Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Kuna wanyasa Malawi na kuna wanyasa Tanzania (wanaongea lugha moja) na asili ya hawa watu sio Bantu ni Żulu (wahamiaji).

Sasa utagawa vipi ziwa bila ya kugawa watu. Si baadae watasema Ruvuma pia ni yao.

Hata Masai ni Nilo-Hamites, sio mbantu, Masai asili yake ni South Sudan; Tanzania ni muhamiaji tu.

Tuheshimu mipaka ya nchi iliyopo.
 
Weka hapa tuzijali...usiongelee vitu vya kusadikika
Siwezi kuweka humu masuala nyeti ya wizara ya katiba na sheria pamoja na mambo ya nje. Aliyeshughulikia suala hili na Tanzania ikashinda kesi kwa Malawi kuingia mitini ni Hamza Johari kwa sasa ni mwanasheria mkuu wa Tanzania AG.

Ofisi zake zipo pale pembeni ya mahakama kuu kama unaelekea wizara ya ardhi, ibuka tu na uombe hizo nyaraka naamini utapewa ingawa itabidi ueleze sababu haswa ya kuzihitaji ni ipi.
 
S
Sawa basi.
Malawi tutaipa zanzibar halafu itupatie hio sehemu ya ziwa case closed.
 
HUNA na hujawahi kuiona na hutakaa uione kwasababu hazipo Africa...
 
Nani alikuambia hivyo wewe mkimbizi wa Kamuzu Banda.Unakumbuka Berlin Conference 1884 -1885 kuhusu Maziwa na mito wewe????Punguza hoja za kuchukiza kwanza mpaka sasa ilitakiwa Malawi achapwe kwanza ili tuheshimiane.
 
Nakumbuka miaka ya 90 mwanzoni nilipokuwa shule ya msingi na sekondari kabla ya uwepo wa google map tukichora ramani ya tanzania, mstari wa mpaka kati ya Tz na Malawi katika ziwa nyasa tulikuwa tunauchora katikati ya ziwa.
 
Kuna wanyasa Malawi na kuna wanyasa Tanzania (wanaongea lugha moja) na asili hawa sio Bantu ni Żulu.

Sasa utagawa vipi ziwa bila ya kugawa watu. Si baadae watasema Songea pia yao.
Siyo wanyasa tu.. Kuna Wanyakyusa wa Malawi na Wanyakyusa wa Tanzania...
Kuanzia Songwe, Iponga,Kaporo, Pusi, Mwanitete, Ngerenge,pote huko wanaoishi ni Wanyakyusa tu....,siyo Wanyakyusa wahamiaji,ni Wanyakyusa ambao walikuwe kabla hata ya uhuru wa Malawi na Tanganyika.
 
Sasa hapo google map istumike mashulen wakati hzo google map tunazo kwa simu zetu. Watamdanganya nan
 
Wamalawi si wajinga kama tunalitaka hilo Ziwa tulinunue sasa..ramani ya mjerumani ambaye ndio alionganisha makabila yote akaitengeneza Tanganyika inaonyesha ziwa Nyasa halipo kwetu, kuna agenda gani nyuma ya hili ?

 
Yes sir.Thanks a lot.
 
Ndio maana mipaka inatakiwa kuheshimiwa. Hakuna sehemu majirani hawawezi dai eneo fulani ni lao. Halikadhalika Tanzania inaweza kuwa na claim hizo hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…