Utaratibu wa kufatilia Mirathi uko vipi wakuu.

Utaratibu wa kufatilia Mirathi uko vipi wakuu.

Nenda kwa msajili wa vizazi na vifo ukiwa na;
1. Mhutasari wa kikao cha familia kukuteua kuwa msimamizi wa mirathi. Hakikisha kwenye mhutasari kuna wategemezi wote wa marehemu. Mhutasari uwe na muhuri wa mtendaji wa kijiji. Hakikisha umeainisha wategemezi wote na mali zote za marehemu. Epuka kugawa mali kwenye mhutasari wa kuteua msimamizi. Mtagawa baadae baada ya mahakama kupitisha. Na kama mnagawa sasa basi mtenganishe mihutasari

2. Barua ya mtendaji kukutambulisha kama mkazi wa eneo lake. Barua iwe ya mtendaji(mtu wa serikali) sio mwenyekiti wa kitongoji. Hata kama una NIDA.

3. Cheti chako cha kuzaliwa kukutambulisha kama marehemu ni baba yako
4. Kibali cha kifo

Nyaraka hizo zote scan kwa sababu zitaingizwa kwenye mfumo na ndani ya mwezi utapewa Cheti cha Kifo.
Baada ya hapo utaenda mahakama ya mwanzo kufungua shauri.

Mahakama utaenda na;
1. Cheti cha Kifo
2. Kibali cha mazishi
3. Muhutasari wa kuteuliwa kuwa msimamizi
4. Barua ya utambulisho toka kwa mtendaji
5. Barua za utambulisho za wadhamini wako wawili
6. Wosia kama upo
Shauri litafunguliwa kisha utapangiwa tarehe ya kusikiliza ukiwa wewe na nduguzo hasa wanufaika. Hukumu itaandikwa kukuteua na kuendelea na hatua ya kugawa mali.
Kama una haraka uende na hela kidogo za kumpoza hakimu ili akupangie tarehe za karibu na kukupitishia vitu vyako chapchap mf. Ardhi, pensheni nk

Kama usajili wa mali haupo kwenye mataasisi hapo itakuwa simple. Mfano mashamba hayana hati, mifugo viwanja havina hati. Ila kama zimesajiliwa ardhi, au benki au NSSF hapo kuna urasimu mwingi hasa NSSF
 
Wakuu naomba kujua utaratibu umekaa vipi? yani napaswa niwe na vitu gani vya muhimu zaidi Ili mchako uweze kwenda kwa haraka.

Mpaka sasa na muhtasari wa kikao na Kibali cha Mazishi tu na hichi Kibali cha Mazishi nacho jina lililotumiaka la baba mzazi si lile ambalo marehemu alilokuwa analitumia kazini, Kwahiyo nalo naomba kujua nalisolve vipi hili nalo.

Pia naomba kujua barua nayoenda kuchukua kwa mwenyekiti wa mtaa ni ya kunitambulisha kama msimamizi wa Mirathi au ya nini hasa.

Dr Matola PhD OKW BOBAN SUNZU msaada wenu pls na wengine mnaojua haya mambo.
Kwenye jina nenda mahakamani wakupe hati ya kiapo ya kumtambuwa marehemu kwa majina yote kwamba ni majina yake.

Kama death certificate unayo mukhtasari peleka serikali ya mtaa, mukhatasari ulioandikwa kwa mkono ni bora zaidi, serikali ya mtaa watakugongea mihuri utakwenda mahamakama ya mwanzo kufunguwa mirathi.

Mengine yajenge na karani wa mahakama atakuongoza na ndio atakukutanisha na hakimu mnayajenga unakwenda kutowa tangazo la Mirathi kwenye gazeti la ccm ( hapo usiniulize kwa nini, ccm imejikita kila sehemu)

Tangazo likitoka nunuwa gazeti kata kile kipande cha tangazo peleka mahakamani kwa karani.

Note: Mahakamani karani ndio kila kitu kaa vizuri na karani utamaliza mambo yako faster lakini wanufaika wote wa Mirathi lazima waitwe kuhojiwa na hakimu.

Anza na hatua hizo mengine utaendelea na karani atakuongoza.
 
Marehemu ni kaka yangu.
Hapo mkuu kuna mambo ya msingi utatakiwa kujiandaa kukabiliana nayo mahakamani. Unatakiwa kuthibitisha kwa nini wewe ni mnufaika pekee.
Wanufaika wa mirathi ya mwanaume mume ni mke, watoto na wazazi. Ikiwa mke hayupo, ni watoto na wazazi, ikiwa watoto hawapo ni wazazi na ndugu.

Mahakama humpa kipaumbele mke halali wa marehemu kuwa msimamizi wa mirathi, otherwise kuwe na sababu za msingi za kutopendekezwa na kikao cha ndugu. Hata wakati wa kusikiliza shauri utasisitizwa watu muhimu kama hao wasikose,mke, wazazi na watoto. Itaenda hivyo kwa Msajili wa Vizazi na Vifo mpaka Benki watachukua tahadhali hiyo kwamba kwa nini ni wewe na sio mke au watoto.

Ukifanikiwa kuithinishwa na mahakama utapewa fomu na. 6 kujaza mgawanyo wa hiyo fedha ya benki. Itaandikwa barua kwenda kwa meneja wa benki kupitia mahakama ya wilaya ikiielekeza kufanya malipo. Kama mirathi haina changamoto italipwa moja kwa moja kwa wanufaika, tofauti na hapo itakipwa mahakama ili igawe yenyewe.

