Utata muda wa kazi: Bosi amenitaka nifanye kazi 12hrs kila siku kwa siku nne mfululizo ndio nipumzike siku tatu

kisheria unatakiwa kufanya msaa yasiyozidi 12 kwa siku na masaa 45 kwa wiki
 
Swali langu nimeuliza uhalali wa kisheria wa ratiba hiyo
- Je mkataba wako wa kazi umeainisha muda wa kuingia na kutoka kazini?

Kimsingi
- Muda wa kumhudumia mwajiri wako ni masaa 8 kwa siku,
- Iwapo unaanza kazi saa 2 basi saa 10 unakuwa umemaliza.

Kwa waajiri wengine, muda wa ziada (overtime) na siku za sikukuu ambazo kawaida unapswa kuwa nyumbani, huingizwa kwenye hesabu na kupata malipo yako ya ziada ( overtime ) kulingana na idadi ya masaa kwa mwezi husika,

Baadhi ya taasisi wafanyakazi hufurahia sana pindi wanapokuwa na muda wa ziada wa kufanya kazi, na hata siku za sikukuu zikiangukia wakiwa kazini kwao huwa ni furaha sababu mwishoni mwa mwezi yale masaa yatasomeka na fedha ya ziada inakuwepo.

- Ongea na mwajiri wako, kuhusu musaa yako ya kazi stahiki na swala la overtime kwa ule muda wa ziada unao ongezeka.
 
Asante sana.kwa maoni yako mkuu nimeyasoma na luyaelewa
 
Fact! Hapo lazima kuna saa moja ya kula. Mimi binafsi kazi ya hivyo ningeipenda sana maana inanipa siku za kufanya mambo yangu bila kuingiliwa na majukumu ya ofisi. Ktk hayo masaa 12 atoe saa moja ya kula, atapata masaa 44 kwa week ambapo kisheria ipo ndani ya masaa ya mwajiri kwa wiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…