MAPITO Mwanza
JF-Expert Member
- Aug 21, 2018
- 4,236
- 5,907
Bona Mzee huna adabu?Wenzako washagawan a mkate Wewe unaleta mada Uchwara ππππ₯πΌπ
Hapana naona unamsema Mwenyekiti Freeman E. Mbowe mafumbo ya Maswali!! Kuwa makini, huyo ni shida ..waulizwe walioshuhudia wenzako waliocross mstari wa jamaa kilichowakita!!!Sasa Swali letu ni hili
Mkilewa msiingie jfHapana naona unamsema Mwenyekiti Freeman E. Mbowe mafumbo ya Maswali!! Kuwa makini, huyo ni shida ..waulizwe walioshuhudia wenzako waliocross mstari wa jamaa kilichowakita!!!
HahahahahaaasiasaahazinaadabuuTujikite kwenye katiba mpya!!
Nusu mkate unatia hasira!
Kwani mbowe keshafika bei!!?Maana tulikubaliana hakuna uchaguzi bila katiba mpya!
Nje ya madaKwani Mbowe siyo wa milele?
Mambo ya katiba mpya hamtaki tena π€ͺπ€ͺπ€ͺJikiteni kwenye mada
Mbowe amekalia kiti kwa kidingizio kuwa akiondoka chama kitayumba!Wapambe walikuwa wanaangalia ulaji tu. Muswada ungepelekwa bungeni nani angepinga chini ya bunge la chama kimoja? Inahitaji akili ya kawaida tu kujua kwamba hata magufuli tayari alikuwa ameridhia kuendelea kukalia kiti kwa kisingizio cha kukamilisha miradi.
Sasa mkuu mh mbowe anaongoza mpaka lini?Wapambe hawakuelewa hilo
Usiwe mjinga , mada haihusu MboweSasa mkuu mh mbowe anaongoza mpaka lini?
Ujumbe umefika... Karibu. Ha ha haaa!Mkilewa msiingie jf
Walk the talk...!!! Acha blah blah.Usiwe mjinga , mada haihusu Mbowe
Najuwa umeweka hata ushahidi wa picha kuunga mkono hoja yako, na ninakubaliana nawe. Sasa niambie kama hujasikia watu kama hao hao ulioweka picha zao, leo hii wakisema yale yale kwa huyu aliyepo sasa!Tunaendelea na nyuzi zetu za mwezi wa 3, ambao ni mwezi wa Mungu.
Ni wazi kila mwananchi anafahamu kuhusu kampeni za wazi kabisa za kutaka Rais wa awamu ya 5 Dkt John Magufuli aongezewe muda wa utawala wake kinyume kabisa cha Katiba ya Tanzania, yaani baada ya kumaliza utawala wake wa miaka 10, bado aongezewe miaka mingine isiyo na idadi.
Kampeni hii kabambe iliongozwa na kundi lisilo rasmi lililopachichwa jina la "Sukuma gang" na baadaye kuanza kuungwa Mkono hadharani na baadhi ya watu , na hatimaye likatua bungeni likiletwa na mbunge wa ccm Jimbo la Nkasi (zipo taarifa kwamba nyuma yake kulikuwa na kundi kubwa), Huku hoja yake ikiungwa mkono na Spika wa Bunge hilo Job Ndugai , na kwamba inasubiriwa muda ufike lipelekwe bungeni ili lijadiliwe na Katiba ya Nchi ibadilishwe.
View attachment 2938286
Hata baada ya Jambo hilo kupoa kidogo likaibuliwa tena na Mbunge wa Bahi Juma Nkamia , akisisitiza umuhimu wa kumuongezea John Magufuli muda wa uongozi , huku akisisitiza kwamba muhula wa Urais uwe miaka 7 badala ya mitano iliyowekwa kwenye Katiba ya Nchi .
Wale wote waliopinga jambo hili walionekana Wasaliti na walishughulikiwa chini kwa chini na Wateule wa Rais kuanzia kwenye chama hadi serikalini , huku Wateuliwa wengi wakichekelea na kuvimba kwa kiburi wakijua watakuwa wateule milele (Hapa ndipo ilipoanzia sumu aliyolishwa Mangula)
Ushahidi wa wapinga milele kushughulikiwa ulikuja kuthibitishwa na Juma Nkamia mwenyewe , alipokiri hadharani kwamba Alilazimika kutamka kwamba Magufuli aongezewe muda ili kunusuru uanachama wake ndani ya ccm , kwamba kulikuwa na mpango wa kumvua uanachama , na kwa vile mkubwa alifurahishwa na kauli ya Nkamia ya kumuongezea muda , Nkamia hakutimuliwa tena .
View attachment 2938287
Wakati haya yakiendelea , Viongozi karibu wote wastaafu walikuwepo huku wakinyamaza kimya as if hakuna uchafu unaopangwa , Wakuu wa vyombo vya dola wakiwa kimya ikiwa ni ishara ya kuunga mkono uharamia huo .
Sasa Swali letu ni hili , Waliokuwa wanafanya Kampeni hiyo haramu walichagizwa na nini hasa , Je ni Utendaji bora wa Magufuli na kwamba hakuna Mwanaccm mwingine angeweza kutenda kama Yeye , ama walichagizwa na Uroho wa madaraka ili waendelee kula miaka yote baada ya Rafiki yao kuwa madarakani milele ?
NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
Hapana. Huyo jamaa ana pointi sana ambayo wewe ndiye unayetaka kuipindisha kwa maksudi kabisa.Nje ya mada , inasikitisha sana kwa vijana wa ccm kukosa hoja kabisa hapa Jf kiasi cha kutia aibu .
Aiseh!Nusu mkate Sugu katupwa Kwao Makete, Lema katupwa Moshi Mjini na Mchungaji Msigwa Makambako πππ
CCM kiboko
Karibu sana mkuu , nadhani ulichelewa kidogo , hizi mada si za Chadema ni mada zangu kwa ajili ya mwezi wa 3 ambao ni mwezi wa Mungu , kutokana na " Kwaresma na Ramadhan " kukutana , lengo langu ni kuhakikisha haya mambo hayajirudii tenaNajuwa umeweka hata ushahidi wa picha kuunga mkono hoja yako, na ninakubaliana nawe. Sasa niambie kama hujasikia watu kama hao hao ulioweka picha zao, leo hii wakisema yale yale kwa huyu aliyepo sasa!
Nchi hii tatizo letu ni kuwaruhusu watu wa makundi ya aina hii kuwa ndio wanaoongoza akili za wengine wote. Hata watu walio na akili timamu wanaposikia ujinga wa aina hizi na wao akili zinawaruka kichwani, wanabaki kuwa kama mazuzu.
Samahani lakini, sikukusoma humo ndani, nimeona tu kichwa cha habari na kuangalia picha nikaelewa ulichokieleza.
Magufuli alikuwa mbovu sana katika mambo mengi; lakini sasa tunaona tofauti kubwa sana iliyopo, hasa katika yale mazuri aliyokuwa akiyasimamia kwa manufaa ya nchi hii.
Erythro, rafiki yangu, huu siyo wakati wa CHADEMA kuhangaika na haya. Najuwa unafahamu kazi kubwa sana inayosubiri kufanyika. Msitelekeze wajibu wenu huo, kwa kupoteza muda na haya yasiyokuwa na manufaa yoyote kwa waTanzania kwa wakati huu.
Bado sijarudi, lakini kiherehere kimenilazimisha niyaweke haya kwenye mada yako hii.
Labda Mkapa na Mwinyi walinga mkono.Tunaendelea na nyuzi zetu za mwezi wa 3, ambao ni mwezi wa Mungu.
Ni wazi kila mwananchi anafahamu kuhusu kampeni za wazi kabisa za kutaka Rais wa awamu ya 5 Dkt John Magufuli aongezewe muda wa utawala wake kinyume kabisa cha Katiba ya Tanzania, yaani baada ya kumaliza utawala wake wa miaka 10, bado aongezewe miaka mingine isiyo na idadi.
Kampeni hii kabambe iliongozwa na kundi lisilo rasmi lililopachichwa jina la "Sukuma gang" na baadaye kuanza kuungwa Mkono hadharani na baadhi ya watu , na hatimaye likatua bungeni likiletwa na mbunge wa ccm Jimbo la Nkasi (zipo taarifa kwamba nyuma yake kulikuwa na kundi kubwa), Huku hoja yake ikiungwa mkono na Spika wa Bunge hilo Job Ndugai , na kwamba inasubiriwa muda ufike lipelekwe bungeni ili lijadiliwe na Katiba ya Nchi ibadilishwe.
View attachment 2938286
Hata baada ya Jambo hilo kupoa kidogo likaibuliwa tena na Mbunge wa Bahi Juma Nkamia , akisisitiza umuhimu wa kumuongezea John Magufuli muda wa uongozi , huku akisisitiza kwamba muhula wa Urais uwe miaka 7 badala ya mitano iliyowekwa kwenye Katiba ya Nchi .
Wale wote waliopinga jambo hili walionekana Wasaliti na walishughulikiwa chini kwa chini na Wateule wa Rais kuanzia kwenye chama hadi serikalini , huku Wateuliwa wengi wakichekelea na kuvimba kwa kiburi wakijua watakuwa wateule milele (Hapa ndipo ilipoanzia sumu aliyolishwa Mangula)
Ushahidi wa wapinga milele kushughulikiwa ulikuja kuthibitishwa na Juma Nkamia mwenyewe , alipokiri hadharani kwamba Alilazimika kutamka kwamba Magufuli aongezewe muda ili kunusuru uanachama wake ndani ya ccm , kwamba kulikuwa na mpango wa kumvua uanachama , na kwa vile mkubwa alifurahishwa na kauli ya Nkamia ya kumuongezea muda , Nkamia hakutimuliwa tena .
View attachment 2938287
Wakati haya yakiendelea , Viongozi karibu wote wastaafu walikuwepo huku wakinyamaza kimya as if hakuna uchafu unaopangwa , Wakuu wa vyombo vya dola wakiwa kimya ikiwa ni ishara ya kuunga mkono uharamia huo .
Sasa Swali letu ni hili , Waliokuwa wanafanya Kampeni hiyo haramu walichagizwa na nini hasa , Je ni Utendaji bora wa Magufuli na kwamba hakuna Mwanaccm mwingine angeweza kutenda kama Yeye , ama walichagizwa na Uroho wa madaraka ili waendelee kula miaka yote baada ya Rafiki yao kuwa madarakani milele ?
NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO