Uchaguzi 2020 Utata wa muungano wa kisiasa (coalition) wa CHADEMA na ACT-Wazalendo katika macho ya Sheria

Ukimsikiliza mahela, ukamsikiliza mtungi, unajiuliza maswali mengi sana lakini sawali kubwa kuliko yote, NI KWA NINI AWAMU HII WENGI WA WANAOTEULIWA KWENYE NAFASI MUHIMU NI WALE WASOMI (WALIOSOMA BILA KUELIMIKA WALA KUSTAARABIKA) WAJINGA NA WANAFIKI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi huwa naiona ofisi ya msajili na msajili mwenyewe kama makada wa CCM wenye akili fulani za kiuwendawazimu. Kuanzia Jaji Liundi, Tendwa mpaka huyu Mutungi. Yaani kichwani weupe mnoo.

Hili suala la Muungano au Ushirikiano baina ya vyama liko wazi mnoo katika mambo ya kisiasa. Huhitaji hata shule ya kisheria kulidadavua.

Katika mfumo wa siasa za vyama vingi suala la ushirikiano baina ya vyama vya siasa ni jambo la kawaida sana, lipo siku zote, haliwezi kuepukika na wala halihitaji sheria yoyote ile ili kulifanya liwepo au lisiwepo. Nature ya mfumo wa siasa za vyama vingi inalifanya liwepo. Kikubwa katiba inatoa uhuru kwa mtu yoyote kuchagua chama au itikadi anayoitaka, huwezi kuzuia wagombea, wanachama au vyama kushirikiana kwenye uchaguzi.

Kuhusu muungano baina ya vyama vya siasa hilo ni suala lingine tofauti kabisa. Siku zote katika nyanja zote muungano rasmi ni suala la kisheria. Hivyo tafsiri ya kisheria ndio ingehitajika.

Tukirudi kwenye suala la Chadema-ACT, sote tunajua haliwezi kuwa suala la muungano maana muda wa kisheria ulishapita na wahusika wa hivyo vyama hawakusema kama wana mpango wa kufanya muungano bali ushirikiano. Sasa sijui msajili analitoa wapi?

Yaani Lissu kasema CHADEMA inamuunga mkono Maalim Seif na Maalim Seif kasema ACT inamuunga mkono Lissu, ghafla tu msajili anaibuka na kulikemea! Huo ni wazimu wa ofisi ya msajili.
 

Wateule wanalinda ugali.
 
Your talking tooooo much
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…