Utawala wa Nyerere ndio waasisi wa kuteka watu,hawa wa sasa hivi wanajaribu tu

Utawala wa Nyerere ndio waasisi wa kuteka watu,hawa wa sasa hivi wanajaribu tu

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Kipindi Nyerere anachukua nchi kulikuwa na sheria ya kuweka watu kizuizini,sikumbuki ilifutwalini.

Yaani ni ile hali unachukuliwa ubatupwa selo hakuna kupelekwa mahakamani mpaka waone umekoma au umekufa ndio mwisho wako.

Enzi za mwalimu kuna mzee mmoja jirani yetu kule Oysterbay,ilikuja Land Rover 109 ikamchukua mbele ya mkewe na watoto,hawakumuona tena mpaka leo hii..kumbuka enzi hizo ukiona LandRover ujue ni sawa na LC 300 jeusi lienye tinted,gari ilikuwa inaogopeka kama ukoma.

Kule Kenya kabla hawa generation Z hawajazaliwa kuna mtu anaitwa Ouko alichukuliwa kwa style hizo.

Nikiweka orodha ya watu waliotekwa na Nyerere kesho sitaamka najua nami nitatekwa ila itoshe kusema ni wengi sana,kuanzia wanasiasa,wahujumu uchumi nk.

Mwinyi na Mkapa walijitahidi kupambana na wapinzani wao jukwaani,mahakamabi au kuwapotezea tu.

Mzee wangu JK smiling mafia alimuonjesha Dk Ulimboka jinsi ya kung"oa meno kwa kutumia nyundo.

Watekaji wa siku hizi nasikia wasipokuua basi wanakufanyia kitu mbaya huku wakikurekodi,ukifungua mdomo tu inarushwa viral kama connection.

Ndio maana wanaotekwa na kuachiwa huwa kimyaaaaa.

Jamani tunaomba watekaji acheni huu mchezo wa kitekana tekana sio poa
 
Back
Top Bottom