Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
we ni mubaya bana, unatisha, haya mm - mjibu huyu.Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.
Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamungunywa kwa nidhamu,Kungatwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.
Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamungunywa kwa nidhamu,Kungatwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe
Mwanakijiji salaam,natumai u mzima
Nashika nami kalam,Kujibu uliyosema
Nitajaribu maadam,ntasema yalo mema
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe.
Kuna embe nafahamu,Kokwale lilo laini
Lipo tangia Adamu,Yaani enzi za zamani
Lamungunywa kwa nidhamu,Kungatwa katu jamani
Embe liso na kokwa,Si embe hata kwa chembe
Swali nawaulieni,
Magwiji mnijibuni,
Nimetingwa akilini,
Jibu sijalibaini,
Embe lisilo na kokwa, ni embe au kimbembe!?
Babu yangu Mwanakijiji,katu usitingwe akilini
Watakuja wengi wajibuji,na majibu yaso kifani
Haihitaji kumpa mtu mji,ili upate jibu akilini
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe
Embe lisilo na kokwa,kamwe haliwezi tokea
Hata ukienda Rukwa,lenye kokwa watakuelea
Embe lilo na kokwa,vizuri mtini labembea
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe
Amani kweli umenena,kuhusu kokwa lilo laini
Kwa hakika umenikuna,kwa wako ubeti makini
Kokwa laini lililotuna,embe lake ni tamu jamani
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe
Embe lililo na kokwa,kwa nafasi linanyonywa
Laliwa pasi kumenywa,na maganda lamengenywa
Hilo embe lisilo na kokwa,hata bure huwezi pewa
Embe lisilo na kokwa,si embe bali kimbembe
Mkuu kumbe nawe uko!, safi sana
Swali nawaulieni,
Magwiji mnijibuni,
Nimetingwa akilini,
Jibu sijalibaini,
Embe lisilo na kokwa, ni embe au kimbembe!?
Malenga mmenishika,kusema japo kidogo
Kuna embe nakumbuka,nilitafuna kigogo
Kwa kweli nilistuka,japo sikua mdogo
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani
Kwa hamu nilivutika, kulitia mdomoni
Mkeka akatandika,mwenyeji wangu chumbani
Mkono akanishika,akanivuta kwa shani
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani
Hili embe lajificha,kulila siwe papara
Nlikula usiku kucha,tena sio la duara
Mwenzenu sipati picha,embe si masihara
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani?
Nlibaki nalitafuta,kokwale siku kucha
Ulimi nikauvuta,nikatumia na kucha
Mwenyeji akajivuta,akanipa lote bucha
Hili embe liso kokwa,sijui ni embe gani