Utatuzi wa Migogoro kwa njia ya usuluhishi ni kitu bora zaidi

Utatuzi wa Migogoro kwa njia ya usuluhishi ni kitu bora zaidi

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Kuna migogoro mingine hata sio ya kupelekana Mahakamani na kuipatia mahakama mzigo.

Unakuta ni suala la kutatua tu kwa mazungumzo basi Kesi inaisha.

Lakini sasa kwa kuwa watu wengine wana pesa basi watataka kujionesha kuwa anaweza na ukute anayeshtakiwa ni mtu wa kipato cha chini.

Basi mtu huyo akifungwa yeye roho Kwatu.

Mfano kesi za Ardhi hizi Ndio zingetatuliwa kwa njia ya usuluhishi kwa sababu ugomvi wao unakuwa unaeleweka kabisa.

Mfano ugomvi wa mipaka Jamani hadi utafika pabaya wakati kitu kinaeleweka kabisa.

Hata kesi za Ndoa, Mirathi zinafaa kabisa kutatuliwa kwa njia ya usuluhishi.

Kwa kufanya hivo Kutapunguza mlundikano wa kesi mahakamani.

Sio kesi zote zinafaa kutatuliwa kwa njia ya usuluhishi Mfano ubakaji, mauaji, na kesi nyingine kama hizo.

Faida za kutatua kesi kwa njia ya usuluhishi.
Kwanza haipotezi Pesa na muda.
Huleta Amani
Huimarisha uhusiano.
Inapunguza mlundikano wa kesi.
Hupunguza migogoro ndani ya Jamii.

Ni muhimu sana kufanya usuluhishi.@
 
Back
Top Bottom