Utaratibu wa kusitisha ajira kisheria msaada hapa;

Myhope

Senior Member
Joined
Jul 20, 2017
Posts
154
Reaction score
67
Mwajiri kaniachisha kazi bila kufanya haya,
1. Hajatoa nafasi ya kukata rufaa.
2. Hakutoa cheti cha utumishi.
3. Kamati ya kuchunguza tuhuma haikuwa
na kiongozi kutoka chama cha wafanyak
azi.
4. Kikao cha nidhamu kilifanyika nje ya
wilaya tukio lilipotokea.
5. Baada ya kikao cha nidhamu ilipita miezi
miwili ndipo akatoa barua ya termination

Je ni kipi kati ya hivyo siyo sahihi kwenye utaratibu wa kisheria?
 
Jamani naombeni madini hapa mbona kimya?
 
Hayo yote uliyayaainisha yapo sahihi kama unlawful termination ila yatakuwa sisahihi kulingana na kosa ulilofanya, vilevile kama ulikwishapewa onyo kwa barua ama kwa mdomo kabla ya hiyo termination
 
Naomba kujua ulifanya kosa gani, je ulipewa barua ya onyo? Umesoma HR manual ya sehemu yako ya kazi inazungumzia nn kuhusu termination?
 
Hayo yote uliyayaainisha yapo sahihi kama unlawful termination ila yatakuwa sisahihi kulingana na kosa ulilofanya, vilevile kama ulikwishapewa onyo kwa barua ama kwa mdomo kabla ya hiyo termination
Sijawahi pewa onyo lolote mkuu
 
Naomba kujua ulifanya kosa gani, je ulipewa barua ya onyo? Umesoma HR manual ya sehemu yako ya kazi inazungumzia nn kuhusu termination?
Kosa ni kukusudia kuiba polisi wakachunguza wakaona sina kosa, barua ya polisi ninayo pia sijawahi pata onyo lolote kk
 
Mkuu Katus Manumbu
Hiyo namba 1 na namba nne pengine una hoja hapo.

Ila kesi yako ni rahisi ikiwa utapata Wakili mzuri maana ushasema kosa ni kukusudia kuiba na polisi wamechunguza wamekuta huna hatia na barua unayo ni hoja nzuri.

Kuhusu kukata rufaa, ulipaswa uonane na mwanasheria ili ikiwezekana umfungulie mashtaka muajiri wako.

Kufanya kikao cha nidhamu nje ya sehemu husika inaweza isiwe hoja endapo tu ulijulishwa kwa maandishi sababu ya kikao kufanyika huko.

Kesi yako ni rahisi kama tu utakuwa na nia ya dhati ya kupambana.

La zaidi inahitajika pesa tukusaidie kisheria.
 
Ahsante mkuu
 
Pesa wakati hana kazi mkuu!
 
Barua ya termination inasema umefukuzwa kazi kwa sababu ya kukusudia kuiba? Maana wasije wakasema wamekufukuza kwa sababu nyingine.
 
Kosa ni kukusudia kuiba au wizi umetokea kikwelikweli na wewe ukawa mtuhumiwa? Weka wazi kila kitu ili usaidiwe mawazo kwa usahihi
 

1) Katika kikao cha nidhamu uliambiwa ulete shahidi wako? Na ulifanya hivyo?

2) Uliwahi kutuhumiwa kwa kosa lolote kabla ya hilo? Yani una BARUA YA ONYO ambayo uliwahi kupewa? Au ONYO ya mdomo na mwajiri wako? Au uliwahi kukutwa na hatia kabla hapo kazini na kosa lolote lile?

3) Hasara uliosababisha kwa huyo mwajiri wako, ulikatwa kwenye mshahara au ulilipishwa?

4) Kosa ulilofanya ni JINAI (wizi n.k) au ni UZEMBE KAZINI uliosababishia kuachishwa kazi?

Pia weka wazi kosa lililosababisha wewe kufukuzwa, kumbuka ni vyema ukawa mkweli kwetu, kwani ukitudanganya sisi tutaishia kukupa ushauri kutokana na kauli yako usio na mashiko, mwisho wa siku itakua ni kazi bure maana mwajiri wako atakuja na ushauri wenye mashiko.

