Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu

Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
KUNA KIFUNGU HUA KINATENGULIWA

mpango lazima afike mahakamani
 
sasa mkuu kama umepewa amri na boss wako unaanzaje kukataa?
 
Tunasubiri minyukano ya mawakili tuone mchezo mzima ulivyo
 
Natabiri sabaya kuachiwa huru na atapangiwa kazi nyingine na mamlaka za uteuzi.
 
Nimekuelewa vyema mkuu
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
 
Kwanza magufuli angekuwa hai hii isingekuwa kesi, hata gavana akiitwa kumtetea lazima atamluka ili ccm ijisafishe na kadhia hii
 
Tatizo sio kuagizwa ni je ulifanya makosa wakati wa utekelezaji wa maagizo!? Kumbuka kesi ya Zombe. Mwenye kosa hubeba kosa sio alieagiza.
Ume saiti vema, pia ameagizwa kwa ushaidi gani au uko wapi, documented?, Umeagizwa Kama nani, eneo lake la kazi lipi, halikuwa na mipaka Kama ndiyo atoe uthibitisho, maana yeye alikuwa wilaya ya hai akajitia mapembe kinyemela kuendesha ujambazi kwa uroho wa kutajirika
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Hayo maagizo yako wapi, achaneni na muhuni kapatikana
 
Hujawahi kufanya kazi hata kwenye taasisi ndogo? Hakunaga watu wanatumwa kazi maalum kutoka DSM kwenda Mwanza, Mwanza kwenda Mbeya, Mbeya kwenda Moro, Moro Kwenda Arusha, Dodoma kwenda Babati? Huko kote kunawaga hakuna wanaojua hiyo kazi?
Hilo ni genge la mafia, wamepatikana
 
Na kama hayakuwa halali kisheria hao walioyatoa walikuwa na haki kuyatoa? Na kama hawakuwa na haki kuyatoa kwa nini hawapo selo na mahakaman hadi sasa?
Hawapo mahakamani hadi sasa kwa kesi ipi?! Kama mnadhani na wenyewe wanatakiwa kuunganishwa kwenye kesi, basi ni wajibu wa Sabaya kutoa uthibitisho wa hayo maagizo ambayo yalikuwa haramu, vinginevyo, ataonekana ni mfa maji tu!!!
Mzee ukipewa maagizo si unapewa na vitendea kazi vya kutekeleza hayo maagizo!!
Hizo nyaraka ni vitendea kazi au terms of reference kwa ajili ya kutekeleza maagizo.
Hivi unatarajia kabisa official documents zitatoa maagizo yasiyo halali?!

What I see, utakuta docs zimeandika maagizo kwa kufuata kanuni na sheria, lakini hapo hapo akapigiwa simu kupewa maagizo ya ziada yasiyofuata sheria!!! Na kwavile alitaka kumfurahisha mheshimiwa, ndipo si ajabu akafanya hadi in excess!!
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Kama yalikuwa ni maagizo halali, basi alilazimika kutayetekeleza, lakini kama hayakuwa halali, kutotekeleza haiwezi kuwa insubordination!

HOWEVER, ili "kuheshimu" mamlaka, tena mamlaka yenyewe ya Kiafrika, ingekuwa ngumu kwake kusema HAPANA lakini alitakiwa kujihuduhulu ili kupisha wengine ambao wangekuwa tayari kufanya mambo yaliyo kinyume cha sheria!
 
Uthibitisho atatoa tu.
Kwa hiyo kama alipewa maagizo ya ziada yasiyo fuata sheria si ndo maana tunasema wote mtoaji na mpokeaji ni vululuvululu!!
Halafu Sasa cha kujiuliza kama saa mbaya mmoja anakiri alipewa maelekezo yasiyofuata sheria kuwa akaumize watanzania jiulize ni wangap wamepewa maelekezo ya hivyo na ni watanzania wangapi wameumizwa na dikteta? Mkiona watanzania tunalilia katiba mpya ndo mjue twalia kwa mengi.....TUNATAKA KATIBA MPYA
 
Kama sabaya asingetekeleza maagizo haiwezi kuonekana kama insurbodination kwa rais na amiri jeshi mkuu? hapa ndo swala la katiba mpya linapoonekana umuhimu wake hasa kwenye kipengele cha kupunguza nguvu na mamlaka ya rais....
Achilia mbali insurbonation kwanza; Kijana mdogo Jiwe akupe ukuu wa wilaya halafu akuagize jambo eti umjibu vyokovyoko utakuwa unajipenda wewe!!! Majaajii wenyewe na supika waliufyata ije iwe DC?!!! Kwanza simu yake tu ukioona kabla hata hajazangumza si ushajikojolea na kujihar?!!
 
Unapotumwa kufanya uhalifu na boss wako.. na ukafanya Huku ukijua ni kosa utafungwa..hata kama aliyekutuma ni rais..Sheria ni msumeno na hakuna aliye juu ya Sheria nchi hii ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…