Utelezi wa vita ya Ukraine umemwangusha Kenyatta na Raila Odinga Kenya

Utelezi wa vita ya Ukraine umemwangusha Kenyatta na Raila Odinga Kenya

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Maisha yamepanda, maisha ni magumu na hali ni mbaya sana kwa watawala katika kipindi hiki. Ni vigumu kuwashawishi wapigakura kuwa hali hii nguvu ni kwasababu ya vita ya Ukraine na Russia na sio uzembe na ufujaji wa viongozi wao. Kilichomwangusha Raila kwenye sanduku la kura ni kuungwa mkono na Raais kenyatta kwenye kampeni zake. Nchi yoyote duniani itakayofanya uchaguzi wake kwenye kipindi nchi lazima watawala watashindwa tu, bila kujali nchi hiyo iko bara gani.

Hata hivyo, ni vigumu sana wale watakaoshinda kwenye chaguzi kipindi hiki kupata uungwaji mkono kikamilifu na mataifa ya Magharibi ikiwemo marekani, maana kupata ushindi kwenye kipindi hiki ni sawa na kuunga mkono Russia. kama ukimsikiliza vizuri William Ruto sera zake ni kama vile za kijamaajamaa za kila kitu bure.

Nchi za magharibi haziamini kwenye kutoa huduma bure kwa wananchi kama matibabu na elimu ya juu maana hii itapunguza idadi ya cheap labour kwenye mashamba, viwanda na biashara zao.

Wanaamini kuwa kama mtu atakuwa na uhakika wa kutibiwa bure na kuwa na elimu kubwa atakuwa na uwezo mkubwa wa kuchagua kazi na kujadili malipo. Sina uhakika kama Ruto atapewa Urais pale kenya kwenye miradi mingi ya Magharibi.

Ili watawala waeleweke kwa wananchi ni kuacha kupata faida za kiuchumi kwenye kipindi hiki. Yaani watangaze hatua kama kufuta posho za wabunge kwa muda, kusimamisha nafasi za ubunge wa viti maalum, kusimamisha tozo za miamala, serikali kupiga marufuku matumizi ya magari makubwa kwa watumishi na viongozi wote, kutangaza kusitisha safari za nje ya nchi ili kubana matumizi, nk. hatua kama hizo ndizo zinazoweza kuwapa imani wananchi kwamba kweli hali hii ngumu iko nje ya uwezo wa serikali yao, vinginevyo hawawezi ku associate kati ya vita ya ukraine na hali nguvu kwao tu.
 
Putin kwa staili hii anaenda kuyaangusha mataifa yote duniani. Tujiandae kama dunia kuanza moja. Wale wenye vyeo visivyokuwa na tija kwa umma wakae mkao wa kutimua.
 
Nani kakuambia Ruto na Kenyatta ni maadui, wote ni kitu kimoja walichofanya ni kumchezea mchezo Odinga na wananchi wa Kenya pia, kama angekuwa upande wa Ruto automatic Ruto angeshindwa wananchi wangempa Odinga kwa maana ya kusema Serikali au Rais anataka kumuweka mtu wake madarakani yaani Ruto, so wengi wangemnyima Ruto kura kwa kumkomoa Kenyatta na kumpa Odinga.

Hii michezo ndio Kabila na Tsesekedi walimchezea Vita Kamele pia pale ambapo Kabila alikuwa upande wa mpinzani wa Tsesekedi kumbe anataka Tsesekedi awe Rais. Ndicho alichofanya UHURU pia Ili Ruto awe Rais. Hii ni michezo ya siasa.
 
Mtawala yeyeto kusingizia vita vya Ukraine kama chanzo cha vitu kupanda bei au uchumi kuanguka huyo anatafuta tu sababu za kuhalalisha udumavu wake wa akili na kukwepa tu lawama.

Utasema sijui mafuta wakati nchini mwako una malighafi zipo tele ambazo ni kuzigeuza na kupata mbadala wa nishati ya mafuta Ili kuokoa gap. Sio kama vita vya Ukraine kama chanzo cha athari yeyeto ya kiuchumi ni chaka tu la kutupia lawama juu ya kushindwa kwa watawala.
 
Mfano market tu ya China ni kubwa achilia nchi zingine na hatuwezi ijaza. Hatuna ubunifu wa nini tuzalishe. KILA kitu China wanachukua kuanzia chakula, takataka za plastic, chuma chakavu, nk ni sisi tu tumekosa ubunifu.