Kwa hivyo mahakama inapoona mnufaika ni ndugu na sio mke, watoto na wazazi, huchukua tahadhali kubwa sana wasije kukupitisha kisha kesho akaja mtu kuweka pingamizi. Ndio maana husikia kesi za mirathi zinaweza kwenda hata miaka 10.

Wakuu watanisahihisha kama kuna sehemu nimechanganya
 
Hapo mkuu kuna mambo ya msingi utatakiwa kujiandaa kukabiliana nayo mahakamani. Unatakiwa kuthibitisha kwa nini wewe ni mnufaika pekee.
Wanufaika wa mirathi ya mwanaume mume ni mke, watoto na wazazi. Ikiwa mke hayupo, ni watoto na wazazi, ikiwa watoto hawapo ni wazazi na ndugu.

Mahakama humpa kipaumbele mke halali wa marehemu kuwa msimamizi wa mirathi, otherwise kuwe na sababu za msingi za kutopendekezwa na kikao cha ndugu. Hata wakati wa kusikiliza shauri utasisitizwa watu muhimu kama hao wasikose,mke, wazazi na watoto. Itaenda hivyo kwa Msajili wa Vizazi na Vifo mpaka Benki watachukua tahadhali hiyo kwamba kwa nini ni wewe na sio mke au watoto.

Ukifanikiwa kuithinishwa na mahakama utapewa fomu na. 6 kujaza mgawanyo wa hiyo fedha ya benki. Itaandikwa barua kwenda kwa meneja wa benki kupitia mahakama ya wilaya ikiielekeza kufanya malipo. Kama mirathi haina changamoto italipwa moja kwa moja kwa wanufaika, tofauti na hapo itakipwa mahakama ili igawe yenyewe.

Kwa hivyo mahakama inapoona mnufaika ni ndugu na sio mke, watoto na wazazi, huchukua tahadhali kubwa sana wasije kukupitisha kisha kesho akaja mtu kuweka pingamizi. Ndio maana husikia kesi za mirathi zinaweza kwenda hata miaka 10.

Wakuu watanisahihisha kama kuna sehemu nimechanganya
Usahihi ni kwamba pesa za marehemu zilizopo bank account inafungwa zinalipwa kwenye account ya mahakama, wanufaika wanajaza fomu na mgawanyo wa pesa hizo na account number mahakama ndio inawaingizia pesa wanufaika kwenye account zao.
 
Kibali cha mazishi hakihitajiki popote kwenyechakato wa mirathi ni cheti cha kifo

Hiyo mirathi account ya mahakama inaatamia sana pesa za warithi hadi miezi sita unasota huku taratibu zote umekamilisha na una barua ya kitita kuwekwa huko tayari
 
Usahihi ni kwamba pesa za marehemu zilizopo bank account inafungwa zinalipwa kwenye account ya mahakama, wanufaika wanajaza fomu na mgawanyo wa pesa hizo na account number mahakama ndio inawaingizia pesa wanufaika kwenye account zao.
Inachukua muda gani mahakama ikishapokea pesa kama Kila kitu kimekamilika kulipa wahusika,inachukua muda gani?
 
Wakuu OKW BOBAN SUNZU na Dr Matola PhD huwa inachukua mda gani mahakama kuwalipa wanufaika baada ya kumalizika taratibu zote. Nauliza hivyo kwasababu tunasubiria tangu tarehe 22 mwezi uliopita pesa ziingizwe kwenye akunti ya mama ambaye ni mnufaika lakini mpaka sasa ni hakuna kitu.

NB; Pesa zilishahmishiwa kwenye akunti ya mahakama tangu tarehe 20 mwezi 9.
Kama hakuna tatizo ni mapema iwezekanavyo. Fuatilia kwa mhasibu wa mahakama kujua kama kuna shida, kama yeye ameshalipa basi issue itakuwa hazina ndogo huwa wana urasimu usipokuwa msumbufu. Wanaweza kuona tatizo wakakaa kimya bila kusema, kwa hiyo usiache kuwasumbua
 
Wakuu OKW BOBAN SUNZU na Dr Matola PhD huwa inachukua mda gani mahakama kuwalipa wanufaika baada ya kumalizika taratibu zote. Nauliza hivyo kwasababu tunasubiria tangu tarehe 22 mwezi uliopita pesa ziingizwe kwenye akunti ya mama ambaye ni mnufaika lakini mpaka sasa ni hakuna kitu.

NB; Pesa zilishahmishiwa kwenye akunti ya mahakama tangu tarehe 20 mwezi 9.
Ulisema wewe ni ndugu wa marehemu na kwamba ni mnufaika peke yako🤔something’s fishy here! Now unaulizia pesa zima chukua muda gani kuingia kwenye akaunti ya ‘Mama’ ambaye kwa maneno yako naye ni “mnufaika”.
Watch yourself man, your story isn’t giving.
 
Wakuu OKW BOBAN SUNZU na Dr Matola PhD huwa inachukua mda gani mahakama kuwalipa wanufaika baada ya kumalizika taratibu zote. Nauliza hivyo kwasababu tunasubiria tangu tarehe 22 mwezi uliopita pesa ziingizwe kwenye akunti ya mama ambaye ni mnufaika lakini mpaka sasa ni hakuna kitu.

NB; Pesa zilishahmishiwa kwenye akunti ya mahakama tangu tarehe 20 mwezi 9.
Mambo ya mahakama yapo taratibu, sisi tunasubiri huu mwezi wa 4
 
Back
Top Bottom