuwa na kitambulisho, kikiwamo cha uraia.

Vitambulisho vingine ambavyo abiria anatakiwa kuwa na kimojawapo, ni pamoja na cha makazi, kupiga kura, kazi, leseni ya dereva, utambulisho kutoka serikalini au pasi ya kusafiria.

Baadhi ya abiria waliokwama kusafiri, walisema wamechelewa kupata taarifa hizo kwa kuwa hawaujasikia utaratibu huo katika chombo chochote cha habari.

Utaratibu huo ambao maelezo yake yamebandikwa kwenye kuta za ofisi za kukatia tiketi katika bandari za meli zinazokwenda visiwani humo, umeelezwa kuwa ulianza kutumika rasmi Agosti 13, mwaka huu.
 
Tatizo vyombo au taasisi husika huendesha hutekeleza maamuzi yao kwa nguvu ya soda, kuna wakati kule Zanzibar ilikuwa huwezi kupata tiketi bila kitambulisho, lakini ilifanyika hivyo nafikiri labda ndani ya mwezi mmoja tu. SUMATRA wanapaswa kutoa elimu ya kutosha kwanini? mtu anhitaji kutoa utambulisho anapokata tiketi; vile vile inapotokea ajali wanapaswa kuchukua hatua kuhakiki wahanga wanafidiwa, hii itachangia kuonyesha umuhimu wa jambo hilo kwa jamii.
 
Na kama sina hivyo vitambulisho walivyosema hapo juu,kwani Tanzania hatuna vitambulisho vya raia ,hizo pasi kupata ni longolongo na lazima uwe na sababu ya maana,na vya udereva mimi hata baisikeli sina ,na hiyo mifuko ya jamii ndio usisesema mimi ni mchoma mkaa,sasa itakuwaje?je kwenda Mafia nako watadai hizo hati ,na je kwenda bukoba kupitia ziwa victoria au Ukerewe nako Sumatra wanadai hizo hati?basi hata Kigamboni iwe ni hivyo au ndio Zanzibar sio Tanzania?
 
Watanzania tuna matatizo na ni wataalam wa kulalamika kwelikweli.
Hivi mnaosafiri kwa ndege airport mnafika saa ngapi? na kwa nini?
Lack of identification ndiyo tatizo kubwa hasa wakati wa maafa kuwatambua waathirika
SUMATRA baada ya kupewa majukumu na SMZ pamoja na SMT wameanzisha utaratibu unaoeleweka
mmeanza kulalamika ooh nguvu ya soda ooh wanasumbua abiria come on guys mnataka nini hasa?
Tunaweza kuleteana unazi wa kisiasa lakini kwenye element ya safety waacheni wataalam washughulikie mbona zamani zanzibar tulikuwa tunakwenda na passport?????
What sort of society are we in YOU ARE DAMNED IF YOU DO AND YOU ARE DAMNED IF YOU DONT?
 
Maoni yangu ni kuwa sisi kama wananchi nasi tunamatatizo ambayo kuna wakati tunalazimisha uvunjwaji wa sheria kwa sababu ya convenience tu. Mfano kwenye vyombo vya usafiri hata gari ikiwa imejaa tuko tayari kupanda eti kwa sababu ya uharaka wa safari zetu. wenye vyombo wanatambua hivyo na ndiyo maana tunateketea kila siku. dereva anaendesha vibaya lakini tukikutana na polisi njiani hatulalamiki na hata tukiulizwa kama dereva anaendeshaje katika safari response yetu ni passive.
Vyombo kama Sumatra vinaudhaifu wake lakini na sisi wananchi hatusaidii kazi yetu ni kucriticise tu bila kutuo alternative option
 
utaratibu siyo mbaya ingawa nadhani walibidi watangaze ili watu wajue mana hata mimi binafsi huu usumbufu ungenikuta.

ila nadhani sumatra waje hadi uku kwenye usafiri wa nchi kavu ( kwenye magari ya mikoani )mana tunalanguliwa sana ticket na watu wengi wana kasumba ya kuandika majina ya uongo kwenye ticket sijui kwanini na mwisho wa siku likitokea la kutokea inakuwa shida kuwatambua mana majina ya uongo.
 
pata picha huu utaratibu wa vitambulisho upelekwe hadi kwenye guest house na hotel.........upati chumba mpaka uonyeshe kitambulisho.
 
Back
Top Bottom