KILA kitu kipo tena tele shida ni uongozi wa uwajibikaji, tuna uongozi ajira na sio uongozi wito KILA mtu uwaza uongozi Ili akaibe ashibe yeye na sio wito wa kuleta mabadiliko kwenye Jamii, ndo maana wamekalia kukopa, mara tozo na kodi watu wenyewe masikini hawa hata basic needs tu ni mtihani.

Badala ya kuchochea utumiaji wa raslimali tele zimejaa ambazo ni nyingi Sana kuliko idadi ya watu nchini zimetumika ipasavyo wasingehangaika na tozo, kodi, au kukopa. Mkoloni hakutegemea kodi kuendesha nchi na alitufanyia maendeleo makubwa Sana nchini.

Nguvu Kazi tele, malighafi tele, pesa za mitaji tele, soko kubwa Sana ndani na nje tunashindwa nini kujikomboa kiuchumi. Mfano sekta hizi tano tu zinauwezo wa kufuta kabisa tatizo la ajira nchini sekta ya uvuvi, madini, kilimo, usafirishaji, nishati achilia maeneo mengine.
 
Utawala wa Ruto hautokuwa tofauti Sana na utawala wa Moi tuwaombee tu Wakenya roho ya udikteta ishindwe, maana watawala wote wa kiafrica huwa wanaanza kama malaika kabla ya kulewa mvinyo.
 
Mfano market tu ya China ni kubwa achilia nchi zingine na hatuwezi ijaza. Hatuna ubunifu wa nini tuzalishe. KILA kitu China wanachukua kuanzia chakula, takataka za plastic, chuma chakavu, nk ni sisi tu tumekosa ubunifu.

KILA kitu kipo tena tele shida ni uongozi wa uwajibikaji, tuna uongozi ajira na sio uongozi wito KILA mtu uwaza uongozi Ili akaibe ashibe yeye na sio wito wa kuleta mabadiliko kwenye Jamii, ndo maana wamekalia kukopa, mara tozo na kodi watu wenyewe masikini hawa hata basic needs tu ni mtihani.

Badala ya kuchochea utumiaji wa raslimali tele zimejaa ambazo ni nyingi Sana kuliko idadi ya watu nchini zimetumika ipasavyo wasingehangaika na tozo, kodi, au kukopa. Mkoloni hakutegemea kodi kuendesha nchi na alitufanyia maendeleo makubwa Sana nchini.

Nguvu Kazi tele, malighafi tele, pesa za mitaji tele, soko kubwa Sana ndani na nje tunashindwa nini kujikomboa kiuchumi. Mfano sekta hizi tano tu zinauwezo wa kufuta kabisa tatizo la ajira nchini sekta ya uvuvi, madini, kilimo, usafirishaji, nishati achilia maeneo mengine.
Badala ya kwenda kuchimba ile chuma pale Mchuchuma na Liganga tuuze duniani kote tupate pesa kiongozi mwenye akili yake kamili anaona suluhisho ni kuongeza tozo kwa watu maskini sana wanaokosa milo mitatu, viatu vya watoto wao shuleni, maji ya kunywa na hata sabuni ya kufulia. Kaka huu ni ushahidi mwingine kuwa elimu yetu haitoshi kaabisa, yaani PhD yetu ya hapa ni sawa na Diploma ya nchi zenye akili na elimu nzuri.

Kaka Magufuli alikuwa na akili nyingi sana sio ya kusoma lakini ya kuzaliwa kama walivyokuwa akina Nyerere, Kishimba, Diamond, Kanumba, na baadhi ya watanzania ambao wanaajili watu 100 na zaidi kwenye taifa hili.
 
Badala ya kwenda kuchimba ile chuma pale Mchuchuma na Liganga tuuze duniani kote tupate pesa kiongozi mwenye akili yake kamili anaona suluhisho ni kuongeza tozo kwa watu maskini sana wanaokosa milo mitatu, viatu vya watoto wao shuleni, maji ya kunywa na hata sabuni ya kufulia. Kaka huu ni ushahidi mwingine kuwa elimu yetu haitoshi kaabisa, yaani PhD yetu ya hapa ni sawa na Diploma ya nchi zenye akili na elimu nzuri.
Hata mkoloni hakutegemea kodi au tozo kuendeshea nchi na alituletea maendeleo makubwa Sana nchini.
Wao hata waweke tozo KILA sehemu still hawawezi pata pesa watu wenyewe masikini hawa hata mlo mmoja ni tabu
 
