Utatu wa Dkt. Magufuli, Eng. Kijazi na Eng. Mfugale katika ujenzi wa barabara nchi nzima tutaukumbuka milele

Barabara ya Jet corner hadi Davis corner na ile ya kutoka Mbezi hadi Goba zote zilijengwa wakati wa Kikwete tafuteni barabara nyingine alizojenga sio kumpa sifa za mwingine.
Unachosahau Magu alikuwa Waziri wa ujenzi,Kijazi alikuwa katibu na Mfugale alikuwa mkurugenzi wa TANROADS
 
Utatu unaozungumzwa hapa ni: Waziri - Katibu mkuu - DG Tanroads

Utatu huu umeanza kujenga barabara awamu ya mzee wa Lupaso, Ben Mkapa!
Kama mtoa mada alikuwa na maana hiyo, kwanini hakutaja barabara nyingine au walijenga hizi tu?
 
Ngoja team legacy waje 😂😂😂
 
Barabara ya Jet corner hadi Davis corner na ile ya kutoka Mbezi hadi Goba zote zilijengwa wakati wa Kikwete tafuteni barabara nyingine alizojenga sio kumpa sifa za mwingine.

Kajenga Chato
 
Limekugonga utosini jiwe...Pole! Acha hasiara Tanzania ni ya watanzania siyo ya makundi fulani. Mwelewe Mh. Rais yeye hana hizo tabia kutwa kucha kumchonganisha kwasababu zenu binafsi!
Kwahiyo ndio kila kitu kizuri kilichofanywa hata kama kimefanywa na mtu mwingine bado mumsifie yeye na sisi wengine tunyamaze tu!
 
Eneo kubwa la barabara ulizosema zimejengwa kuanzia wakati hao wote wakiwa wizara ya Ujenzi.
Lini mmeanza kuwasifia mawaziri wa sekta husika, Mbona sijawahi kusikia mkimsifia waziri Mbarawa kuhusu ujenzi wa barabara zilizojengwa wakati Magufuli akiwa Rais? Acheni mambo yenu lengo lenu ni kumsifia Magufuli binafsi kwa kila kitu sema mkiumbuliwa mnatafuta pa kutokea.
 
Mimi najua legacy yake kubwa ni roho mbaya na asiyependa kuona mwingine yupo juu yake yaani ni mtu mwenye roho ya kwanini.
 
Unachosahau Magu alikuwa Waziri wa ujenzi,Kijazi alikuwa katibu na Mfugale alikuwa mkurugenzi wa TANROADS
Kwahiyo,mbona sasa hivi amuwasifii hao mawaziri, makatibu wakuu na wakurugenzi au wakati Magufuli akiwa Rais yeye ndiye alikuwa waziri wa kila wizara yeye pia alikuwa katibu mkuu na mkurugenzi kila sehemu?
 
Chato/Geita—Tanga—Iringa. Ndiyo uone Mzee alivyokuwa anafuata ushauri wa kitengo. Alikuwa haangalii eti msukuma mwenzangu au ndugu yangu.
 
Ye katoa post baada ya mizunguko aliyoifanya. Kuna mwingine anaweza kuzungumzia umeme baada ya kuzunguka vijijini na kukuta umeme umetapakaa.
 
Mimi ni kati ya watu niliosikitika kuondoka kwa Prof. Muhongo wizara ya Nishati.

Nilimpondea sana Kalemani mwanzo wa uongozi wake wizara ya Nishati na kumsifia mtangulizi wake.

Na hapo kama umefuatilia mjadala hajasifiwa raisi pekee bali muunganiko wa raisi, waziri wa ujenzi na mkurugenzi wa TANROADS ingawa baadhi ya hizo barabara zilizo sifiwa zipo chini ya TARURA siyo TANROADS.

Nilisikitishwa pia kuondoka kwa Prof. Mbarawa wizara ya ujenzi.

Nafikiri kinachokusumbua ni uzanzibari au/na umagufulification au wewe ni wachukia umagufulification.
 
Kwanza hizo barabara nilizozitaja zote zipo chini ya Tanroads pia wakati ujenzi wa barabara ya Jet corner - Davis corner(Naijua vizuri kuliko zile nyingine) imeanza kujengwa 2008/2009 wakati huo Kijazi na Mfugale hawakuwepo kwenye hizo nafasi sasa huo utatu mnao uzungumzia umetokea wapi? Mimi binafsi nakubali kweli hao watu wamefanya mengi mazuri lakini msiwape sifa za watu wengine basi.
 
Hawafai wote wale, walikuwa wanazua miradi mingi mingi haraka haraka ile wapige mkwanja mrefu haraka haraka; sasa Mungu fundi akwaua wote kwa haraka haraka pia!
 

Anatwambia, kiala kila kinakifu, vikana.

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Dah mkuu ni typing error au Hasira?
 
Unachosahau Magu alikuwa Waziri wa ujenzi,Kijazi alikuwa katibu na Mfugale alikuwa mkurugenzi wa TANROADS
Kwanini wote wanekufa ndani ya miezi 5 mwaka huu?

Kabla hawajakufa kwa nafasi zao walihakikisha wanayapa madaraja na mastendi majina yao. Mfugale flyover, Magufuli bus stand na Kijazi interchange??

Kuna kitu kuhusu utatu wa uovu (evil triangle) wa hawa tutakuja kuujua siku ikifika.
 
Kwani kabla yao barabara hazikujengwa? Baada ya kufa barabara zimesimama kujengwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…