Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

UMEWAZA SANA
 
Mkuu ningependa kujua kama serikali ya Tanzania imeshawasiliana na Google kuhusu utata ulioko kwenye mpaka wa Ziwa Nyasa na kuwataka wasiuonyeshe ulivyo. Aidha, kuna hatua zozote rasmi zinazoendelea kujadili suala hili kati ya wahusika wakuu (GTZ na GM) ikiwa ni pamoja na taasisi husika kimataifa?

Huko nyuma, Nyerere alianza lakini akalipa uzito mdogo kwa vile hakukuwa na mgogoro. Kikwete pia alianza mazungumzo. Inaelekea hayakufika popote. Kwa vile maisha yanaendelea kawaida naona serikali haioni ulazima wa kusumbukia sana suala hilo.

Kisheria Google wako sahihi lakini huwa wanaweza kutilia maanani masuala ya kisiasa (penye utata) wakiwasilishiwa facts za msingi rasmi na kuweka footnote. Km wadau walivyosema wanaweza wasiweke mpaka wowote na kuweka majina yote mawili ya ziwa.

Google ni kampuni ya kiteknolojia sio ya kiutawala au kisiasa. Haimiliki taarifa. Inazionyesha tu. Inafanyia kazi facts rasmi zilizopo katika kutengeneza documents zao. Kama serikali haijawasiliana nao kuhusu hizo ramani na utata wa kihistoria katika hilo ziwa basi si vyema kuwajia juu kama vile wamefanya kosa.
 
Mipaka ya kikoloni hiyo ukimeet terms and conditions zao unaweza kua kama Israel.
 
Mkuu mipaka ya kikoloni ndio iliyoidhinishwa na OAU kuwa mipaka halisi ya nchi zote za kiafrika zilizopata uhuru. Kumbuka pia ili kuipata ardhi kati ya makoloni ilikuwa ni kwa mapigano ya kivita. Anayeshinda ndiye anapata nchi au kwa makubaliano ya kuuziana.
Wakoloni wa kiingeleza na wajerumani walipeana maeneo ziwa Nyasa lote likagawiwa kwa Malawi 1890. Huu mgawanyo wa mipaka ya majini umekuja baadaye. Kwa maana hiyo hata ukienda kwenye mahakama za kimataifa mshindi ni Malawi ndio wenye ziwa lao.
Kumbuka pia Nyerere mwenyewe alikiri kuwa mipaka ya kikoloni ilituathiri kwani mpaka wetu ni pwani ya ziwa Malawi, ukiingia kwenye maji ujue uko Malawi.
Mgogoro huu unahitaji kutatuliwa kidiplomasia aidha tuwape malawi eleo la pwani yetu au bandari ya Mtwara ili tupate access ya ziwa Malawi au tuanzishe command ya jeshi la wanamaji liwe eneo la kijeshi tayari kwa vita
 
Mkuu 'Drifter', mimi sijui, kwa sababu sipo huko serikalini; lakini ni wazi kabisa kuna uzembe mkubwa sana kwa wahusika huko serikalini kuhusu jambo hili. Wizara ya Mambo ya nje ni dhahiri haitimizi wajibu wake sawasawa kuhusu jambo hili.
Huko nyuma, Nyerere alianza lakini akalipa uzito mdogo kwa vile hakukuwa na mgogoro. Kikwete pia alianza mazungumzo. Inaelekea hayakufika popote. Kwa vile maisha yanaendelea kawaida naona serikali haioni ulazima wa kusumbukia sana suala hilo.
Hapana. Huko nyuma Kamuzu Banda alipo jaribu kulazimisha alionyeshwa wazi asithubutu kufanya hivyo. Kuna vimashua vyake vilizamishwa ziwani. Kwa hiyo halikuwa jambo dogo na wala halikupewa "uzito mdogo".

Kwa mara ya mwisho, kwa kumbukumbu nilizo nazo harakaharaka ni kuwa swala hili lilipelekwa kwenye usuluhishi wa nchi za SADC; kwa kuwa wahusika wote ni wa ushirika huo. Matokeo ya usuluhishi huo sijui, na sijui kama ulitoa majibu yoyote. Hii nadhani ndiyo hiyo uliyo itaja kwenye awamu ya Kikwete.
Baada ya hapo, sijasikia tena juhudi nyingine zozote zilizo fanyika.

Lakini, katika mfululizo wa yote haya, na kwa muda wote, tokea enzi za Banda, Malawi wameendelea jambo hili na kulifanyia kazi bila ya kutustusha; kama huko kueneza ramani zinazo onyesha mipaka yao. Sisi huko hatukufanya chochote.

Bila shaka, ni kama ulivyo eleza hapo kwamba; hawa viongozi wetu hawaoni 'urgency' ya kulishughulikia hili jambo kwa ukuamini kuwa hakuna chochote kitakacho badilika (locally). Wananchi wataendelea kufanya shughuli zao bila kubughudhiwa na Malawi; lakini huko nje, Malawi wanaendelea na juhudi zao za kuimarisha madai yao kwa vitendo.