Hata mkoloni hakutegemea kodi au tozo kuendeshea nchi na alituletea maendeleo makubwa Sana nchini.
Wao hata waweke tozo KILA sehemu still hawawezi pata pesa watu wenyewe masikini hawa hata mlo mmoja ni tabu
Akili ya kawaida ambayo hata babu zetu wanaifahamu ni kwamba ili ng'ombe atoe maziwa mengi ni lazima umchungie kwenye malisho mengi, umpe maji mengi na umtibu awe na afya. Falsafa hii ndiyo inayosababisha ugomvi kati ya wafugaji na wakulima. Hivyohivyo kama unataka kupata kodi na tozo nyingi kutoka kwa wananchi lazima mishahara ya watumishi iwe mikubwa, ajira ziwepo, masoko ya uhakika mazao, madini, mifugo, samaki, bidhaa za wanyama na misitu viweko, lazima kuwe na mashamba makubwa (plantations) mengi ya mazao na wanyama nchini yanayoendeshwa kisasa ambako vijana watakwenda huko kupata ajira ya kuchuma matunda, mkonge, mahindi, ngano, alizeti, kuchuna na kuanika ngozi, kuvua kwenye mameli, nk
 
Putin kwa staili hii anaenda kuyaangusha mataifa yote duniani. Tujiandae kama dunia kuanza moja. Wale wenye vyeo visivyokuwa na tija kwa umma wakae mkao wa kutimua.
Watawala wetu Afrika wako kama panya, wanamjua adui yao paka lakini hawachukui hatua dhidi yao siku zinapita wakilalama. Leo hii ukiwauliza watawala wetu kwanini sisi hatupigi hatua kiuchumi watakutajia sababu zote kwanini sisi ni maskini. Watakwambia biashara haiko sawa, masoko ya dunia hayako sawa, mikataba haiko sawa, madeni makubwa mengi, vikwazo vingi, masharti mengi, hawataki tufanye hiki na kile. Bahati nzuri mataifa yanayotukwamisha wanayafahamu kwa majina yake lakini hawana cha kufanya wote mmoja mmoja na kwapamoja pia kupitia kanda zao za EAC, SADC, ECOWAS, AU sawa na wanachofanya panya kwa paka wao. Tunafahamu mafuta ya bei nafuu yaliko lakini tunashindwa kwenda kuyachukua. Hivi kungetokea nini kama Afriva Union ikiamua kwenda kuyachukua mafuta ya bei nafuu yaliko?

Ile divide and rule bado inafanyakazi Afrika, mtu akipewa pelemende 3 kwa pamoja anakesha kucheza ngoma akisherehekea upendo na heshima aliyopewa na mtoa pipi huyo atakaeondoka na tones za dhahabu yetu.
 
Utawala wa Ruto hautokuwa tofauti Sana na utawala wa Moi tuwaombee tu Wakenya roho ya udikteta ishindwe, maana watawala wote wa kiafrica huwa wanaanza kama malaika kabla ya kulewa mvinyo.
Ruto hata kabla ya kuapishwa ameanza kununua wapinzani. Yale yala ya kuunga mkono juhudi.
 
Watawala wetu Afrika wako kama panya, wanamjua adui yao paka lakini hawachukui hatua dhidi yao siku zinapita wakilalama. Leo hii ukiwauliza watawala wetu kwanini sisi hatupigi hatua kiuchumi watakutajia sababu zote kwanini sisi ni maskini. Watakwambia biashara haiko sawa, masoko ya dunia hayako sawa, mikataba haiko sawa, madeni makubwa mengi, vikwazo vingi, masharti mengi, hawataki tufanye hiki na kile. Bahati nzuri mataifa yanayotukwamisha wanayafahamu kwa majina yake lakini hawana cha kufanya wote mmoja mmoja na kwapamoja pia kupitia kanda zao za EAC, SADC, ECOWAS, AU sawa na wanachofanya panya kwa paka wao. Tunafahamu mafuta ya bei nafuu yaliko lakini tunashindwa kwenda kuyachukua. Hivi kungetokea nini kama Afriva Union ikiamua kwenda kuyachukua mafuta ya bei nafuu yaliko?

Ile divide and rule bado inafanyakazi Afrika, mtu akipewa pelemende 3 kwa pamoja anakesha kucheza ngoma akisherehekea upendo na heshima aliyopewa na mtoa pipi huyo atakaeondoka na tones za dhahabu yetu.
Watawala hao ni maskini? Ukijua hilo, utajua
 
Vita hii ikiendelea hadi 2025 na hali ya maisha na tozo vikibaki hivihiviii, sijui bhana!!!
 
Back
Top Bottom