Utaratibu wa kuingiza mashine za mbao Tanzania

Utaratibu wa kuingiza mashine za mbao Tanzania

Mashine zetu tunauzia Zanzibar. Ushuru wana calculate used items zilizomo kwenye container la 40ft.Sijawahi kulipa zaidi ya milioni 5. Sifahamu wanacharge kiasi gani kwa brand new machine.
 
cha kukushauri pitishia Zanzibar au bandari ya Mombasa kwani hakuna longolongo sana na hautaumia ukipitishia bandari ya dar utauimia na mzigo wako waweza kukaa sana na usipate kitu nakushuri tu mkuu
 
Hivi ukipitisha Zanzibar... Hakuna gharama nyingine ambazo naweza kumbuna nazo pindi ninapo taka kuzileta Dar, ukichilia gharama za usafiri wa Zanzibar to Dar?
 
Hivi ukipitisha Zanzibar... Hakuna gharama nyingine ambazo naweza kumbuna nazo pindi ninapo taka kuzileta Dar, ukichilia gharama za usafiri wa Zanzibar to Dar?

Ukitaka kuzileta Dar watakutoza kodi nyengine.
 
Kama lengo ni kuja nazo tz bara na kushauri pitishia bandari ya Dar Es salaam vinginevyo garama itaongezeka +muda + usumbufu.
Nilisha wahi pitishia container moja Zanzibar nilijuta na niliona nimelipa zaidi kuliko ningepitishia Dar.
 
cha kukushauri pitishia Zanzibar au bandari ya Mombasa kwani hakuna longolongo sana na hautaumia ukipitishia bandari ya dar utauimia na mzigo wako waweza kukaa sana na usipate kitu nakushuri tu mkuu
Mi niliagiza machine zangu toka China, nilifuata procedure za kawaida. Nisafirisha kwa Container ya 40ft mwenyewe na walinichaji $1150 to dsm.

Gharama za kodi zinategemeana na aina ya Mzigo. Kuna kitabu chao cha kodi kinaelezea kila category na aina/kiwango cha kodi (Kiasi cha Import Duty - Maximum ni30% ya CIF na VAT 18%).

So, kudetermine kodi, tafuta kitabu cha kodi wanachotumia customs uangalie category utaona kodi. Kuna machines zingine hazina kabisa import duty so unalipia VAT tu plus others charges kama shipping line, Rail Devel. Levy (5%), nk.
 
Back
Top Bottom