Utaratibu wa Kutaja Itifaki ya Viongozi Tanzania uangaliwe upya

Utaratibu wa Kutaja Itifaki ya Viongozi Tanzania uangaliwe upya

Kirchhoff

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
5,735
Reaction score
8,541
Nimekuwa nikifuatilia matukio mbalimbali ya Kiserikali na kijamii mara nyingi. Niseme tuu Sipendwezwi na Utaratibu Wa Kutaja na kutambuana Viongozi kabla ya kuanzia hotuba au salamu zao.

Mfano Leo Hapa Arusha, Jukwaa kuu Lina Viongozi Zaidi ya Ishirini na Kila kiongozi anayetaka kuongea analazimika Kutaja na kutambua Viongozi wote waliopo.

Kiongozi anatumia dakika Tano Kutaja Viongozi waliopo ambao tena watatajwa na Viongozi wengine wanaofuata.

Ni Kwa Nini kusiwe na Mtaja ITIFAKI Mmoja Tuu Mwanzoni atambue uwepo wa watu wote? Kisha Kila Mtoa Hotuba amtaje tuu Mgeni Rasmi labda na Mwenyeji wake na pia Mgeni Rasmi pia katika hotuba yake atambue uwepo wa hao watu katika hotuba yake.

Hii itaondoa uchovu wa kusikiliza marudio ya Majina na vyeo vya Viongozi waliohudhuria jambo Husika.
Wakati wa Maghufuli Mwanasayansi Mbobevu alizingatia Mda na mara nyingi hakutaka watu warudie rudie kutajanatajana hovyo.

Nawasilisha.
 
Nimekuwa nikifuatilia matukio mbalimbali ya Kiserikali na kijamii mara nyingi. Niseme tuu Sipendwezwi na Utaratibu Wa Kutaja na kutambuana Viongozi kabla ya kuanzia hotuba au salamu zao.

Mfano Leo Hapa Arusha, Jukwaa kuu Lina Viongozi Zaidi ya Ishirini na Kila kiongozi anayetaka kuongea analazimika Kutaja na kutambua Viongozi wote waliopo.

Kiongozi anatumia dakika Tano Kutaja Viongozi waliopo ambao tena watatajwa na Viongozi wengine wanaofuata.

Ni Kwa Nini kusiwe na Mtaja ITIFAKI Mmoja Tuu Mwanzoni atambue uwepo wa watu wote? Kisha Kila Mtoa Hotuba amtaje tuu Mgeni Rasmi labda na Mwenyeji wake na pia Mgeni Rasmi pia katika hotuba yake atambue uwepo wa hao watu katika hotuba yake.

Hii itaondoa uchovu wa kusikiliza marudio ya Majina na vyeo vya Viongozi waliohudhuria jambo Husika.
Wakati wa Maghufuli Mwanasayansi Mbobevu alizingatia Mda na mara nyingi hakutaka watu warudie rudie kutajanatajana hovyo.

Nawasilisha.
Kichwa chako kimejaa sana mkuu, umezungumza jambo la msingi mno. Na mimi nafuatilia haya maadhimisho kwenye Luninga ila kiujumla yanaboa sana kwenye 'segment' ya hizo itifiki.
 
Nakubaliana na wewe, ni vema hili jambo likaangaliwa na ikipendeza mwenyeji wa shughuli ndio atambue uwepo wa wote aliowaalika.
 
Mambo ya kipuuzi hufanywa na wapuuzi...
Na upuuzi ukizidi sana huondoa uzuri wa jambo.
 
Back
Top Bottom