Ushauri wa kesi sio kama ushauri wa kuuza nyanya au bamia, unapaswa kua mkweli kabisa, ili watu wajue wanakushauri vipi.

Nafasi bado unayo ya kukata rufaa;

1) Mediation & Arbitration centre (Labour Court).
2) High Court Labour Division.
 
1.Niliambiwa ila kikao kilipelekwa wilaya nyingine nikashindwa gharama za kupeleka mashahidi.
2.Sijawahi fanya kosa wala kupewa onto lolote.
3.Hakuna hasara yoyote iliyosababishwa.
4.Ni kosa la jinai (kukusudia kuiba).

Kesi ilikuwa hivi;
Nilikaimishwa nafasi 2 za uongozi, kama meneja pia mkuu wa idara. Likaja gari la mafuta invoice na delivery note za mzigo zinaonyesha Lita 15,000. Kihualisia mafuta yaliyokuwa ndani ya tanker la gari ni Lita 18,000 ambapo kiasi cha Lita 3,000 zikawa zimezidi.

Nikapokea mafuta Lita 15,000 kama documents zilivyosema na kuacha Lita 3,000 zilizokuwa zimezidi zirudishwe zilipotoka kama dereva alivyokuwa amesema, nikaandika barua kuelezea jinsi ilivyokuwa na nilichokifanya. Gari likaondoka kufika wilaya jirani likakamatwa na polisi, likarudishwa lilipotoka kesi ikaanzia hapo.

Wakaja watu kuchunguza hawakukuta upungufu wowote wa mafuta kisha Jeshi la polisi nao wakafanya uchunguzi na wakaona sina hatia kwa kuwa ktk mali ya Mwajiri hakuna loss yoyote. Hivyo tuhuma ya wizi haipo. Polisi waliandika barua kwenda kwa mwajiri na kusema kwamba hawaoni kosa langu.

Mwajiri yeye akaamua kunichukulia hatua za kinidhamu na kuniachisha kazi.
Naombeni mawazo yenu hapa.
 
Kama ni hivyo ulivyoelezea katika maelezo yako, basi mwajiri amekuonea na haki yako unaweza ukaipata (nakushauri tafuta mwanasheria akusimamie swala lako ili iwe rahisi kupata haki yako, ila kama utaweza kujisimamia mwenyewe pia sawa). Kuna njia mbili unaweza ukatumia;

Njia ya kwanza, mwanasheria waki amwandikie barua muajiri wako (DEMAND NOTICE) kumuamuru akulipe fidia mtakayoitaka ndani ya siku mtakazompa (either siku 14 au 21 au zaidi), akimalizia kwa onyo kua asipotimiza maombi yenu ndani ya hizo siku basi mtamchukulia hatua kali za kisheria dhidi yake. (TAMBUA barua hii lazima iwe imeandikwa kisheria kwa kuchambua makosa aliofanya mwajiri, ushahidi uliopo dhidi yake, na ushahidi wa hasara uliopata ili iwe na nguvu). Hii inasaidia kuokoa muda wa kwenda mahakamani kama muajiri ataamua kukulipa fidia na kuepuka kwenda mahakamani.

Njia ya pili,

1) Andaa vithibisho na document zote za ushahidi (copy na original). ***Hio barua ya Police ni muhimu sanaa uwe nayo.

2) Kafungue madai ya UNFAIR TERMINATION katika mahakama ya kazi.

Maombi yako mbele ya mahakama unaweza ukaomba;

i) Mahakama ITOE TAMKO/TAFSIRI/HUKUMU kua umefukuzwa kazi kwa uonevu/kinyume na sheria/bila kufuata utaratibu wa sheria za kazi.

ii) Pili, kumshtaki mwajiri kwa kukufukuza kazi bila uhalali/kufuata sheria na kudai fidia unayoitaka kutokana na hasara ulizopata kwa kufukuzwa kazi (mfano mshahara wa mwaka mmoja/hasara za fedha ulizo/utakazomlipa mwanasheria wako/hasara za kuendesha kesi mpaka iishe/na gharama nyingine).

Ushauri wangu tafuta mwanasheria/wakili akusaidie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…