Ni wakati sahihi serikali ilipe uzito jambo hili na kuzima yanayo fanywa na Malawi kujitambulisha kuwa ndiye mmiliki wa ziwa hadi ufukweni kwetudh
 
Mpaka HUO uliwekwa HIVYO na wakoloni baada ya mWALIMU Nyerere kuwaondoa wakoloni. Google earth hawako SAHIHI, NI wachonganishi
 
Sawa. Lakini katika dunia ya leo si rahisi kuanzisha vita kugombea mipaka. Maazimio ya AU na UN yanatosha kuweka mambo sawa.

Hata Malawi wanajua ule mpaka wa enzi za wakoloni hauna uhalisia. Ndio maana wametulia na kuacha ziwa litumike upande wa Tanzania.

Kinachotakiwa ni kwa serikali yetu kuweka msimamo kuhusu eneo letu halali la ziwa na kuwasilisha nia ya majadiliano na Malawi. Period.

Kuhusu Google ni juu ya serikali kuwasilisha hoja kuhusu utata uliopo na kukubaliana namna ya kufanya marekebisho kwenye machapisho yao bila kuathiri facts zilizoko.
 
Mkuu sio rahisi kutatua mgogoro huu kwa kupitia channels za UN wala AU kwa sababu maamuzi ya kikoloni yalifanyika kibabe hata kabla ya hiyo UN au AU zamani OAU. Njia pekee inayoweza kutumika ni kwa nchi hizi mbili kukubaliana kuachana na mikataba ya kikoloni na kukubali kumiliki ziwa kwa pamoja au kuuziana kwa kubadilishana mali kwa mali.

Mgogoro huu huibuka pale ambapo nchi moja inapotaka kuionyesha nyingine kuwa ndio mmiliki na kupanga mipango ya matumizi bila kumshirikisha mwingine. Kumbuka awamu ya nne ya Kikwete, Malawi walileta kampuni la kiingeleza kutafiti uwepo wa mafuta, tukataka kushikana mashati hadi mgogoro ukazimwa na usulihishi wa Joackim Chisano. Angarau kwa muda kulikuwa kimya, ingawa Serikali haitaki kusema kilichoamuliwa .... Nadhani tuliangukia pua.

Serikali haiwezi kuwazuia Google wasitoe facts kwa msingi wa historia, Serikali inapaswa kufungua njia ya majadiliano ya kidiplomasia yanayolenga kutatua mgogoro na kukubaliana, baada ya kuafikiana ndipo inafuata taarifa kwa UN AU au hata Google kufanya marekebisho ya taarifa. Ni bahati mbaya sana kuwa Serikali badala ya kufanya ziara zinzolenga kutatua matatizo kama hili la ziwa Malawi, Viongozi wetu wanachoma mafuta na makundi ya watumishi wa Serikali na wasanii kwenda kula bata na kufanya shopping wakati wangepiga kambi Lilongwe hadi kieleweke.

Huu mgogoro hauna tofauti na mchakato uliounda taifa la Israel, mfano mwingine ni huu wa Ukraine, maeneo yaliyotwaliwa na Russia hadi hivi sasa baada ya mapigano na kuyateka, kamwe hayawezi kurudishwa kwa Ukraine hivi hivi kama zawadi na UN hawana namna ya kufanya.
 
South Sudan ilikuwepo katika mipaka ya Uhuru wa Sudan.
Usikariri mambo, mambo mengi yaliyowekwa na wakoloni na hayana tija kwa waafrika yamebadilishwa ikiwemo na hilo la mipaka.

Yaani watanzania wakichota maji ya ziwa hilo ni kuwa wamekunywa maji ya Malawi. Ni shetani tu anaweza kukubali mpango huo.

Kutokana na mkataba wa wakoloni, Mto Nile mwenye haki ya kutumia maji ya mto huo ni Misri peke yake. Nani atakubaliana na ujibga huo ikiwa mto huo umepitia nchi kadhaa za Afrika. Waafrika amkeni. Hata Suezi kanal ilibadilishwa mkataba wake.
 
Nimemaliza.

Jamaa kaenda deep sana. Nimejifunza mengi sana kuhusu huu mgogoro.
 
Ukweli usemwe na sio kupotoshwa.
Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi kisheria, Tanzania mpaka leo tunaendelea kudai haki ya kudhurumiwa kupata sehemu ya ziwa. Hicho ndio google map wamefanya.
Wewe google imekuja lini na Ziwa lilikuwepo tangu lini? Ina maana watu wakipindi hiko chote walikuwa hawajui?

NB: Sijasoma maelezo Yako maana najua umeandika Mafi ya mbusi tu
 
Kwa sababy hujui sheria za kimataifa kuhusu mipaka ya majini. Kwa mfano kina cha ziwa kikipunguka mpaka utakuwa wapi.
 
Kama wewe ni mtanzania basi hufai kuishi, yaani tena usije kuongea mbele za watu tukakusikia...

Ila naimani wewe siyo mtanzania ila ni mmalawi unayejiita Zanzibar.
 
Huna akili mkuu. Toka lini water bodies ikawa ya upande mmoja yote..? Wewe mmalawi dawa tukujue na tukupeleke mahakamani.
 
Hapo sikuungi mkono kipindi kile tunataka kupigana watu tulikuwa tunajamba jamba unadhani tulikomalia kisicho halali we we inatakiwa mamlaka ikuchunguze
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…